Mbunge wa Geita Mjini anatia mashaka. Anataka kusema Musukuma ni muongo?

Mbunge wa Geita Mjini anatia mashaka. Anataka kusema Musukuma ni muongo?

Na kama kuna wakurugenzi wengine wanalionunuliwa V8?

Amandla...
Kama ni utaratibu unaokubalika kwa wote basi hana makosa kisheria japo bado morally ana makosa. Halmashuri zenye hospital ambazo wajawazito wanaambiwa wanunue hata gloves kupoteza fedha kwa kununua gari kama hili ni zaidi ya ushetani.
 
Nimemsikiliza mbunge wa Geita mjini ndugu Costantine Kanyasu kwa kweli anashangaza sana. Nini kimemfanya akurupuke kuanza kutoa maoni kama haya kabla ya uchunguzi?

Nilimsikiliza waziri Jaffo alipopewa kazi yake ya kwanza kuunda tume kuchunguza ubadhilifu halimashauri ya Geita,alisema pesa mil 400 zilizotumika hazikupitishwa na baraza la madiwani.

Nashangaa nimemsikiliza mbunge wa Geita anaongea na media na kudai kuwa amepitia document hapo halmashauri na amebaini kuwa pesa hizo zilipitishwa na baraza la madiwani,pia anasisitiza Gpsa walitumiwa kununua hilo gari la mil 400,kwa hiyo taratibu zote zilifuatwa maana Gpsa ndie wakala wa manunuzi wa serikali.

Mbali na hayo anasema mkurugenzi aliyesimamishwa ni muadilifu na amekuwa akipambana na ufisadi kwa muda mrefu. Je ina maana Mbunge wa Geita vijijini ni muongo? Anaropoka hovyo na kumdanganya rais,maana huyu ndie aliyemlipua mkurugenzi kuwa alifanya ubadhirifu wa mil 400.
Kumuamini Msukuma unahitaji kwanza kuondosha ubongo kichwani... ama si yeye aliyeaminisha watu kuwa "mamvi" alikuwa "akijinyea!!??"
 
Tatizo we huelewi sababu zinazofanya wanunue magari ya mil 400.

Ni hivi!, sababu inayofanya wanunue magari ya bei kubwa ni kwa sababu yanadumu muda mrefu na hayaharibiki ovyo ovyo.

Ni bora kununua gari ya mil 400 itakayodumu kwa miaka 15 kuliko kununua gari ya milioni 70 itakayokuwa inahitaji matengenezo ya mara kwa mara na haiwezi kudumu kwa muda mrefu

Ni sababu za kiuchumi zaidi na sio kwamba walikaa wakakurupuka kwa matakwa yao binafsi, na hizi standard zimewekwa na serikali yenyewe na sio kwamba mkurugenzi kajiamulia tu!.
Hili utawafunga kamba wajinga lakini siyo watu wanaojua. Kwamba gari likiwa la bei kubwa ndiyo linadumu? Are you serious? Mimi nina uzoefu na magari na nakukuhakikishia kuna magari ya bei ndogo zaidi ya hili na servises zake + spare parts ni rahisi kuliko hili.
 
Kwani mimi nimekataa kwamba siyo wajumbe wa mabaraza ya madiwani ? Mbona una mambo ya ajabu sana wewe ? Nimesema msukuma siyo diwani wa GTC bali ni diwani wa GDC. Sasa wewe unalazimisha eti anaweza kuhudhuria Baraza la GTC kwa kigezo kipi ? Unajua kiwango cha elimu yangu au unajitekenya tu. Uwe na adabu basi unapoongea na watu wanaojua.
Kaa kimya, kama huwezi kasome sheria ya Tawala za mikoa serikali za mitaa,ndio maana Msukuma anakomaa anajua anachokifanya. Wote ni wajumbe wa wa mabaraza ya madiwani.
 
Mbona chaguzi za maigizo za waunga juhudi zilitumia mabilioni ya shiling, lakini hatukuskia izi kelele za matumizi mabaya ya pesa?

Ifikie kipindi watanzania tuache unafiki, haya yote ni kwa sababu rais kaongelea hili suala. na tunachokiona hapa ni unafikk wa baadhi ya watu kujifanya wana uchungu wa fedha za kodi za watanzania .....cha ajabu wanachagua fedha gani wawe na uchungu nazo!.
Hukusikia kelele? Ulikuwa wapi? Mbona wapinzani walilia sana na kusema ni upotevu wa muda, fedha na hakuna faida yoyote zaidi ya hasara? Kama unazungumzia hao wabunge basi ni kundi la mafisadi. Hata kelele wanazopiga ni kwa sababu wamezidiana maslahi na siyo kweli kuwa wana uchungu. Lakini haindoi ufisadi wa gari uliofanyika.
 
Hili utawafunga kamba wajinga lakini siyo watu wanaojua. Kwamba gari likiwa la bei kubwa ndiyo linadumu? Are you serious? Mimi nina uzoefu na magari na nakukuhakikishia kuna mgari ya ndogo zaidi ya hili na servises zake + spare parts ni rahisi kuliko hili.
Kwa hyo unafananisha ki vitz chako kinachozunguka hpo hpo mjini hakimalizi hta km 20 kwa siku na gari ya mkurugenzi ambayo iko very busy kila siku ikitembea kilomita za kutosha tena kwenye barabara mbovu za vijijini?

Kwa mikiki ya kazi za serikali ukinunua gari ya mil 70 haitomaliza miaka 3 itakuwa ishakufa.
 
Msukuma alinyimwa mgao!

Nilitaka nisiandike lakini imebidi kuandika tuu
Ukweli huwa nakukubali sana Post zako Mkuu!
Unaongea Ukweli haswa zinazohusu CCM!
Msukuma kakosa Mgao tuu!
Yaani mi ningekuwa Mkubwa Nchi hii au Dunia hii...
Siwezi Kushawishiwa na Mtu kufanya Maamuzi eti kwa kuwa anaenishawishi ni Muongeaji sana au Ameshasema kwenye Media!
Hivi Kuna Magari mangapi ya Aina hiyo serekalini Mashirika,Halmashauri,Nk,nk?
Ika Kaongea Musukuma kasikilizwa Kafurahiiii katukuzwa kuwa akiongea kitu tuu kazima Kisikilizwe na Kitekekezwe!
Sometime inauma Ukiona Mtu anaonewa,
Basi tuu!
Hongera Kanyasu kwa kusema hivyo ingawa Unaweza Usisikilizwe kabisa,Sababu alieanza Kashasikilizwa na Kutekelezewa aliyoyasema!
 
Uchaguzi huwa unarudiwa kwa mujibu wa sheria,je bajeti ya kurudia uchaguzi mdogo huwa ni sh ngapi? Je huwa zinachachuliwa?
Kwa hyo hilo gari limenunuliwa kwa mujibu wa nn!?

Maana tunaambiwa hadi ofisi ya waziri mkuu iliridhia.
 
Kwa hyo unafananisha ki vitz chako kinachozunguka hpo hpo mjini hakimalizi hta km 20 kwa siku na gari ya mkurugenzi ambayo iko very busy kila siku ikitembea kilomita za kutosha tena kwenye barabara mbovu za vijijini?

Kwa mikiki ya kazi za serikali ukinunua gari ya mil 70 haitomaliza miaka 3 itakuwa ishakufa.
Kwanini umekimblia kusema Vitz? Ndiyo gari la rahisi tu au ni ndiyo gari la rahisi unalolijua tu?
 
Hapana tunazungumzia mambo yenye ushahidi,,hili la wabunge kununuliwa mimi sina hakika,,labda utuletee uthibitisho
Naona una act km umeona utupu wa mama mkwe, unaona live kbsa yupo uchi ila unajifanya huoni.

Na huu unafiki ninaoukataa.
 
Mbona kwenye kampeini za mkulu misafara yake ilikuwa imesheeni magari hayo hayo ya bei mbaya,na hakuna aliyehoji.
Au Geita ndiyo halmashauri pekee yenye gari la aina hiyo nchini?.
Acheni kumtoa kafara mkurugenzi wa watu.
Wabongo wanafiki sana mkuu.
 
Kwani mimi nimekataa kwamba siyo wajumbe wa mabaraza ya madiwani ? Mbona una mambo ya ajabu sana wewe ? Nimesema msukuma siyo diwani wa GTC bali ni diwani wa GDC. Sasa wewe unalazimisha eti anaweza kuhudhuria Baraza la GTC kwa kigezo kipi ? Unajua kiwango cha elimu yangu au unajitekenya tu. Uwe na adabu basi unapoongea na watu wanaojua.
Ahaaaa, mbona anamandate ya kuingia kwenye vikao vya baraza la madiwani? Sababu ni mbunge wa jimbo ndani ya wilaya ya Geita. Mbona anahoji juu ya pesa za Csr bil 10? Mbona alipigwa mabomu ili wapate pesa za Csr yeye na madiwani wenzake na kuswekwa ndani

Unaweza kuwa umesoma lakini hujaelimika,ndio maana hujui muundo wa baraza la madiwani.
 
Hawa wasukuma Bwana Naona wanashida vichwani mwai.Infact ulimsikiliza yule mkurugenzi inaonekana taratibu zote zilifuatwa Kama mpaka ofisi ya waziri mkuu ilitia nataka then Naona yule mkurugenzi Hana kosa na ninachokiona Hapo kuna hidden agenda.Mgao
Tatizo kubwa ni origin ya wazo! Hakuna anayebisha kuwa taratibu hazikufuatwa. Unapopanga kitu lazima uwe na uhakika kama kipo katika sheria na taratibu za kazi katika daraja lako. Hivi unajua kuwa ukikuta katika akaunti yako imeigizwa let say million 100 ukazitumia ni kosa la jinai? Kosa lake ni kuomba kibali cha kununua gari lililo juu ya stahiki yake. @nyankurungu200
 
Nimemsikiliza mbunge wa Geita mjini ndugu Costantine Kanyasu kwa kweli anashangaza sana. Nini kimemfanya akurupuke kuanza kutoa maoni kama haya kabla ya uchunguzi?

Nilimsikiliza waziri Jaffo alipopewa kazi yake ya kwanza kuunda tume kuchunguza ubadhilifu halimashauri ya Geita,alisema pesa mil 400 zilizotumika hazikupitishwa na baraza la madiwani.

Nashangaa nimemsikiliza mbunge wa Geita anaongea na media na kudai kuwa amepitia document hapo halmashauri na amebaini kuwa pesa hizo zilipitishwa na baraza la madiwani,pia anasisitiza Gpsa walitumiwa kununua hilo gari la mil 400,kwa hiyo taratibu zote zilifuatwa maana Gpsa ndie wakala wa manunuzi wa serikali.

Mbali na hayo anasema mkurugenzi aliyesimamishwa ni muadilifu na amekuwa akipambana na ufisadi kwa muda mrefu. Je ina maana Mbunge wa Geita vijijini ni muongo? Anaropoka hovyo na kumdanganya rais,maana huyu ndie aliyemlipua mkurugenzi kuwa alifanya ubadhirifu wa mil 400.
hayo yote ni matapeli ya CCM
 
Nimemsikiliza mbunge wa Geita mjini ndugu Costantine Kanyasu kwa kweli anashangaza sana. Nini kimemfanya akurupuke kuanza kutoa maoni kama haya kabla ya uchunguzi?

Nilimsikiliza waziri Jaffo alipopewa kazi yake ya kwanza kuunda tume kuchunguza ubadhilifu halimashauri ya Geita,alisema pesa mil 400 zilizotumika hazikupitishwa na baraza la madiwani.

Nashangaa nimemsikiliza mbunge wa Geita anaongea na media na kudai kuwa amepitia document hapo halmashauri na amebaini kuwa pesa hizo zilipitishwa na baraza la madiwani,pia anasisitiza Gpsa walitumiwa kununua hilo gari la mil 400,kwa hiyo taratibu zote zilifuatwa maana Gpsa ndie wakala wa manunuzi wa serikali.

Mbali na hayo anasema mkurugenzi aliyesimamishwa ni muadilifu na amekuwa akipambana na ufisadi kwa muda mrefu. Je ina maana Mbunge wa Geita vijijini ni muongo? Anaropoka hovyo na kumdanganya rais,maana huyu ndie aliyemlipua mkurugenzi kuwa alifanya ubadhirifu wa mil 400.


Hawa waliokosa uwaziri wana mambo mengi kichwani. Halafu pengine hawaelewani na Msukuma. Siasa nazo mara nyingine mtihani sana
 
Tungetanguliza utu, uzalendo, upendo, na uadilifu, maamzi ya kufanya hicho mlichofanya Geita na maeneo mengine kisingefanyika.

Gari moja 400M, tena sio ambulance wala grader kwa ajili ya kutengeneza miundombinu, ni gari la kumbeba kiongozi! Hizo fedha za ndani ni fedha mlizokusanya kwenye shughuli za mikono ya walalahoi, bila huruma, mkurugenzi na menejiment yako mkakusudia kununua gari hilo.

Kuweni na utu jamani. Mnataka hadi maamuzi ya kizalendo aje Mh awasimamie? Sasa Mh Rais atafanya kazi ngapi?

Wakati Mh Rais anahangaika kutafuta pesa kwa ajili ya kujenga miundombinu wakati mwingine hadi kukopa, wengine huku mnatumia hela kwa utaratibu huo, kuna haja gani ya kukopa na kuongeza deni la Taifa wakati hela matumizi yetu yanakuwa kama hayo?

Tumtangulize Mungu katika maamuzi yetu, na utu kwanza.
Hapo kwenye sentensi ya kwanza nimepapenda!
Kwani hizo sifa ulizozitaja zinapatikana wapi hapa duniani nje ya utawala wa awamu ya 5 chini ya JPM? ....au hili limefanyika nchi nyingine/awamu nyingine?
Haya, tunaosubiri tuendelee kusubiri viwanda vikubwa vya kuzalisha nguo na hata magari na badae kuwapelekea wazungu 'used' kutoka tz
 
Tatizo kubwa ni origin ya wazo! Hakuna anayebisha kuwa taratibu hazikufuatwa. Unapopanga kitu lazima uwe na uhakika kama kipo katika sheria na taratibu za kazi katika daraja lako. Hivi unajua kuwa ukikuta katika akaunti yako imeigizwa let say million 100 ukazitumia ni kosa la jinai? Kosa lake ni kuomba kibali cha kununua gari lililo juu ya stahiki yake. @nyankurungu200
Kama anakosa la kuomba kibali ambacho ni juu ya uwezo wake kwa nini Gpsa walinunua? Kwa nini PM alitoa kibali? Kwa nini ujenzi watoe spicifications?
 
Wakati huo alikuwa ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa GEITA
Ahaaaa, mbona anamandate ya kuingia kwenye vikao vya baraza la madiwani? Sababu ni mbunge wa jimbo ndani ya wilaya ya Geita. Mbona anahoji juu ya pesa za Csr bil 10? Mbona alipigwa mabomu ili wapate pesa za Csr yeye na madiwani wenzake na kuswekwa ndani

Unaweza kuwa umesoma lakini hujaelimika,ndio maana hujui muundo wa baraza la madiwani.
 
Back
Top Bottom