Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Kuna watu wanauliza Wafuasi wa Mbowe(Wanachadema) walikuwa wapi wakati kiongozi wao anakamatwa na Askari pale kwenye Magomeni.
Wapo wapi anaowapigania?
Wapo wapi waliopatwa na madhila, majanga ambao Mbowe na viongozi wenzake anawasemea na kuwapigania?
Yesu naye alikuwa mwenyekiti kama alivyo Mbowe, Yesu aliwatendea watu wengi miujiza na kufanya makubwa sana ambayo yalivuma na kuwa maarufu katika Judea, Samaria, mama nchi jirani.
Lakini siku alipokutana na Mkono wa Dola, watu wote walimkimbia.
Sio wanafunzi wake.
Sio wale aliowaponya,
Sio wale ambao aliwafufua,
Sio wale aliowalisha chakula.
Wote walimkimbia, zaidi ya yote alisulubishwa.
Kuna mambo ya kujifunza katika mambo haya. Hasa unapoingia katika mambo Ya kisiasa;
1. Usitegemee watu walionyuma yako, hakikisha unajiweza.
Elewa kuwa walionyuma na chini yako wewe ndiye kiongozi wao hivyo endapo utapoteana basi hata wafuasi wako watapoteana.
Kiongozi hategemei Waliochini yake. Kiongozi anategemewa.
2. Kiongozi lazima uwe na Way forward ya namna ya kukabiliana na adui zako..
Maandamano hayawezi kufanikiwa kwa sababu wanaoyaratibu na viongozi wao huruhusu kukamatwa mapema kabla picha halijaanza.
3. Kiongozi wa kisiasa ni muhimu kuwa na Mafunzo ya kijeshi na elimu ya Kijasusi.
Yesu hakufanikiwa kufanya jambo lolote la maana kisiasa na alishindwa kukomboa taifa la Kiyahudi kwa sababu hakuwa na mafunzo ya kivita, kijeshi na mambo ya Kijasusi. Ingawaje washabiki na wafuasi wake humtetea kwa kusema ilimbidi auawe ili wakombolewe kiroho lakini kisiasa hizo tunaita porojo au propaganda za kuwapa moyo mashabiki wake.
Hii ni tofauti na Ma legend wengine kama Musa, Daudi, Ibrahim, Yusufu, Yakobo n.k. hawa wote walikuwa viongozi na walikuwa wanamafunzo ya kivita, kijeshi, na intellijensia.
Na wote misheni zao zilifanikiwa.
Kwa sababu Jeshi, ujasusi, mapigano ni sehemu ya field katika Utawala na Mamlaka.
Ni rahisi kwa mwanajeshi, mwanasheria, jasusi, Polisi, au jeshi kwa aina zake kufanikiwa kutawala au kuchukua Utawala kuliko mtu ambaye wa fani kama Ualimu, udaktari, uinjinia, n.k.
Daudi kabla hajawa Mfalme alikuwa naye na wafuasi wake. Yaani Daudi alikuwa Mwenyekiti katika genge ambalo lilikuwa linamuamini.
Daudi kitaaluma alikuwa mchungaji wa mifugo, mwanamuziki lakini kumbe kwa Siri huko porini alikuwa anajifunza mapigano ya kivita.
Hii ni kusema hata siku anakutana na Goliath hakuwa amekurupuka, alijua kuwa anauwezo wa kupigana na Goliath na Mungu angemsaidia.
Ukitaka ujue kuwa Daudi pia alikuwa Jasusi na kapteni sio tuu tukio la kumuangusha Goliath bali hata harakati za kukabiliana na Mfalme Sauli ambaye hakutaka kumuachia Ufalme kwa njia ya Amani. Daudi alijiepusha sana na Dola, alikimbia na kuepuka mitego yote ya Dola ambapo kwa mtu wa kawaida angekuwa ameshapigwa mapema.
Tundu Lisu na Mbowe wanachokosea ni kudhani kuwa siasa wanazozifanya ni sahihi wakati sio sahihi.
