Mbunge kusimama Bungeni kutaka Rais aongezwe muda wa kukaa madarakani. Je, Umewasiliana na waliokutuma uwawakilishe hapo Bungeni au ni mawazo yako?

Ukitaka kuua nyoka anza kuangalia miguuni kwako, usianzie nyumba ya pili wakati chumba chako kinaweza kuwa na nyoka.

Demokrasia ya vipindi vya uongozi tunge anza kwenye vyama vyenu tungesikilizwa sana. Lakini vipindi au muda wa uongozi sisi hatutaki heshima na tunataka wenzetu wa heshima ni double speak.

Mbowe tumempa miaka 25 ya kuongoza, wana CCM wanataka wamuongezee mwenyekiti wao miaka 5, ili iwe jumla miaka 15 sisi midomo juu kama vile nchi ni mbili.

Wao wanataka kumuongezea muda Mwenyekiti wao CCM miaka mingine mitano akimaliza hii mitano, tatizo ni nini? Au kwa kuwa Mwenyekiti wa CCM ni mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania?
 
Hicho chama kimejaa wachumia tumbo tupu,
 
Katiba yetu hairuhusu jambo hilo.
Nakumbuka Mwalimu Nyerere alikemea jambo hilo,lakini na yeye alishutuka baada ya kuondoka madarakani.
Magufuli mwenyewe hataki kuongeza hata dakika mmoja.
Kama Chadema wamebadilisha ukomo wa uongozi, CCM wakibadilisha katiba yao taabu iko wapi?

Wote wenye akili timamu ya Siasa ya nchi hii wanajua katiba tulio nayo ni ya CCM na sio ya wananchi, wanaweza kuibadili kwa kuwa ndio walio iweka.
 
Kwa hoja hii, inashangaza Sana na inasikitisha, sijui wamechoka amani waliyonayo au shibe imepitiliza katiba tulinayo ipo wazi. Kama gains Cha kuongea bungeni piga usingizi, ujatumwa hayo na wananchi
 
Kwani wewe mleta mada unajuaje kama mbunge hajatumwa na watu wake kutoa hayo maoni. Nyinyi si waumini wa demokrasia? Na demokrasia si maana yake uhuru wa kutoa maoni. Sasa kwa nini umfundishe mtu maoni haya mazuri yale mabaya. Ukiufuata ujinga unaufuata mpaka mwisho. Vivyo hivyo ukiifuata demokrasia unaifuata mpaka mwisho.

Kusema watu wasijadili ukomo wa urais ni udikteta. Kama wewe unadhani ukomo wa vipindi viwili ndiyo sahihi yupo mwingine yeye anataka kiwe kimoja. Kuna mwingine anataka viwe vitatu! Ndiyo, ndiyo demokrasia hiyo.

Maoni yangu: Suala la ukomo wa mihula ya urais linahitaji busara ya hali ya juu. Maamuzi yoyote sharti yafanyike kwa uwazi na iwe juu ya wananchi wenyewe kuamua. Wala bunge lisijitwike madaraka hayo.

Ikiwa bunge litaona linataka kufanya hivyo sharti likabidhi suala hilo kwa wenye nchi wenyewe waamue wanachotaka kupitia mchakato wa wazi.

Hapana shida yoyote wananchi kumwongezea rais wao muda wa kukaa madarakani. Vivyo hivyo wananchi wakiamua wampunguzie rais muda wa kukaa madarakani. Ndiyo demokrasia hiyo.

Tuache maigizo kwenye demokrasia kama wanavyoigiza wamiliki wa JamiiForums. Nje wanapigania demokrasia. Lakini huku ndani ukisajili ID huwezi hata kuibadili kirahisi. Ukitaka kuifuta ndiyo sahau kabisa! Ila unaambiwa ni wanaharakati wa uhuru wa habari na demokrasia na tuzo wanapewa! Siyo kwa chuki, ni ukweli tu; demokrasia.
 
Kuna baadhi ya binadamu wana hulka za kibinafsi ma kinafiki sana. Ngoja tuone mpaka hiyo 2025 itakuwaje.

Akiongezewa/Akijiongezea huo muda, hakika Wafanyakazi wengi wa umma wenye mioyo myepesi tutaacha/tutafukuzwa kazi.

Mwisho wa uvumilivu wa huu unyonyaji na dhuluma dhidi yetu, ni 2025!
 
Mbunge hufanya kazi bungeni kwa kufuata mawazo ya wananchi wake,na pia ana haki ya kutumua conscious yake binafsi,mradi kama ni kwa faida ya umma
 
Wabunge na rais lao moja wamefanya kiini macho kuwa wanaomba rais aongezewe muda lakini hilo liko kwenye ilani yao kisiri siri ukitaka kujua rejea uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 na uchaguzi mkuu 2020 hapo ndiyo utajua lengo la serikali iliyopo madarakani.
 
Nitarudi kukujibu kwanini Magufuli apewe 5 miningine.
 
Jiwe linatutega boss ,si kweli kama halitaki kubakia
Katiba yetu hairuhusu jambo hilo.
Nakumbuka Mwalimu Nyerere alikemea jambo hilo,lakini na yeye alishutuka baada ya kuondoka madarakani.
Magufuli mwenyewe hataki kuongeza hata dakika mmoja.
 
Mkuu mbona umeongea kana kwamba wewe haya hayakuhusu?
 
Ukitaka kujua huyu Mzee ana kasoro kubwa sana aachie madaraka japo mwezi mmoja halafu sikia hizo kashfa zitakazoibuliwa.
 
Ukitaka kujua huyu Mzee ana kasoro kubwa sana aachie madaraka japo mwezi mmoja halafu sikia hizo kashfa zitakazoibuliwa.
 
Wabunge msijisahau Wananchi wamewatuma muwawakilishe tafadhali msifanye mambo kama mmejipeleka wenyewe Bungeni msiwe walafi wa madaraka
Mbunge amewakilisha maoni ya wananchi wake: wewe kwanini unapinga?, wananchi wamekutuma uwasemee?
 
Ukitaka kujua huyu Mzee ana kasoro kubwa sana aachie madaraka japo mwezi mmoja halafu sikia hizo kashfa zitakazoibuliwa.
Kila jambo lina sura mbili
 
Umeandika maneno mengi sana yenye mantiki lakini umesahau malengo ya ndugai,magu,mwigulu na ccm kwa ujumla subiri muda wenyewe utaongea na hapo ndipo utakapoamini kuwa mawazo yako yalikuwa hasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…