Mbowe, Lissu, Dkt Kitima, Jenerali Ulimwengu, Dkt Slaa - ni wapotoshaji kuhusu DP World?

First.. tunaomba hizo faida za kimaslahi kwa Taifa, kuhusu kuingiza Taifa kweny mikataba ya hovyo hilo ni kwel usidanganye umma hata JPM hili hakusita kusema ukwel juu ya mikataba ya hovyo!! Wakati mwingine acheni mahaba ya CCM ongeeni facts hata kama utakosa posho ya kujikimu na maisha, hapo mtaliokoa Taifa!!!
 
CCM hakiwezi kuunza nchi, CCM hakiwezi kuingia ktk Mikataba inayotutia hasara, CCM hakiwezi kuingia Mikataba mibovu.
Are you for real? Kwa miaka 47 ambayo CCM imeng'ang'ania uongozi wa taifa hili, hivi leo ndio wanatoa sababu kuu ya kuwapa Waarabu bandari ya Tanganyika ni kukosekana kwa uadilifu wa kuendesha chombo kama hicho, really?

Kwa nini CCM ilikuwa tayari kutumia nguvu, kutesa, kuiba, na kufanya kila uovu ndani ya taifa hili, mradi hawaachii madaraka! Kila baada ya miaka mitano wanalazimisha ushindi haramu mradi wanabaki madarakani.

Unaweza ukajiuliza kwa nini walikuwa wanalilia madaraka kama baada ya miaka karibu hamsini wanakiri hakuna Watanzania wenye sifa, uwezo pamoja na uadilifu wa kuweza kuendesha taasisi yoyote ile kwa ufanisi?

Je sababu ni kuwa mfumo kitaifa ni wa hovyo?
Je sababu ni kuwa viongozi kitaifa ni wa hovyo?
Je sababu ni sera pamoja na malengo ni ya hovyo?
Je sababu ni serikali na vyombo vya dola kuwa hovyo?

Au sababu kuu ni kwamba chombo kinachounda serikali hiyo ndicho cha hovyo. Je hicho chombo ni kipi? Bila shaka hata kilaza wa kutupwa hawezi kushindwa kulitaja hicho chombo.

Huu sio mkataba wa kwanza wa aina hii hapa nchini na matokeo yake tumeyashuhudia na kuyaishi...Kwa wana hesabu LCM ya matatizo ndani ya taifa hili ni CCM, Chama cha Mapinduzi, period.

Kuitegemea au kuiamini CCM hiyo hiyo leo itatue matatizo hayo kwa hakika ni uendawazimu! Mkataba huu unatudhihirishia jinsi chama hicho kilivyo na uhaba wa watu wenye sifa, uwezo na uadilifu
 
YOU ARE HOPELESS, MADINI, GESI TUNAPATA NINI? WALIFANYA AKINA NANI SI CCM? WHY TUWAAMINI KWA HILI?
 
Hiyo aya ya pili umeandika kwa kudhamiria kabisaa ? Kwamba
CCM haiwezi kuingia mikataba mibovu
Kwamba CCM haiwezi kuingia katik mikataba inayotutia hasara !
Vili kuhusu mikataba ya RICHMOND,IPTL n.k
Vipi kuhusu baadhi ya eneo katika mbuga ya Ngorongoro linalolalamikiwa kuwa aliuziwa mwarabu na Mh. Mwinyi
Vipi kuhusu mikataba ya ununuzi wa rada,
Vipi kuhusu kununua kivuko kibovu kisha wakakabidhi kwa jeshi ili kisiongelewe !
Vipi kuhusu mikataba ya madini ambapo Taifa linapata mrabaha wa 3% tu pekee
Orodha ni ndefu sana kama unadhamira ya kutetea issue ya bandari tafuta hoja mpya nje ya hapo na wewe unonekana ni wale wale tu
 
Ni kweli Mikataba yote ya Madini, IPTL etc chini ya Utawala wa CCM ilikuwa yenye masilahi mapana kwa Nchi hasa Tanganyika.
 
CCM hakiwezi kuunza nchi, CCM hakiwezi kuingia ktk Mikataba inayotutia hasara, CCM hakiwezi kuingia Mikataba mibovu.
CCM au chama kingine chochote cha siasa ni watu na miongoni mwao ni mafisadi na wala rushwa wakubwa pia wana ushawishi mkubwa, kama walifanikiwa kuuza mineral deposits, gas, wanyama mbugani nk watashindwaje kuuza bandari?
 
Inawezekana mkataba n mzur kwetu.

Selikali badala ya kuwaandama watu jitahidini kujibu hoja....

Toeni elimu Kwa wananchi ....

Mkataba wenye maslah makubwa Kwa nchi kwnn Bunge limetumia massa tu kuujadili???
Ulitaka litumie muda gani, hivi kweli mbunge kama msukuma unataka achambue mkataba?
 
ILI kudhihirisha uongo wao weka mkataba hapa wenye lugha yetu adhimu ya kiswahili ww kama mwanaccm ili kuwaondolea watanzania wenzako na wanaccm sintofahamu juu ya hili jambo.naamin kuanzia leo watanzania wataanza kuwaona hao watu uliowataja ni maadui wa Taifa.Weka ukweli hapa boss.
 
Bila kupepesa macho, aisee wewe ni chawa!
 
Off point!!! Ndiyo mitazamo kama hii inayoliangamiza taifa letu. Watu wametoa hoja kwa kuvitaja vifungu tatanishi vilivyomo kwenye mkataba badala ya kituelimisha uzuri wa vifungu hivyo mnatuletea ngonjera.
 
Tangu ukoloni lami ilikuwepo nchi, shule za boding'i zilikuwa na vitanda, chakula kila siku mablanketi, madaftari kalamu na vitabu, maji ya bomba yalikuwepo na kubwa zaidi shilingi iliyokuwepo nchini ilikuwa na thamani kama ya uingereza, pia usafiri saa 24 kila siku na elimu ya kembriji siyo ya CCM ya kuungaunga kila siku inabadilishwa.
CCM imetuacha nyuma huku viongozi wakiwa mabilionia japo hawawahi kufanya biashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…