Mbunge wa Gairo, Shabiby ataka fedha za bima kwa wote zikatwe kwenye laini za simu

Mbunge wa Gairo, Shabiby ataka fedha za bima kwa wote zikatwe kwenye laini za simu

Mbunge wa Gairo (CCM), Ahmed Shabiby ameishauri Serikali kukata Sh2,000 kila mwezi kwenye laini za simu huku wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi wakikatwa Sh10,000 ili fedha hizo ziwe chanzo cha mapato kwa Bima ya Afya kwa wote.​


Amesema kuna wamiliki wa laini za simu milioni 72 nchini ambao makato yao kwa mwaka yataingiza Sh1.72 trilioni na zikijumlishwa za Sh10,000 kwa mwezi za wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi, Serikali itapata kwa mwaka takribani Sh2 trilioni.

Shabiby amesema hayo leo wakati akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Pia, ameshauri vituo vya kutolea huduma – hospitali, zahanati na vituo vya afya – vinavyomilikiwa na Serikali vibinafsishwe kama ilivyo Abu Dhabi na Korea Kusini.

Ameshauri madaktari na wauguzi waliopo nchini wajiunge na kubinafsishiwa hospitali badala ya kuwa chini ya Serikali. Shabiby alisema maana ya kutaka laini za simu zitumike kama chanzo cha mapato ni kutokana na anavyoona baada ya Bunge kupitisha muswada wa Bima ya Afya kwa wote na kusainiwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa sheria, kuna hatari bima hiyo ikachangisha wananchi ambao awali walishindwa kuchangia hata Sh10,000 na Sh30,000 za mfuko wa CHF.

Kwa mujibu wa Shabiby, wanufaika wa bima katika Watanzania 100 ni watu wanane ambao wanalipa bima.

“Hasa ukiichukulia hii hatuna chanzo maalumu cha kupata pesa ambazo zinaweza zikasaidia wananchi wa vijijini na watu masikini pamoja na wananchi wa mijini, hata mijini wapo masikini wengi tu, tena hata zaidi ya hao wa vijijini,” amesema na kuongeza:

“Nimeona tulizungumzie bila woga, najua kuna mawazo tutatoa na watu watatukana kwenye mtandao, lakini acha watukane. Hii bima ya afya, ushauri ninaotoa tupende tusipende lazima tuingize chanzo cha muhimu ambacho tutakipata kwa urahisi,” amesema.

Amesema fedha hizo zinaweza kusaidia wananchi hasa wa vijijini ambao kipato ni kidogo kwa kutowawekea ukomo wa matibabu, kwamba wenye fedha ndogo na matibabu yao yanakuwa hayahusu magonjwa mengine makubwa.
Shabiby alishauri baada ya vyanzo hivyo, Serikali ihamie kwenye vyanzo vingine kama mazao kwa kutoza kila kilo moja Sh1 au Sh2.

“Kama mtu hana laini ya simu ina maana huyo masikini wa kutupwa, huyo hafai hata kuchukuliwa Sh200, atatibiwa kutokana na mifuko,” amesema.

“Sasa hiki kinachokuja, najua wengi mtanishangaa lakini ndio ukweli. Hizi hospitali, zahanati na vituo vya afya vijijini vifikie hatua ya kubinafsishwa. Huo ndiyo ukweli, tuige habari ya Korea Kusini, tusiwe wavivu, nendeni mkaangalie Korea Kusini wanafanya nini Abu Dhabi wanafanya nini,” amesema.

“Korea Kusini hakuna hospitali ya kijijini ambayo ni ya Serikali, hakuna kituo cha afya ambacho ni cha Serikali, zahanati zote zimeingizwa kwenye mfumo mmoja, vituo vya afya vyote vimo kwenye mfumo mmoja,” alisema.

