#COVID19 Mbowe ni nani hadi atangaze vifo vya wagonjwa wa Corona?

Acha kuchonganisha watu! Yeye katangaza msiba wa kaka yake wewe unasema katangaza wagonjwa wanaokufa na sasa ulitaka afiche ugonjwa ulomuua nduguye ili iweje? Kama mtu kapewa mamlaka kama msemaji wa familia huwezi tangaza msiba wa mtu bila kutaja chanzo chake!
Tujiepushe na uchochezi na uchonganishi zama zake zimeshapita!
 
Alitangaza yeye kwamba amepata chanjo na hakuna aliposema na kaka yake pia alipata chanjo. Tusichanganye mafaili
 
sisi yanatuhusu nini sasa.hayuhusu na sisi tuna ya kwetu mbona hatuyatangazi humu ndani.
Akitangaza wewe inakuhusu nn mpaka kupiga makelele kwenye mitandao! Kama hayakuhusu unapiga kimya tu!!
 
Kwani yeye anazo chanjo za kuchanja watu?

Hujui serikali haitaki chanjo kuingizwa nchini?

Serikali haiwezi kukwepa lawama kwa vifo vyote hivi tokea enzi za michai chai, nyungu, malimao na upuuzi wote wa awamu ile.
Lakini mbowe amechanjwa
 
Nawasalimia wakuu wachangiaji wa uzi huu
 
Mkuu

Huyu ni wakala wa usambazaji wa dawa na chanjo za UVIKO kwa hiyo kutangaza hivyo ni kuonesha uhalisia ya mahitaji yanavyohitajiwa
 
Sheria ya nchi gani hiyo ambayo inazuia hata familia kuongelea ugonjwa uliomwua ndugu Yao. Wee subiri siku ikitokea kwenu usitangaze. Kama hospitali waamethibitisha Hilo kuna Shida gani familia kuelezana. Mwisho tutaanza kupangiana hata ni siku ngapi tulale na wake zetu.
Hivi hizi siasa za kipumbavu watanzania zinatusaidia nini?
 
Nafikiri dhambi ni kutotangaza kafa kwa ugonjwa gani....

Ila yupo sahihi sana kwa kutuamsha kwa kuwa inabidi tuwe waangalifu...
Ila kama anamlengo wa kisiasa hiyo ni juu yake.
 
Kama amekufq kwa ukimwi ,malaria je?
 
Kijoogodi hii sentensi yako imenipa raha umenikumbusha mbali sana

Nanukuu

Licha ya hivyo Mbowe haaminiki mbele ya uma wa Tanzania tokea siku ile alipoangushwa na konyagi alafu akaitangazia dunia kuwa amepigwa na wasiojulikana ili tu apate kiki kisiasa.

Ila Mkiti msanii sana yani alileta taharuki kumbe alikuwa na mchepuko

Nitacheka mpaka kesho
 
Mbona kuna ndugu zake waliokufa kwa magonjwa mengine lakini hakutangaza?

'Think long-distance; act short distance for risk avoidance.'
 
Wewe shida yako ulitaje tu hilo jina la Mbowe.
Uzi wenyewe unamuhusu Mbowe halafu wewe unashangaa mimi kumtaja Mbowe? Mbowe ni binaadamu tu kama mimi na wewe sasa sijui unaona shida gani akitajwa au mwenzetu Mbowe ni zaidi ya binaadamu kwako?
 
Kwani kaka yake au kaka yangu akifa kwa corona ndio nini? What is sospecial??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…