Mkuu
Tindo , kwanza naungana na wewe, haki ni kitu stahiki na sio hisani, ndio maana haki haiombwi na hauletewi kwenye kisahani cha chai!, haki hudaiwa na ikibidi hupiganiwa, na gharama zake sometimes hugharimiwa kwa machozi, jasho na damu!. -
Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
Unapoamua kutumia njia ya mkato kwa kualikwa karamuni, na ukaukubali mwaliko, ukakaa mezani karamuni meza Kuu, mkajilia vinono na kukubaliana kugawana nusu mkate, lazima uwe ni mtu wa shukrani!, baada ya kukubali kula fadhila, mtu yule yule hawezi kugeuka na kupeleka watu barabarani kupigania haki.
The right thing to do baada ya maridhiano kuvunjika, ni Mbowe kukaa pembeni, akawapisha wengine, Lissu au Heche ndio waongoze mapambano ya kudai haki.
Mtu ukiwa ni mlafi, unapenda kufakamia mkate, hakuna mkate mgumu mbele chai, lazima utalainika tuu!. Huo mkate wenu baada ya kulainishwa na ule mdomo laini, lipstick Nyekundu, na yale macho legevu, utadhani mtu kala kungu!, hata ningekuwa mimi, kiukweli kabisa lazima ningelainika!.
Mkate mgumu ukiisha lainika, hauwezi kuwa mgumu tena, huo ni laini kama mlenda!.
P