“Lipo jengo kubwa wamejenga watu wa intaneti wapo hapo, ripoti zote zinakwenda kule mtu mwenye zahanati akitaka kulipwa na bima, wale lazima wanakague ile zahanati ilimtibu nini X hapa, kwamba nilimpiga x-ray, lakini nikaona nimtibu malaria nikampa Kwinini (Quinine), wale hawatalipa gharama za x-ray kwa sababu ni utapeli na watalipa gharama za matibabu ya malaria pekee,” alisema.

Alishauri Serikali iwe na mfumo wa aina hiyo utakaobaini wenye vitendo vya utapeli kwenye hospitali na zahanati. Shabiby alisema hospitali zinazopaswa kubaki chini ya Serikali ni zile za rufaa kama Hosptali ya Taifa ya Muhimbili.

Alisema utaratibu huo pia utaondoa tabia ya baadhi ya madaktari wa hospitali za Serikali na ambao wanafanya kwenye hospitali binafsi kuwa madalali wa kupeleka wagonjwa kwenye hospitali binafsi kwa kuziponda za Serikali kwamba hazina vifaa vya kutosha.

Mipango iliyopo ya Serikali ni kuwezesha huduma za bima kwa wote kwa mapato yatokanayo na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vyenye kaboni, vinywaji vikali, bidhaa za vipodozi, michezo ya kubahatisha, ada ya vyombo vya moto, na mapato yatokanayo na ushuru wa miamala ya kielektroniki kwa kadri itakavyopendekezwa.

View attachment 2954755
Nilitaraji ataitaka serikali ijibane na pia iwabane wote waliofisidi michango ya bima na kusababisha kadhia hii.
 
Shabiby nakwambia haya maoni Yako yakipitishwa utalipia line zangu. Ninazo mbili... Wewe kweli wa kitugeuka sisi Ili tukamuliwe... Nimesikitika sana
Kila mbunge angetoa nusu ya mapato wanayovuna wakiwa usingizini...... Wangestahili wapate milioni 5 na the rest zikatumike bima ya afya !!
 
Ni pendekezo la hovyo sana...

1. 2,000 kwa kila mwenye simu its a regressive tax..
2. Simu si kipato au asset, wengi ni kiwezeshi cha mawasiliano. kuanza kukiona kuwa ni mtaji na asset ni uduni wa mawazo.
3. lazima ifanyike study kubwa in the formal na informal sectors na kuainisha kipato kwa kila mmoja katika hizo sector then kuweka kiwango ambacho ni progressive kadiri ya kipato
4. Tusirudie kosa la kodi uzalendo wa sh 1,000 kila mwezi, matozo ukituma na ukipokea muamala etc... na hatuwahi kupata hesabu kamili ya kipato kile kiukaguzi...

Bima ya Afya kwa wote si jambo la kukurupuka..

Wapo wanaokatwa hadi laki 2 kwa mwezi na sasa dawa na huduma nyingi hatupati au tutatoa pesa mfukoni..
 



MY TAKE:

huyu mbunge kwanza hana njaa! magari yake mpaka nauli Tsh 49,000 kutoka Dar kwenda dodoma yaan kila sku yeye anaingiza mamilioni ya hela

Anachukulia poa kuwakamua maskini ili wasaidie maskini wenzao!

yeye anapata mshahara 17Milioni kwa mwezi - Mwalimu anapata laki 3 kwa mwezi! halafu wote mkatwe kwenye simu

Namuombea afe mdomo wazi kama vile anafosi kutoa haja kubwa iliyokaza

Dah! Hayo maombi yako ni haramu mbele za MUNGU
 
Ni pendekezo la hovyo sana...

1. 2,000 kwa kila mwenye simu its a regressive tax..
2. Simu si kipato au asset, wengi ni kiwezeshi cha mawasiliano. kuanza kukiona kuwa ni mtaji na asset ni uduni wa mawazo.
3. lazima ifanyike study kubwa in the formal na informal sectors na kuainisha kipato kwa kila mmoja katika hizo sector then kuweka kiwango ambacho ni progressive kadiri ya kipato
4. Tusirudie kosa la kodi uzalendo wa sh 1,000 kila mwezi, matozo ukituma na ukipokea muamala etc... na hatuwahi kupata hesabu kamili ya kipato kile kiukaguzi...