Siasa za Mbowe na Lisu ni sahihi katika ulimwengu wa Dunia ya kwanza huko kwa Wazungu wenye mambo ya Demokrasia. Lakini kwa Afrika sio sahihi kabisa kwa sababu;
Mosi, Afrika Bado ipo nyuma kwa karibu Karne mbili nyuma ya Wazungu. Yaani tupo nyuma ya Wakati.
Pili, Waafrika pia akili, mitazamo, na Mila zetu Bado ipo nyuma.
Sio ajabu Watanzania wengi hawawezi kuelewa kile wanachokifanya Mbowe na Lissu.
Watanzania na Waafrika wengi hawaelewi Uhuru ni kitu gani, Haki ni nini, Mila potofu ni zipo,
Lakini tumaini ni kuwa kidogokidogo mambo yatabadilika.
Kwa hiyo njia pekee ambayo Watanzania na Waafrika huilewa ni njia ya mabavu na maguvu.
Watu wasiotambia Haki zao, uhuru wao, kipi kizuri na kipi kibaya huwezi kuwaongoza kwa njia za kidemokrasia. Ubabe, udikteta, maguvu ndio njia sahihi.
Huwezi kuleta Demokrasia kwa ulimwengu ambao Bado unaamini katika Mwanamke anatakiwa kutolewa Mahari. Alafu ukiwaambia wakupe hoja hakuna hata Moja ya maana.
Huwezi leta Demokrasia kwenye jamii ya watu ambao wanaaminj hawafanikiwi kwa sababu wamelogwa au Kuna mtu kamtupia Jini. Hiyo Demokrasia ya kazi gani?
Huwezi leta Demokrasia au kuwapa watu uhuru wanaoamini kuwa Mzazi anaweza kukutamkia maneno mabaya(Laana) Ati yakashika au baraka ikashika jambo ambalo ni uongo wa mchana Kabisa.
Huwezi leta au kupigania Demokrasia kwenye jamii ambayo Albino wanauliwa kisa mambo ya kishirikina.
Huwezi leta Demokrasia kwa watu ambao wanaamini kiongozi wa dini akiwapa mafuta au kitu Fulani watafanikiwa. Hizi ni akili za wakati wa Yesu, zama za zamani sana.
Ambapo miaka hiyo Wafalme walidanganya wanaowatawala kuwa wao ni miungu na wanauwezo wa kimungu.
Huwezi leta Demokrasia kwa watu ambao huona mzazi au mkubwa Hakosei. Hiyo jamii Bado ipo gizani.
Huwezi leta Demokrasia kwa watu wanaoamini mwanamke ni kumbe cha kukaa nyumbani. Kiumbe kisicho na Haki kama Mtu.
Na wanawake wenyewe wanaoamini vivyohivyo. Huwezi peleka Demokrasia huko.
Huwezi kupeleka Demokrasia kwa watu hao kwa Sababu zifuatazo:
1. Wataitumia vibaya Demokrasia na uhuru utakaowapa.
Waafrika tunashuhudia wakilalamika Kila pembe ya Afrika kuwa mbona walipigania uhuru lakini mambo ni kama yamewashinda. Uhuru unapiganiwa na watu waliojiandaa na waliokomaa.
Hata mtoto mdogo ukimpa uhuru kabla ya Wakati wake sio ajabu ukamkuta anavuta mibangi, madawa ya kulevya na kufanya mambo ndivyosivyo.
2. Kundi dogo kukandamiza kundi Kubwa.
Demokrasia ni watu wengi ndio husikilizwa na kunufaishwa. Lakini watu ambao hawajaandaliwa kupata Demokrasia huwa kinyume chake, kwamba kundi dogo kusikilizwa na kuneemeka dhidi ya kundi Kubwa.
3. Kutokueleweka.
Unamwambia Mtu wewe ni mtu lazima ufanye kazi ili uwe Huru, unahaki ya kuchagua au kuchaguliwa kiongozi, hakuelewi.
Unamwambia Mtu hutakiwi kutolewa Mahari, hawezi kukuelewa na hana Makosa kwa sababu amefungwa macho yake. Anaona kiza mbele.
