Mbowe aligombeaje urais mwaka 2005 kama hana degree?

Mbowe aligombeaje urais mwaka 2005 kama hana degree?

Mtu kama Mbowe anakosaje Degree au ndio siasa za kuchafuana. 😁
Niliwahi wasikia madingi flan wa kichaga wanasema Baba yake Mbowe hata uhuru hujapatikana alikuwa na hela, exposure na mali hatari, kwa mujibu wa wale wazee Nyerere amewahi pewa "Support" na baba yake Mbowe eti kupambania uhuru. 😁

Maana yeke Mbowe ni wa kishua "Born to extremely rich parents".
-kunakingine unatuficha sana,hukusikia wakisema lingine au walikonyezana hukuelewa

FUNGUKA
 
Kigezo kimojawapo cha kugombea urais Tanzania ni mgombea kuwa na angalau kiwango cha elimu cha degree moja, pia huwa kuna rumours mtaana kwamba Freeman Mbowe aliishia kidato cha sita tu, sasa kama ni kweli Mbowe aliwezaje kupitishwa na tume ya uchaguzi kugombea Urais mwaka 2005??

Wanasiasa wanaogombea nafasi kuanzia udiwani, ubunge hadi Urais wanapaswa kuweka wazi CVs zao wapiga kura wawafahamu vizuri kwa manufaa ya umma. George Bush Jr. wa Marekani yeye alikuwa haoni haya kusema hadi matokeo yake ya darasani kwamba hakuwa kipanga na hadi aliwahi kutania kwamba wanafunzi wa daraja C kama yeye wanaweza kuwa marais pia.
KIZIMKAZI ANA DEGREE YA NINI?
 
Sheria imetungwa baada ya uchaguzi huo 2005

Ilifanya mpaka mzee mrema kwenda kupiga buku
Hakwenda kupiga shule popote, alinunuaga cheti cha degree kutoka Maryland university. Then akaibukaga mtaani akiwa na gamba lake mbele ya waandsihi wa habari akasema 'ile degree wanayotakaga si hi hapa, nani anasema Mrema hana degree?". It was so funny🤣🤣🤣🤣
 
Hakwenda kupiga shule popote, alinunuaga cheti cha degree kutoka Maryland university. Then akaibukaga mtaani akiwa na gamba lake mbele ya waandsihi wa habari akasema 'ile degree wanayotakaga si hi hapa, nani anasema Mrema hana degree?". It was so funny🤣🤣🤣🤣
Aise! unakumbukumbu sana yaani miezi 6 tu mzee kukaa zake Amerika akarudi na degree yake

Na
Mkwara juu semeni Sasa ,njooni na lingine
 
Ninachojua kikatiba ili uwe mbunge ujue tu kusoma na kuandika, ya raisi sijui. Ila hicho ni kifungu cha "aibu" kibadilishwe. Ndicho kilichomuweka msukuma bungeni.
 
Mbowe ana degree kitambo sana
Kwa Hisani ya Martin MM

Freeman Aikael Mbowe alizaliwa tarehe 14.09.1961 katika wilaya ya Hai, mkoa wa Kilimanjaro.

Freeman Aikaeli Mbowe alisoma elimu ya msingi katika shule ya Msingi Lambo na kufanikiwa kufaulu kwenda shule ya Sekondari Kibaha mkoa wa Pwani.

Alipohitimu kidato cha 4 Kibaha Sekondari, alifanikiwa kujiunga na kidato cha 5 IHUNGO Sekondari Manispaa ya Bukoba. Baadae alielekea nchini Uingereza kwa masomo zaidi. Uingereza alisoma programu inaitwa PPE (Politics, Philosophy, and Economics).

Ni programu ambayo ilianzishwa na Uingereza kwa ajili ya watumishi serikalini. Baadaye nchi nyingine kama US na RSA zimeshaanzisha programu hiyo. Kwa UK inatolewa kama first degree tu. Mbowe akamalizia MBA in Leadership & Sustainability kutoka Chuo Kikuu cha Cumbria, UK.

Freeman Mbowe ni miongoni mwa Watu waliofanya kazi katika Bank kuu ya Tanzania kama Afisa wa Bank Kuu (BoT) huko ndipo alipofifanikiwa kukutana na Mzee Edwin Mtei, Mzee Bob Makani.

Source:
====
Vigezo gani vilikuwa vinatumika kupata hiyo scholarship ya UK?
 
Aise! unakumbukumbu sana yaani miezi 6 tu mzee kukaa zake Amerika akarudi na degree yake

Na
Mkwara juu semeni Sasa ,njooni na lingine
Hahahahahah . . ...Mrema hakuwa mtu wa kawaida. Ile courage ya kusema Ile degree wanayosemaga si hii hapa, watu wote flat🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom