Pameibuka tabia ya wabunge wa viti maalumu kuvaa vinyela momo(skin tight) wawapo kwenye vikao vya bunge, hii haikubaliki.
Ukivaa kimnyelala momo basi vaa gauni juu yake ili kulinda heshima na utamaduni wa kitanzania.
Ni angalizo tu.
Huyo mbunge ni wa jimbo LA Nyang'hwale mkoa wa Geita.Hivi hiyo mibichwa yenu huwa inawaza kabla ya kupost? Wewe umeambiwa mbunge aliyetoa hoja ni wa Nyang'wale umekurupuka huko bila kuchamba umeanza na wapemba. Ukiona kofia tuu huwazi mara 2.Pumbavu sana
Kaka siyo huyo mbunge wenu tu, bado kuna huyu pia sijui unasemaje hapo, hii no tabia yao tena imejengeka haswa, utaendaje bungeni namna hii?Huyu Mbunge katuaibisha sana wana Momba, yaaani badala ya kuvaa nguo zinazo endana na Bunge letu tukufu yeye anavaa nguo za casino!!
Hata kama hujaolewa lkn unapaswa ujiheshimi.
lkn pia kama alivyo sema Spika kuwa kuna kina MAMA pia huvaa nguo zisizo na heshima wala adabu.
unavaaje suruali imeshika makalio na mapaja halafu unaenda BUNGENI?!! huo ni utovu wa nidhamu na kulikosea heshima jengo la Bunge.
Sehemu zenye Heshima ambazo hatutegemei Mwanamke mwenye kujiheshimu kuvaa mavazi ya ajabu ni;
1. IKULU
2. JESHINI
3.BUNGENI
4.MAHAKAMANI.
maeneo yote hayo niliyo tlyataja hapo juu yanaongozwa na nidhamu za mavazi.
ukitaka kuvaa vimini vyako na tight nenda casino.
Spika katoa maelekezo kuwa kuanzia kesho yeyote atakaye kuja Bungeni huku amevaa nguo zilizo bana makalio asiruhusiwe kuingia getini, lkn pia tunawaomba wawe wanaturushia picha zao ili tuwaweke kwenye orodha mwaka 2025.
Muwamba ngoma huvutia kwake. Nimekuelewa vizuri.Sa hilo vazi lina shida gani, ukizingatia mbunge mwenyewe wala hana maajabu hapo kati....huyo alietoa hoja ana wingu tu
kanuni zinazo ongoza JENGO LA BUNGE ndio zinakataza nguo za kuchora shepu, sio spika wala mbunge aliye sema.Nikajua labda shati limebana nyonyo kweli kifua kimetuna, suruali tight hips lote njee nje; kumbe matatizo binafsi tu ya huyo mzee hivi utasemaje yale mavazi hayana maadili.
Hizo picha ukiziangalia kuna shape yeyote unayoona hapo zaidi ya ngozi yake ya shingo na juu ya kifua kidogo (sehemu ambazo hata mama zetu wanaacha wazi kulingishia mikufu yao).kanuni zinazo ongoza JENGO LA BUNGE ndio zinakataza nguo za kuchora shapu, sio spika wala mbunge aliye sema.
wabunge wetu haswa wanawake wakae wajitathimini, maaana Spika kasema kuna hata kina mama watu wazima wanavaa nguo za disco wanatinga nazo mjengoni.
Karibu tenaM
Muwamba ngoma huvutia kwake. Nimekuelewa vizuri.
Mbunge wa Momba Condester Michael Sichalwe ametolewa ndani ya ukumbi wa Bunge ili akabadilishe mavazi yake baada ya Mbunge wa Nyangw'ale Hussein Nassor Amar kuomba muongozo wa Spika kuwa kuna baadhi ya Wabunge wamevaa mavazi yasiyo na maadili.
Spika baada ya kumuamrisha kuondoka Bungeni pia aliwaambia askari wa Bunge, kuanzia sasa mbunge yeyote atakaevaa mavazi yasiyo na Staha na kinyume na kanuni waishie getini. Sakata hilo lilianza kwa mbunge mwenzake kuomba muongozo wa spika akimtolea mfano kama mbunge aliyevaa mavazi yasiyo na staha.
haiongezi chochote wala haipunguzi chochote, na hizo sio suala la msingi sana kulifanya bungeni kuliko kufanya mambo yenye maslahi mapana kwa wananchi. wabunge wana nini cha kujivunia? tabia njema? wakati wakitoka pale getini wanafanya mambo ya ajabu, mioyo imejaa uchafu ila kwa nje ndio wanataka wajifanye wasafi? watu kibao hao wanaloga, wanakula hadi uchafu wa ajabu ili wapate huo ubonge, kila mtu hapo ana siri zake, halafu wanataka kujifanya watakatifu? wakitoka tu kwenye geti hapo hata hao wengine wanavaa nguo za ajabu na wanafanya mambo yakifirauni balaa. ngoja mtu aishi vile alivyo moyoni, sio kwa kuigiza. na hivyo ndivyo sote twahukumiwa hata mbele za Mungu.
Nyie mawazo yenu ngono tu. Hamuwezi ku imagine mtu anaweza kum admire mwanamke alivyopendeza bila kumtaka kingono? Au kuwa mwanamke ana haki na uwezo wa kumkatalia mtu akimtongoza.Huoni ukiwa umevaa vazi la hijab na baibui hakuna mwanaume atakae kutamani!!!!! Lakini dada zenu mnawaachilia hovyo na vinguo vinaonyesha ndani, chupi, sidilia, mipaja yote wazi, nywele zimesimama kama mwendawazimu, kiufupi nguo mnazowaachia dada zenu/mama zenu ni aibu, na ndiomaana wana shawishika kwa wanaume na hupelekea kubakwa na kutongozwa. Hii sio sifa ya mwanaume kuwaachia dada/mama zako wakijiachia. Watu wa ajabu nyie sijapata kuona, mpo kidunia zaidi.
Wangelikuwepo wakina ottoman empire/Sultan/Eturgrul n.k mngenyooka tu.
Mtu anaejitambua hawezi sapoti huu ujinga. Zindukeni!Wewe nawe kwani kutongozwa dhambi? Si amkatae tu mwanaume kama hampendi... Mfundishe mkeo/ mwanao/ dada zako kukabiliana na yaliyopo duniani. Wafundishe kujitambua na kusema NO. Kuna wanaume wanabaka bibi zao, watoto zao huko nako wameona nini cha kuwavutia?
Nyie mawazo yenu ngono tu. Hamuwezi ku imagine mtu anaweza kum admire mwanamke alivyopendeza bila kumtaka kingono? Au kuwa mwanamke ana haki na uwezo wa kumkatalia mtu akimtongoza.
Basi wanawake wenu wasiingie kabisa bungeni ili tusiwatamani. Kama vile wakina Taliban walivyokuwa wanafanya. Waficheni tusiwaone kabisa. Wapuuzi wakubwa nyie.
Amandla...