4. Machafuko.
Uhuru, Demokrasia na Haki haiwafai watu ambao hawajajiandaa kwa Sababu huweza kusababisha machafuko.
Sio ajabu watu wanaona mbona ndoa siku hizi zinapasuka vipandevipande, wanasema mwanamke kapewa Uhuru au suala la HAKI Sawa.
Mtu anapopewa uhuru kabla hajaandaliwa kinachofuata ni machafuko.
Lazima mtu aandaliwe kuwa Huru.
Kumpa mtu uhuru kabla hujamuandaa ni sawa na Ndama aliyekata Kamba.
Katika Level ya Familia,
Wazazi Bora hujua kabisa Uhuru na Demokrasia ni muhimu sana kwa mtu. Hivyo huwaandaa watoto wao hatua kwa hatua namna ya kuwa watu Huru na watu wa Haki na Demokrasia.
Mtoto akipewa uhuru bila kuandaliwa sio ajabu akifika chuo kikuu anaanza kuparangana huko kwenye ma-club na makasino bila AKILI. Kuparamia wanawake hovyo, kunywa mapombe na mavyakula pasipo AKILI.
Mwishowe mtoto huweza kudhurika na wakati mwingine kufa kabla ya Wakati
Uhuru unaenda kwa Hatua. Uhuru unaenda sambamba na AKILI.
Uhuru bila AKILI yaani uhuru ambao haujaandaliwa huleta machafuko na anguko.
Zipo hatua za watu kupigania au kupewa Uhuru. Hilo litakuwa Somo jingine. Kwa sababu uhuru nao ukicheleweshwa huleta machafuko na maanguko.
Taikon nimeandika mpaka nimepotea njia lakini naamini nilichoandika ukitulia kitatusaidia wote.
Lakini kama hakijakusaidia au hakitakusaidia nakupa Pole sana.
Mimi acha nipumzike, leo nitakula ugali, mlenda na Samaki wa kuchoma.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Mtibeli
Kuna watu wanauliza Wafuasi wa Mbowe(Wanachadema) walikuwa wapi wakati kiongozi wao anakamatwa na Askari pale kwenye Magomeni.
Wapo wapi anaowapigania?
Wapo wapi waliopatwa na madhila, majanga ambao Mbowe na viongozi wenzake anawasemea na kuwapigania?
Yesu naye alikuwa mwenyekiti kama alivyo Mbowe, Yesu aliwatendea watu wengi miujiza na kufanya makubwa sana ambayo yalivuma na kuwa maarufu katika Judea, Samaria, mama nchi jirani.
Lakini siku alipokutana na Mkono wa Dola, watu wote walimkimbia.
Sio wanafunzi wake.
Sio wale aliowaponya,
Sio wale ambao aliwafufua,
Sio wale aliowalisha chakula.
Wote walimkimbia, zaidi ya yote alisulubishwa.
Kuna mambo ya kujifunza katika mambo haya. Hasa unapoingia katika mambo Ya kisiasa;
1. Usitegemee watu walionyuma yako, hakikisha unajiweza.
Elewa kuwa walionyuma na chini yako wewe ndiye kiongozi wao hivyo endapo utapoteana basi hata wafuasi wako watapoteana.
Kiongozi hategemei Waliochini yake. Kiongozi anategemewa.
2. Kiongozi lazima uwe na Way forward ya namna ya kukabiliana na adui zako..
Maandamano hayawezi kufanikiwa kwa sababu wanaoyaratibu na viongozi wao huruhusu kukamatwa mapema kabla picha halijaanza.
3. Kiongozi wa kisiasa ni muhimu kuwa na Mafunzo ya kijeshi na elimu ya Kijasusi.
Yesu hakufanikiwa kufanya jambo lolote la maana kisiasa na alishindwa kukomboa taifa la Kiyahudi kwa sababu hakuwa na mafunzo ya kivita, kijeshi na mambo ya Kijasusi. Ingawaje washabiki na wafuasi wake humtetea kwa kusema ilimbidi auawe ili wakombolewe kiroho lakini kisiasa hizo tunaita porojo au propaganda za kuwapa moyo mashabiki wake.
