Tetesi: Mbunge wa Simanjiro, James Ole Millya kuhamia Chama cha Mapinduzi muda wowote kuanzia sasa

Tetesi: Mbunge wa Simanjiro, James Ole Millya kuhamia Chama cha Mapinduzi muda wowote kuanzia sasa

Baada ya kuhamia CCM utasikia majibu ya upande wa pili kuwa 'hata hivyo tulikuwa mbioni kumsimamisha na kumfukuza kabisa uanachama kwa tuhuma kadha wa kadha'.
Wakisema kwani kuna tatizo
 
Umeongea hoja nzuri.
Tatizo ni kutopokea ushauri.
Dr. Slaa aliuliza kama hawa watu ni asset au liability.

Kabla hajajibiwa kastukia washapewa nafasi za ugombea kuwakilisha chama kwenye uchaguzi mkuu.
Mfuate huyo slaa wako sisi kwetu ni sawa na busati
 
Si huwa mnajisifu humu kwamba watu wa kaskazini mnajitambua.
Sasa haya yanayotokea yanawavua nguo.

Kuna mzee mmoja aliniambia wafrika wote akili zao zinafanana. Uende west east north au south wote sawa tu.
 
Ole Milya na yule Mbunge wa Monduli ni vijana wa Lowasa, wote kuondoka ndani ya muda wa wiki moja ni meseji tosha nini kinafuata kuhusu Lowasa. CDM walifanya kosa kubwa sana 2015 kumpa Lowasa kijiti mbaya zaidi ni kama wamechanganyikiwa hawana akili wala uwezo wa kuonyesha nini cha kufanya.

Magu amedhamiria kuidondosha CDM, na kweli inaenda kudondoka, wote ambao walikuwa wana akili au uwezo wa kuisaidia CDM walishafukuzwa au kuwekwa pembeni. Mnyika na kina Prof Baregu ni wazi wamemsusia Mbowe azame na “jahazi” lake. Nimeikumbuka ile cream ya CDM ikiongozwa na Dr Slaa, Zitto na Mnyika. Nyuma ya pazia kukiwa na wana mikakati kama Prof Baregu na Prof Mkumbo. Hii ndio cream iliyoipaisha CDM, Wote hao hawapo CDM saivi au wameamua kuwa viongozi wafu, CDM jahazi linazama.

Mwisho na muhimu, nyumbxxx wa CDM watambue kinachouliwa ni CDM na sio upinzani, ilikufa NCCR ikija CUF, ikafa CUF ikaja CDM, na sasa CDM tayari ina kiharusi 2020 tunaizika, wazee wa fursa ni muda wa kujiongeza tu huu.
Wewe una akili gani wakati unaburuzwa kama punda au mbuzi kupelekwa malishoni?
 
Ina maana baada ya kushindwa kumshawishi aje kwenu ndio maana mkamtafutia wasiyo julikana hadi sasa wamuondoe dunuani?
unachokijibu na nilichokiandika ni vitu viwili tofauti kma una jeuri kawazuie hayo madude yenu mliyokuwa mnajitapa nayo yasinunuliwe, chama gani kinakuwa na watu wa kununuliwa halafu kinataka kitawale nchi...toa boliti ya jicho lako kwanza..
 
Mbunge wa Simanjiro James Ole Millya,kuhamia Chama cha Mapinduzi muda wowote kuanzia sasa. Millya ni miongoni mwa wabunge wa Upinzani wenye ushawishi kanda ya kaskazini kutokana na uzoefu wa siasa za kanda hiyo.

=======
Sijawahi kutilia shaka taarifa zako mkuu , Tunamtakia kila la heri
 
unachokijibu na nilichokiandika ni vitu viwili tofauti kma una jeuri kawazuie hayo madude yenu mliyokuwa mnajitapa nayo yasinunuliwe, chama gani kinakuwa na watu wa kununuliwa halafu kinataka kitawale nchi...toa boliti ya jicho lako kwanza..
Jibu swali kwanza wewe kindururu
 
Hii biashara haiwasaidi lakini kwa aibu hawawezi kuiacha maana watachekwa (wataulizwa imeleta tija gani) hivyo watajitutumua tu kuendelea nayo kuliko ku-surrender.

Eti hawa ndio watu wa kuipeleka Tanzania kufikia katika uchumi wa kati!!

Wabongo mtasubiri sana!!
Biashara ya kipumbavu kuwahi kutokea duniani. Inatia kinyaa kumuunga mkono Rais kwa kuliiingiza taifa hasara ya mabilioni?
 
Jibu swali kwanza wewe kindururu
hapa tunaongelea wabunge wenu kununulika, hoja y lissu kupigwa lisasi ilishaisha, ukitaka kuijadilI nenda kwenye hizo nyuzi, zipo kibao...hlf usiwaite watu kwa majina ya kishamba jadili kilichopo hpa, kma huna majibu piga kimya.
 
Hii style mpya tutakuwa kumepewa na jamaa wa Rwanda maana yeye kule wapinzani ameshawamaliza wote; kabakia yule dada naye kesi kibao kila kukicha ni mahakamani...Mungu anawaona wajue...
 
Biashara ya kipumbavu kuwahi kutokea duniani. Inatia kinyaa kumuunga mkono Rais kwa kuliiingiza taifa hasara ya mabilioni?
Hapa ndipo inafikia hatua unajiuliza hivi CCM hawa wana nia njema kabisa na taifa hili
 
Wewe una akili gani wakati unaburuzwa kama punda au mbuzi kupelekwa malishoni?
Matusi, dharau na kejeli hayajibu matatizo yenu. CDM inadondoka kutokona kuwa na wanazi wa aina yako, hamko tayari kuupokea ukweli, sasa kesheni mkitukana na kujiliza liza hapa ila 2020 hiyo Saccos inadondoshwa:
 
Mfuate huyo slaa wako sisi kwetu ni sawa na busati
Busati lina thamani kuliko suruali ya suti kama lilikuwa linakusitiri usiteleze na kuchana suruali ukaacha msamba nje.
Thamani yake ni kubwa kuliko hiyo suruali ambayo imechanika msamba inakuacha mtupu.
Busati linaweza kukusitiri usipigwe na baridi ya sakafuni ukiwa miguu tupu

Dr. Slaa alikuwa busati ambalo linamsitiri Mbowe asioneshe mapungufu yake kiuongozi. Sasa halipo mapungufu yapo wazi mbowe ana adhirika na huku baridi kali linawapiga CHADEMA miguuni kiasi wanashindwa kutembea kusonga mbele wapo wanarudi sakafuni kwenye baridi kali zaidi kama enzi za chama kikiwa kichanga.
 
Back
Top Bottom