Bima ya Afya kwa wote si jambo la kukurupuka..

Wapo wanaokatwa hadi laki 2 kwa mwezi na sasa dawa na huduma nyingi hatupati au tutatoa pesa mfukoni..

Ni pendekezo la hovyo sana...

1. 2,000 kwa kila mwenye simu its a regressive tax..
2. Simu si kipato au asset, wengi ni kiwezeshi cha mawasiliano. kuanza kukiona kuwa ni mtaji na asset ni uduni wa mawazo.
3. lazima ifanyike study kubwa in the formal na informal sectors na kuainisha kipato kwa kila mmoja katika hizo sector then kuweka kiwango ambacho ni progressive kadiri ya kipato
4. Tusirudie kosa la kodi uzalendo wa sh 1,000 kila mwezi, matozo ukituma na ukipokea muamala etc... na hatuwahi kupata hesabu kamili ya kipato kile kiukaguzi...

Bima ya Afya kwa wote si jambo la kukurupuka..

Wapo wanaokatwa hadi laki 2 kwa mwezi na sasa dawa na huduma nyingi hatupati au tutatoa pesa mfukoni..
Hakika hili suala la bima kwa wote linahitaji akili kubwa maana regressive tax huwa ni mzigo mzito kwa wenye kipato duni au wasio na kipato na kingine kwa ufanisi upi serikali inaweza simamia hayo makusanyo maana kama hapo awali pesa zimechotwa kwenye mfuko (NHIF) na hazilipwa mpaka leo. Kwanini wasije na mpango wa kupunguza matumizi ya wabunge kama posho, mishahara yao, mafao kwa wake za viongozi, manunuzi ya magari ya kifahari kila mwaka, kudhibiti mianya ya ufisadi ripoti za CAG zinabainisha ufisadi kila mwaka, kuacha safari zisizo na ulazima kwa viongozi hasa nje ya nchi nk. Waache kufikiria mambo rahisi kwa mambo tata kama bima kwa wote
 

Mbunge wa Gairo (CCM), Ahmed Shabiby ameishauri Serikali kukata Sh2,000 kila mwezi kwenye laini za simu huku wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi wakikatwa Sh10,000 ili fedha hizo ziwe chanzo cha mapato kwa Bima ya Afya kwa wote.​


Amesema kuna wamiliki wa laini za simu milioni 72 nchini ambao makato yao kwa mwaka yataingiza Sh1.72 trilioni na zikijumlishwa za Sh10,000 kwa mwezi za wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi, Serikali itapata kwa mwaka takribani Sh2 trilioni.

Shabiby amesema hayo leo wakati akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Pia, ameshauri vituo vya kutolea huduma – hospitali, zahanati na vituo vya afya – vinavyomilikiwa na Serikali vibinafsishwe kama ilivyo Abu Dhabi na Korea Kusini.

Ameshauri madaktari na wauguzi waliopo nchini wajiunge na kubinafsishiwa hospitali badala ya kuwa chini ya Serikali. Shabiby alisema maana ya kutaka laini za simu zitumike kama chanzo cha mapato ni kutokana na anavyoona baada ya Bunge kupitisha muswada wa Bima ya Afya kwa wote na kusainiwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa sheria, kuna hatari bima hiyo ikachangisha wananchi ambao awali walishindwa kuchangia hata Sh10,000 na Sh30,000 za mfuko wa CHF.

Kwa mujibu wa Shabiby, wanufaika wa bima katika Watanzania 100 ni watu wanane ambao wanalipa bima.

“Hasa ukiichukulia hii hatuna chanzo maalumu cha kupata pesa ambazo zinaweza zikasaidia wananchi wa vijijini na watu masikini pamoja na wananchi wa mijini, hata mijini wapo masikini wengi tu, tena hata zaidi ya hao wa vijijini,” amesema na kuongeza:

“Nimeona tulizungumzie bila woga, najua kuna mawazo tutatoa na watu watatukana kwenye mtandao, lakini acha watukane. Hii bima ya afya, ushauri ninaotoa tupende tusipende lazima tuingize chanzo cha muhimu ambacho tutakipata kwa urahisi,” amesema.

Amesema fedha hizo zinaweza kusaidia wananchi hasa wa vijijini ambao kipato ni kidogo kwa kutowawekea ukomo wa matibabu, kwamba wenye fedha ndogo na matibabu yao yanakuwa hayahusu magonjwa mengine makubwa.
Shabiby alishauri baada ya vyanzo hivyo, Serikali ihamie kwenye vyanzo vingine kama mazao kwa kutoza kila kilo moja Sh1 au Sh2.

“Kama mtu hana laini ya simu ina maana huyo masikini wa kutupwa, huyo hafai hata kuchukuliwa Sh200, atatibiwa kutokana na mifuko,” amesema.

“Sasa hiki kinachokuja, najua wengi mtanishangaa lakini ndio ukweli. Hizi hospitali, zahanati na vituo vya afya vijijini vifikie hatua ya kubinafsishwa. Huo ndiyo ukweli, tuige habari ya Korea Kusini, tusiwe wavivu, nendeni mkaangalie Korea Kusini wanafanya nini Abu Dhabi wanafanya nini,” amesema.

“Korea Kusini hakuna hospitali ya kijijini ambayo ni ya Serikali, hakuna kituo cha afya ambacho ni cha Serikali, zahanati zote zimeingizwa kwenye mfumo mmoja, vituo vya afya vyote vimo kwenye mfumo mmoja,” alisema.

“Lipo jengo kubwa wamejenga watu wa intaneti wapo hapo, ripoti zote zinakwenda kule mtu mwenye zahanati akitaka kulipwa na bima, wale lazima wanakague ile zahanati ilimtibu nini X hapa, kwamba nilimpiga x-ray, lakini nikaona nimtibu malaria nikampa Kwinini (Quinine), wale hawatalipa gharama za x-ray kwa sababu ni utapeli na watalipa gharama za matibabu ya malaria pekee,” alisema.

Alishauri Serikali iwe na mfumo wa aina hiyo utakaobaini wenye vitendo vya utapeli kwenye hospitali na zahanati. Shabiby alisema hospitali zinazopaswa kubaki chini ya Serikali ni zile za rufaa kama Hosptali ya Taifa ya Muhimbili.

Alisema utaratibu huo pia utaondoa tabia ya baadhi ya madaktari wa hospitali za Serikali na ambao wanafanya kwenye hospitali binafsi kuwa madalali wa kupeleka wagonjwa kwenye hospitali binafsi kwa kuziponda za Serikali kwamba hazina vifaa vya kutosha.

Mipango iliyopo ya Serikali ni kuwezesha huduma za bima kwa wote kwa mapato yatokanayo na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vyenye kaboni, vinywaji vikali, bidhaa za vipodozi, michezo ya kubahatisha, ada ya vyombo vya moto, na mapato yatokanayo na ushuru wa miamala ya kielektroniki kwa kadri itakavyopendekezwa.

View attachment 2954755
Idea NI nzuri, Ila rekodi ya usimamiz na matumiz ya pesa za watu ndo mbaya Sana, kuamini CCM NI dalili nyingine ya tatizo la kufikiri na akiri finyu...TUTAFIKA hatua tutaanza kumshambulia MTU binafs badala ya mfumo ili kuondoa generalisation. Shabib kuwa bungeni NI matumiz mabaya ya Bunge, aende kwenye biashara zake apambane na kile wafanyabashara walioko nje ya Bunge kadhia wanazopata .
Asome Sera ya JOE BIDEN kuhusu BIMA ya afya na nia aliyokuwa nayo OBAMA..
 

Attachments

  • FB_IMG_1712248285243.jpg
    FB_IMG_1712248285243.jpg
    77.3 KB · Views: 2
Kukurupuka ndo huku tozo (Mwigulu) ziliishia wapi hata kiasi kilichokuwa kikikusanywa hakijulikani
Kuna uwezekano hawa mawaziri kila wiki wana mgao wa pesa kila mmoja si chini ya milioni 10 kwa kila wiki.
Maana pesa ni nyingi sana na wenye pesa wananchi wanezubaa
 
Wanashindwa kujipunguzia pesa za anasa wanazopata, magari ya gharama wanayotumia wao wabunge, mawaziri na manaibu wao, wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi nk wanalipana mishahara minono, posho na kusukuma ndinga za maana bila haja yoyote.

Wapunguze huko mbona hiyo bima inawezekana tu.
 
Kwa staili hii naona huduma ya Posta ya kusafirisha barua ikiimarika kadri siku zinavyosogea!!!
 
Safi sana safi sana mh mbuge wetu hakika umewakilisha mawazo yetu huku jimboni,hiyo elfu 2000 ni ndogo sana ukizingatia uchumi wa mtu mmoja mmoja umeongezeka.Tukatwe elfu 10 TU alafu nyie wawakilishi wetu kwasababu mnakazi ngumu ya kulipigania taifa msikatwe hata 100.
 
Safi sana safi sana mh mbuge wetu hakika umewakilisha mawazo yetu huku jimboni,hiyo elfu 2000 ni ndogo sana ukizingatia uchumi wa mtu mmoja mmoja umeongezeka.Tukatwe elfu 10 TU alafu nyie wawakilishi kwasababu mnakazi ngumu ya kulipigania taifa msikatwe hata 100.
 

Mbunge wa Gairo (CCM), Ahmed Shabiby ameishauri Serikali kukata Sh2,000 kila mwezi kwenye laini za simu huku wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi wakikatwa Sh10,000 ili fedha hizo ziwe chanzo cha mapato kwa Bima ya Afya kwa wote.​


Amesema kuna wamiliki wa laini za simu milioni 72 nchini ambao makato yao kwa mwaka yataingiza Sh1.72 trilioni na zikijumlishwa za Sh10,000 kwa mwezi za wabunge, wafanyabiashara na wafanyakazi, Serikali itapata kwa mwaka takribani Sh2 trilioni.

Shabiby amesema hayo leo wakati akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Pia, ameshauri vituo vya kutolea huduma – hospitali, zahanati na vituo vya afya – vinavyomilikiwa na Serikali vibinafsishwe kama ilivyo Abu Dhabi na Korea Kusini.

Ameshauri madaktari na wauguzi waliopo nchini wajiunge na kubinafsishiwa hospitali badala ya kuwa chini ya Serikali. Shabiby alisema maana ya kutaka laini za simu zitumike kama chanzo cha mapato ni kutokana na anavyoona baada ya Bunge kupitisha muswada wa Bima ya Afya kwa wote na kusainiwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa sheria, kuna hatari bima hiyo ikachangisha wananchi ambao awali walishindwa kuchangia hata Sh10,000 na Sh30,000 za mfuko wa CHF.

Kwa mujibu wa Shabiby, wanufaika wa bima katika Watanzania 100 ni watu wanane ambao wanalipa bima.

“Hasa ukiichukulia hii hatuna chanzo maalumu cha kupata pesa ambazo zinaweza zikasaidia wananchi wa vijijini na watu masikini pamoja na wananchi wa mijini, hata mijini wapo masikini wengi tu, tena hata zaidi ya hao wa vijijini,” amesema na kuongeza:

“Nimeona tulizungumzie bila woga, najua kuna mawazo tutatoa na watu watatukana kwenye mtandao, lakini acha watukane. Hii bima ya afya, ushauri ninaotoa tupende tusipende lazima tuingize chanzo cha muhimu ambacho tutakipata kwa urahisi,” amesema.

