Pre GE2025 Mbowe: Uchaguzi wa kwanza Lissu akiwa CHADEMA nilimpa gari yangu akafanyie kampeni. Nyumba ya Dodoma nilipewa na Serikali, nikampa yeye

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Watoto wadogo na washamba ndio mnamhusisha Mbowe na pesa za Abdul. Kwa taarifa yako Mbowe ni tajiri tangu Mwalimu Nyerere anafundisha Pugu Sekondari! Nini Abdul! Ahahahahaha!!!
Hiyo historia tunaifahamu labda wafundishe watoto wenzako huko CCM.
 
Haahaa hizo ndo sera zake za kutaka uongozi? Mbowe akili zimepotelea wapi? Amwage sera asilielie
 
Lissu kumbe hana uungwana kwa kiwango hiki.
 
Hata Lisu akipata huu uongozi utamtesa,alipaswa kuweka akiba ya maneno,leo anasema biashara za Mbowe hazina TIN kumbe alikuwa anatumia magari ya mtu asiye na TIN.Kama anamfanyia hivyo Mbowe wasio na uwezo itakuwaje!!?
 

Leo hii Mbowe kama Dj tu na form four failure au sio? hata shukurani mnakosa, ila tafuteni chama cha kwenda CHADEMA sio
 
Ni Kama anaweka zuio kistaarabu ili zisije kuvuja zaidi.
Upo sahihi sana ndugu Gautten Potten .
Mbowe anamjua Lissu vyema sana na anajua kuwa Lissu anazo siri zake nyingi sana, na ushahidi juu.

Mbowe anaogopa sana kwamba Lissu anaweza "kuropoka" mambo yake makubwa sana yatakayoishtua Taifa, hivyo anachojaribu ndio hicho cha kumsihi kistaarabu kuwa akumbuke fadhila zake za huko nyuma ili Mbowe asitiriwe.

Naamini Lissu akiwa provoked zaidi na Team FAM, anaweza kuendelea kutumia WMD zake kama ile moja ya "vikao vya siri kwa siku tatu".

Lissu anajua kucheza kete zake vyema na Mbowe analijua hilo, na linamuogopesha sana sana.
 
Kuna waziri aliwahi kuhonga nyumba ya serikali kwa hawara yake.

Kuna waziri aliwahi gonga gari ya serikali (gari ya waziri) ikiwa na namba binafsi akiwa anaendesha yeye na pembeni amekaa kimada wake.

Tanzania kila kitu kinawezekana.
 
Watoto wadogo na washamba ndio mnamhusisha Mbowe na pesa za Abdul. Kwa taarifa yako Mbowe ni tajiri tangu Mwalimu Nyerere anafundisha Pugu Sekondari! Nini Abdul! Ahahahahaha!!!
Pesa haijawahi kutosha hata siku moja, tena sana sana kwa mwenye fedha nyingi sana.

Ukishakuw tajiri, kila fursa unayoiona na kuipata ya kutengeneza shilingi kumi, utaitumia vyema hiyo fursa, sembuse fursa ya kupata fedha za bure ambazo ni kodi ya Watanzania!!
 
Napata taabu sana kuamini maneno yanayoandikwa kuwa yamesemwa na Mbowe mpaka nipate kuyasikia na kumuona akiyanena hayo, maana nimejiuliza sana FAM yule yule ninayemfahamu ndiye huyu huyu anayeongea haya kweli!!???

Busara zake zimeenda wapi!!??

Ama kweli madaraka hupofusha.
Ama kweli fedha hupofusha.
Ama kweli rushwa hupofusha macho, akili, mwili, roho, nafsi, mdomo,masikio na mwili mzima.

Ndugu yangu kaka Mbowe vipi kuhusu ile Zaburi 1: 1 -6 uliyowahi kuniambia nilipokutambulisha kwa shemeji yangu ambaye alikuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa mwaka 2014!!???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…