Hii ni tofauti na Ma legend wengine kama Musa, Daudi, Ibrahim, Yusufu, Yakobo n.k. hawa wote walikuwa viongozi na walikuwa wanamafunzo ya kivita, kijeshi, na intellijensia.
Na wote misheni zao zilifanikiwa.
Kwa sababu Jeshi, ujasusi, mapigano ni sehemu ya field katika Utawala na Mamlaka.
Ni rahisi kwa mwanajeshi, mwanasheria, jasusi, Polisi, au jeshi kwa aina zake kufanikiwa kutawala au kuchukua Utawala kuliko mtu ambaye wa fani kama Ualimu, udaktari, uinjinia, n.k.
Daudi kabla hajawa Mfalme alikuwa naye na wafuasi wake. Yaani Daudi alikuwa Mwenyekiti katika genge ambalo lilikuwa linamuamini.
Daudi kitaaluma alikuwa mchungaji wa mifugo, mwanamuziki lakini kumbe kwa Siri huko porini alikuwa anajifunza mapigano ya kivita.
Hii ni kusema hata siku anakutana na Goliath hakuwa amekurupuka, alijua kuwa anauwezo wa kupigana na Goliath na Mungu angemsaidia.
Ukitaka ujue kuwa Daudi pia alikuwa Jasusi na kapteni sio tuu tukio la kumuangusha Goliath bali hata harakati za kukabiliana na Mfalme Sauli ambaye hakutaka kumuachia Ufalme kwa njia ya Amani. Daudi alijiepusha sana na Dola, alikimbia na kuepuka mitego yote ya Dola ambapo kwa mtu wa kawaida angekuwa ameshapigwa mapema.
Tundu Lisu na Mbowe wanachokosea ni kudhani kuwa siasa wanazozifanya ni sahihi wakati sio sahihi.
Siasa za Mbowe na Lisu ni sahihi katika ulimwengu wa Dunia ya kwanza huko kwa Wazungu wenye mambo ya Demokrasia. Lakini kwa Afrika sio sahihi kabisa kwa sababu;
Mosi, Afrika Bado ipo nyuma kwa karibu Karne mbili nyuma ya Wazungu. Yaani tupo nyuma ya Wakati.
Pili, Waafrika pia akili, mitazamo, na Mila zetu Bado ipo nyuma.
Sio ajabu Watanzania wengi hawawezi kuelewa kile wanachokifanya Mbowe na Lissu.
Watanzania na Waafrika wengi hawaelewi Uhuru ni kitu gani, Haki ni nini, Mila potofu ni zipo,
Lakini tumaini ni kuwa kidogokidogo mambo yatabadilika.
Kwa hiyo njia pekee ambayo Watanzania na Waafrika huilewa ni njia ya mabavu na maguvu.
Watu wasiotambia Haki zao, uhuru wao, kipi kizuri na kipi kibaya huwezi kuwaongoza kwa njia za kidemokrasia. Ubabe, udikteta, maguvu ndio njia sahihi.
Huwezi kuleta Demokrasia kwa ulimwengu ambao Bado unaamini katika Mwanamke anatakiwa kutolewa Mahari. Alafu ukiwaambia wakupe hoja hakuna hata Moja ya maana.
Huwezi leta Demokrasia kwenye jamii ya watu ambao wanaaminj hawafanikiwi kwa sababu wamelogwa au Kuna mtu kamtupia Jini. Hiyo Demokrasia ya kazi gani?
Huwezi leta Demokrasia au kuwapa watu uhuru wanaoamini kuwa Mzazi anaweza kukutamkia maneno mabaya(Laana) Ati yakashika au baraka ikashika jambo ambalo ni uongo wa mchana Kabisa.
Huwezi leta au kupigania Demokrasia kwenye jamii ambayo Albino wanauliwa kisa mambo ya kishirikina.
