Mbona kama Dualis zinaanza kushuka?

Kwenye umeme sawa nimekuelewa, vipi na kuhusu hiyo gear box ambayo wadau wanasema ni kimeo?
Suala la gear box mkuu siwezi kulisemea sana kwa sababu mimi binafsi sijawahi kukutana Na Dualis yenye shida ya Gear box...
Isipokuwa kuna baadhi ya model flani ya gari inaweza ikatoka kiwandani ikiwa na tatizo lake common, mfano hear box..

Ila watumiaji wakiwasilisha malalamiko, mtengenwzaji anaboresha kwenye model inayofuata
 

Kwa maelezo yako, hata harrier, prado 120, Nissan Y61 etc zinakuja zimepasuka dashboard ni gari mbovu zote 😁😁

Ukipasua reserve tank basi gari yako ina-over heat, utakua unakaribia kukaanga engine (rekebisha tatizo kwa watalaamu, lasivyo utabadilisha reserve tank mpaka uchoke)
 
Tupo kwenye roof na reserve tank....ebu nitajie gari ambazo zinapasuka hiyo mitungi hata zikichemsha?

Maana dualis inapasuka bila hata ya kuchemsha kinaanza kuvuja.

Binafsi nilikuwa naipenda sana hii gari ila mapungufu yake ni mengi kama vile gearbox, roof, reserve tank, pia inatapia ya kula transmission fluid n.k.

Tuelimishane zaid
 
Roof issues:
Most German cars, Toyota - brevis, harrier, crown, LX 70/79 series, Hiace, coaster etc

Mtungi kuvuja - most German cars, other brands sijakutana nazo (sababu kubwa ni kutumia maji badala ya recommended coolant)
 
🤣🤣 utaskia hizi gari zilikosewa sana gia box
 
Wewe jamaa inaonekana unataka gari ambalo haliharibiki kabisa.sasa hilo utalipata wapi.Hadi vitasa unalalamika.Mambo mengine ni matumizi yako yalivyo.cha msingi gari kama inamatatizo common toka kwa mtengenezaji lazima yatakua yameshatolewa taarifa sana.kwasababu hizo gari zinatumika maeneo mengi duniani.Kwahiyo tutofautishe makosa yetu watumiaji na matatizo ya gari toka kiwandani.ilo lako kama hukununua jipya unajuaje aliyekua analitumia alilitumiaje ili ufikie hitimisho kua zote ziko hivyo.
 
Iv hujiulizi kwann malalamiko ni mengi kuhusu hyo gari, mbona husikii hayo mapungufu yakizungumziwa kweny aina nyingine ya nissan, xtrail ni nyingi kuliko hyo dualis lakini mbona husikii malalamiko makubwa hvyo.

Nilinunua used kutoka japan wala sio mkononi tena marambili, nilidhani labda ni ile ndio ilikuwa na shida, ilivyoungua niliagiza tena nyingine mambo ni yale yale.

Wengi wanaoyamiliki hawasemi ukweli zaidi ya kulisifia tu. Ni kama vile watu wanavyotolewa makamasi na magar ya mzungu ila hawasemi hadi aliuze ndio utasikia kilio. Dualis kwenye body ni nzuri sana inavutia sana.
 
Hii gari inatatizo pia la kuporomoka roof na kupasuka mtungi wa coolant reserve tank, kataa na hyo pia.

Hyo gari ukiinunua inakulazimu kbadili roof vinginevyo litaporomoka, hyo nayo uongo?
Nakubaliana na wewe, upo sahihi kabisa....huyu mdau yawezekana gari yake bado haijaanza kusumbua ila ni suala la muda tu.
 
Nakubaliana na wewe, upo sahihi kabisa....huyu mdau yawezekana gari yake bado haijaanza kusumbua ila ni suala la muda tu.
Kuna wengine huwa wanapenda kutetea gari akiwa nalo hata kama linamtoa kamasi.
 
Hii gari inatatizo pia la kuporomoka roof na kupasuka mtungi wa coolant reserve tank, kataa na hyo pia.

Hyo gari ukiinunua inakulazimu kbadili roof vinginevyo litaporomoka, hyo nayo uongo?
Nikajua ni kwangu tu! Kumbe ni kwa wote!
 
TRA ndio shida. Gari ina re-sale price ya chini plus high but guaranteed maintenance cost halafu wanataka inunuliwe kwa bei utadhani ndio unaichukua ikiwa mpya, TRA hamna thinking tank vilaza ni wengi pale.
 
Dualis Zina tatizo la kuungua moto
Assumptions tu. Kuungua moto ni matokeo ya ufundi local ingekuwa ni default ya gari basi Dualis zote zingekuwa kuungua ni lazima. Ila kuna watu wanatumia zaidi ya miaka 20 na hawajakutana na hizo incidences.

So it only means kuna tabia ya kuzichokonoa na kuoveride mfumo wa umeme na matokeo yake lazima gari ipate shida na kuleta matokeo ya moto. But sio fault ya gari ni watumiaji wanaoleta ufundi juu ya technology wasioifahamu hata kidogo.
 
18 ni bei sana, bei ya mkononi kwa hapa bongo ni kuanzia 14 hadi 10 hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…