Mbunge Condester Michael atimuliwa Bungeni kwa kuvaa ovyo. Spika awaagiza askari wa bunge kuwazuia getini wavaa ovyo

Mbunge Condester Michael atimuliwa Bungeni kwa kuvaa ovyo. Spika awaagiza askari wa bunge kuwazuia getini wavaa ovyo

Mbunge wa Momba Condester Michael Sichalwe ametolewa ndani ya ukumbi wa Bunge ili akabadilishe mavazi yake baada ya Mbunge wa Nyangw'ale Hussein Nassor Amar kuomba muongozo wa Spika kuwa kuna baadhi ya Wabunge wamevaa mavazi yasiyo na maadili.

Spika baada ya kumuamrisha kuondoka Bungeni pia aliwaambia askari wa Bunge, kuanzia sasa mbunge yeyote atakaevaa mavazi yasiyo na Staha na kinyume na kanuni waishie getini. Sakata hilo lilianza kwa mbunge mwenzake kuomba muongozo wa spika akimtolea mfano kama mbunge aliyevaa mavazi yasiyo na staha.



Mbona haijabana!!!! Hao wazee vipi!!!! Yaani inaonyesha aina ya wabunge tulio nao. Watajadili masuala muhimu ya taifa kweli? Ubaya wa hiyo suruali sijauona kabisa!!!! Wazee wasichaguliwe kuingia bungeni!!!!
 
Fisi wakikosa windo wanakulana[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Thanks but no thanks. Vaeni nyie sie dada zetu na wake zetu watavaa wanavyoona wanapendeza. Kuvaa baibui na hijab hakumaanishi kuwa mvaaji ni mtakatifu. Mbona Zanzibar na Pemba kuna wakina dada wengi wanajiuza wakiwa wamevaa baibui na hijab?

Amandla...

Huoni ukiwa umevaa vazi la hijab na baibui hakuna mwanaume atakae kutamani!!!!! Lakini dada zenu mnawaachilia hovyo na vinguo vinaonyesha ndani, chupi, sidilia, mipaja yote wazi, nywele zimesimama kama mwendawazimu, kiufupi nguo mnazowaachia dada zenu/mama zenu ni aibu, na ndiomaana wana shawishika kwa wanaume na hupelekea kubakwa na kutongozwa. Hii sio sifa ya mwanaume kuwaachia dada/mama zako wakijiachia. Watu wa ajabu nyie sijapata kuona, mpo kidunia zaidi.


Wangelikuwepo wakina ottoman empire/Sultan/Eturgrul n.k mngenyooka tu.
 
Huoni ukiwa umevaa vazi la hijab na baibui hakuna mwanaume atakae kutamani!!!!! Lakini dada zenu mnawaachilia hovyo na vinguo vinaonyesha ndani, chupi, sidilia, mipaja yote wazi, nywele zimesimama kama mwendawazimu, kiufupi nguo mnazowaachia dada zenu/mama zenu ni aibu, na ndiomaana wana shawishika kwa wanaume na hupelekea kubakwa na kutongozwa. Hii sio sifa ya mwanaume kuwaachia dada/mama zako wakijiachia. Watu wa ajabu nyie sijapata kuona, mpo kidunia zaidi.


Wangelikuwepo wakina ottoman empire/Sultan/Eturgrul n.k mngenyooka tu.
Wishful thinking! Hawapo hao!!!
 
Huoni ukiwa umevaa vazi la hijab na baibui hakuna mwanaume atakae kutamani!!!!! Lakini dada zenu mnawaachilia hovyo na vinguo vinaonyesha ndani, chupi, sidilia, mipaja yote wazi, nywele zimesimama kama mwendawazimu, kiufupi nguo mnazowaachia dada zenu/mama zenu ni aibu, na ndiomaana wana shawishika kwa wanaume na hupelekea kubakwa na kutongozwa. Hii sio sifa ya mwanaume kuwaachia dada/mama zako wakijiachia. Watu wa ajabu nyie sijapata kuona, mpo kidunia zaidi.


Wangelikuwepo wakina ottoman empire/Sultan/Eturgrul n.k mngenyooka tu.
Wewe nawe kwani kutongozwa dhambi? Si amkatae tu mwanaume kama hampendi... Mfundishe mkeo/ mwanao/ dada zako kukabiliana na yaliyopo duniani. Wafundishe kujitambua na kusema NO. Kuna wanaume wanabaka bibi zao, watoto zao huko nako wameona nini cha kuwavutia?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Yupo sawa kabisa, hongera yake. Kwanzia leo watavaa kistaarabu.
haiongezi chochote wala haipunguzi chochote, na hizo sio suala la msingi sana kulifanya bungeni kuliko kufanya mambo yenye maslahi mapana kwa wananchi. wabunge wana nini cha kujivunia? tabia njema? wakati wakitoka pale getini wanafanya mambo ya ajabu, mioyo imejaa uchafu ila kwa nje ndio wanataka wajifanye wasafi? watu kibao hao wanaloga, wanakula hadi uchafu wa ajabu ili wapate huo ubonge, kila mtu hapo ana siri zake, halafu wanataka kujifanya watakatifu? wakitoka tu kwenye geti hapo hata hao wengine wanavaa nguo za ajabu na wanafanya mambo yakifirauni balaa. ngoja mtu aishi vile alivyo moyoni, sio kwa kuigiza. na hivyo ndivyo sote twahukumiwa hata mbele za Mungu.
 
Hivi mavazi yanaingilia uhuru wa mwingine ? Wewe unapungukiwa nini mti mwingine kuvaa anavyojisikia. Tunapinga umagharibi kwa kutetea umagharibi.
Wapi haki ya vazi la masai, kwa nini tutukuze mila za kiarabu na kizungu.
Waafrika mavazi yao ya asili mwili 80% unakuwa wazi leo umagharibi umetawala wabunge. Sheria zingine za mkoloni sie tunasema za bunge.
Hizo sheria zilizingatia mavazi ya kiafrika pindi zinatungwa na mkoloni ?
 
Uvaaji wa mtu it got nothing na kile kinachofanyika ndani ya Bunge,wapiga kura wanataka kusikia mbunge wao anawatetea vipi sio kavaa nini,mbunge huyu aliyesababisha naye ana matatizo ya kisaikolojia ,kabla ya kuzungumzia hii issue bila shaka mind yake ilimpeleka kwenye sex
Salamu wakuu, Hebu na mm nitie neno juu ya suala hili. Ukifika jimbo LA Nyang'hwale liko huko Geita utahuzunika na umasikini uliokithiri pale. Lkn ndo watz tujifunze namna bora ya kuchagua wabunge wasomi wenye impact chanya majimboni kwetu. Huuyo Hussin in kundi LA kina Joseph Msukuma. Wote majimbo yao yako mkoa mmoja.
Mhandisi Everist Ndikilo aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Pwani aliwahi kugombea ubuge katika Jimbo hilo lakini hakufanikiwa katika kura za maoni kwa kuwa alishindwa vibaya sana na Akina Hussein kutokana na ukwasi was pesa. Wapigakura was CCM Hawakujali kama Ndikilo ni mzaliwa was jumbo hilo pia( kwao in sehemu moja panaitwa Busolwa)
Wapiga kura wangeweka MTU yeyote aliye soma na mwenye uwezo wa kuzisemea shida za jimbo lake, Nyang'hwale ingekuwa na maendeleo makubwa kuliko ilivyo hivi Leo, maana haishangazi mradi was maji toka ziwa Victoria ambalo liko umbali was km 15 hivi haujakamilika zaidi ya miaka 10 sasa na mbuge Hugo yupo haoni hayo ila mavazi ya mbunge mwenzie.
Kweli nimeshangaa, huyu Hussein Nassor alikosa kabisa kero yenye masilahi kwa jimbo lake akaishia kuona mavazi ya mbunge mwenzie? Kuna kituo cha Afya Khatumwa, huduma ni mbovu balaa huku kukiwa hakuna dawa kwa wagonjwa, hill hajaliona Ila mavazi ya mbunge mwenzie. Barabara ya Kharumwa -Mwanza na Kharumwa kwenda Kahama INA hali mbaya. Lkn mbunge huyo hill hajaliona ila mavazi ya mbunge mwenzie. Ninayo mengi ya kusema khs jimbo lake Huyo mheshimiwa lkn itoshe tu kusema kuwa SAA nyingine wapiga kura wawe na uelewa juu ya MTU wanayekusudia kumtuma bungeni bila kuangalia ukwasi wake au wingi was chawa alionao.
 
Huyu Mbunge katuaibisha sana wana Momba, yaaani badala ya kuvaa nguo zinazo endana na Bunge letu tukufu yeye anavaa nguo za casino!!
Hata kama hujaolewa lkn unapaswa ujiheshimi.

lkn pia kama alivyo sema Spika kuwa kuna kina MAMA pia huvaa nguo zisizo na heshima wala adabu.
unavaaje suruali imeshika makalio na mapaja halafu unaenda BUNGENI?!! huo ni utovu wa nidhamu na kulikosea heshima jengo la Bunge.

Sehemu zenye Heshima ambazo hatutegemei Mwanamke mwenye kujiheshimu kuvaa mavazi ya ajabu ni;

1. IKULU
2. JESHINI
3.BUNGENI
4.MAHAKAMANI.
maeneo yote hayo niliyo tlyataja hapo juu yanaongozwa na nidhamu za mavazi.
ukitaka kuvaa vimini vyako na tight nenda casino.

Spika katoa maelekezo kuwa kuanzia kesho yeyote atakaye kuja Bungeni huku amevaa nguo zilizo bana makalio asiruhusiwe kuingia getini, lkn pia tunawaomba wawe wanaturushia picha zao ili tuwaweke kwenye orodha mwaka 2025.
 
aina hii ya wabunge wasio jiheshimu na kufuata kanuni za Bunge hawafai kuwapa ridhaa mwaka 2025.

sisi wananchi tumewatuma mkatusemee kero zetu halafu nyinyi mnaenda kuuza sura!! na kuonyesha shepu?!!
 
Mbona haijabana!!!! Hao wazee vipi!!!! Yaani inaonyesha aina ya wabunge tulio nao. Watajadili masuala muhimu ya taifa kweli? Ubaya wa hiyo suruali sijauona kabisa!!!! Wazee wasichaguliwe kuingia bungeni!!!!
Nimeshangaa kweli kweli. Vazi alilolivaa halina kasoro yoyote, tena amependeza sana. Huu ni mfumo dume kazini. Halafu kuna wanaume wengine hawawezi kuji-control. Kuna jamaa alifungua thread hapa eti yale masanamu yanayowekwa maduka ya nguo, akiona ya jinsia ya kike hayajavalishwa nguo anakwazwa!
 
Wivu tu wa wapemba, mdada wa watu kapendezaaa !!! afu we ustadhi mtoa hoja usituudhi kwanza hapa siyo Zenji ..!!
Hivi hiyo mibichwa yenu huwa inawaza kabla ya kupost? Wewe umeambiwa mbunge aliyetoa hoja ni wa Nyang'wale umekurupuka huko bila kuchamba umeanza na wapemba. Ukiona kofia tuu huwazi mara 2.Pumbavu sana
 
Back
Top Bottom