Mbowe na siasa zake za "I am the only negro incharge in here"

Mbowe na siasa zake za "I am the only negro incharge in here"

Huko walikopita wameacha hamasa gani?Operation wanazofanya akina Mbowe ni utapeli na uhujumu kodi za wananchi. Wananchi wamechoka na ccm na hakuna asiyejua ubaya wa ccm saizi.Kinachotakiwa ni mass action tu na sio kuendelea kuleta porojo. Swala l bandari halikuhitaji porojo zaidi ya Mbowe kuitisha maandamano nchi nzima. Huko Kenya mbona hatusikii porojo za kutoa elimu wanapokua na jambo lao?Bei ya unga imepanda,Odinga ye ni kuwaingiza wafuasi wake barabarani. Hakuna porojo kama za akina Mbowe huku
Mazingira ya kisiasa na utamaduni wa kisiasa yametofautiana sana kati ya Kenya na Tz.
 
Ni maoni na mawazo yako, binafsi nayaheshimu...

Lakini bado, hii siyo hoja ya kuitumia kuilaumu CHADEMA na Freeman Mbowe kama ndiyo kikwazo cha wengine kuliamsha kwa namna yao na kwa njia zozote zile halali...

Mtu kama Dr Wlbroad Slaa anatoa wapi political moral authority ya kutoa maagizo kwa taasisi kubwa kama CHADEMA huku historia ya siasa za usaliti dhidi ya wenzake haohao ikimsuta?

Na wakati huohuo ukumbuke kuwa, siasa za ki - Afrika zikiwemo za kwetu Tanzania ni za utata sana na kubebwa na watu watata sana kama huyu Dr Wlbroad Slaa..

Anaweza kujitokeza mtu na kujifanya ni mwanaharakati na mpambanaji mpigania haki mwenzenu na akaonekana hivyo kwa macho ya damu na nyama, lakini kumbe ni kibaraka na ni mkono wa walewale mnaopambana ulingoni...!

Nina maana kuwa, ktk kila hatua ya maamuzi ya kisiasa ndani ya taasisi makini kama CHADEMA, umakini ni wa lazima sana kuepuka kujikuta mmejitia kitanzi wenyewe kwa uamuzi wa kipupa...

Ilisemwa zamani kuwa si vyote ving'aavyo ni dhahabu na wahenga wengine walisema; it's better late than never..."

Freeman Mbowe na CHADEMA wako sahihi na kwa kweli ni mjinga pekee anayeweza kuwalaumu CHADEMA kwa kukataa kupewa maagizo na amri na watu kama kina Dr Slaa ambaye moral authority yake kisiasa ina mashaka makubwa..!

However, bado hakuna kilichoharibika. Muda bado upo. Warudi kwenye drawing board na waweke mikakati ya pamoja...

By the way, mtu kama Wakili Boniface Mwambukusi na Mdude Nyangali mbona ni wanachama active wa CHADEMA!
..!!

Inakuwaje wanatumia jukwaa jingine kusukuma ajenda zao hizo nje ya utaratibu wa kichama na mwisho wa siku wanarudi tena chamani na kuanza kukilaumu kuwa hawaungi mkono mambo yao? Mbona kama haiingii akilini vile?
MBOWE ni msaliti hilo halitaki elimu ya PHD.
Ni manyumbu tu ndio kawashika akili.
Alituletea aliyemwita fisadi mkuu aje agombee Urais kupitia UKAWA. yaani Umoja wa Katiba ya Wananchi.

Wakati huyo Lowasa hakuwa hata na mpango na hiyo katiba ya wananchi. Alipokatwa CCM akakimbilia UKAWA kwa vipande vya pesa akanunua ugombea urais usiopingwa wala kushindanishwa.

Bila aibu leo manyumbu wake mnamtukana Dr Slaa eti ni msaliti
wakati msaliti wa kweli ni Mbowe.
 
Mbowe na Chama chake wanafanya siasa za kujiandaa kushika dola.

Siasa ambazo ACT-Wazalendo imefanikiwa kulinganisha Chadema.
 
Mwamba tumeshamzoea na Speeches zake nzuri nzuri za hamasa. Ni kweli kipaji cha kuzungumza anacho, anavutia kusikiliza. Lakini utamu wa speeches zake hautupi katiba mpya, tume huru ya uchaguzi wala kuzuia bandari zetu kwenda kwa mwarabu. Tunataka chama kiunge mkono next level ya struggle ambayo ni mass action,

Miaka 20 ya kukaa kwenye uwenyekiti wewe unaongea tu, unaongea tu, unaongea tu. Sasa leo wananchi wanataka kuraise stake juu, beef up the ante, kubonyeza kitufe cha kuongeza joto kwa CCM, na katika kuwezesha hilo tunahitaji kushirikiana na Taasisi ya Chadema ambayo na sisi kuna jasho letu humo wewe unakuja na blahblah za oooh, hamkunishirikisha, ooooh sisi siyo pressure group, kama siyo pressure nyie ni nani, ni kundi la wacheza singeli na vigodoro au kitu gani?

