Mbowe aligombeaje urais mwaka 2005 kama hana degree?

Mbowe aligombeaje urais mwaka 2005 kama hana degree?

Kigezo kimojawapo cha kugombea urais Tanzania ni mgombea kuwa na angalau kiwango cha elimu cha degree moja, pia huwa kuna rumours mtaana kwamba Freeman Mbowe aliishia kidato cha sita tu, sasa kama ni kweli Mbowe aliwezaje kupitishwa na tume ya uchaguzi kugombea Urais mwaka 2005??

Wanasiasa wanaogombea nafasi kuanzia udiwani, ubunge hadi Urais wanapaswa kuweka wazi CVs zao wapiga kura wawafahamu vizuri kwa manufaa ya umma. George Bush Jr. wa Marekani yeye alikuwa haoni haya kusema hadi matokeo yake ya darasani kwamba hakuwa kipanga na hadi aliwahi kutania kwamba wanafunzi wa daraja C kama yeye wanaweza kuwa marais pia.
Ibara ya ngapi ya katiba au sheria gani omesema mgombea awe na degree? Lete ushahidi wa kisheria sio wa kihisia.
 
Kuna kipindi niliwahi kusoma katiba ya nchi niliona kigezo cha elimu kwa mtu anaegombea urais lazima awe na degree.
Ibara ya ngapi? Sifa za mtu kuchaguliwq kuwa rais zimeainishwa kwenye ibara ya 39 na hakuna kigezo cha elimu
 

Attachments

  • Screenshot_20240818_210604_PDF Reader - Hi Read.jpg
    Screenshot_20240818_210604_PDF Reader - Hi Read.jpg
    190.8 KB · Views: 2
Freeman Mbowe ni Alumni wa Chuo Kikuu Mzumbe, Shahada ya Public Adminsitration inayotolewa na School ya Utawala maarafu kama (SOPAM).

Hope Wana Mzumbe wenzangu tuliopita hapo wengi wetu tulipata bahati ya kusoma na Mbowe japo kwa uchache some tutorials but alisoma na aligradaute kimya kimya..
 
Hapo kuna umuhimu wa kujua kipi kina faida kuliko kingine, unaweza kuangalia hoja ya kuweka ukoma wa mihula ya Urais pia kama mfano. Wengine watakuambia kutokuwepo kwa ukomo wa Urais ni faida kwa taifa kutomuondoa Rais mzuri, lakini hawafikirii vipi ikiwa rais ni mbovu na hakuna ukomo wa rais, huo ukomo ndio sehemu ya gharama yenyewe ya kuendeleza demokrasia. Tukirudi kwenye elimu vipi ikiwa kiongozi anaweza kushawishi watu kumchagua lakini hana uwezo mzuri wa kuchambua mambo na kufanya maamuzi yenye mashiko kutokana na ukosefu wake wa wa uelewa unaosababishwa na kukosa elimu nzuri na sahihi??
Bottom line ni kwamba elimu si degree.

Haya mataifa kama US na Uingereza hakuna kigezo cha degree kuwa rais wala Prime Minister. Up to John Major UK ilikuwa na PM ambaye hana degree. Up to Truman US ilikuwa na rais ambaye hana degree.

Ukiwa na mgombea ambaye hana degree wala uwezo ila anaweza kuwadanganya wananchi, hapo una tatizo kubwa zaidi ya mgombea ambaye hana degree. Una tatizo la wananchi wajinga.

Kabla ya kuweka viwango vya elimu kubwa kwa wagombea, elimisha jamii yako isiweze kudanganywa kirahisi.

Ukishakuwa na wananchi wengi wenye degrees tu, automatically wagombea urais wote watakuwa na degree bika ya kigezo cha degree kuwapo.

Ndivyo walivyofanya US na UK.
 
Hii dhana ya kuwa na Degree ndio kuwa na maarifa au akili ni dhana ya kishamba sana, nchi za kiafrika ndio unataka sana wako obsessives sana na mambo kama hayo.
 
Kigezo kimojawapo cha kugombea urais Tanzania ni mgombea kuwa na angalau kiwango cha elimu cha degree moja, pia huwa kuna rumours mtaana kwamba Freeman Mbowe aliishia kidato cha sita tu, sasa kama ni kweli Mbowe aliwezaje kupitishwa na tume ya uchaguzi kugombea Urais mwaka 2005??

Wanasiasa wanaogombea nafasi kuanzia udiwani, ubunge hadi Urais wanapaswa kuweka wazi CVs zao wapiga kura wawafahamu vizuri kwa manufaa ya umma. George Bush Jr. wa Marekani yeye alikuwa haoni haya kusema hadi matokeo yake ya darasani kwamba hakuwa kipanga na hadi aliwahi kutania kwamba wanafunzi wa daraja C kama yeye wanaweza kuwa marais pia.

mkuu wazungu hawapo obsessives sana na ukubwa wa elimu yako kwenye makarati, always focus yao ipo kwenye nini unaweza kufanya.
 
Elimu ni muhimu lakini kuweka kigezo cha elimu cha degree sio tu si muhimu, lakini pia ni kigezo cha kibaguzi. Hususan kwenye nchi ambayo watu wengi sana wana uwezo mzuri tu lakini hawana elimu rasmi ya degree.

Inatupasa tuelewe unaweza kuwa na elimu bila degree na unaweza kuwa na degree bila elimu.

Rais wa sasa wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva hana degree, lakini watu wamemkubali sana hawakujali hilo.

Zaidi, kitu muhimu kuliko kukosa degree, ni sababu ya kukosa degree.

Mtu kama Lula hana degree, lakini hakuwa na uwezo wa kusoma,alianza kufanya kazi akiwa mdogo, akafanya kazi sana na kupanda ngazi katika Labor Unions za Brazil, akafika juu kabisa.

