Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
Eneo la Mbagala lililomo kwenye wilaya ya Temeke ni eneo chafu sana sana, ili uweze kuelewa ninachokisema kabla haujanipinga ni vizuri utembelee eneo la Rangitatu nina uhakika hata hizo Rangitatu hautaziona kutokana na uchafu ulioko huko.
Mbagala ina barabara kuu ya Kilwa japo kote inaonekana safi ila ukifika Mbagala inatoweka kwa uchafu na unaiona tena ukiivuka Rangitatu! Mitaa yote ya Rangitatu ambalo ndilo eneo la biashara ni michafu na yenye vumbi na mashimo na ndiyo inayozalisha kura za ushindi wa ubunge kwa CCM huku wanyamwezi ardhi kama hiyo wanazalisha viazi vitamu.
Rangitatu kuna maduka yanauza nafaka ambazo humwagika na zikilowa huchacha na kusababisha harufu kali na joto linalotokana na pumba za mahindi zilizolowa, Mbagala ni chafu na inachangiwa zaidi na Serikali kuruhusu wamachinga kujazana barabarani wakifanya biashara na kukojoa hovyo kwani hakuna vyoo vya jiji licha ya jiji kukusanya kodi ya maendeleo na kutofanya usafi!
Tahadhari, usije Mbagala wakati wa mvua.
Mbagala ina barabara kuu ya Kilwa japo kote inaonekana safi ila ukifika Mbagala inatoweka kwa uchafu na unaiona tena ukiivuka Rangitatu! Mitaa yote ya Rangitatu ambalo ndilo eneo la biashara ni michafu na yenye vumbi na mashimo na ndiyo inayozalisha kura za ushindi wa ubunge kwa CCM huku wanyamwezi ardhi kama hiyo wanazalisha viazi vitamu.
Rangitatu kuna maduka yanauza nafaka ambazo humwagika na zikilowa huchacha na kusababisha harufu kali na joto linalotokana na pumba za mahindi zilizolowa, Mbagala ni chafu na inachangiwa zaidi na Serikali kuruhusu wamachinga kujazana barabarani wakifanya biashara na kukojoa hovyo kwani hakuna vyoo vya jiji licha ya jiji kukusanya kodi ya maendeleo na kutofanya usafi!
Tahadhari, usije Mbagala wakati wa mvua.