Mbowe, Lissu chukueni hatua kurejesha nidhamu kwenye chama

Mbowe, Lissu chukueni hatua kurejesha nidhamu kwenye chama

"Huu ni ushauri wa bure kwenu waungwana."

Ni muhimu kuyatambua yafuatayo:

1. CHADEMA kimekuwa ni chama chaguo la wengi kwa muda mrefu.

2. Si kwa sababu ni chama bora sana, ila ni kwa kuwa kinayo nafasi ya kufanya maboresho.

3. Kwamba ndani ya changamoto zilizopo, hatimaye tutafika.

4. Haipo siri kuwa katika siku za karibuni hali inataka kuelekea kubaya badala ya kuliko tarajiwa (changamoto safarini).

5. Kauli za kushangaza (kibri, matusi, kejeli, nk) kutokea kwa baadhi ya wenye kujinasibu kuwa wanachama, zimekuwa zikisikika.

6. Imekuwa ni kama zogo la magenge ya wahuni.

7. Hali hii haiwezi kuwavutia wenye akili zao kwa binafsi zao au hata kwa makundi yao.

9. Ukombozi unahitaji uungwaji mkono kutokea makundi mbalimbali hasa asasi za dini, kiraia, nchi, vyama washirika, nk.

10. Uhuni au wahuni hawawezi kuwa sehemu, kwenye uvutiaji wa uungwaji mkono huo.

11. Hali hii haipaswi kuachwa kuendelea au hata kuvumiliwa.

12. Ni muhimu zikachukuliwa hatua sahihi zenye kuonekana ili kuweka nidhamu kamili chamani.

13. Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama.

14. "Lissu, Mbowe chukueni jukumu hili sasa."

CHADEMA inaweza kufanya vizuri zaidi na mno, kuliko kumwendekeza mhuni yeyote.

Mhuni ni mhuni tu!
Nidhamu inabidi iwepo nje na ndani ya chama lakini kwa mikutano yao wanayofanya nje ya chama ni dhahiri hakuna nidhamu humo.
 
Mkuu kwa maoni yangu nadhani ungetangaza upande wako wa kisiasa kabla ya hujaweka hoja yako hapa ili tuweze kuchangia kujadili hoja objectively.

Nianzie hapa kwenye "msingi" wa hoja yako.

a) Mkuu una maoni nje ya mada. Ni ustaarabu uliojengeka kujikita kwenye mada. Si kujihangaisha na mleta mada.

b) Huoni kama yakiendekezwa maoni yako, labda tuanze na wewe kujiuliza swali hilo hilo?

c) Kwani hata nikiweka utambulisho huo, si bila shaka utataka uthibitisho?

d) Fuatilia mada nzima kujiona kutambua kuwa:

"Huu ni ushauri wa bure kwa walengwa wawili. Yaani Mbowe na Lissu." Haipo shuruti.

e) Hata kama ni kweli kuwa labda wewe ni kiziwi au kipofu:

4. Haipo siri kuwa katika siku za karibuni hali inataka kuelekea kubaya badala ya kuliko tarajiwa (changamoto safarini).

11. Hali hii haipaswi kuachwa kuendelea au hata kuvumiliwa.

Mbowe, Lissu chukueni hatua kurejesha nidhamu kwenye chama

f) Kwamba wewe hujui kwenye jumuiko lolote nidhamu ni muhimu?

g) Kwamba umekereka kusikia kuitishwa nidhamu? Hivyo tuache mada tuanze kuongelea milengo ya kisiasa ya watu?

h) Wewe hautakuwa ni CCM au kibaraka wao kwa kujua au kutokujua? Bila shaka Lissu akiwaongelea watu kama wewe?

Tundu Lissu: Kauli ya Diaspora watuache ni ya CCM, anayesema kauli hiyo anafanya kazi ya CCM

i) Kumbe hoja zako zote zilizojengwa kwenye msingi usiokuwa na maana zitakuwa na thamani gani ndugu?

"Kimsingi kwa majibu yangu ningeishia hapa. Zaidi ya hapa ninaamua kukupa msaada kukusaidia tu."

"Wanasema, ukivuliwa nguo chutama."

Au nasema uongo yangu?

