Mbagala Dar es Salaam ni chafu sana, inanuka

Mbagala Dar es Salaam ni chafu sana, inanuka

Eneo la Mbagala lililomo kwenye wilaya ya Temeke ni eneo chafu sana sana, ili uweze kuelewa ninachokisema kabla haujanipinga ni vizuri utembelee eneo la Rangitatu ninauhakika hata hizo Rangitatu hautaziona kutokana na uchafu ulioko huko.
Unashauri solution gani juu ya changamoto tajwa?
 
Viongozi wote wa CCM wameitelekeza, si mbunge, mkuu wa wilaya wala mkuu wa mkoa wanaiogopa Mbagala!
Hii sio solution bali una-complain. Wameitekeleza sababu wananchi hawana cha kusema wala cha kushauri, wamekaa kimya.

Sasa toa ushauri na solution nini kifanyike ili kuondoa tatizo.
Otherwise dhumuni lako la kuanzisha mada ni lipi?
 
Kuna maeneo ukitembelea utagundua bado sisi ni maskini sana.

Na ukisikiliza mazungumzo ya watu ndio utazidi kusikitika kwa kugundua kwamba uelewa wa wananchi wengi wa mambo muhimu yanayowahusu ni mdogo sana.
 
Eneo la Mbagala lililomo kwenye wilaya ya Temeke ni eneo chafu sana sana, ili uweze kuelewa ninachokisema kabla haujanipinga ni vizuri utembelee eneo la Rangitatu ninauhakika hata hizo Rangitatu hautaziona kutokana na uchafu ulioko huko.

Mbagala ina barabara kuu ya Kilwa japo kote inaonekana safi ila ukifika Mbagala inatoweka kwa uchafu na unaiona tena ukiivuka Rangitatu! Mitaa yote ya Rangitatu ambalo ndilo eneo la biashara ni michafu na yenye vumbi na mashimo na ndiyo inayozalisha kura za ushindi wa ubunge kwa CCM huku wanyamwezi ardhi kama hiyo wanazalisha viazi vitamu.

Rangitatu kuna maduka yanauza nafaka ambazo humwagika na zikilowa huchacha na kusababisha harufu kali na joto linalotokana na pumba za mahindi zilizolowa, Mbagala ni chafu na unachangiwa zaidi na serikali kuruhusu wamachinga kujazana barabarani wakifanya biashara na kukojoa hovyo kwani hakuna vyoo vya jiji licha ya jiji kukusanya kodi ya maendeleo na kutofanya usafi!

Tahadhari, usije Mbagala wakati wa mvua.
Nakuunga mkono lakini usifanye generalization, Mbagala kubwa na kuna maeneo mengi tu masafi na hayana shida.

Ungeenda kutaja maeneo ya Mbagala directly Kama Rangi tatu nk hapo ingekuwa vizuri zaidi

ILA KIUKWELI RANGI TATU NI CHAFU HASA IKINYESHA MVUA
 
Imekuwa too much mkuu,, maeneo mengi Tanzania hii ikinyesha mvua ni kisanga.

Na sehemu nyingi zenye masoko, mvua ikiwepo panazidi kuchafuka.
Ushawahi fika TMK sterio pakinyesha? Heeee kama unanata unaweza ishia nje.
D unapajua sokoni sterio Kumbe!? Siku ukija tena nicheki nikupe parachichi na passion bure ukatengeneze juice.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Hata vyakula vya ovyo unaweza kulishwa huko sijui nyama ya chura, kenge, panya, nguruwe yaani Pako ovyo kinoma , nyumba hazina ustaarabu ,kukabwa nje nje Tena hata saa Saba.
Unaweza kuta huyu anayeisema Mbagala rangi tatu namna hii anaishi kwenye kibanda huko uswekeni. Usiku akilala ukuta umeachia nyufa amezuia na mti unamuuliza nikuue au nikuache? Dirishani ameweka pazia khanga za CCM za kampeni za 2010 "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA".

Social media life versus really life.

Halafu mkuu katika nyama za hovyo ulizoziorodhesha hapo, ondoa huyo nguruwe. Mpe heshima yake hata kama wewe hutumii tafadhali.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Nakuunga mkono lakini usifanye generalization, mbagala kubwa na Kuna maeneo mengi tu masafi na hayana shida



Ungeenda kutaja maeneo ya mbagala directly Kama Rangi tatu nk hapo ingekuwa vizuri zaidi



ILA KIUKWELI RANGI TATU NI CHAFU HASA IKINYESHA MVUA
Nimesema Rangitatu na nikatoa tahadhari usiende mvua ikinyesha sasa Rangitatu nyingine ya Mbagala iko wapi! Kila mara zingatia simama, soma, tafakari kisha chukua hatua.
 
Imekuwa too much mkuu,, maeneo mengi Tanzania hii ikinyesha mvua ni kisanga.

Na sehemu nyingi zenye masoko, mvua ikiwepo panazidi kuchafuka.
Ushawahi fika TMK sterio pakinyesha? Heeee kama unanata unaweza ishia nje.
Mabibo soko la ndizi?
 
Hata Buguruni sokoni ni pachafu sana, wamama wanapanga bidhaa zao chini tu matope na watu wananunua tu.
 
Hii sio solution bali una-complain. Wameitekeleza sababu wananchi hawana cha kusema wala cha kushauri, wamekaa kimya.

Sasa toa ushauri na solution nini kifanyike ili kuondoa tatizo.
Otherwise dhumuni lako la kuanzisha mada ni lipi?
Kama wewe umezoea kuoga baada ya kushauriwa utakuwa na tatizo, ni ajabu haujui wajibu wa kiajira kwa hao niliowataja.
 
Maeneo mengi zaidi ya nchi hii yako hivyo.
Kuna maeneo ukitembelea utagundua bado sisi ni maskini sana.

Na ukisikiliza mazungumzo ya watu ndio utazidi kusikitika kwa kugundua kwamba uelewa wa wananchi wengi wa mambo muhimu yanayowahusu ni mdogo sana.
 
Ukiondoa Kariakoo, Mbagala ni eneo la pili mkoani Dar es Salaam kwa kuwa na idadi kubwa ya watu/wafanyabiashara, pili hapo Mbagala katikati fremu ya biashara kama huna milioni 3, million 2 na au milion 1 hupati.

Pana mzunguko mkubwa sana wa biashara na Manispaa ya Temeke tunaona inajenga flats za biashara hapo Zakhem ambazo japo sijui kama zitatosha; zitawachukua wafanyabiashara wote walioko barabarani. Hosptali ya Zakhem inapanuliwa kwa kujengwa kwa ghorofa nyingi zaidi.

Tunatarajia pia, kulivunja soko kubwa la Mbagala ili kulijenga kwa mtindo wa ghorofa kama Zakhem ili kuweza kuwachukua wafanyabiashara maelfu walioko katika maeneo yasiyo rasmi.

Mbagala inatarajiwa kujengwa kwa mfumo wa kisasa na bajeti imeanza na Chamanzi ambapo tunataka uwe SATELLITE CITY ya kulisha southern coridal(Ushoroba wa kusini) yaani Mtwara, Lindi, n.k tayari bajeti ipo tayari. Itajengwa hosptali kubwa kabisa hapo eneo la Muhimbili ukiwa unaianza Kata ya Chamazi ukitokea kipande cha Majimatitu.

Kwa yeyote mwenye eneo Mbagala asilichezee kwani masterplan yake inafanyiwa review na patajengeka kwa haraka na kupendeza zaidi.

Ujenzi wa barabara za Mwendokasi unakamilika na kuanza kutumika mwezi wa tatu mwakani nadhani wote tunaona ubora wa Barabara ile na flyover ya Uhasibu pale.

Pia stand kubwa ya mwendokasi mkoani Dar es Salaam ni ile iliyoko Mbagala inaanza kutumika mwakani na ishakamilika tayari wote tunaona.

Barabara ya Mbagala-Mbande-Kisewe-Chanika itapanuliwa na kuwa njia nne pia kuna Barabara nyingine inaitwa CHALINZE EXPRESS inatokea Kibada inakatiza pale Kokoto inapitia ndani katikati ya Kata za Mianzini, Chamazi mpaka Chanika kwenda Chalinze itakuwa ya malori kutokea bandari. Itajengwa kwa njia nne.

Mbagala kwasasa ni mji wenye watu wengi pengine kuliko maeneo yote ndani ya mkoa wa Dar es Salaam. Kwa mfanyabiashara yeyote lazima apatolee jicho kwani fursa ni kubwa sana.

Swala la uchafu ni changamoto ya master plan maana idadi ya watu ni kubwa sana kuliko uwezo wa eneo, Serikali imeliona hili na wataalam wapo kazini kuliweka sawa.

Muda si mrefu inakuwa Wilaya mpya ambapo tunaangalia Makao makuu yake yawe Chamazi UVIKIUTA au Pale eneo la Muhimbili au tukichukue kipande cha Vikindu kiingizwe Mbagala na Makao makuu yawe Mwandege hilo eneo kubwa opposite na shule ya St. Matthew.

Badae patazaliwa Mkoa mpya utakao jumlisha Mbagala, Kigamboni, na Mkuranga ili kurahisha Huduma za jamii kwa wananchi wa eneo hilo.

Wakazi wasiuze maeneo yao kwani kwa mujibu wa waziri husika, wawekezaji wakija itabidi mtu atoe ardhi na mwekezaji atoe hela hivyo Kuleta manufaa kwa wote na kwa vizazi vijavyo.

Mbunge wa eneo hili ambaye pia nimwenyekiti wa Kamati ya serikali za mitaa Tanzania Mhe. Chaurembo anajitahidi sana kuhakikisha Barbara za ndani zinarekebishwa kwa kiwango cha lami/zege nadhani wakati mmeona barabara za Kirungule, Kiburugwa, Kijichi, Charambe na sasa Mianzini zinavyoboreshwa.

Barabara mpya na ya kisasa kutokea Njia panda ya Nzasa kuelekea kwa MPA..NGE-Bi kibonge itarahisha Huduma ya usafiri maana imebakiza kisehemu kidogo tu pale kwa mp..nge darajani.

Mbagala mpya kwa Maendeleo mapya kwa wakazi na Watanzania kwa ujumla! KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
 
Back
Top Bottom