Huwezi leta Demokrasia kwa watu ambao wanaamini kiongozi wa dini akiwapa mafuta au kitu Fulani watafanikiwa. Hizi ni akili za wakati wa Yesu, zama za zamani sana.
Ambapo miaka hiyo Wafalme walidanganya wanaowatawala kuwa wao ni miungu na wanauwezo wa kimungu.
Huwezi leta Demokrasia kwa watu ambao huona mzazi au mkubwa Hakosei. Hiyo jamii Bado ipo gizani.
Huwezi leta Demokrasia kwa watu wanaoamini mwanamke ni kumbe cha kukaa nyumbani. Kiumbe kisicho na Haki kama Mtu.
Na wanawake wenyewe wanaoamini vivyohivyo. Huwezi peleka Demokrasia huko.
Huwezi kupeleka Demokrasia kwa watu hao kwa Sababu zifuatazo:
1. Wataitumia vibaya Demokrasia na uhuru utakaowapa.
Waafrika tunashuhudia wakilalamika Kila pembe ya Afrika kuwa mbona walipigania uhuru lakini mambo ni kama yamewashinda. Uhuru unapiganiwa na watu waliojiandaa na waliokomaa.
Hata mtoto mdogo ukimpa uhuru kabla ya Wakati wake sio ajabu ukamkuta anavuta mibangi, madawa ya kulevya na kufanya mambo ndivyosivyo.
2. Kundi dogo kukandamiza kundi Kubwa.
Demokrasia ni watu wengi ndio husikilizwa na kunufaishwa. Lakini watu ambao hawajaandaliwa kupata Demokrasia huwa kinyume chake, kwamba kundi dogo kusikilizwa na kuneemeka dhidi ya kundi Kubwa.
3. Kutokueleweka.
Unamwambia Mtu wewe ni mtu lazima ufanye kazi ili uwe Huru, unahaki ya kuchagua au kuchaguliwa kiongozi, hakuelewi.
Unamwambia Mtu hutakiwi kutolewa Mahari, hawezi kukuelewa na hana Makosa kwa sababu amefungwa macho yake. Anaona kiza mbele.
4. Machafuko.
Uhuru, Demokrasia na Haki haiwafai watu ambao hawajajiandaa kwa Sababu huweza kusababisha machafuko.
Sio ajabu watu wanaona mbona ndoa siku hizi zinapasuka vipandevipande, wanasema mwanamke kapewa Uhuru au suala la HAKI Sawa.
Mtu anapopewa uhuru kabla hajaandaliwa kinachofuata ni machafuko.
Lazima mtu aandaliwe kuwa Huru.
Kumpa mtu uhuru kabla hujamuandaa ni sawa na Ndama aliyekata Kamba.
Katika Level ya Familia,
Wazazi Bora hujua kabisa Uhuru na Demokrasia ni muhimu sana kwa mtu. Hivyo huwaandaa watoto wao hatua kwa hatua namna ya kuwa watu Huru na watu wa Haki na Demokrasia.
Mtoto akipewa uhuru bila kuandaliwa sio ajabu akifika chuo kikuu anaanza kuparangana huko kwenye ma-club na makasino bila AKILI. Kuparamia wanawake hovyo, kunywa mapombe na mavyakula pasipo AKILI.
Mwishowe mtoto huweza kudhurika na wakati mwingine kufa kabla ya Wakati
Uhuru unaenda kwa Hatua. Uhuru unaenda sambamba na AKILI.
Uhuru bila AKILI yaani uhuru ambao haujaandaliwa huleta machafuko na anguko.
Zipo hatua za watu kupigania au kupewa Uhuru. Hilo litakuwa Somo jingine. Kwa sababu uhuru nao ukicheleweshwa huleta machafuko na maanguko.
Taikon nimeandika mpaka nimepotea njia lakini naamini nilichoandika ukitulia kitatusaidia wote.
Lakini kama hakijakusaidia au hakitakusaidia nakupa Pole sana.
Mimi acha nipumzike, leo nitakula ugali, mlenda na Samaki wa kuchoma.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam