Vikwazo vya meli zake za mafuta hujaviona au ?Zinafanyaje magendo wakati Urusi haijawekewa vikwazo vya mafuta?
Wafuasi wa CCM mna matatizo.
Propaganda kazini.Hawajasomea urusi, na mtoto mmoja alikuwa kaolewa na muholanzi na ndoa ilivunjika kutokana na kutaka mume aende akaishi Russia akakataaa.
Vita hii inetumia akili Sana,Naweka miguu apa umeiandika Kwa uhalisia kabisaa ata Ile hotuba ya kwanza alisema anaenda kulinda maeneo ya RUSSIAN SPEAKER na siyo kuichukua Ukrein alijua akienda maeneo ya eastern tu watanyukana sana Ila kutengeneza conyoy ya nguvu
Soma uelewe,Na ule msafara mrefu wa vifaru kuelekea kyiv huku wakiwaambia wanajeshi wa Ukraine wamtoe Rais wao wenyewe na wajisalimishe ilikuwa ndani ya mpango?
Umeenda nje ya mada chiefPutin aliingiza Urusi mfumo wa kibepari na yeye na magenerali wa Jeshi na vigogo wa Serikali,mahakama na bunge na ndugu zao wakawa na utajiri wa kufa mtu ambao waliuficha nchi za Magharibi watoto wao ba ndugu zao wakiwa wanasoma au kuishi Ulaya na Marekani na wao wakienda kutumbua maisha Ulaya na Marekani wanakomiliki mali na pesa ns mi akaunti yao ya benki na hisa misoko ya Ulaya na Marekani ikisoma ma trilioni ya dola!!
Ulaya na Marekani wanewapiga pini viongozi wa Serikali wote wa Russia,Wabunge wote wa Russia ,viongozi wote wa mahakama wa Russia na wafanyabiashara wote wa Russia ma Raia wote wa Russia mali zao na akaunti zote waliweka benki za Ulaya na nchi za Magharibi
zimekuwa frozen hata awe na ATM card haifanyi kazi
Putin muda wowote atauawa au kupinduliwa ns hao wenye pesa na mali ambazo ziko frozen
Ambao weekend walikuwa wanaenda kula bata london,new York na visiwa vya maraha ulaya na Marekani
Juz juz,Siyo rahis mkuu Urusi ni hatari sana huwa ina mbinu za kushangaza
Nakazia,Angekuwa analia pesa yake isingekuwa imara muda woote
Jamaa kageuka mchekeshaji Kama Raisi yule wa yukreini[emoji16]Unabonyeza ngapi kupata ichi kichekesho
Huko donbass mkuu wa vikosi vyote keshakabidhiwa kadyrov.Vita sio ya kuishabikia lakini kitakacho kwenda kutokea Donbas ndio litakuwa anguko la Bwana Vladmir, huyu Zelensky anatumia mbinu ya kujifanya yupo weak na kulia lia ili kumdanganya Mrusi amu underestimate ila moto utakaowaka hapo basi ndio utakuwa mwanzo na mwisho wa enzi za rafiki yake Medved.
Benedict ni papa?punguza ujuajiYote Tisa kumi,
Nmependa mbinu ya Russia ya encycling,
Yaan wanashambulia kwa kutengeneza kiduara kumzunguka adui pande zote.
Inashambuliwa unazidiwa unataka KUOMBA msaada wa silaha,maji Wala chakula huupati maana Haina pa kupitia.
Unaishia kuchimba handaki na kujificha humo, ukisubiri upige kwa kuvizia.
Walivyo wajanja,
nao hawakufati kwenye handaki lako,wanakusubiri TU hapo nje utoke ujisalimishe mwenyewe au ugome kutoka humo ujifie kwa njaa,kiu au majeraha.
Hii mbinu ya chechens imewatesa Sana Ukraine uko mariupol mpaka kiongozi wa vikosi vya Ukraine Jana ameomba msaada kwa Dunia nzima Hadi kwa Papa Benedict wa Vatican.
Sasa sijui ndo kachanganyikiwa au vipi?
Maana mpaka sahv Nmeshindwa kuelewa alikua anataka msaada gani kutoka kwa Papa uko Vatican
Alitaka Msaada wa Silaha, maombi ya uzima au Misa ya mazishi kutoka kwa Papa benedict[emoji16]
Dalili za kachanganyikiwa [emoji4]Zinafanyaje magendo wakati Urusi haijawekewa vikwazo vya mafuta?
Wafuasi wa CCM mna matatizo.
Muulize Basi uyo kamanda wa ukriane aliemtaja kwenye mwenyewe, Mimi huo ubenedict haunihusu[emoji4]Benedict ni papa?punguza ujuaji
Dah wanatolewa kafaraHao wanaenda kutolewa kafara
Astaghfirullah arbaa mallahDah wanatolewa kafara
SawaHuo ni uongo wa wazi kabisa, Russia nia yake ilikuwa ni kulitwaa Ukraine yote, kumpindua rais Zelenskyy na kupachika kibaraka wake Kyiv.
