Mbunge Mohammed Issa aliyesema yeye si Mtanzania, kwanini bado yupo Bungeni?

Mbunge Mohammed Issa aliyesema yeye si Mtanzania, kwanini bado yupo Bungeni?

View attachment 2991526

Mbunge anasema na au anakana kwamba yeye si Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania “Mtanzania”.

Sasa Humo Bungeni anafanya nini?

Hatuna Nchi inayoitwa Zanzibar wala nchi ya Tanganyika. Tuna Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “ Tanzania”

Sasa kama yeye ni Mzanzibar na hatuna nchi hiyo, humo ndani kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anafanya nini? Kiti cha Speaker kingefaa kimtoe nje pale pale kwa kauli yake mwenyewe kwamba hapokei taarifa ya yeye ni raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kiti cha Speaker mumepwaya sana maana, Hatuna dual nationality, tuna Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mtu anasema na anakana kwamba yeye sio Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( Principle of legal estoppel), sasa kwa nini aendelee kuwemo humo Bungeni?
Hatuna dual nationality, hakuna raia wa Burundi, Rwanda au nchi ya “Zanzibar” anayeweza kuwemo Humo Bungeni.

Ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pekee anayeweza kukaa humo, vinginevyo ni magumashi tu, bila chenga chenga na mkosi ni Mkosi tu- Haijalishi unatokea wapi.

Povu ruksa bila Matusi.

Zanzibar mpaka ina Rais wake na bendera yake, sasa atashindwaje kujiita mzanzibari!

Zanzibar ni Nchi
Tanzania ni Nchi

So, ana haki kusema yeye ni mzanzibari, na sio Tanzania
 
Zanzibar mpaka ina Rais wake na bendera yake, sasa atashindwaje kujiita mzanzibari!

Zanzibar ni Nchi
Tanzania ni Nchi

So, ana haki kusema yeye ni mzanzibari, na sio Tanzania
Raisi aliyewekwa na Magufuli?
 
Kusema serikali moja ni kuwachokoza wanaokana Utanzania kutokea ule upande wa visiwani umeliwazia au umebandika tu " Serikali moja"? Hawa watu hawataki kuchokozwa wao ni Zanzibar tu, haya ya Muungano hawataki kuyasikia.
Wazo la Serikali moja nashindwa kuelewa wanaolitoa wanapata wapi uthubutu.
Nani atawapa au kuwabeba W'bar kama ilivyo sasa na bado hawaridhiki. Kila kitu kuna sehemu ya Zanzibar
Na Wazanzibar wasiotaka kusikia Tanzania wataishi vipi bila Uzanzibar. Hili wazo ni DOA (Dead on arri
-Mara wanajaribu kila kitu, mara njooni na Passport- wakibanwa sana wanasema hawakumaanisha hivyo.
Hili la Passport ni Tusi kubwa sana halafu likaongezewa na kuukana Utanzania ndani ya Bunge la Tanzania
-Mara wanakuja na kauli ya wao sio watanzania- na tuone Bunge/serikali itawafanya nini?
Tena wanajadili 90% ya mambo ya Tanganyika yasiyowahusu, ya Muungano kwa mujibu wa mkataba ni 11 na kwa mujibu wa Tume ya Warioba yangekuwa 7 tu. Wakiwa wanajadili au kula na kulala wanatukana Watannganyika.

Ni Watanganyika hao hao wanaolipa mishahara , posho na bili za umeme za wake zao huko Zanzibar.
Ni Watanganyika wanaolipa mfuko wa Jimbo la watu 3,338 sawa na jimbo la Serengeti, Ilala, Tanga, Tunduru, Ifakara, Katavi au Kibondo. Na huyo anayeukana Utanzania kasomea Tanganyika tena bure.
-wanajaribu kila mbinu - ili mradi tu Zanzibar ijichomoe humo kwenye Muungano.
Sio kwamba hawawezi la hasha! kuna mambo yanawazuia. Ukisikia wanataka mkataba ni kwa kuelewa kwamba gharama za ulinzi na usalama, mambo ya ndani , nje n.k. yatakuwa mzigo kwao. Wanatambua kwamba soko lao ni Tanganyika, si biashara bali ajira pia. Tanganyika inaajiri Wazanzibar wengi kuliko SMZ kwa upendeleo hata kuumiza watu wake.
-Mwisho wakishindwa, watafanya mengine ya hatari zaidi na bado hawatafanywa kitu.
Kama wanaweza kudai Rais wa nchi moja watumie passport kuingia kwao na wakiwa ndani ya Bunge la JMT wanaukana Utanzania kuna hatari gani imebaki? Hawa wanaweza kuona hatari wasijali kwasababu si Watanzania.
Kuna Mbunge anaitwa Ali Salehe, yeye alisema '' Ninafurahi nasikia bandari ya Bagamoyo imekwama''

Ifike mahali mamlaka itoe kauli, kwamba kama mtu ni kiongozi, yumo kwenye chombo cha kutunga sheria, halafu anakana kwamba hastari kuwemo humo ( Principel ya legal estoppel) maana yake ni kwamba hata hizo sheria zote alizoshiriki kutunga ni batili ab nitio. Haya ndio madhara makubwa zaidi ya kumyamazia huyi Mbunge.
Kauli ya kuukana Utanzania na kuomba passport imetolewa Bungeni
1. Spika wa Bunge yupo kakaa kimya
2. Waziri Mkuu yupo kakaa kimya
3. Makamu wa Rais yupo kakaa kimya
4. Raia wa SMZ yupo kakaa kimya
5. Rais wa JMT yupo kakaa kimya

6. Mstaafu Kikwete kimyaa! anasubiri aseme Mbowe. Tunaombwe la 'statesman'

Kimya kinawawezesha Wazanzibar kusema hoyo. Walianza kwenye mikutano sasa ndani ya Bunge
Ni kama vile viongozi hao wanakubaliana . Haikuanza na Passport, ilianza na katazo la ndizi, passport sasa wanaukana Utanzania. Hatudhani kwama wanahitaji Muungano!
Hatuwezi kutungiwa sheria na wanyarwanda wa visiwani maana ili uwe Mbunge, kigezo mojawapo ni Uraia, na yeye kakana na hata kwenye Hansard ipo, au landa waifute.
Haiwezi kufutwa bila kujadiliwa tena Bungeni, wakifanya hivyo watakuwa wamekiuka sheria zao wenyewe
Yaani Wazanzibar wanaukana Utanzania, tumebaki na nini?
Tena hawa Wazanzibar wanaiukana Utanzania ndio wanajadili mambo ya ''Tanzania'' hatuwahitaji ni wakati sasa wakijadili ya Muungano(kama wana japo wazo) waondoke watuache!
Ipo siko wanasheria watenda mahakamani na kuitumia hiyo kauli yake kubadilisha vifungu vyote vya sheria vilivyo pitishwa na huyu Mbunge na mahakama itakubali bila ajizi, na hili hawa viongozi wa Bunge hawalioni labda mpaka wavae miwani...
Natamani kama wanasheria wataliona hili
 
Ni kawaida baadhi ya watu kuwa na apathy na mtu fulani, ukiishakuwa na apathy, huyo mtu hata afanye mazuri vipi, huwezi kuyaona!, na ndivyo ilivyotokea kwa JPM, kuna watu wanaona udikiteta wake tuu, lakini mazuri yake hawayaoni.
Wakati naendesha kipindi cha Kiti Moto, kuna jamaa akasema nikitokea tuu ana zima TV!.

Japo mimi ni mwana CCM, lakini siko ndani ya CCM!, mimi sio insider, hivyo sina any influence yoyote na hakuna wa kunisikiliza, ila uzuri wangu mmoja, ni I always speak out my mind, atakayesikia, na asikie, na kila nikishauri jambo, pia huwa naweka na the consequences za kupuuza ushauri huo, hizo consequences zikitokea, kazi yangu ni kukumbushia tuu, nilishauri nini na lini, na matokeo ni nini!, "Ombeni Mtapewa", "Tafuteni Mtapata", "Bisheni Hodi Mtafunguliwa" Je, Wajua Kuna "Kauli" na "Kauli Umba" Ambazo Huumba? Shuhudia

Kwanza kwa nature ya CCM hakuna mtu wa kumbishia Mwenyekiti jambo lolote, ila kuna waliomzunguka kuna vitu wanaviona, hawawezi kumshauri kwa kumuogopa!. Kwa upande wangu, kuna vitu vinavyohitaji intellect ya level fulani, Rais Samia, lazima asaidiwe na watu kutoka nje ya waliomzunguka, mfano mzuri ni madudu ya ile IGA ya DPW na Bandari zetu, waliomzunguka wote wanampoteza!, serikali na Bunge wamepotosha!, akina sisi tukawauleza ukweli, Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! ile HGA iliachana na madudu ya IGA!.

Sasa ni kila mtu anamuimbia wimbo wa mitano tena!, washauri huru tupo na tumeisha mshauri hapa kwenye HII

P
Paskali, sijui nisemeje(utaniwia radhi kwa hilo jina, kwetu hulitamka na kuliandika hivyo).
Sitapenda kuandika mengi hapa leo kukuhusu wewe, ila niseme tu wazi kwa nini nilikuwa 'put off' kabisa na 'approach' yako ya uandishi hata katika maswala ambayo ni nyeti kabisa. Unapiga 'zigzag' nyingi sana kiasi kwamba unawachanganya watu unasimamia wapi kwenye maswala hayo.
Unapokuwa 'straight to the point', kama unavyofanya kwenye mada hii, unaeleweka vizuri kabisa.
Kwa hiyo, hata huko ndani ya CCM inawezekana unashindwa kuwavuta wanachama wenzako kwa mawazo yak ambayo yanapiga holela. Nitumie mfano wa mimba, pengine nitaeleweka kidogo ninalenga nini. Kuna mimba zinazosemekana kuwa 'ectopic pregnancy', kitaalam. Mimba hizi ni za matatizo kwa sababu zimekaa nje ya hali isiyokuwa kawaida.
Mada zako ziko nyingi sana humu JF, ukizichambua utanielewa nasema nini. Kuna neno la kiingereza ambalo ningependa kulitumia kuhusu uandishi wako. Neno lenyewe ni ':disambiguation.'Uandishi wako mara nyingi unafanya nione hali hiyo kutoka kwako. Inachanganya sana!
 
Tuko pamoja! Kuna watu wanadhani hatutaki Muungano hapana issue ni Muungano wa aina gani? Kwa nn wengine wanatudai passport na ss tuwadai?
Watanganyika wapo tayari kwenda Zanzibar kwa Passport
Watanganyika wamebeba Muungano 100% hawapaswi kuulizwa kama wanataka au la
Watanganyika hawana cha kupoteza, waulizwe nini?

Wasiotaka Muungano ni Wazanzibar, na sasa hawataki kusikia hata Utanzania.
 
Wazo la Serikali moja nashindwa kuelewa wanaolitoa wanapata wapi uthubutu.
Nani atawapa au kuwabeba W'bar kama ilivyo sasa na bado hawaridhiki. Kila kitu kuna sehemu ya Zanzibar
Na Wazanzibar wasiotaka kusikia Tanzania wataishi vipi bila Uzanzibar. Hili wazo ni DOA (Dead on arri

Hili la Passport ni Tusi kubwa sana halafu likaongezewa na kuukana Utanzania ndani ya Bunge la Tanzania

Tena wanajadili 90% ya mambo ya Tanganyika yasiyowahusu, ya Muungano kwa mujibu wa mkataba ni 11 na kwa mujibu wa Tume ya Warioba yangekuwa 7 tu. Wakiwa wanajadili au kula na kulala wanatukana Watannganyika.

Ni Watanganyika hao hao wanaolipa mishahara , posho na bili za umeme za wake zao huko Zanzibar.
Ni Watanganyika wanaolipa mfuko wa Jimbo la watu 3,338 sawa na jimbo la Serengeti, Ilala, Tanga, Tunduru, Ifakara, Katavi au Kibondo. Na huyo anayeukana Utanzania kasomea Tanganyika tena bure.

Sio kwamba hawawezi la hasha! kuna mambo yanawazuia. Ukisikia wanataka mkataba ni kwa kuelewa kwamba gharama za ulinzi na usalama, mambo ya ndani , nje n.k. yatakuwa mzigo kwao. Wanatambua kwamba soko lao ni Tanganyika, si biashara bali ajira pia. Tanganyika inaajiri Wazanzibar wengi kuliko SMZ kwa upendeleo hata kuumiza watu wake.

Kama wanaweza kudai Rais wa nchi moja watumie passport kuingia kwao na wakiwa ndani ya Bunge la JMT wanaukana Utanzania kuna hatari gani imebaki? Hawa wanaweza kuona hatari wasijali kwasababu si Watanzania.
Kuna Mbunge anaitwa Ali Salehe, yeye alisema '' Ninafurahi nasikia bandari ya Bagamoyo imekwama''


Kauli ya kuukana Utanzania na kuomba passport imetolewa Bungeni
1. Spika wa Bunge yupo kakaa kimya
2. Waziri Mkuu yupo kakaa kimya
3. Makamu wa Rais yupo kakaa kimya
4. Raia wa SMZ yupo kakaa kimya
5. Rais wa JMT yupo kakaa kimya

6. Mstaafu Kikwete kimyaa! anasubiri aseme Mbowe. Tunaombwe la 'statesman'

Kimya kinawawezesha Wazanzibar kusema hoyo. Walianza kwenye mikutano sasa ndani ya Bunge
Ni kama vile viongozi hao wanakubaliana . Haikuanza na Passport, ilianza na katazo la ndizi, passport sasa wanaukana Utanzania. Hatudhani kwama wanahitaji Muungano!

Haiwezi kufutwa bila kujadiliwa tena Bungeni, wakifanya hivyo watakuwa wamekiuka sheria zao wenyewe
Yaani Wazanzibar wanaukana Utanzania, tumebaki na nini?
Tena hawa Wazanzibar wanaiukana Utanzania ndio wanajadili mambo ya ''Tanzania'' hatuwahitaji ni wakati sasa wakijadili ya Muungano(kama wana japo wazo) waondoke watuache!

Natamani kama wanasheria wataliona hili
Ndugu yangu Nguruvi3 , asante sana kwa chapisho lako na kwa jinsi ilivyojibu hapo juu. Watu kama wewe muna uelewa Mkubwa sana wa kuchanganua mambo. Sijui kwa nini hizi PhD za Heshima zinawaendea akina Msukuma lakini si kwa watu wa aina yako... ?
 
Kulikuwa kuna kadingi fulani bungeni, sijui kabunge kaCCM kule Nkasi, kalikuwa kanalipukaga balaa wazenji tukianza kufungua midomo bungeni kuhusu huu muungano.
Kale kadingi kangekuwepo leo hapo bungeni pasingekalika.
Mzee wa tulia nikupashe hujui chochote
 
Ndugu yangu Nguruvi3 , asante sana kwa chapisho lako na kwa jinsi ilivyojibu hapo juu. Watu kama wewe muna uelewa Mkubwa sana wa kuchanganua mambo. Sijui kwa nini hizi PhD za Heshima zinawaendea akina Msukuma lakini si kwa watu wa aina yako... ?
Hizo Phd zakina Musukuma unalipia milioni 5 unapewa.
 
Hatuhoji usahihi wake bali ni nini anafanya ktk bunge la Tanzania wakati yeye si mTanzania.

Hakuna mwenye tatizo na Uzanzibari wake.
Safi sana kwa kumjibu huyu CCM, wao wanaona ni sawa tu mtu/Mbunge kuukana na bad ikawa sawa kuendelea kuwemo mule, anawachafua watunga sheria wote mule ndani kwa uelewa wao wa sheria wanazozitingua ambazo zitakuwa batili kuanzia siku ile alipo jikana hadi bunge litapo muondosha.
 
Shida ni elimu za wabunge kuwa chini, bunge litunge kanuni graduates tu waingie mjengoni, hii ndo shida ya kujaza vilaza kama huyu mpemba!!
 
Back
Top Bottom