Pre GE2025 Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hiyo picha ni mali yake ana haki ya kuifanya atakavyo

Bendera za Israel na Marekani kila mara zinachomwa moto ndio sembuse chura kiziwi.

Yupo mwamba mpaka nakala za Qurani kapiga moto ni mali yake huwezi kumpangia.

Wanajitahidi kwa kila jinsi ... lakini huweza kuwalazimisha watu wampende Mtu.

Yaani, unaweza kumlazimisha punda kwenye mtoni, lakini huwezi kumlazimisha anywe maji.
 
Hiyo picha ni mali yake ana haki ya kuifanya atakavyo

Bendera za Israel na Marekani kila mara zinachomwa moto ndio sembuse chura kiziwi.

Yupo mwamba mpaka nakala za Qurani kapiga moto ni mali yake huwezi kumpangia.
Mkuu Matola,

Kuchoma picha ya mtu maana yake nini?

Viongozi ni watu kama sisi tu.
Tuwakosoa na kuwapinga kwa hoja, siyo matendo yasiyo na staha.

Mwananchi yeyote ana haki ya kumkosoa ama kumpinga Raisi Samia, lakini bado huyo ni Mkuu wa nchi na ni mama.

Kumuita majina kama chura kiziwi ni utovu wa nidhamu usiokuwa na tija yeyote kwa taifa hili.

Matola wewe ni msomi wa Phd, pamoja na uhuru unaoletwa na mfumo wa vyama vingi, tunatarajia busara zaidi kutoka kwa watu kama nyie.
 
Yeye si ndo alijiita ye Chura Kiziwi
 
Wilayani Rungwe ambae inadaiwa amemkashifu Rais Samia na Kuichoma Picha yake.
Adhabu hiyo, isiishie hapo....iende moja kwa moja kwa viongozi wote wa Mikoa na wilaya ambao wameweka picha za Mama kwenye mabango Hata stika lakini picha hizo zimeishachakaa...na nyingine zimechanika ama kutobolewa...! Yaani Mkuu huyo, wa Mkoa apambane kweli kweli kuhakikisha hili linafanyika maana kero nyingine za wananchi watashughulikia viongozi wengine.
 
Hio picha Samia ndio alinunua ? Haya ni matumizi mabaya ya rasilimali muda na Kodi zetu..., Na huyu dogo amepoteza hata hio njiti ya kiberiti angeifanyia jambo la maana
 
Jana tulikuwa tunaongea na Wakili Peter Madeleka kuwa Wakuu wa Wilaya na Mikoa hawana haki ya kuamrisha hizi kamatakamata za Polisi.

Na hizi habari za Lese Majeste (sheria za kuadhibu watu wanaomvunjia heshima mtawala) zimepitwa na wakati. Ukimkataza mtu asiichome picha ya Samia kama sehemu ya freedom of speech, unamualika amchome moto Samia mwenyewe.
 
Alijiita yeye kumbe?

Kama ni hivyo, sawa.
Unaona madhara ya kudandia kitu bila kuelewa?

Fuatilia mabandiko yangu kuhusu huyu mama aliporithi Urais kutoka kwa Magufuli tulimpa full support matokeo yake amechange gia angani ameungana na wahuni kuwafukarisha Watanzania.

Ni big dissapontment and betray.
 
Yeah, tumpinge kwa hoja. Kuchoma picha ni vitendo vya kihuni, na ninaamini mkuu huwa hauungi mkono uhuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…