Mbowe ahusishwa na UFISADI wa kuimaliza NSSF

Mbowe ahusishwa na UFISADI wa kuimaliza NSSF

je wewe usha lipa hela unazodaiwa dukani kwa Mpemba?
Sera zenu dhaifu ndizo zinazosababisha mifuko ya hifadhi igeuke Saccos....

Aliahidi kulipa mwishoni mwa Aprili, mpaka sasa bado hajalipa.
 
Wadau, baada ya kipindi cha Maswali na Majibu, kulikuwa na miongozi ya Wabunge kwa Naibu Spika. Moja ya hoja zilizojitokeza ni madai ya Lissu kuwa Wabunge wa CCM wanachukua fedha kutoka kwenye mifuko ya jamii.

Hata hivyo, waziri Gaudensia Kabaka alisema kuwa si kweli kuwa wabunge wanaenda kuchukua fedha kwenye mifuko ya kijamii na kuweka mfukoni mwao bali wanaomba fedha kwenye mifuko hiyo kwa ajili ya maendeleo kwenye majimbo yao.

Alisema kuwa ni wabunge wa CCM ndio wanaojitokeza kuomba kwa ajili ya majimbo yao jambo ambalo amesema kuwa ni jema. Anawashangaa wabunge wa upinzani kulalamika kuwa wabunge wa CCM wanaomba fedha kwenye mifuko yao ilhali wao hakuna anayewazuia kuomba.

Kibaya zaidi waziri Kabaka alisema ni pale Mbunge ambaye anajitokeza kukopa fedha kwenye mifuko hiyo na akakaa na deni kwa muda mrefu hali inayomfanya awe kwenye risk ya kukamatwa na kufunguliwa mashtaka. Alisema kuwa kuna kiongozi mmoja wa upinzani ambaye amekopa fedha nyingi NSSF na mpaka sasa anakwepa kulipa.

Katika majibu ya nyongeza, Waziri wa TAMISEMI, HAWA GHASIA alimtaja mtu huyo kuwa ni Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ambaye alitumia mamlaka yake kama KUB kukopa kiasi kikubwa cha fedha (kiwango hakikubainishwa) na mpaka sasa hajalipa na haoneshi nia ya kulipa hivyo kujiweka kwenye uwezekano mkubwa wa kukamatwa
 
Mafisadi wa ccm wanarudisha pesa wanazoiba? Kwani mbowe kakataa kulipa nssf? Hawa ghasia anajua makubaliano ya mbowe na nssf?
 
Wadau, baada ya kipindi cha Maswali na Majibu, kulikuwa na miongozi ya Wabunge kwa Naibu Spika. Moja ya hoja zilizojitokeza ni madai ya Lissu kuwa Wabunge wa CCM wanachukua fedha kutoka kwenye mifuko ya jamii. Hata hivyo, waziri Gaudensia Kabaka alisema kuwa si kweli kuwa wabunge wanaenda kuchukua fedha kwenye mifuko ya kijamii na kuweka mfukoni mwao bali wanaomba fedha kwenye mifuko hiyo kwa ajili ya maendeleo kwenye majimbo yao. Alisema kuwa ni wabunge wa CCM ndio wanaojitokeza kuomba kwa ajili ya majimbo yao jambo ambalo amesema kuwa ni jema. Anawashangaa wabunge wa upinzani kulalamika kuwa wabunge wa CCM wanaomba fedha kwenye mifuko yao ilhali wao hakuna anayewazuia kuomba.

Kibaya zaidi waziri Kabaka alisema ni pale Mbunge ambaye anajitokeza kuomba fedha kwenye mifuko hiyo na akakaa na deni kwa muda mrefu hali inayomfanya awe kwenye risk ya kukamatwa na kufunguliwa mashtaka. Alisema kuwa kuna kiongozi mmoja wa upinzani ambaye amekpa fedha nyingi NSSF na mpaka sasa anakwepa kulipa. Katika majibu ya nyongeza, Waziri wa TAMISEMI, HAWA GHASIA alimtaka mtu huyo kuwa ni Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ambaye alitumia mamlaka yake kama KUB kukopa kiasi kikubwa cha fedha (kiwango hakikubainishwa) na mpaka sasa hajalipa na haoneshi nia ya kulipa hivyo kujiweka kwenye uwezekano mkubwa wa kukamatwa

Kwa kuongezea tu, Kabaka amesema NSSF tayari wana "Arrest Warrant" kwa huyo mkopaji. Nijuavyo hii hotolewa na mahakama baada ya mkopaji kushindwa kesi na kushindwa kulipa.
 
Embu wataje kiasi kama ni kweli..bongo kuna utoto mwingi na excuses nyingi sana zisizo na msingi..ila na huyu jamaa aliyeleta uzi namuonaga kama mapepe mno..
 
kwani kukopa kwa taratibu za kisheria ni dhambi?....
 
Kwa kuongezea tu, Kabaka amesema NSSF tayari wana "Arrest Warrant" kwa huyo mkopaji. Nijuavyo hii hotolewa na mahakama baada ya mkopaji kushindwa kesi na kushindwa kulipa.
Hakika Dada. Lissu alijifanya anaumbua ufisadi wa CCM kumbe anamkaanga kiongozi wake
 
Embu wataje kiasi kama ni kweli..bongo kuna utoto mwingi na excuses nyingi sana zisizo na msingi..ila na huyu jamaa aliyeleta uzi namuonaga kama mapepe mno..
Kiasi anajua Mbowe mwenyewe na Waziri Kabaka amesema kuwa si vema kutaja majina na kiasi kwani hayo ni masuala binafsi
 
Sheria ya NSSF imetioa 'powers of arrest without warrant' iwapo kuna mdaiwa wa muda mrefu kama Mbowe kumkamata na kufikisha mbele ya vyombo vya sheria. Hivyo Mbowe wakati wowote anaweza kukamatwa.
 
Yaani kwa Mbowe kwa kuwa KUB tu anakataa kulipa deni. Je akiwa kiongozi wa serikali?
 
Back
Top Bottom