Mbunge wa Geita Mjini anatia mashaka. Anataka kusema Musukuma ni muongo?

Mbunge wa Geita Mjini anatia mashaka. Anataka kusema Musukuma ni muongo?

Nafahamu sana mkuu wa wilaya ni mmoja tu lakini Halmashauri ni mbili na majimbo ya uchaguzi ni matatu. Geita mjini, Geita vijijini na Busanda. Mchakato uliopo ni kuanzisha Wilaya kamili si Halmashauri tu ya Katoro/Buseresere. Nadhani umenipata
Ndio maana nakuambia kuna namna hapa. Any way tusubiri tume ya Jaffo.
 
Mleta mada, kumbuka kuwa Musukuma ni mbumbumbu wa darasa la 7 tu...yeye uwa anakurupuka tu vitu kama vile Trump.
 
Tungetanguliza utu, uzalendo, upendo, na uadilifu, maamzi ya kufanya hicho mlichofanya Geita na maeneo mengine kisingefanyika.

Gari moja 400M, tena sio ambulance wala grader kwa ajili ya kutengeneza miundombinu, ni gari la kumbeba kiongozi! Hizo fedha za ndani ni fedha mlizokusanya kwenye shughuli za mikono ya walalahoi, bila huruma, mkurugenzi na menejiment yako mkakusudia kununua gari hilo.

Kuweni na utu jamani. Mnataka hadi maamuzi ya kizalendo aje Mh awasimamie? Sasa Mh Rais atafanya kazi ngapi?

Wakati Mh Rais anahangaika kutafuta pesa kwa ajili ya kujenga miundombinu wakati mwingine hadi kukopa, wengine huku mnatumia hela kwa utaratibu huo, kuna haja gani ya kukopa na kuongeza deni la Taifa wakati hela matumizi yetu yanakuwa kama hayo?

Tumtangulize Mungu katika maamuzi yetu, na utu kwanza.
Wakati wanasaidia kuiba kura nadhani utu ulikuwa likizo maana hutukuona post hizi wakati huo
 
Hii ishu wa ununuzi wa gari Geita ina agenda za siri kwani serikali ilishatoa muongozo wa ununuzi wa magari serikalini ambapo
haiwezekani taasisi ya seriakali kununua gari bila ya kuwa na kibali cha WAZIRI MKUU mwenyewe (Kasim Majaliwa)
halafu magari yote ya serikali kwa sasa yananunuliwa kupitia GPSA baada ya kibali cha PM.
Kwa mtazamo wangu hata kama halmashauri ilipanga imnunulie Mkurugenzi gari la Fedha hiyo na ikatenga fedha za ununuizi wa gari hilo na madiwani wakapitisha bajeti hiyo
Waziri Mkuu angeweza kuzuia kibali cha ununuzi wa gari hilo kama vipi na yeye awajibiswe kwani utaratibu ulibadilishwa na yeye kufanywa ndio muidhinishaji wa ununuzi wa magari ya serikali ili kuzuia taasisi kununua magari ya kifahari na pia ununuzi wa magari yasiyokuwa na kazi ya msingi au ulazima.
Yaani kwa utaratibu uliopo sasaivi ili kununua gari serikalini taasisi pamoja na kutenga fedha hizo kwenye bajeti lazima ijipange na sababu za msingi za kumshawishi WAZIRI MKUU ili awape kibali cha kununua gari na mara nyingine alikuwa anazikatalia taasisi nyingine , kwa hili la geita imetokea nini kwa waziri mkuu
Kanyasu ni mbunge na diwani wa halmasauri ya geita inawezekana anafahamu huo mchakato na kufahamu kwamba taratibu zilifuatwa hivyo anaona DED ameonewa
DED mbuzi wa kafara tu

Ova
 
Mitano Teeena[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Hata kama hawezi kujiamulia mambo. Kitendo cha kupeleka pendekezo la kununua gari la kutembelea lenye thamani ya mil 400 kwenye nchi yenye ufukara kama Tanzania kinaonyesha hafai kuwa kiongozi. Uongozi ni pamoja na kuwa na busara ya kutotumia gharama fedha za umma bila ulazima hata kama taratibu zinaruhusu. Labda tuseme kinachotakiwa kufanywa ni huyo mkurugenzi kuondolewa mara moja pamoja na wote waliopitisha huo mchakato.
Na kama kuna wakurugenzi wengine wanalionunuliwa V8?

Amandla...
 
Ka uekwa wangu manuuzi ya Serikali huwa ya kafuata taratibu zote. Lazima hao gpsa wafanya yao. Na ununuzi wa gari lazima Timu ya wataalam, Fullcouncil, OR TAMISEMI la,IMA washiriki. Haina shaka kwamba DED hatakutwa popote km ubadhirifu,labda tu why anunue la 400 wkt ya 120 yapo.
True, ila kumbukeni Gari kama hilo mara nyingi ni kwa ajili ya Council Chair, maana ni mtu mukubwa na anapoongozana na viongozi wakubwa na yeye awe na hadhi stahili. Hao ndio waliomshinikiza DED kununua gari hilo.
 
Unamlaumuje Mkurugenzi wa Halmashauri kutumia pesa ambayo haikiidhinishwa na baraza la madiwani ilhali Rais anatumia fedha ambazo hazijaidhinishwa na bunge?

Tukimuwajibisha Mkurugenzi, nani atamuwajibisha Rais.
 
Back
Top Bottom