Hii naivety ya Mwenyekiti ya namna ya kudeal na CCM inaturudisha nyuma sana.
Hahahaha hahaha
Mkuu nimecheka si kwa sababu ninacheka ujumbe wako, la hasha. Bali umeongea point kubwa, ngumu na yenye mantiki kubwa. Umeongea kwa lugha ya mwalimu anayewahamasisha wanafunzi wake kabla ya kuingia kwenye final exams, umeongea kama kocha wa basketball anayewahamasisha wachezaji ktk last quarter.

CHADEMA kina mamluki wengi ndo maana unaona wengi waliokuwemo humo wakarudi zizini wamepewa nafasi kubwa ndani ya chama na serikali. Ninaowona kuwa serious ni Lissu, Boniface Jacob, Lema, Masese na Erythrocyte kwa nafasi ya juu huko.


Institutionally CHADEMA inapaswa kwa sasa kuziba ombwe la mkwamo huu wa kisiasa na kiuongozi kwa kuja na mikakati inayojenga ari, uthubutu na uzalendo kwa wananchi kuikataa dhambi (CCM) kivitendo.

Upo sahihi
 
Kila zama na mambo yake, kwa mika 20 Mbowe amafanikiwa kuijenga Chadema kama taasisi imara, na hiyo itabaki kuwa legacy yake.

Sasa baada ya ukuaji na kujiimarisha chama kinahitaji kufanya kazi yake muhimu ya kushika dola, na kwa hakika Mbowe hana speed hiyo.

Kabla ya kuwekwa mahabusu kulikuwa na vuguvugu kubwa kuhusu katiba mpya, nq nilitegemea kungekuwa na nguvu ile ile pengine zaidi baada ya kesi yake kuisha, ila ni tofauti, baada ya kutoka speed yote ikazima mpaka leo.

Mbowe anapunguza speed ya mabadiliko, na hilo ndio furaha ya chama tawala.
 
Mazingira ya kisiasa na utamaduni wa kisiasa yametofautiana sana kati ya Kenya na Tz.

Labda kama una maana Kenya hawana adui wala rafiki wa kudumu. Pia Kenya vigogo huhamasisha na kushiriki maandamano.

Kauli za mazingira tofauti ni potofu.
 
Wanasiasa wengi Afrika, ni wezi, wanafanya primitive accumulation of wealthy, kwao siasa is a "means to an end" Kupiga pesa, kupata influence, na power,
 
MBOWE ni msaliti hilo halitaki elimu ya PHD.
Ni manyumbu tu ndio kawashika akili.
Alituletea aliyemwita fisadi mkuu aje agombee Urais kupitia UKAWA. yaani Umoja wa Katiba ya Wananchi.

Wakati huyo Lowasa hakuwa hata na mpango na hiyo katiba ya wananchi. Alipokatwa CCM akakimbilia UKAWA kwa vipande vya pesa akanunua ugombea urais usiopingwa wala kushindanishwa.

Bila aibu leo manyumbu wake mnamtukana Dr Slaa eti ni msaliti
wakati msaliti wa kweli ni Mbowe.
Sina hakika kama unaelewa mantiki ya hiki ulichokiandika hapa...

Unasema kuwa Freeman Mbowe na CHADEMA ni wasaliti kwake kwa sababu ya Edward Lowassa wa 2015...

Well. Kama anatambua hilo, anatafuta kitu gani tena huko? Amesahau kitu gani tena huko CHADEMA kiasi cha kuanza kulilia msaada wao kwenye harakati zake za kisiasa na hao wenzake?

Je, umeweza sasa kuona kuwa hoja yako hii haina connectivity ya kimantiki kabisa?

Na jibu ni moja tu kuwa, likey Dr Wlbroad Slaa hana nia njema na CHADEMA na ndiyo maana watetezi wake mnajichanganya bila hata kujua...

Na huu sasa ndio unyumbu halisi..!!
 
Sina hakika kama unaelewa mantiki ya hiki ulichokiandika hapa...

Unasema kuwa Freeman Mbowe na CHADEMA ni wasaliti kwake kwa sababu ya Edward Lowassa wa 2015...

Well. Kama anatambua hilo, anatafuta kitu gani tena huko? Amesahau kitu gani tena huko CHADEMA kiasi cha kuanza kulilia msaada wao kwenye harakati zake za kisiasa na hao wenzake?

Je, umeweza sasa kuona kuwa hoja yako hii haina connectivity ya kimantiki kabisa?

Na jibu ni moja tu kuwa, likey Dr Wlbroad Slaa hana nia njema na CHADEMA na ndiyo maana watetezi wake mnajichanganya bila hata kujua...