Amesema fedha hizo zinaweza kusaidia wananchi hasa wa vijijini ambao kipato ni kidogo kwa kutowawekea ukomo wa matibabu, kwamba wenye fedha ndogo na matibabu yao yanakuwa hayahusu magonjwa mengine makubwa.
Shabiby alishauri baada ya vyanzo hivyo, Serikali ihamie kwenye vyanzo vingine kama mazao kwa kutoza kila kilo moja Sh1 au Sh2.

“Kama mtu hana laini ya simu ina maana huyo masikini wa kutupwa, huyo hafai hata kuchukuliwa Sh200, atatibiwa kutokana na mifuko,” amesema.

“Sasa hiki kinachokuja, najua wengi mtanishangaa lakini ndio ukweli. Hizi hospitali, zahanati na vituo vya afya vijijini vifikie hatua ya kubinafsishwa. Huo ndiyo ukweli, tuige habari ya Korea Kusini, tusiwe wavivu, nendeni mkaangalie Korea Kusini wanafanya nini Abu Dhabi wanafanya nini,” amesema.

“Korea Kusini hakuna hospitali ya kijijini ambayo ni ya Serikali, hakuna kituo cha afya ambacho ni cha Serikali, zahanati zote zimeingizwa kwenye mfumo mmoja, vituo vya afya vyote vimo kwenye mfumo mmoja,” alisema.

“Lipo jengo kubwa wamejenga watu wa intaneti wapo hapo, ripoti zote zinakwenda kule mtu mwenye zahanati akitaka kulipwa na bima, wale lazima wanakague ile zahanati ilimtibu nini X hapa, kwamba nilimpiga x-ray, lakini nikaona nimtibu malaria nikampa Kwinini (Quinine), wale hawatalipa gharama za x-ray kwa sababu ni utapeli na watalipa gharama za matibabu ya malaria pekee,” alisema.

Alishauri Serikali iwe na mfumo wa aina hiyo utakaobaini wenye vitendo vya utapeli kwenye hospitali na zahanati. Shabiby alisema hospitali zinazopaswa kubaki chini ya Serikali ni zile za rufaa kama Hosptali ya Taifa ya Muhimbili.

Alisema utaratibu huo pia utaondoa tabia ya baadhi ya madaktari wa hospitali za Serikali na ambao wanafanya kwenye hospitali binafsi kuwa madalali wa kupeleka wagonjwa kwenye hospitali binafsi kwa kuziponda za Serikali kwamba hazina vifaa vya kutosha.

Mipango iliyopo ya Serikali ni kuwezesha huduma za bima kwa wote kwa mapato yatokanayo na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vyenye kaboni, vinywaji vikali, bidhaa za vipodozi, michezo ya kubahatisha, ada ya vyombo vya moto, na mapato yatokanayo na ushuru wa miamala ya kielektroniki kwa kadri itakavyopendekezwa.

View attachment 2954755
Hayo ndio mawazo ya watu wenye akili nzuri !
Sio hoja kuwa na madigirii mengi kwenye makaratasi halafu kichwani ni peupe inakuwa ni Kazi bure !

Naunga mkono wazo la Shabiby !
Jamaa yupo vizuri !
 
Na vipi Hela wanazojikopesha, na hazirudi kukopi mambo ya Korea kusini TAIFA ambalo liko mile 1000000000 zaidi yetu Kwa Kila kitu ni uzwazwa
Umeme tu shida hyo mifumo SI ndo itadukuliwa umeme ukiwa umezima na kuchota Hela zote, naona kama Mzee wa SKAFU SHINGONI ANATIKISA KALAMU NJISI SHA-BABY ALIVYOMUKOSHA NA DILI JINGINE BAADA YA TOZO
 
Back
Top Bottom