Nasema hivyo kwa sababu:

1. Huwezi kutoa ushauri chanya na wenye nia njema kwa mhindani wako.

a) Ushauri ni kwa Mbowe na Lissu si kwako au awaye yote mwingine. Si lazima. Kuuchukua au kuukataa, hiari yao. Sasa hapo mshindani wangu Mbowe au Lissu?

b) Ningekuelewa sana kama ungejikita kuwashauri kuuchukua au kuukataa.

c) kama unadhani maoni hapa ni kwa mujibu wa mlengo wa mtu kwanini yako yasiwe pia hivyo hivyo? Kwani mlengo wako uko hapa?

d) Bila kusahau hoja hapa tokea msingi mbovu, hoja yako hii Ina thamani gani?

2. Taasisi yoyote hai lazima pawepo na ushindani au misigino ya mawazo, hoja na fikra.

a) Tofautisha uliyoorodhesha na matusi. Zaidi sana zingatia maneno haya: "ridhaa ya chama:"

13. Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama."

b) Sambamba na hili nikualike kwenye uzi huu kuona uko nje ya mada:

CHADEMA wakaneni hadharani chawa hawa wa mitandaoni

3. Tofautisha mawazo, mitazamo na misimamo binafsi ya mwanachama dhidi ya taasisi husika.

a) Maneno .. bIla ridhaa ya chama[ uliweza kuyaona mara zote?

13. Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama."

b) Maneno hayo hayo yamu humu pia:

CHADEMA wakaneni hadharani chawa hawa wa mitandaoni

c) Kulikoni kulia machozi ya mamba ndugu?

4. Tofautisha katika ya kukosoa, kufikirisha na kusema ukweli dhidi ya kutukana au kukashfu.

a) Kwamba hata ni siri ndugu? Kuwa hali siyo hii?

5. Kauli za kushangaza (kibri, matusi, kejeli, nk) kutokea kwa baadhi ya wenye kujinasibu kuwa wanachama, zimekuwa zikisikika.

6. Imekuwa ni kama zogo la magenge ya wahuni.


b) Kwamba ni wewe peke yako ndiyo huoni hivyo? Kama ndivyo nikuitishe kujipapasa, kujisachi na kujiangalia vyema. Huenda unaweza kuwa mmoja wao!

5. Tuache watu aongee kwa uhuru ili mradi hawavunji sheria ya nchi. Tukubaliani kutofautiani bila ugomvi.

a) Wapi unasoma kuzuiliwa kuongea au hata kuzuiliwa kuvunja sheria za nchi kama ndivyo wanavyotaka?

5. Kauli za kushangaza (kibri, matusi, kejeli, nk) kutokea kwa baadhi ya wenye kujinasibu kuwa wanachama, zimekuwa zikisikika.

6. Imekuwa ni kama zogo la magenge ya wahuni.


b) Kwamba ni maoni yako haya yaachwe kuendelea kwa ridhaa ya chama? Kwamba ni kwa maono yako huo ni uhuru wao?

c) Zingatia maneno haya:

13.Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama.

d) Tunachokataa ni kujinasibu kwa jina la chama na bila ridhaa kama ndicho kinachotokea labda kama ridhaa hiyo wanayo:

CHADEMA wakaneni hadharani chawa hawa wa mitandaoni

(e) Au wanayo ridhaa ya chama ndugu?

Kumalizia tusitake taasisi shindani ifanane na taasisi tuliomo kwa itikadi, mawazo, mitazamo na misimamo. Hiyo itakuwa midoli sasa!

a) Kumalizia nikukumbushe kuwa hitimisho lako hili kutokea kwenye msingi dhaifu mno, halina thamani yoyote.

b) Zaidi sana kwa sababu naona yawezekana hukusoma vizuri, ninakazie kwa kuyaweka haya hapa chini:

"11. Hali hii haipaswi kuachwa kuendelea au hata kuvumiliwa.

12. Ni muhimu zikachukuliwa hatua sahihi zenye kuonekana ili kuweka nidhamu kamili chamani.

13. Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama.

14. "Lissu, Mbowe chukueni jukumu hili sasa."

CHADEMA inaweza kufanya vizuri zaidi na mno, kuliko kumwendekeza mhuni yeyote.

Mhuni ni mhuni tu!"


Koleo ni vyema kuliita kwa jina lake mapema asubuhi, kuliko kukomalia kujidanganya vinginevyo.

Habari ndiyo hiyo.
 
Haya sio matusi?
F0v5tYZXgAEPFoz.jpg


Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Nidhamu inabidi iwepo nje na ndani ya chama lakini kwa mikutano yao wanayofanya nje ya chama ni dhahiri hakuna nidhamu humo.

Waonekana kuchachawa ndugu. Peleka mrejesho :

"Hatudanganyiki!"

Tunachokitaka tunakijua, namna ya kukipata tunaijua na tumedhamiria kukipata.

Habari ndiyo hiyo.
 
Yupo humu ,huyo mtu yeye kila kitu anajua,,siku moja kuna jamaa alimvaa kumbe anamjua akaanza kumtolea siri jinsi anavyodandia mali za wanaume wenzake na kutamba nazo mjini ikiwemo magari kwa mara ya kwanza alishindwa hiyo vita.
Jamaa ni chawa wa mbowe nasikia
 
Na jee CCM wenye kijana kama Suphian Juma unadhani waungwana wanawafikiriaje hicho chama? Vijana wengi wamefedheheka na chama kutumia vijana wenye tabia kama zake kutetea chama.
Kuna msemo kuwa ukitaka kukijua chama au kikundi tazama wafuasi wake. Jee ccm tuijue kwa kumtazama huyo kijana?

F92tYI_XQAA481Q.jpg


Wahuni ni wahuni tu! Ni wahuni! Alisikika mwanasiasa mmoja nguli akisema.
 
CHADEMA MMEKUFIANA SIKU MINGI CHAMA GANI HADI KIONGOZI WAKE ANAWEKWA MMBARONI .
CCM NAYO INAPUMULIA GESI HADI IMEMLETA MAKONDA ASUMBUE SUMBUE WATU NA MIWANI YAKE HANA SERA HUYOO KACHUJA. TANZANIA HATUNA VYAMA VINGI VIMEKUFA NA KIMOJA KINAPUMULIA GESI MAISHA NI MAGUMU SANA WANAPUMULIA GESI
 
Mabadiliko yaanze na uongozi, mbowe atoe nafasi sasa kwa mtu mwingine...yeye abaki mshauri wa chama
 
Nimesema hivyo nina hakika,we nenda kule twitter mseme Mbowe kwa jambo la ukweli utaona hizo comment na pia mseme na Lissu kwenye jambo pia la ukweli au hata uongo utaona comment zake ,kisha rudi hapa tujadili.

1. Mkuu Uzi huu umejengwa kutokea katika nyuzi 2 hizi:

a) "CHADEMA wakaneni hadharani chawa hawa wa mitandaoni"

b) "Lissu rudini ubaoni, Majukwaani hakutamng'oa CCM"

Uzi huu haujengwi kutokea Twitter au kwingineko ambako wengine hatuna mahaba nako.

2. Wahuni hawa wapo hata humu JF. Kwa vile hata huko Twitter nako ni mitandaoni, haitakuwapo ajabu kuwa:

"Wapenda ngono na wachawi siyo kwenu tu, hata kwetu wapo." Alisikika msanii mmoja akiimba.

3. Hivyo mkuu sidhani inahitaji kwenda popote zaidi kupata kuyatafiti ya wahuni hawa.

4. Mbona hata humu JF kunatosha sana ndugu?
 
CHADEMA MMEKUFIANA SIKU MINGI CHAMA GANI HADI KIONGOZI WAKE ANAWEKWA MMBARONI .
CCM NAYO INAPUMULIA GESI HADI IMEMLETA MAKONDA ASUMBUE SUMBUE WATU NA MIWANI YAKE HANA SERA HUYOO KACHUJA. TANZANIA HATUNA VYAMA VINGI VIMEKUFA NA KIMOJA KINAPUMULIA GESI MAISHA NI MAGUMU SANA WANAPUMULIA GESI

Mpigania haki yupi hakupata misuko suko ya kuwekwa mbaroni na wengine hata kuuwawa?

Ni Mandela, Nyerere, Kenyatta, Seif, Mtikila, Hichilema, nk? Mrejesho wako tafadhali.

Usiku saa sana hizi. Isije kuwa "kibongo bongo" waandika ukiwa usingizini na hapo upo ndotoni?

Usiige, wengine tuko night shift, macho makavu!
 
"Huu ni ushauri wa bure kwenu waungwana."

Ni muhimu kuyatambua yafuatayo:

1. CHADEMA kimekuwa ni chama chaguo la wengi kwa muda mrefu.

2. Si kwa sababu ni chama bora sana, ila ni kwa kuwa kinayo nafasi ya kufanya maboresho.

3. Kwamba ndani ya changamoto zilizopo, hatimaye tutafika.

4. Haipo siri kuwa katika siku za karibuni hali inataka kuelekea kubaya badala ya kuliko tarajiwa (changamoto safarini).

5. Kauli za kushangaza (kibri, matusi, kejeli, nk) kutokea kwa baadhi ya wenye kujinasibu kuwa wanachama, zimekuwa zikisikika.

6. Imekuwa ni kama zogo la magenge ya wahuni.

7. Hali hii haiwezi kuwavutia wenye akili zao kwa binafsi zao au hata kwa makundi yao.

9. Ukombozi unahitaji uungwaji mkono kutokea makundi mbalimbali hasa asasi za dini, kiraia, nchi, vyama washirika, nk.

10. Uhuni au wahuni hawawezi kuwa sehemu, kwenye uvutiaji wa uungwaji mkono huo.

11. Hali hii haipaswi kuachwa kuendelea au hata kuvumiliwa.

12. Ni muhimu zikachukuliwa hatua sahihi zenye kuonekana ili kuweka nidhamu kamili chamani.

13. Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama.

14. "Lissu, Mbowe chukueni jukumu hili sasa."

CHADEMA inaweza kufanya vizuri zaidi na mno, kuliko kumwendekeza mhuni yeyote.

Mhuni ni mhuni tu!
Sahihi
 
Mpigania haki yupi hakupata misuko suko ya kuwekwa mbaroni na wengine hata kuuwawa?

Ni Mandela, Nyerere, Kenyatta, Seif, Mtikila, Hichilema, nk? Mrejesho wako tafadhali.

Usiku saa sana hizi. Isije kuwa "kibongo bongo" waandika ukiwa usingizini na hapo upo ndotoni?

Usiige, wengine tuko night shift, macho makavu!
Correct
 
Waonekana kuchachawa ndugu. Peleka mrejesho :

"Hatudanganyiki!"

Tunachokitaka tunakijua, namna ya kukipata tunaijua na tumedhamiria kukipata.

Habari ndiyo hiyo.
Mtabaki Wabwabwajaji na watoa taarifa
 
Huku CCM nidhamu itarudishwa lini?
 
"Huu ni ushauri wa bure kwenu waungwana."

Ni muhimu kuyatambua yafuatayo:

1. CHADEMA kimekuwa ni chama chaguo la wengi kwa muda mrefu.

2. Si kwa sababu ni chama bora sana, ila ni kwa kuwa kinayo nafasi ya kufanya maboresho.

3. Kwamba ndani ya changamoto zilizopo, hatimaye tutafika.

4. Haipo siri kuwa katika siku za karibuni hali inataka kuelekea kubaya badala ya kuliko tarajiwa (changamoto safarini).

5. Kauli za kushangaza (kibri, matusi, kejeli, nk) kutokea kwa baadhi ya wenye kujinasibu kuwa wanachama, zimekuwa zikisikika.

6. Imekuwa ni kama zogo la magenge ya wahuni.

7. Hali hii haiwezi kuwavutia wenye akili zao kwa binafsi zao au hata kwa makundi yao.

9. Ukombozi unahitaji uungwaji mkono kutokea makundi mbalimbali hasa asasi za dini, kiraia, nchi, vyama washirika, nk.

10. Uhuni au wahuni hawawezi kuwa sehemu, kwenye uvutiaji wa uungwaji mkono huo.

11. Hali hii haipaswi kuachwa kuendelea au hata kuvumiliwa.

12. Ni muhimu zikachukuliwa hatua sahihi zenye kuonekana ili kuweka nidhamu kamili chamani.

13. Wahuni hawawezi kuachwa kujinasibu kwa niaba ya chama kwenye lolote lisilokuwa na ridhaa ya chama.

14. "Lissu, Mbowe chukueni jukumu hili sasa."

CHADEMA inaweza kufanya vizuri zaidi na mno, kuliko kumwendekeza mhuni yeyote.

Mhuni ni mhuni tu!
Haileweki msemaji wa Chama ni nani ,leo hii Lema anayo sauti kwenye chama kuliko hata katibu mkuu wa chama aisee
 
Back
Top Bottom