Mbowe, mkanye Lissu

Mbowe, mkanye Lissu

Lisu anaandika yaliyo moyoni mwake, mimi nimemuelewa kuwa hataki unafiki. Ningeshangaa sana kama Lisu angemsifia JPM na kwa kweli angekuwa mnafiki wa hali ya juu.
Wapo watu humu wanajifanya kumlilia JPM hadharani lakini ungeweza kufungua mioyo yao ungeona unafiki mtupu; nadhani ndiyo maana serikali iliamua kutangaza kwa nguvu zote kuwa kipindi hiki watu wasifanye sherehe yoyote. Kwa utamaduni wetu hatukupaswa kuambiwa hili kwani kwenye majonzi huwa hatufanyi sherehe lakini hadi serikali inaamua kutangaza hivyo basi iliona kuwa kuna watu watafanya sherehe na hao hao kabla ya msiba walikuwa mbele kusifia.
Ni suala la muda tu yote yataisha
 
Meko kafa huku Lissu (aliyekuwa amepangiwa na kina farao afe) bado yu hai. Huyo ndiye Mungu!
Kwani kufa ni adhabu? Mbona hamtaki kumaliza masomo ya shule za msingi kabla ya kujiunga na kumbi kama hizi?
 
Kwani kufa ni adhabu? Mbona hamtaki kumaliza masomo ya shule za msingi kabla ya kujiunga na kumbi kama hizi?
Kama kufa si adhabu mbona alimmiminia mwenzie risasi 16? Ona sasa kilichomfika!
 
Afadhali umenena, kuna siku nilikuta katweet mambo ya ajabu kuhusu Mh. Rais nikadhani ni account feki.

Hadhi yake na anayoandika hayaendani kabisa.

Alipaswa kuandika ideas na sio kumgeuza chigogwo role model wake.

Huwa simkubali lkn siku hizi anazidi kuwa mweupe sana. Mwambieni atulie aandike vitu ambavyo hata wajukuu wa taifa hili wakisoma waseme huyu ni mtu aliyewahi kuwepo nchini nap kuleta tija

Kama mwanaharakati sawa ila Kama presidential candidate aibu aisee
Hayo mambo ya hadhi hebu weka pembeni kwanza. Subiri amalize!
 
kama mnakumbuka kipindi cha Bunge la Katiba Tundu Lissu alimtukana Hayati Mwalimu Nyerere sasa yupo tena Hayati Magufuli, naamini angekuwa na fedha anamdai pia angeenda kumshtaki hayati. Eti huyu alitaka kuwa Rais wa Tanzania shame on him
 
Popote ulipo mwenyekiti wa chama.

Tunakufikishia salamu hizi sisi Watanzania tusio na chama na wanachama wa CHADEMA.

Mwambie Tundu Lissu akae kimya wakati huu, aache tabia za kuropoka ropoka na kujibishana asiye jibishane naye.

Mwambie kwenye msiba tamaduni zetu ni kuungana na kua wamoja huo utofauti anaoulazimisha utazidi kumuumbua na kukiumbua chama chenu.

Mwambie hata kama ana uchungu na kisasi kwa yale aliyofanyiwa mwambie kwa nafasi yake hastahili kufanya anayoyafanya labda kama hana mpango wakugombea.

Mwambie anaharibu image ya chama, kama anajua hatarudi wala kugombea mwambie anawaponza wenzake. Mbona wewe (Mbowe) hupost post au anadhani huna bando au smartphone?

Mwambie au mumkanye adharani au mumfute uanachama. Tundu Lissu behave like gentleman.
Ungekuwa ni wewe ulipigwa risasi ukanusurika kufa ungepangiwa cha kuongea? Ungekuwa ni wewe umefanyiwa uonevu unyanyasaji uovu kibao ikiwemo kubambikiwa kesi kibao kisha upangiwe cha kuongea ungekubali? Ebu jaribu na wewe upitie mateso kama aliyopitia Lisu ndipo utajua kuwa alichokiandika hapo juu hukuzingatia haki za binadamu zaidi ya kusaka uteuzi kwa njia haramu za kishetani.
 
kama mnakumbuka kipindi cha Bunge la Katiba Tundu Lissu alimtukana Hayati Mwalimu Nyerere sasa yupo tena Hayati Magufuli, naamini angekuwa na fedha anamdai pia angeenda kumshtaki hayati. Eti huyu alitaka kuwa Rais wa Tanzania shame on him
Aliyekuwa Rais Mbona hakutumia demokrasia kama mkapa na kikwete? Kutumia wasiojulikana kupiga watu risasi ndiyo kaleta tabu zote hizi , kuwatumia task force kupora mali za watu, kufunga biashara za watu, Account za watu kuwapora cash zao kuwatishia kuwabambikia kesi za utakatishaji fedha uhujumu uchumi , huyo ndiyo Rais bora?
 
