Mbunge wa CCM (Tabora) amdhalilisha mkewe hadharani

Mbona hata mbowe huwa anatoga sikio. Haya mambo ya kishabiki ya maisha binafsi ya watu mkome kuyaleta majukwaani
 
Waswahili wanasema kwamba "ndoa ni elimu ya kipekee iliyo ngumu na isiyo na mwisho ambayo mtu unatunukiwa cheti Kwanza na Kisha mitihani inafuata".

Kwa hiyo, Mikasa kama hii inatakiwa kuchukuliwa kwa tahadhari kubwa sana, huenda 'root cause' yake imeanzia mbali sana na hatma yake huwa ni mbaya pia endapo kama uangalifu mkubwa hautazingatiwa katika ku-deal na matatizo kama haya.
Aidha, matukio ya Homicide mara nyingi sana chanzo chake huwa kinaanzia na hatua kama hizi.
 
Halafu clip imeanzia katikati na kuishi kabla ya mwisho. Hatujui nini kilitokea kabla na baada ya clip hii. Halfu mtoa mada, embu nitajie matusi unayosema yametajwa
 
Domestic violence huwa Haina tajiri Wala maskini, Haina msomi Wala asiyesoma, Haina kiongozi Wala anayeongozwa

⚠️ Matajiri, wasomi, viongozi wa Kisiasa wapo katika risk kubwa ya migogoro ya ndoa kwa sababu ya kwanza huoa ma konki ya mjini yaliyojibadilisha rangi , yaliyofanya upasuaji huko uturuki ya kubadilisha muonekano na yaonekane vijana hata kama umri umeenda, .au kuonekana kama mazungu au maarabu au waliowanyanganya vijana masela wa mjini wasio na fedha
,,kumbe walishashindikana hivyo kwa tamaa ya macho na umaarufu na fedha WALIZOKUWA nazo hubeba matatizo hayo na kuyapeleka nyumbani kwenda kupambana nayo. Siku za mwanzo atakupetipeti utaona umepata subiri Sasa afungue makucha yake
 
Hakika umesema vyema sana
 
Acha lawama za kipumbavu mbona umeegemea kwa mwanamke tu,matatizo yao unayajua!?
 
Mbunge alipandwa na hasira hakuikumbuka nafasi yake kwenye jamii, wajanja wakampiga picha, matokeo yake sasa ni lawama kwake hata kama kosa hatujui lilipoanzia.
Hata kwenye DP WORLD wanafanyaga hivi hivi.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…