Mbivu na Mbichi za kuzalishwa ukiwa bado ni Mwanafunzi wa Chuo

Mbivu na Mbichi za kuzalishwa ukiwa bado ni Mwanafunzi wa Chuo

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
3,925
Reaction score
8,853
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wanafunzi wengi kuanzia kidato cha tano na Sita wanadhani Maisha ya Chuo ni ya Starehe sana bila kujua undani wake.

Baadhi ya wanafunzi huenda Chuo wakiwa na matumaini makubwa sana ya kutimiza ndoto zao.

Lakini Ndoto hizo hukwamishwa na vitu vingi hasa kwa wale wenye tamaa na pupa.

Kwa kuanza na watoto wa kike ambao huwaona dada zao wamemaliza Chuo na kurudi nyumbani na watoto hutamani na wao wafanye hivyo bila kujua madhara yake.

Mara nyingi wanapoanza Mwaka wa Kwanza huwa ni wanafunzi wapole na watiifu.

Lakini baada ya Muda kidogo makundi hujigawa na kuanza kuonyesha tabia zao halisi.

Mara mtoto wa kike anajikuta amenasa mimba kutoka kwa mtu asiyemtarajia, anaishi na mimba kwa kumficha mzazi wake hadi anajifungua.

Changamoto katika hilo huanza pale atakapokosa matunzo kutoka kwa mhusika aliyekutana nae Chuo.

Kiwango cha masomo kinashuka, maisha huanza kuwa magumu na badala ya kuzingatia masomo na kutafuta fursa za ajira unazingatia malezi malezi zaidi.

Wazazi wanashindwa kupata kile walichokitarajia kutoka kwa mtoto wao kutokana hizo changamoto anazokumbana nazo.

Mnachopaswa kukifahamu watoto wa Chuo hao watu mnaokutana nao Chuo tayari walishadanganya wanafunzi wengi waliopita hapo.

Mnapaswa kukumbuka kuwa nyie sio wa kwanza. Umakini unapaswa kuchukuliwa mapema zaidi.

Maisha ya Chuo ni kusoma na kutafuta Fursa na sio kulea watoto.

Ingawa kuna wachache waliofanikiwa baada ya kupambana sana.
 
Hawa waliotoka bush na kuketwa mjina na chuo, bila chuo mji wangeliusikia tu. Hawa ndo wanadanganywa kirahisi na kujaa maana kila kitu kwao ni kipya.

Kama sio kuzaa basi wanafanya abortion hawa watoto.
 
Haya yalimkuta mdogo wangu fulani ,alafu mama yake alijua akawaficha ndugu zake Ila akatengeneza mazingira kuwa binti katolewa mahari ,Sasa kamaliza chuo hawataki aende mkoani kwao wanafosi aende kwa watu wengine .
Sasa watamficha hadi lini Jamani? Ila ni aibu sana
 
Hawa waliotoka bush na kuketwa mjina na chuo, bila chuo mji wangeliusikia tu. Hawa ndo wanadanganywa kirahisi na kujaa maana kila kitu kwao ni kipya.

Kama sio kuzaa basi wanafanya abortion hawa watoto.
Wanavamia Jiji kwa
Wale wale wanaoharibu wanafunzi miaka yote.
 
Sasa watamficha hadi lini Jamani? Ila ni aibu sana
Sijui wao ,walitaka eti wamlete niishi naye Mimi wakati huo hakuna matunzo yoyote watakayotoa nikajizima data nikamkataa ,yaani nilee mtu mzima na mtoto wake alafu baba yake mtoto yupo na mama yake nikaona ni utumwa.
 
Kuna wengine wanawishi kuzalishwa.. sio kama wanazalishwa kwa bahati mbaya ila tu wanataka wenyewe..
Kipindi nikiwa 4th yr nilitamani na mm nipate mtoto kwani marafiki zangu wengi walikuwa Wana mimba nawengine wamezalishwa..
Kidogo nami nilitaka kuhamasika😁
Ila nilikosa mtu WA kunitongoza...
Ila lait kama ningelipata mtu wa kunitongoza na nikamridhia huenda na mm ningezalishwa mapemaa saiv ningekuwa na watoto
N.B wale marafiki zangu waliozalishwa kipindi wapo chuo wachache wameolewa na hao hao waliowazalisha na wengine wanalea watoto wao ki mpango
wao..
 
Kuna wengine wanawishi kuzalishwa.. sio kama wanazalishwa kwa bahati mbaya ila tu wanataka wenyewe..
Kipindi nikiwa 4th yr nilitamani na mm nipate mtoto kwani marafiki zangu wengi walikuwa Wana mimba nawengine wamezalishwa..
Kidogo nami nilitaka kuhamasika😁
Ila nilikosa mtu WA kunitongoza...
Ila lait kama ningelipata mtu wa kunitongoza na nikamridhia huenda na mm ningezalishwa mapemaa saiv ningekuwa na watoto
N.B wale marafiki zangu waliozalishwa kipindi wapo chuo wachache wameolewa na hao hao waliowazalisha na wengine wanalea watoto wao ki mpango
wao..
Wewe umeolewa?

Nataka nikusaidie kutimiza ndoto yako just in case
 
Sijui wao ,walitaka eti wamlete niishi naye Mimi wakati huo hakuna matunzo yoyote watakayotoa nikajizima data nikamkataa ,yaani nilee mtu mzima na mtoto wake alafu baba yake mtoto yupo na mama yake nikaona ni utumwa.
😅😅😅mtoto aende kwa bibi ake umchukue ndugu yako
 
Kuna wengine wanawishi kuzalishwa.. sio kama wanazalishwa kwa bahati mbaya ila tu wanataka wenyewe..
Kipindi nikiwa 4th yr nilitamani na mm nipate mtoto kwani marafiki zangu wengi walikuwa Wana mimba nawengine wamezalishwa..
Kidogo nami nilitaka kuhamasika😁
Ila nilikosa mtu WA kunitongoza...
Ila lait kama ningelipata mtu wa kunitongoza na nikamridhia huenda na mm ningezalishwa mapemaa saiv ningekuwa na watoto
N.B wale marafiki zangu waliozalishwa kipindi wapo chuo wachache wameolewa na hao hao waliowazalisha na wengine wanalea watoto wao ki mpango
wao..
😅😅😅 Bora hukuhamasika ila huwa inavutia sana
 
Back
Top Bottom