Nakukumbusha mkuu nchi uchaguzi huwa geresha hivyo 2025 kitu pengine kinaweza saidia ni kutiana adabu ila kwa karatasi haiwezekani kamwe kuiondoa CCM.
Uzito wa kuwa na mfedheheko hufanya binadamu kuwa na woga.
Sintofahamu iliyowapeleka CCM kutafuta mbadala kutoka kwa wale wenye Uchu wa madaraka ndio ni huu huu.
Kwa masikitiko makubwa, nadiriki kusema CCM ilipofikia ni lie CCM ya Ben(R.I.P) kuelekea awamu ya pili. Alikuwa hana jinsi bali kutafuta njia ya Kuiacha CCM kileleni, manake alikuwa akiona aibu; kuwa dhamana aliyopewa na Chama ikiwa pamoja na sense of confidence aliyopewa na Mwalimu, Baba wa Taifa ilikuwa inapotea, sio tu machoni mwa Wananchi bali hata moyoni mwake!
Kuwa Mwenyekiti wa CCM sio lele mama na hakuna ambaye anataka aondoke madarakani huku akijuwa ndiye aliyeangusha Chama kikubwa in all sense of the word-Afrika na Duniani chini. The pressure is tremendous na ndio maana nimekuwa nikisema kuwa Vyama hivi vya Siasa, vitafute njia kumega Uzito huo-through Demokrasia ndani ya Vyama vyao. Hili naamini litasaidia kuondoa mzigo anaokuwa nao Mwenyekiti wa Chama na Raisi wa Nchi....Chama peke yake ni balaa(muulizeni Mbowe) sasa fikiria na Urais wa Nchi! Bandugu, najua hili linauma, lakini usongo alioupata Benjamin Mkapa sina haja ya kurudia....naona ndii yanayomtokea SSH-upande mmoja anataka kuhakikisha Kuwa ni Rais na upande mwingine kama Mwenyekiti wa Chama. Kwa siasa za Kileo, one has to give. Sasa katika kuokoa CHama ndimo kunaenda kumuangusha na balaa zaidi ni hili la kuweka dhamana Bandari!
Hakuna geresha, ni mbinu tu tofauti walizotumia kubakia madarakani kila wakati wakivurunda. Safari hii wanafikiri Fedha itawavusha! Wenye akili wameona hilo na wametumia udhaifu uliojitokeza kupenyeza ajenda za Ukoloni mamboleo.
CCM imeshindwa kulinda yale iliyopigania, nayo ni Uhuru wa Uchumi wa Mwafrika.
CCM pekee, inahitaji Revolution.