Hiyo kazi aliyoifanya huko katika vyama vya wafanyakazi, ni jubwa kuliko degree.

Sasa mtu kama huyo naye utasema huyu hafai kuwa rais kwa sababu hana degree?

Elimu yake practical aliyoipata kwenye siasa za vyama vya wafanyakazi imepita kikwazo chochote cha degree yoyote mtakachoweka.

Sasa hatuoni tukiendeleza kigezo cha degree tutawanyima kina Lula wetu nafasi ya kutuongoza?

ni fikra mbovu sana ambazo hata hao waliotuletea hiyo elimu hawaizingatii.
 
Ni ulimbukeni tu.

Ukiweka hivi viwango vya elimu wenyewe waliotuletea hiyo elimu na demokrasia wanatuona malimbukeni tu.

huu ulimbukeni unazitesa sana nchi za Africa, na nashindwa kuelewa wanaolazimisha hizi ajenda wanasumbuliwa na nini ikiwa wao wanaamini kuwa na Degree ndio uwezo mzuri wa kisiasa na uongozi kwanini huwa wanakuwa unsecured kwa watu walioshindwa kuwa na degree?
 
Ni ulimbukeni tu.

Ukiweka hivi viwango vya elimu wenyewe waliotuletea hiyo elimu na demokrasia wanatuona malimbukeni tu.
Hata wao waliotuletea demokrasia hawako perfect, kuna ulimbukeni fulani wanao ambao sio afya katika kuongoza nchi(iwe demokrasia au vinginevyo). Kigezo cha elimu ni muhimu katika nchi inayoendelea hata kama sio degree. Mazingira yaliyowaharushu wao kuendelea bila elimu rasmi hayapo tena au ni finyu zaidi karne hii ya sasa.
 
huu ulimbukeni unazitesa sana nchi za Africa, na nashindwa kuelewa wanaolazimisha hizi ajenda wanasumbuliwa na nini ikiwa wao wanaamini kuwa na Degree ndio uwezo mzuri wa kisiasa na uongozi kwanini huwa wanakuwa unsecured kwa watu walioshindwa kuwa na degree?
Yani tabu sana.

Tumeondoa midahalo ya wagombea urais, ambayo inaweza kuonesha nani ana uwezo gani wa kuongelea issues muhimu na kujibimu maswali hapo kwa papo, kitu kinachoonesha wazi uele2a wa mtu, kiukweli mtihani wa taifa wa wagombea wote kwenye real issues in real time.

Halafu tunaweka kigezo cha degrees ambazo mtu yeyote anaweza kununua au kuhonga afanyiwe kazi na wengine!
 
Hata wao waliotuletea demokrasia hawako perfect, kuna ulimbukeni fulani wanao ambao sio afya katika kuongoza nchi(iwe demokrasia au vinginevyo). Kigezo cha elimu ni muhimu katika nchi inayoendelea hata kama sio degree. Mazingira yaliyowaharushu wao kuendelea bila elimu rasmi hayapo tena au ni finyu zaidi karne hii ya sasa.
Address tatizo la elimu rasmi kwa jamii nzima hilo suala la kudai degree kwa wagombea urais litatoweka automatically.

Ukiweka kigezo cha degree kwenye ugombea urais katika nchi ambayo asilimia kubwa ya watu wake hawana degree, kigezo hicho kinakuwa undemocratic na hata unconstitutional.

Acha watu wamkubali au kumkataa mtu kwa uwezo wake.

Usiweke mwanya wa watu kumtaka mtu awaongoze lakini wakashindwa kumchagua kwa sababu artificial ya degree.

Huelewi wapi?
 
Address tatizo la elimu rasmi kwa jamii nzima hilo suala la kudai degree kwa wagombea urais litatoweka automatically.

Ukiweka kigezo cha degree kwenye ugombea urais katika nchi ambayo asilimia kubwa ya watu wake hawana degree, kigezo hicho kinakuwa undemocratic na hata unconstitutional.

Acha watu wamkubali au kumkataa mtu kwa uwezo wake.

Usiweke mwanya wa watu kumtaka mtu awaongoze lakini wakashindwa kumchagua kwa sababu artificial ya degree.

Huelewi wapi?
Kwanza sijasema kiwekwe kigezo cha degree au kwamba degree ni muhimu zaidi, nimesmea "elimu rasmi", Inaweza kuwa kidato cha nne, cha sita, diploma, certificate n.k, Inaweza pia kuwa ni equivalency.
Pili hata kama kigezo kingekuwa ni degree na taifa halina watu wengi wenye degree sio lazima kiwe undemocratic au unconstitutional kwa sababu hao watu wasio na degree wenyewe wanaweza kwa wingi wao wakaamua hicho ni kigezo muhimu kwa kiongozi kwa maslahi ya wote.
 
huu ulimbukeni unazitesa sana nchi za Africa, na nashindwa kuelewa wanaolazimisha hizi ajenda wanasumbuliwa na nini ikiwa wao wanaamini kuwa na Degree ndio uwezo mzuri wa kisiasa na uongozi kwanini huwa wanakuwa unsecured kwa watu walioshindwa kuwa na degree?
Mimi naamini watu kama Msukuma, Babu Tale, Kishimba au Kibajaji ni vigumu sana kutunga sheria nzuri hata kama tungekuwa na bunge huru, lakini ni vigumu zaidi kwao kuongoza kama Marais katika karne hii hata kama tungekuwa na katiba bora kiasi gani na sababu kubwa hasa ni uwezo wao mdogo kielimu. Kwa upande mwingine naamini watu kama Mpina, Mwigulu, Kabudi, Bashe n.k wanaweza kuwa viongozi bora sana ukiwa na katiba imara.
 
Back
Top Bottom