Na huu sasa ndio unyumbu halisi..!!
Dr Slaa hajaitafuta CHADEMA na wala hajaonba kurudi CHADEMA.
Wazalendo wa kweli Dr Slaa, Adv Mwabukusi, Mdude nk baada ya kuona inchi inaingizwa kwenye mikataba ya kilaghai huku vyama vya siasa vikiwa kimya ndipo waka form hicho kinachoitwa Sauti ya Watanzania.
Lengo ni kuunganisha nguvu za vyama vyote na hata taasisi zote kuungana kudai katiba mpya nakupinga uuzwaji wa bandari.

Mbowe Kagoma kushirikiana na sauti ya watanzania kupinga uuzwaji wa bandari wala kudai katiba mpya.
Anadai hakushirikishwa!
Buliaga alienda kufanya nini?

Hadi hapo bado huoni usaliti wa Mbowe?
Huoni km anamaslahi binafsi ktkt hili na sio maslahi ya kitaifa?
 
Bado hujui usemalo..!
Dr Slaa hajaitafuta CHADEMA na wala hajaonba kurudi CHADEMA.
Wazalendo wa kweli Dr Slaa, Adv Mwabukusi, Mdude nk baada ya kuona inchi inaingizwa kwenye mikataba ya kilaghai huku vyama vya siasa vikiwa kimya ndipo waka form hicho kinachoitwa Sauti ya Watanzania.
Well and good. Mpaka hapo hakuna shida. Ni haki yao kabisa
Lengo ni kuunganisha nguvu za vyama vyote na hata taasisi zote kuungana kudai katiba mpya nakupinga uuzwaji wa bandari.
Wameshaunganisha vingapi? Ni kipi na kipi kwa majina?
Mbowe Kagoma kushirikiana na sauti ya watanzania kupinga uuzwaji wa bandari wala kudai katiba mpya.
Anadai hakushirikishwa!
Ooh, kumbe ni Mbowe ndiye kagoma na sio CHADEMA? Sasa kama kweli hakushirikishwa, shida yako ni nini? Si urudi kwake Tena ili umshirikishe vizuri aone kama anaweza kushirikiana nawe au la?
Hadi hapo bado huoni usaliti wa Mbowe?
Unaelewa hata maana ya maneno "Usaliti" na "msaliti" kweli wewe? Kukataa kuridhia ombi lako yawezekana vipi iwe ni usaliti?
Huoni km anamaslahi binafsi ktkt hili na sio maslahi ya kitaifa?
Kwani akiwa na maslahi binafsi Kuna shida gani? Wewe huna maslahi yako binafsi?

Fikiri kwanza unapojenga hoja ndipo useme au uandike. Hapa unaoendelea kujichanganya tu Kwa sababu hakuna mantiki ya Kila unachoandika!!
 
Bado hujui usemalo..!

Well and good. Mpaka hapo hakuna shida. Ni haki yao kabisa

Wameshaunganisha vingapi? Ni kipi na kipi kwa majina?

Ooh, kumbe ni Mbowe ndiye kagoma na sio CHADEMA? Sasa kama kweli hakushirikishwa, shida yako ni nini? Si urudi kwake Tena ili umshirikishe vizuri aone kama anaweza kushirikiana nawe au la?

Unaelewa hata maana ya maneno "Usaliti" na "msaliti" kweli wewe? Kukataa kuridhia ombi lako yawezekana vipi iwe ni usaliti?

Kwani akiwa na maslahi binafsi Kuna shida gani? Wewe huna maslahi yako binafsi?

Fikiri kwanza unapojenga hoja ndipo useme au uandike. Hapa unaoendelea kujichanganya tu Kwa sababu hakuna mantiki ya Kila unachoandika!!
Basi sawa,
Wewe humuamini Dr Slaa
Mimi simuamini Mbowe
 
Basi sawa,
Wewe humuamini Dr Slaa
Mimi simuamini Mbowe
Haa haa 🥺

Umenena vyema. Lakini mimi niko tofauti kidogo na nitakushangaza kwa kusema..

Nyakati zingine naweza nisimwaamini yeyote na pia wakati mwingine naweza kumwaamini yeyote. Waswahili husema......inategemea....

Na actually, hii ndiyo sifa anayopaswa kuwa nayo binadamu yeyote aliye perfect..

Wa kumwaamini kwa 100% siku zote ni mmoja tu. Ni Mungu muumba pekee..!!

Kwa heri na Asante kwa kushiriki mjadala..
 
Haa haa 🥺

Umenena vyema. Lakini mimi niko tofauti kidogo na nitakushangaza kwa kusema..

Nyakati zingine naweza nisimwaamini yeyote na pia wakati mwingine naweza kumwaamini yeyote. Waswahili husema......inategemea....

Na actually, hii ndiyo sifa anayopaswa kuwa nayo binadamu yeyote aliye perfect..

Wa kumwaamini kwa 100% siku zote ni mmoja tu. Ni Mungu muumba pekee..!!

Kwa heri na Asante kwa kushiriki mjadala..
Mkuu nazungumzia ktkt huu mjadala ulio hapa jamvini.
Wewe humuamini Dr Slaa
Mimi simuamini Mbowe
 
Back
Top Bottom