Tetesi: Mbunge wa Arusha Mjini pamoja na Meya wasakwa na Jeshi la Polisi

Tetesi: Mbunge wa Arusha Mjini pamoja na Meya wasakwa na Jeshi la Polisi

Ushauri mzuri sana kwa Gambo
Japo mara nyingi huwa ushauri haufuatwi lakini nadhani ka ccm haitaki kujifuta yenyewe Arusha na sehemu nyinginezo Tz wateule wa rais waliopelekwa huko waende kuitengeneza ccm iliyo kwisha haribika sana machoni mwa Watz.
Picha mbaya haiondolewi kwa matendo mabaya. Wateule wa rais, hebu onesheni mambo mema saana ya ccm. Heshima, utu, na haki kwa kila mtu bila ubaguzi.
Mh Gambo, twajua kuwa una imani kuwa Chadema hawawezi lolote, sasa, tafuta mbinu ya kuonesha zaidi makubwa ya ccm. Hospitali ziongezewe uwezo, barabara zipanuliwe vizuri, projects zinazofanyika Ar sasa hivi uzisimamie zionekane kweli ni bora. Achana na kushindana kimwili na Lema, shindana naye kwa kuonesha mema ya ccm.
Kamata kamata ni kumwongezea umaarufu Lema &Co. Sikio la kufa halisikii dawa. Usiwe sikio la kufa Gambo.
 
Kwa taarifa yenu kuna mpango mkakati wa kuhakikisha kuwa jiji la Arusha linadhohofishwa na "rire lijiji retu kure kwetu" kupandishwa chati...

Kuna kamati maalum imeundwa kufanikisha zoezi hilo...
Wataanza na vurugu ili wazoroteshe sekta ya utalii Arusha.
Kilele kitakuwa ufunguzi wa viwanja vikubwa vya ndege Mwanza (Serengeti Intl. Airport) na Chato (Rubondo Intl. Airport)..

Wao wanasema ware jamaa wamekura sana sasa ni zamu yetu..!!
Mimi humu ni mjumbe tu kuwafikishieni hizi dondoo...
Hata wakidhoofisha watalii huangalia tourism package kinachoibeba arusha na Kilimanjaro ni vivutio vingi mtalii anaweza kuanzia kupanda mlima then akaenda Ngorongoro, arusha national park. Kudhoofisha na fujo ni ujinga mtupu kuinvest kwenye utalii kuna involve vtu vingi
 
Magesa ndo yule alikuwa Arusha alikuwa anapambana sana na Lema ?kuna siku nimekutana kwenye basi naelekea Dar amechoka sana mpaka huruma
Tatizo watu wakipata madaraka hujisahau mno na kujiona Mungu watu, pole yake kwa kuisoma number.
 
Nahisi wewe ndo Lema mwenyewe na kama siyo basi wewe unaweza kua unawatetea watu bila kuwajua,mtu hawezi nyanyuka tu bila sababu eti akaenda kuliamulu jeshi limkamate Lema,lazima kuna shida mahala,umeeleza ukiegemea upande mmoja na kumlaumu mkuu wa mkoa lakini yamkini kuna jambo,siku hzi waTanzania tunaakili tunaweza kuyapima maneno mnayotoa
Nimejsribu kufuatilia muda mrefu huyu mbunge wa arusha akiwa bungeni na jimboni na kwingineko anako kuwepo, kwa jinsi navyomtathmini yeye pamoja na mwenzake mmoja anaitwa Sugu, nawaona kama bado hawajakua kiakili au wana matatizo ya ukosefu wa busara na hekima ukilinganisha na wabunge wenzake wa upinzani na ndio maana hata hapa Arusha anakuwa amehusishwa sana na wale vijana wahuni na wasio na elimu ya kutosha au mambumbumbu. Hii kwa kweli haimpi status nzuri kwa watu walioelimika na wenye maono. Naomba achukue mfano wa mwenzake Mnyika. Mwerevu na yuko focused. Nadhani background yake ndio contributor wa behaviour zake, Afande Zombe aliwahi kusema Lema aliwahi kuhusika na biashara ya wizi wa magari kutoka Kenya, habari ambazo hakuzikanusha.
 
Adui wa Mwafrica ni yeye mwenye

Halafu utawaskia watu wenye akili za mende wanawatukana wazungu Kurudisha africa nyuma!

Kumbe wenyewe mnajirudisha nyuma kwa ujinga wenu!!
 
Jeshi la polisi mkoani Arusha linajipanga kumkamata mbunge wa Arusha Mjini na Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha leo usiku au alfajiri sana kesho
Taarifa za uhakika zinasema kuwa polisi wanashinikizwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha Bwana Mrisho Gambo kumkamata mbunge huyo kutokana na mgogoro mkubwa uliopo kati ya wawili hao.Shinikizo la RC Gambo limewachukiza baadhi ya maofisa wa polisi hasa kitengo cha upepelezi kwa kuwa wao polisi hawana sababu ya kumkamata,hata hivyo Bwana Mrisho Gambo amesisitiza kuwa lazima wakamatwe kutokana na kile yeye RC anachodai kuwa Mbunge amemkosea yeye binafsi na mh Rais.
Katika mikutano ya hadhara aliyofanya mbunge pamoja na madiwani akiwepo Mstahiki meya walitangaza kutompa ushirikiano wowote RC na DC kwa kile walichoita matumizi mabaya ya madaraka yanayofanywa na RC na DC.Tamko hilo limeungwa mkono na wananchi mbalimbali katika jiji la Arusha na viunga vyake.Kufuatia uungwaji mkono huo RC amekosa amani na imani ya kutembea bila ulinzi mkali wa polisi.
Itakumbukwa kuwa mke wa Mh. Mbunge wa Arusha mjini Bi. Neema Lema alishikiliwa na jeshi la polisi kwa masaa manne juzi Jumatano wiki hii Octoba 26 . Neema Lema alishikiliwa kwa amri ya mkuu wa mkoa wa Arusha Bwana Mrisho Gambo! Inadaiwa kuwa Neema amekuwa nguzo kuu ya ujasiri wa mumewe na katika kila hatua amekuwa na mchango mkubwa sana kwa mumewe ambaye ni mbunge aliyechaguliwa kwa zaidi ya kura 65,000. Taarifa zinazidi kusema kuwa mkuu wa mkoa amechukizwa na kitendo cha line ya simu ya Mbunge kuwa na jina la Neema ambaye ni mkewe.
Baada ya kuhojiwa kuhusu line inayohisiwa kutuma sms yenye neno *Shoga* Bi Neema Lema alikana kuhusika na kumiliki line iliyotuma sms hiyo,hata hivyo alisema neno Shoga sio tusi bali ni rafiki,na akatoa mfano kuwa kwa utamaduni wa wanawake huitana Shoga!
Baada ya kushikiliwa kwa muda wa masaa manne Bi. Neema ametolewa bila masharti, wala bila kuwa na kesi yoyote ya kujibu.

My take
RC acha kutumia madaraka vibaya,je ni hasira ya kuzomewa kula burka ulikotaka kupotosha umma?Je ni hasira ya hotuba kali za Mbunge?Hizi hotuba zinaeleza ukweli?je utaweza kushindana na Ukweli?
Kamwe mtu aliyeteuliwa na mtu mmoja hawezi kushinda mbunge mwenye kura 65,000 ni swala la muda tu.
Lema is a criminal. Time will tell, over.
 
Mbona hawa wakuu wa mikoa amabao upinzani wameshika hatamu sehemu kubwa kila siku wao kwenye vyombo habari hawakauki ? Au ndio wanatumika kisiasa na mkulu ili kuwadoofsha hao wapinzani wao?
 
Gambo na Lema mbona wote ni vijana tu, wanatupa picha gani wanapo tuonyesha kutokuaminiana, Yaani wamefika mahara pabaya sana, hata salam itakuwa ngumu sasa. Hayo mambo ayawapendezi na nyinyi bado vijana wadogo sana.
 
Back
Top Bottom