Mbeya: Msanii wa Nyimbo za Injili, Sifa Bujune ashikiliwa kwa tuhuma za kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi

Mbeya: Msanii wa Nyimbo za Injili, Sifa Bujune ashikiliwa kwa tuhuma za kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
MWIMBAJI_WA_NYIMBO_ZA_INJILI_ATUHUMIWA_KUIMBA_WIMBO_WENYE_MAUDHUI.jpg

Mwimbaji huyo Sifa Boniventure Bujune (25) ni Mkazi wa Isyesye anatuhumiwa kuimba wimbo unaojulikana kwa jina la “Tanzania Inaelekea Wapi?” wenye maudhui ya uchochezi na kisha kuurusha katika Mitandao ya Kijamii pamoja na YouTube.

Kamanda wa Polisi Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema Mtuhumiwa alikamatwa Septemba 13, 2023 huko Isyesye Jijini Mbeya baada ya kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuusambaza kupitia mitandao ya kijamii pamoja na mtandao wa kurusha maudhui wa YouTube.

Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Huu ndo wimbo anatuhumiwa nao

Pia, soma:
- Mbeya: Mwimbaji wa Wimbo wa "Mnatuona Nyani" afikishwa Mahakamani, asomewa mashtaka

Utata: Msanii Roma Mkatoliki na wenzake wakamatwa/tekwa nyara
 
Hao ni vijana wa Mbarikiwa Mwakipesile na huwa tunamshauri sana aache kushindana na dola na kama anainba kuisema serikali aimbe na kusema yeye kama yeye na asihusishe kanisa na Ukristo kwenye mambo yake. Yule ana shida kidogo kwa. Suala lake binafsi liniiuma sana kwani nilikuwa nampenda na kupenda zile tenzi wanazoimba.

Sasa amejiingiza kushambulia serikali bila sababu akisema wamemuulia mwanaye tena Mkurugenzi wa usalama wa Taifa ndio kafanya hivyo. Jamaa hashauriki, vijana wake hao waliokamatwa hawashauriki wao wanatokana na kujiona wajuaji kama genta alivyo. Kiburi, kutojinyenyekesha, ujuaji mara nyingi huenda kwenye anguko.

Sasa kumezuka wimbi kubwa la watumishi wanaosimama na kuoneshana umwamba na serikali. Hakuna duniani mtumishi wa Mungu aliwahi ishinde dola nasi wajibu wetu ni kushauri na kuiombea mamlaka na siyo kushindana nayo.

Mimi ni kiongozi wa Kanisa na ni miongoni mwa wajumbe CPCT Taifa, kama wapentecoste tulishauri na kutoa maoni yetu kwa Mamlaka kuhusu Bandari kwani nasi tunaaminiwa na watu hatuwezi mshutumu mfalme mbele za watu.


Tulikumbushia kwa Spika wakati wa mkutano wetu mkuu pale CBC Miuji Dodoma kuhusu maoni yetu na msimamo wetu ki sio kushindana wala kupinga hadharani.
 
Hao ni vijana wa Mbarikiwa Mwakipesile na huwa tunamshauri sana aache kushindana na dola na kama anainba kuisema serikali aimbe na kusema yeye...
Unasoma BIBLIA Gani?

Nenda kasome mkasa wa Nabii Elia vs Mfalme Ahabu dhidi ya Yezebeli na Yehu utajua nini anafanya Mbarikiwa.( 1 Wafalme 1, 2, 3, 4Hadi mwisho wa kitabu utaona.

Kila mtumishi ameumbwa na kupewa utumishi Kwa nafasi yake.

Usijihesabie HAKI.
 
Kamanda wa Polisi Mbeya, Benjami Kuzaga amesema Mtuhumiwa alikamatwa Septemba 13, 2023 huko Isyesye Jijini Mbeya baada ya kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi dhidi ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuusambaza kupitia mitandao ya kijamii pamoja na mtandao wa kurusha maudhui wa Youtube. Mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa kwa hatua zaidi za kisheria.
Watu wamechoka
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mwimbaji wa nyimbo za injili SIFA BONIVENTURE BUJUNE [25] Mkazi wa Isyesye Jijini Mbeya kwa tuhuma za kuimba wimbo wenye maudhui ya uchochezi na kuurusha kwenye mitandao ya kijamii...
Mwambie basi huyo Kamanda atuwekee huo wimbo ili na sisi tuusikilize na kuupima kama kweli una viashiria vya huo uchochezi. Hatutaki maneno mengi.
 
Unasoma BIBLIA Gani?

Nenda kasome mkasa wa Nabii Elia vs Mfalme Ahabu dhidi ya Yezebeli na Yehu utajua nini anafanya Mbarikiwa.( 1 Wafalme 1,2,3,4.......... )Hadi mwisho wa kitabu utaona...
Acha nawe kupotosha. Kuna sehemu Eliya alimtukana Ahabu? Kuna sehemu Eliya alimshutumu Ahabu? Mnampotosha na yule kuanguka hashauriwi namfahamu nawafahamu wale vija wake na mkewe na wala sijihesabii haki na mwache kumpampu ujinga.

Kuna sehemu Eliya alimshinda ahabu? Akina Petro, Yakobo na Paulo waliuliwa na Dola. Yesu aliuliwa na Dola. Hakuna mtumishi wa Mungu aliyewahi ishinde dola narudia na afanyavyo ni watu wasio na akili pekee ndio wanamuunga mkono. Akina Eliya walienda kuonya na sio kutukana. Wacha maneno yako haya.

Kama CPCT tulishatuma mtu kumuonya, kumshauri na kumueleza aache haya. Anajibu hovyo na kiburi. Kiburi kile sio cha Kimungu hata usemaji na sasa mnajifichia kuhukumu nankujihesabia haki.

Kwake namhukumu na najihesabia haki. Mi nakaa na kutumika Mbeya, tumemuita na kuongea, hasikii wala haambiliki yule.
 
Back
Top Bottom