Vaa uhusika wake na upigwe risasi 16, uvuliwe ubunge, unyimwe stahiki zako zilizopo kikatiba!!!. Bado mwenye mamlaka hakuguswa na lolote kuhusu yeye afu unataka ahuzunike na nini kuhusu yeye? Tunaolia ni sisi tusiojua ubaya wa marehemu tuendelee kumlilia ila sio tulazimishe vilio nyeti viwe vya kila mtu.
Ukiona mtu anashabikia Unyama unyanyasaji mateso aliyofanyiwa Tundu na utawala wa marehemu ujue huyo mtu ni mnufaika kupitia huo mfumo mateso, wanufaika wote sasa hawana Amani hawajui mama anawaza nini juu yao
 
Huyo anaweza akarudi Tz wananchi wenye hasira Kali wakamuteka bila serikali kujua
Hakuna mwananchi mjinga kiasi hicho wananchi wenye Akili timamu wanajua machungu ya kunusurika kuuawa wanafahamu machungu ya kubambikiwa kesi, uonevu unyanyasaji uovu wote aliofanyiwa Tundu lisu
 
Ungekuwa ni wewe ulipigwa risasi ukanusurika kufa ungepangiwa cha kuongea? Ungekuwa ni wewe umefanyiwa uonevu unyanyasaji uovu kibao ikiwemo kubambikiwa kesi kibao kisha upangiwe cha kuongea ungekubali? Ebu jaribu na wewe upitie mateso kama aliyopitia Lisu ndipo utajua kuwa alichokiandika hapo juu hukuzingatia haki za binadamu zaidi ya kusaka uteuzi kwa njia haramu za kishetani.
Natamani lisu aseme zaidi kwa upande ule wa (wasiojulikana)
Baada ya mch. Mtikila sasa yupo lisu, asiposema lisu kuna mzalendo gani mwingine anaweza sema na hata kujulikana wote waliokuwa (wasiojulikana)?

Ni kama kuna fukuto mioyoni, kuna vitu vingi watu wanatamani kuujua ukweli na kuona hatua stahiki zikichukuliwa.
 
Ni wazi jamaa alikuja kugombea ili kulipiza kisasi, vizuri hakufanikiwa maana ingekuwa hatari zaidi.
Sasa hivi huwezi amini kama ni Mzee wa miaka 50+, ni kama mtoto wa miaka 15 hivi. Anahitaji counseling na maombi maana mentally hayuko fit. Nashauri ni muda sasa yule rafiki ambaye ni Askofu, atumie muda kumuombea sana ili kumponya kiroho.
Wewe ndiyo huna Akili hata za kuazima tu kwa polepole, Yaani ulitaka mtu apigwe risasi aporwe ubunge anyimwe haki zake abambikiwe kesi kibao kisha akae kimya? akae kimya ili iweje? Unyanyasaji unyama wote huo haujauona? Acha kujitoa fahamu kiasi hicho
 
Natamani lisu aseme zaidi kwa upande ule wa (wasiojulikana)
Baada ya mch. Mtikila sasa yupo lisu, asiposema lisu kuna mzalendo gani mwingine anaweza sema na hata kujulikana wote waliokuwa (wasiojulikana)?

Ni kama kuna fukuto mioyoni, kuna vitu vingi watu wanatamani kuujua ukweli na kuona hatua stahiki zikichukuliwa.
Ulaya America wameendelea kwa kuambizana ukweli la cha ajabu Tanzania msema ukweli huwa Adui wa CCM na hata kupigwa risasi
 
Sasa walio mpiga risasi mbona Ni Ngozi nyeupe ili wachafue inchi kama walivyo fanya inchi Za kiarabu
Hii propaganda ni ya enzi zileee zamani sana wakati watanzania wamelala hawajaamka, sasa Tambua kuwa watanzania wana upeo mkubwa hizo propaganda zibakize huko huko kwa akina Le mutuz watu wenye IQ ndogo
 
mwendo ni ule ule kasi mpya ari mpya msitegemee mtelemko HAPA KAZI TU
Kazi kazi ni jambo jema lakini uonevu unyanyasaji mateso manyanyaso kwa wapinzani wakiiga vya marehemu lazima wataishia kufeli zaidi, warithi mazuri pekee yale mabaya waache azikwe nayo mwenyewe
 
Mimi nashauri aendelee hivyo hivyo kuropoka, atafanya nini zaidi ya hilo? Hebu mwacheni mbaba wa watu azidi kutema nyongo. Inapunguza machungu

Sent from my Infinix X5515 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom