Mbunge Shabiby aibua ufisadi wa kutisha EWURA, Waziri wa Nishati Kalemani asema walishavunja mkataba na kampuni fisadi

Mbunge Shabiby aibua ufisadi wa kutisha EWURA, Waziri wa Nishati Kalemani asema walishavunja mkataba na kampuni fisadi

Mbunge wa Gairo, Shabiby amesema kuna kampuni inalipwa kati ya sh bilioni 5 hadi 7 kila mwezi kwa kazi ya kuweka rangi kwenye mafuta yanayotumika nchini.

Shabiby amesema 'fee' hizo ni nyingi mno kulinganisha na kazi ndogo sana inayofanywa na kwamba kazi hiyo ingeweza kufanywa bure na TBS

Shabiby kasema kazi hiyo wamepewa kampuni binafsi ambayo inatupiga haswa.

Waziri wa nishati mh Kalemani alitoa taarifa kwamba mkataba wa kampuni hiyo ya kifisadi ulishasitishwa lakini Shabiby aliikataa taarifa hiyo na kusema hata jana aliiwaona watendaji wa kampuni hiyo wakiendelea na kazi hiyo ya kitapeli

Chanzo: ITV Habari

Ramadhan Kareem
Hilo ni kweli,mtu wangu wa karibu anahusika huko.
 
Tutasikia na kuona mengi sana hivi sasa.


Ni heri wabwabwajaji tulijikalia pembeni. Ubabe usio na maono ulitushinda.
Jirani yangu FaizaFoxy ,huo ndio tunaita unafiki na upumbavu.
Yaani mtu anafanya madudu ya kutisha halafu wewe badala ya kukemea,eti unakaa pembeni sababu ya kuogopa ubabe wa mtu mmoja!!.
Kweliii!!???
Ninakuheshimu mno kama mtu mwenye uelewa mpana sana lakini kwa hili umeniudhi kwa kweli jirani.
Nipo Mkuranga nachimba mabwawa ya kufugia samaki hapa Mwanambaya.
 
Jirani yangu FaizaFoxy ,huo ndio tunaita unafiki na upumbavu.
Yaani mtu anafanya madudu ya kutisha halafu wewe badala ya kukemea,eti unakaa pembeni sababu ya kuogopa ubabe wa mtu mmoja!!.
Kweliii!!???
Ninakuheshimu mno kama mtu mwenye uelewa mpana sana lakini kwa hili umeniudhi kwa kweli jirani.
Nipo Mkuranga nachimba mabwawa ya kufugia samaki hapa Mwanambaya.
Mpishe mwenye nguvu apite.

Binaadam mwehu tu anaeanza kubishana na jiwe. Kukaa kimya ni ukomavu wa fikra.
 
Mpishe mwenye nguvu apite.

Binaadam mwehu tu anaeanza kubishana na jiwe. Kukaa kimyani ukomavu wa fikra.

Mpishe mwenye nguvu apite.

Binaadam mwehu tu anaeanza kubishana na jiwe. Kukaa kimyani ukomavu wa fikra.
Lakini dadangu FaizaFoxy , mimi, wewe na yule ,kwa umoja wetu tukipiga kelele na kushauri, hakika wahusika watafanya yale yenye tija kwa ustawi wa Tanzania.
Mtu kama wewe ni mkongwe,una elimu na umeelimika,una exposure nzuri sana,ushauri wako unahitajika sana kwenye kuijenga Tanzania iliyo bora zaidi.
Usikae kimya kwa kuogopa wauao mwili dada.
 
Wanaficha nje, halafu wanatapeliwa🤣🤣🤣

Na hela wanatapeliwa Pia ?🤣🤣🤣🤣 najua wanafungua companies kwa majina ya watu , wanafungua hotels mfano panone kwa majina ya watu maloli ya kusambaza mafuta kwa majina ya watu, halafu wanazulumiwa
 
Tumechoka kusikia hizi habari za ufisadi zisizoisha

Ova
 
Na hela wanatapeliwa Pia ?🤣🤣🤣🤣 najua wanafungua companies kwa majina ya watu , wanafungua hotels mfano panone kwa majina ya watu maloli ya kusambaza mafuta kwa majina ya watu, halafu wanazulumiwa
Nasubilia mmoja aingie mkenge tu 🤣🤣
 
Mbunge wa Gairo, Shabiby amesema kuna kampuni inalipwa kati ya sh bilioni 5 hadi 7 kila mwezi kwa kazi ya kuweka rangi kwenye mafuta yanayotumika nchini.

Shabiby amesema 'fee' hizo ni nyingi mno kulinganisha na kazi ndogo sana inayofanywa na kwamba kazi hiyo ingeweza kufanywa bure na TBS

Shabiby kasema kazi hiyo wamepewa kampuni binafsi ambayo inatupiga haswa.

Waziri wa nishati mh Kalemani alitoa taarifa kwamba mkataba wa kampuni hiyo ya kifisadi ulishasitishwa lakini Shabiby aliikataa taarifa hiyo na kusema hata jana aliiwaona watendaji wa kampuni hiyo wakiendelea na kazi hiyo ya kitapeli

Chanzo: ITV Habari

Ramadhan Kareem
nitakuwa wa mwisho kumuamini huyo mbunge. huyo ni mfanyabiashara apo ukute lazima itakuwa maslahi yake yamekanyagwa. haya mambo ya biashara na uongozi ndo maana nyerere aliyakataa
 
Hivi Mkurugenzi wa EWURA sasa hivi ni nani? Baada ya Felix Ngamlagosi Kusimamishwaga Kazi?
 
Lakini dadangu FaizaFoxy , mimi, wewe na yule ,kwa umoja wetu tukipiga kelele na kushauri, hakika wahusika watafanya yale yenye tija kwa ustawi wa Tanzania.
Mtu kama wewe ni mkongwe,una elimu na umeelimika,una exposure nzuri sana,ushauri wako unahitajika sana kwenye kuijenga Tanzania iliyo bora zaidi.
Usikae kimya kwa kuogopa wauao mwili dada.
Kuna njia nyingi za kufikisha ujumbe. Jamiiforums ya kufikisha ujumbe ilikwisha zamani sana.

Hata kukaa kimya ni kufikisha ujumbe.
 
Hii Nchi Tajiri sana!
Hii Nchi imechezewa sana1
Hii Nchi ni ya Wanyonge!
Kwa kweli nenda tu
 
Back
Top Bottom