Lakini baada ya hilo kushindikana kivita ndio ile hadithi ya sizitaki mbichi hizi ikaanza ya kwamba sasa wanataka eneo la Donbas.
Watu mko humu tu lakini hamjaelewa nia kamili ya Putin ni nini. Putin amesema mara nyingi kwamba kuporomoka kwa himaya ya USSR ilikuwa ni kosa la karne ambalo halikupaswa kuruhusiwa kutokea.
Pia amekuwa akisisitiza wazi kabisa kwamba kihalali Nato inapaswa warudi pale walipokuwa kabla ya 1997 ambapo walikuwa na wanachama 16 tu na wale 14 waliongezeka baada ya hapo inafaa wasiwemo kwenye jumuiya hiyo.
Hivyo ni kwamba nia ya Putin ni kurejesha USSR kinamna na atashindwa tu kwa sababu hawezi kuishinda Nato ktk medani ya kivita.
Ngoja nikulekebishe Urussi ilikuwa na Marengo na Ukraini kuzichukua Ukrain nzima kama ulikuwa una fatilia hoja za Moscow mwanzon mwa vita dinazifican na disarmy Ukrain option mbili zimeshindikan ndo wamebaki na kuigawa Ukrain.Urusi kiukweli wameonesha umahiri wa kutumia mbinu za enzi ya kina hitla na dola la kirumi katika uvamimizi.Kabla sijaelezea mbinu hizo naomba ufahamu kuwa Urusi haikua na malengo ya kuivamia Ukraine yote,bali ililenga maeneo ya eastern part yaliyopakana na mipaka yake ,lengo ikiwa ni kuyasaidia majimbo yaliyikua yanataka kujitenga na Ukraine ,kumbuka mipango iliandaliwa tangu 2010,na propaganda nyingi ziliundwa na mrusi ili kuchochea majimbo hayo kujitenga.sitaki kwenda deep mnaelewa hizo siasa za mrusi.
Sasa nije kwenye mbinu ya kuhakikisha wanyakwapua majimbo hayo,maana walielewa fika wakienda kichwakichwa wangeumbuka mno.
Kwanza kabisa walijigawa makundi matatu ,ambapo kundi la kwanza lilitangulia upande wa mji mkuu Kiev kama vile wanataka kuingia mjini,ila walikua wanazuga tuu ili kuvuruga mipango ya jeshi la Ukraine ,na kweli lilivurugika kweli maana Ukraine ilijikita kutumia nguvu nyingi kuzuia jeshi la Russian kuingia mji mkuu Kiev, huku wakisahau kuna kundi lilikua linazunguka Eastern na kujiimarisha huko
Kundi la pili lilijikita kama linataka kutokea upande wa kaskazin kupitia Belarus ila nao ilikua zuga tuu.
Kundi la tatu ndilo la kifo lilijikita majimbo ya mashariki likiwa na shehena ya silaha nyingi na kujiimarisha huko ,huku wenzao wakiendelea kuzuga ,mbinu hii inaitwa cover the main target
Wakati mataifa ya ulaya na dunia wakimzomea puttin kwamba kashindwa kutimiza lengo lake la kuingia Kiev ,yeye aliendelea kujiimarisha zaidi
Baada ya kuhakikisha ameshajiimarisha vikosi hivyo vilirudi kwenda kuungana na wenzao huko mashariki.
Nataka niwaambie tuu majimbo yote ya mashariki kamwe Ukraine hawezi tena kuyakomboa ,hata wazungu wamepigwa na butwaaa kuchezewa akili na Putin
Ila kwa hitimisho sijapenda mbinu hii maana inagharama sana ,maisha ya RAIA wasio na hatia, uharibifu mkubwa wa miundombinu ,pia hata hasara kwa jeshi la urusi maana wengi wanaotumwaga kufanya coverage huwa ni askari wasio weled na mara nyingi hawapewi zana za kisasa, hivyo wengi hupoteza maisha ili kumpa moyo anayevamiwa akidhani anapata ushindi kumbe anaelekea shimon.
Wengi mkisikia mrusi ni mbabe wa vita huwa mnaona ni neno dogo ila Mrusi ni hatari sana ana mbinu za kushangaza na ambazo adui hawezi fikiria.
Anadanganya huko Ukrain mochwari zime jaa maiti za hao jamaaaVipi kuhusu askari 1300 walofarik ambao putin amekiri ktk speech yake kuwa amewapoteza? Watu wanajitoa ufahamu humu ila uhalisia unabaki palepale, resistance alokutana nayo mrusi mpaka sasa bado haamini.