SI KWELI Mboga za majani aina ya Chainizi husababisha upungufu wa Nguvu za kiume

SI KWELI Mboga za majani aina ya Chainizi husababisha upungufu wa Nguvu za kiume

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kumekuwa na Madai ya kwamba matumizi ya mboga za majani aina ya chainizi yamekua na madhara katika ufanisi wa tendo la ndoa kwa wanaume. Kuna ukweli gani katika hilo suala?

maxresdefault.jpg

Naomba nijibiwe kitaalam niweze kuelewa.
 
Tunachokijua
Chainizi hupatikana kwenye familia kubwa ya mboga za majani inayofahamika kwa jina la Brassica. Mfano wa mboga zingine zilizopo kwenye familia hii ni Kabichi (Cabbage) na Brokoli (Broccoli).

Asili ya Mboga hii ni nchi ya China ilikoanza kutumika Zaidi ya miaka 1500 iliyopita.

Bara la Amerika ya Kaskazini limeanza kulima mboga hii kwa zaidi ya miaka 100. Taarifa nyingi za kiuchunguzi na tafiti zinaonesha kuwa mboga hii kwa sasa imesambaa sehemu nyingi duniani, Tanzania ikiwemo.

Viambato na Kemikali zake
Kwa mujibu wa USDA, Mboga hii huwa na nishati, maji, protini, wanga, nyuzilishe, madini chuma, calcium, magnesium, phosphorus, selenium, potassium, sodium, zinc, copper na manganese.

Ni chanzo kizuri cha folate, vitamini C, viondoa sumu vya beta carotene pamoja na vitamin E.

Faida zake kiafya
Mjumuisho wa virutubisho vinavyopatikana kwenye Chainizi huwa na faida kubwa kwa afya ya binadamu. Kwa ujumla wake, mboga hii hufanya mambo yafuatayo-
  • Kutoa kinga dhidi ya aina mbalimbali za Saratani hasa ile ya utumbo mpana
  • Huzuia uvimbe (Inflammation)
  • Hupunguza nafasi ya kuugua magonjwa ya mfumo wa damu na moyo
  • Huimarisha afya ya mifupa
  • Huboresha afya ya macho
  • Huongeza uwezo wa kinga za mwili katika kupambana na magonjwa
  • Ni nzuri kwa afya mama mjamzito katika kuongeza damu na kumkinga mtoto asipatwe na changamoto za kimaumbile, hasa tatizo la kuzaliwa na mgongo wazi
Uhusiano wake na kupunguza nguvu za kiume
JamiiForums imefuatilia hoja hii kwa kuzungumza na wataalamu wa lishe na kugundua kuwa haina ukweli.

Chainizi haina kemikali sumu zinazoathiri ufanisi wa mwanamme kwenye kushiriki tendo la ndoa, pia hakuna tafiti za kiafya zinazoelezea madhara haya kwa binadamu.

Kwa kuwa msingi wa hoja za kisayansi hasa upande wa tiba huboreshwa, kupingwa na kuthibitishwa kwa tafiti, madai yanayohusisha mboga hii na upungufu wa nguvu za kiume hayabaki kuwa uzushi.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Afya ya Marekani (NHI), upungufu wa nguvu za kiume husababishwa na uwepo wa magonjwa sugu mwilini Pamoja na changamoto zingine zinazohusisha saikolijia, mfumo wa kati wa fahamu, homoni za mwili, mtindo wa Maisha Pamoja na matumizi ya baadhi ya dawa.
Pumbafu zao watu wanakula chainizi kwa karibia karne nzima na wanapiga shoo kama kawaida, sema tu wanaume wengi wa Dar, wamwevurugwa nguvu hamna hivyo kila kitu wanaona ndio kimesababisha ulegelege wao.
 
Ni kweli inapunguza nguvu mm ni shuhuda
Mkuu, kwanza pole kwa kupungukiwa nguvu. Nakuombea kwa Mungu azirejeshe maana ndio uanaume wenyewe.

Naomba unipe shule kidogo, umetumia njia gani kufikia hitimisho hili? Pia, zinasababishaje upungufu huo?
 
Nguvu zinapungua kwa asilimia kubwa kwa Magonjwa(pressure, kisukari etc). Ingekuwa zinapungua kwa virutubisho basi wasio na vipato wala mlo mmoja wa ugali chukuchuku wangekuwa hawasimamishi kabisa.
 
Labda unasema kinyume, mimi nazichapa sana na nguvu zinaongezeka, ni kama mkuyati kwangu.
 
Habarini za majukumu wana jamvi wote wa Jamii intelligence page.

Tangu miaka ya zamani kumekuwa na uvumi au hoja mbalimbali kuhusiana na mboga majani chainizi, watu wengi wanasema mboga hii inahusishwa na kuchangia au kuongeza tatizo la upungufu wa nguvu za kijinsia hasa kwa wanaume. Je kuna ukweli wowote kuhusu hoja hizi?

Nawasilisha.
 
Sisi hayo majani tunayaita Mavunja Ndoa sitaki kuamini kuwa hilo jina lilikuja ghafla tu.
 
Nguvu zinapungua kwa asilimia kubwa kwa Magonjwa(pressure, kisukari etc). Ingekuwa zinapungua kwa virutubisho basi wasio na vipato wala mlo mmoja wa ugali chukuchuku wangekuwa hawasimamishi kabisa.
Kuna kula, kushiba na kupata virutubisho.

Hivyo vitasema afya ya mwili iweje
 
Nime notice kitu kutoka huko uraiani ni zaidi ya mara kumi nimeona wanaume wakiikataa mboga ya majani ya chainizi migahawani na hata mahotelini..

Watu kibao utasikia aaa chainizi toa situmiagi kabisa wakati Mimi nazitandikaga tu. Sasa wazee kwani zina shida gani hizi?

Usikute najimaliza bila kujua maana mimi huwa nazifakamiaga balaa
 
Back
Top Bottom