Mbowe: Masharti ya DP World na Bandari yanazuia Serikali kujitoa, kuahirisha, kusitisha au kuvunja Mkataba

Kama bandari Haina ufanisi ni jukumu la kiongozi kuhakikisha Efficiency inapatikana.

Nyoka akiingia ndani ya nyumba HATUUZI nyumba, HATUCHOMI nyumba, tunamtoa nyoka!!!!

Sa100 must go!!!
Na nyoka mwenyewe ni wa kijani.
 
Shame on you
 
Nakukumbusha mkuu nchi uchaguzi huwa geresha hivyo 2025 kitu pengine kinaweza saidia ni kutiana adabu ila kwa karatasi haiwezekani kamwe kuiondoa CCM.
Uzito wa kuwa na mfedheheko hufanya binadamu kuwa na woga.

Sintofahamu iliyowapeleka CCM kutafuta mbadala kutoka kwa wale wenye Uchu wa madaraka ndio ni huu huu.
Kwa masikitiko makubwa, nadiriki kusema CCM ilipofikia ni lie CCM ya Ben(R.I.P) kuelekea awamu ya pili. Alikuwa hana jinsi bali kutafuta njia ya Kuiacha CCM kileleni, manake alikuwa akiona aibu; kuwa dhamana aliyopewa na Chama ikiwa pamoja na sense of confidence aliyopewa na Mwalimu, Baba wa Taifa ilikuwa inapotea, sio tu machoni mwa Wananchi bali hata moyoni mwake!
Kuwa Mwenyekiti wa CCM sio lele mama na hakuna ambaye anataka aondoke madarakani huku akijuwa ndiye aliyeangusha Chama kikubwa in all sense of the word-Afrika na Duniani chini. The pressure is tremendous na ndio maana nimekuwa nikisema kuwa Vyama hivi vya Siasa, vitafute njia kumega Uzito huo-through Demokrasia ndani ya Vyama vyao. Hili naamini litasaidia kuondoa mzigo anaokuwa nao Mwenyekiti wa Chama na Raisi wa Nchi....Chama peke yake ni balaa(muulizeni Mbowe) sasa fikiria na Urais wa Nchi! Bandugu, najua hili linauma, lakini usongo alioupata Benjamin Mkapa sina haja ya kurudia....naona ndii yanayomtokea SSH-upande mmoja anataka kuhakikisha Kuwa ni Rais na upande mwingine kama Mwenyekiti wa Chama. Kwa siasa za Kileo, one has to give. Sasa katika kuokoa CHama ndimo kunaenda kumuangusha na balaa zaidi ni hili la kuweka dhamana Bandari!

Hakuna geresha, ni mbinu tu tofauti walizotumia kubakia madarakani kila wakati wakivurunda. Safari hii wanafikiri Fedha itawavusha! Wenye akili wameona hilo na wametumia udhaifu uliojitokeza kupenyeza ajenda za Ukoloni mamboleo.
CCM imeshindwa kulinda yale iliyopigania, nayo ni Uhuru wa Uchumi wa Mwafrika.

CCM pekee, inahitaji Revolution.
 
wamemshauri vibaya, na WAtanganyika tunatakiwa kujiimarisha na kujitafakari sana 2025
Unataka kutwambia kiongozi wetu Hana uwezo wa kukataa ushauri mbaya?

Incompetent leader?

Sa100 must go!!!
 
Nakukumbusha mkuu nchi uchaguzi huwa geresha hivyo 2025 kitu pengine kinaweza saidia ni kutiana adabu ila kwa karatasi haiwezekani kamwe kuiondoa CCM.
Mkuu hii ni kauli mbiu yangu humu ndani muda wote, uchaguzi hapa Tanzania ni kupotezeana muda tu, machafuko pekee yake ndio yataondoa huu uhuni.
 
Tumuunge mkono Mbowe na Chadema kwa ujumla wake!

Huu mkataba unapaswa kuwa daraja la kuiondoa CCM na Bunge lake!

Hii inafaa kuwa ticket ya Samia kurudia Zanzibar!

Uhuni ufike mwisho sasa!

#kataawahuni
Usisahau remote iko musonga
 
Tumuunge mkono mbowe mubaguzi, dikiteta hataki kuashia ofs toka 1992 mpaka leo, hivi nyie ufipa mnatuonaje? Mtu anatoa kauli za kiubaguzi wazi wazi loh! nyie chadema wahuni wahuni sana.
SAMIA MPAKA 2023
 
Nyerere aliambiwa ukweli kwamba Tz ni Taifa la mauti/marehemu.
Loliondo
Ngorongoro
Kia, leo wanauza Bandari afu mijitu tupo tunashanga?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…