Pre GE2025 Mbowe: Lissu alikuwa Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, na ndiye alitunga vifungu vya kuondoa ukomo wa uongozi kwa viongozi wakuu na wajumbe wa Kamati Kuu

Pre GE2025 Mbowe: Lissu alikuwa Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, na ndiye alitunga vifungu vya kuondoa ukomo wa uongozi kwa viongozi wakuu na wajumbe wa Kamati Kuu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ungesikiliza mahojiano na si kuweka neno kwenye tafsiri ya mahojiano ya mtu mwingine. Mbowe amesema Katiba imeweka utaratibu wa kufuata ili kufanya mabadiliko ya Katiba, na mtu akiwa na hoja anatumia huo utaratibu, na kisha wajumbe wanaupitisha kama wakiona unakidhi mahitaji. Kuhusu katiba yao, Mbowe anasema ni Lissu mwenyewe aliyeiweka kisheria, lakini leo zigo zima anasukumiwa yeye peke yake as if Lissu anayetoa tuhuma mbalimbali hakushiriki kuitunga. Ninavyo mimi, mambo yote kasukimiwa Mbowe, maana ni rahisi Kwa baadhi ya watu kupanda juu Kwa kukanyaga mabega ya wenzao. Mfano, Lissu amekuwa akimsukumia Mbowe kuhusu maridhiano na tuzo ya Samia. Hebu sikiliza mwenyewe Lissu alisema nini kuhusu vyote viwili:
View: https://youtu.be/rTWpnMO7kto?si=DZRFiyxHR9M69dGp

Aliyesema ogopa technology hakukosea, imesaidia sana kusaidia watu vigeugeu kuwabana kwa maneno yao waliyowahi sema na wanayakana
 
Lissu hajawahi kusema kuwa hakushiriki katika kuwe ukomo wa madaraka. Kinyume chake amekiri kushiriki na kama mwanasheria mkuu wa chama sehemu yake ilikuwa kubwa.

Alichokisema Lissu ni kwamba wakati wa kuuondoa ukomo wa madara sasa umewadia baada ya chama kujengeka na kuimarika kuwa chama kikuu cha uponzani.

Mimi namuunga Lissu mkono katika hoja hii. Wewe pia ukielewa hoja yake, tafakari na chukua hatua.
Tueleze Sababu za msingi zilizokuwepo wakati ule ambazo sasa hazipo zilizopelekea yeye kama mwanasheria kusimamia kuondoa ukomo uliowekwa na waasisi wa chama hicho.
 
Mwenyekiti ndiye hurekebisha katiba? Chama ni wanachama… kwanini Lissu hakuwahi peleka hiyo hoja ili iungwe mkono au laa?

Lissu ana agenda zake na muda ni hakimu wa yote tupo hapa siku moja tutasimuliana jinsi gani samia anamtumia Msigwa kuivuruga CHADEMA!
..kwani lazima apeleke muda gani? Muda ilikuwa haujafika, mbowe Jana kachemka, alipaswa kujibu kiongozi kwamba muda utafika katiba itarekebishwa, kwa chadema bila mbowe kukaa pembeni kitakuwa kimefika mwisho
 
Tueleze Sababu za msingi zilizokuwepo wakati ule ambazo sasa hazipo zilizopelekea yeye kama mwanasheria kusimamia kuondoa ukomo uliowekwa na waasisi wa chama hicho.
Mkuu mfuatilie lissu utaelewa vizuri, lissu kanyooka kama rula
 
Huu wako udini, muislam Hana haki ya kutoa maoni humu? Kabendera sheikh wa wapi?
Pole kwa kutoelewa.

Tafuta Pepsi bariidi ukae hapo pembeni mwa duka omba kiti usome kwa kutulia ili uelewa!.
 
Mbowe ameyasema hayo wakati akihojiwa na Salim Kikeke katika kipindi cha Kasri kinachorushwa na CrownFM

Mbowe amesema kwamba Lissu anashiriki vikao vyote vya chama lakini hajawahi kuwasilisha hoja katika vikao ya kuomba wajadili kuondoa ukomo wa uongozi
MWONGO MKUMBWA

Mbowe HAJASEMA Lissu alitunga vifungu vya kuondoa ukomo wa uongozi.

Mbowe amesema Lissu hajawahi kuleta kwenye chama hoja ya kupendekeza kufuta ukomo.

Upeo wako wa kuelewa ni finyu mno, au unaongopa makusudi.
 
MWONGO MKUMBWA

Mbowe HAJASEMA Lissu alitunga vifungu vya kuondoa ukomo wa uongozi.

Mbowe amesema Lissu hajawahi kuleta kwenye chama hoja ya kupendekeza kufuta ukomo.

Upeo wako wa kuelewa ni finyu mno, au unaongopa makusudi.
Kasikilize vizuri
 
Mwanasheria mkuu ndio anarekebisha katiba?

Chadema ni Wahuni sana 😂😂😂
Bwashee ina maana hujui kuwa katiba ndiyo sheria mama ya chama? Wasiojua sheria wanaweza kubadilisha vifungu vya katiba bila kuhusisha mwanasheria mkuu wa chama?
 
Back
Top Bottom