TANZIA Mbunge wa zamani, Nimrod Mkono amefariki dunia nchini Marekani

TANZIA Mbunge wa zamani, Nimrod Mkono amefariki dunia nchini Marekani

Huyu mtu achana naye, amejenga masecondary Butiama kwa pesa zake binafsi akazipa majina ya machifu wa kizanaki na kuzikabidhi shule zote serikalini ni Mali ya serikali, Hakuna hata shule moja amejipa jina lake, siyo Utapeli kama wa kina Gertrude Lwakatare na Saint Marys zake kumbe zilitakiwa kusomesha yatima bure.

Leo kuna majitu yanapenda tu vitu vya umma kupachika majina yao kiholela tu.
Kamrisho Gambo kapuuzi ka juzi tu, na kenyewe kalijipa shule, kakiwa kamkuu ka mkoa. Kalionea na kuibia watu sanaaa
 
Nailaumu sana Serikali ya Awamu ya Tano ( ya Hayati Magufuli ) na Watendaji wake hasa Ofisi ya Bunge chini ya aliyekuwa Spika Ndugai.

Kwanini?

Kuondoka kwa Marehemu Mzee Mkono kwenda huko alikofia ( nchini Marekani ) hakukutokana na Matakwa yake bali ni Utashi wa Mkewe ( Mama Leah ) na Binti mkubwa wa Marehemu Leah.

Mgogoro

Ndani ya miaka Mitano au Sita hii kumekuwa na Mgogoro mkubwa kwa Familia ya Marehemu Mzee Mkono ulioratibiwa vyema na Mkewe ( ambaye nimeshangaa leo kusikia eti nae alikuwa analia ) wakati Yeye na .Bintiye huyo Leah wamechangia Kumtesa na Kumdhalilisha Mzee wa Watu Marehemu Nimrod Mkono.

Tamaa ya Mali

Sababu Kuu ya Marehemu Mzee Mkono kupelekwa kuishi Kimasikini ( katika Nyumba za Kulea Wazee wasiojiweza ) huko Marekani ni Mkakati wa Bintiye Leah na Mama yake ( Mjane ) kujimilikisha Mali za Baba yake ambazo wamefanikiwa kwa 85% japo kuna mahala walikwama ili kumalizia hiyo 15% iliyobakia.

Cha Kusikitisha

Mkewe ( Mjane ) tokea amsafirishe Mumewe huko nchini Marekani amekuwa akimzuia Marehemu Mzee Mkono asiwe anawasiliana na Nduguze ( Wadogo zake ) Mzee Zadock Mkono ( Baba Mzazi wa Msanii Nahreel ) na Dokta Japhet Mkono mwenye Vituo vyake vya Afya viitwayo Salama Kimara Baruti na Sinza.

Kila mara Ndugu Hawa Watajwa wa Marehemu Mzee Mkono walipokuwa wakijaribu Kumpigia Simu Kaka yao huko Marekani alikokuwa Mkewe ( Mjane Mama Leah ) alikuwa akimpokonya Simu Mumewe huku akiwajibu hovyo Mashemeji zake hawa.

Miaka Minne ( 4 ) iliyopita Mzee Mkono ( sasa Marehemu ) alipokuwa bado hajapelekwa Nyumba za Kutunzia Wazee Wasiojiweza alidiriki kuamka Usiku na kwenda Chooni kisha kuwapigia Simu Wadogo zake walioko Tanzania ( Zadock na Dokta Japhet ) kuwa wamfuate kwani anateseka na anataka kurudi Tanzania ila Mkewe Mama Leah ( sasa Mjane ) akawa anawajibu kuwa Mzee Mkono haumwi na hana shida.

Kwanini lawama kwa Hayati Magufuli na Spika Ndugai?

Baada ya kutokea kwa hali hii na huu Mgogoro baadhi ya Marafiki Wakubwa na Wazanaki Wenzake Mzee Butiku na Mzee mwingine ( namhifadhi ) aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Nje na Msaidizi wa Karibu wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa Kushirikiana na Wadogo hawa wa Marehemu Mzee Mkono waliomba Msaada kutoka Serikalini na Bungeni ili Mzee Mkono arejeshwe Tanzania ila Bintiye Leah kwa Kushirikiana na Watu wa Serikali na Bungeni waliweza Kudanganya Watu wa Ikulu na Ofisi ya Bunge huku baadhi ya Nyaraka za Hali ya Mzee Mkono zikifojiwa ( kwa Msaada wa Mbunge Mmoja ) ambaye amezaa na Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu ) Kuonyesha kuwa Mzee Mkono hana matatizo huko aliko.

Lengo Kuu la Bintiye Mzee Mkono ( sasa Marehemu ) la kufanya hivyo ni kuendelea Yeye kama Yeye kupokea Pesa zote za Mshahara wa Bunge wa Baba yake na Malipo mengine yote ya Bungeni Kitu ambacho kwa 99% alifanikiwa na Pesa zingine akawa Anamtumia Mama yake ( Mratibu Mkuu wa Mateso ya Mzee Mkono huko alikofia nchini Marekani ) na Pesa zingine zikitumika Kuhongea Watu wa Serikalini na Bungeni ili Waamini Uwongo wa Leah kuhusu hali ya Baba yake ( sasa Marehemu )

Balaa alilolisababisha Binti wa Marehemu Leah Mkono

Leah Mkono ndiye kasababisha Kampuni ya Uwakili ya Baba yake Kufilisika na Kufungwa huku baadhi ya Floor pale Exim Bank kupokonywa.

Leah Mkono amesababisha Kampuni ya Baba yake kuwa na Madeni makubwa ambayo kwa sasa yanamfanya aishi kama DigiDigi kwa Kukimbia, Kujificha na Kuhamahama Mitaa na Mikoa.

Leah Mkono kasababisha mpasuko mkubwa baina ya Watoto wa Marehemu Wambura, Walter ( Mkono Junior ) na Mirembe.

Miaka Minne ( 4 ) nyuma Leah kwa Tamaa zake alitaka Kuiuza Nyumba ya Baba yake ( sasa Marehemu ) Mzee Mkono ila Kaka yake Mkono Junior ( Walter Mkono ) Mtoto pekee wa Kiume wa Marehemu akakataa ndipo Dada yake akapiga Simu Kituo cha Polisi cha Oysterbay na Kuwadanganya kuwa Kaka yake anamfanyia Fujo ambapo kweli alikamatwa ila aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani kipindi hicho Kangi Lugola na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ( sasa IGP ) Camilius Wambura ( Wote hawa kutokea Mkoa wa Mara atokako Marehemu Mzee Mkono ) Mmoja akiwa ni Mkurya ( Lugola ) na mwingine akiwa ni Mzanaki ( IGP Wambura ) waliingilia kati na Kijana huyo wa Mkono Walter kutoka Polisi Oysterbay.

Leah ametengeneza Uadui mkubwa baina ya Wafanyakazi ( hasa Chacha aliyekuwa Dereva Mkuu wa Marehemu Baba yake ), Waliokuwa Wafanyakazi wa Kampuni ya Uwakili ya Baba yake, Ndugu za Baba yake na Marafiki Wakubwa akiwemo Mzee Butiku ( Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ) na huyo Mzee mwingine ( niliyemhifadhi Jina ) aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Nje na Msaidizi wa Karibu wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

Tetesi zilizokuwepo tokea mwaka Juzi

Ni kwamba inadaiwa / inasemekana kuwa pamoja na kwamba Utawala wa Hayati Magufuli ulikuwa unamdai Pesa nyingi Mzee Mkono ila baada ya Ukaguzi wa Kina kufanyika ikagundulika kuwa Yeye Marehemu Mzee Mkono ndiyo anaidai hasa Serikali ( Mabilioni ) kutokana na Kusimamia Kesi zao ( mojawapo iliyoihusu TANESCO ) ila akawa anazungushwa Kulipwa.

Hata hivyo baada ya Ujio wa Rais Samia na Serikali yake kuingia Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu Mzee Mkono ) akisaidiwa na Mpenzi wake ( Mbunge wa Jimbo ninalolihifadhi kwa sasa ) waliyezaa nae Mtoto Mmoja wakapeleka tena Ombi na kusemekana kuwa waliahidiwa Kulipwa hivyo sijajua kama walishalipwa tayari ndiyo maana zinazomstahili ameshatangulia mbele ili Binti, Mpenziwe na Mama Mzazi wazigawane na Kuzisosomola huku Watoto wengine wa Marehemu Daktari Wambura, Mkono Junior ( Walter ) na Mirembe wagawiwe kidogo.

Nimeupokeaje huu Msiba

Nimeupokea huu Msiba kwa Machungu mno na Umeniumiza kwakuwa Marehemu Mzee Mkono kachangia 35% ya Ustawi wangu Kimaisha tokea nikiwa Mdogo na Kanisaidia vingi sana.

Pole zangu hasa nazipeleka kwa Wanawe Watatu tu Wambura, Walter na Mirembe ila kamwe abadan ( Mwenyezi Mungu anisamehe ) Mkewe ( sasa Mjane ) na Bintiye Mkubwa Leah siwapi Pole zangu sana sana nitamwachia Mwenyezi Mungu Jukumu Kuu la Kuwahukumu kwa waliyomfanyia huyu Mzee wa Watu Mkono ambaye hakuwa na baya.

Pole zangu nyingi kabisa nazipeleka kwa Wadogo zake Marehemu Mzee Zadock Mkono na Mzee Dokta Japhet Mkono pamoja na Ndugu wote wa Marehemu pale Kijijini Uzanakini Busegwe.

Pole zangu za mwisho ( kwa Umaalum wake ) nazipeleka kwa Marafiki zake Wakubwa ( waliosoma Wote na Kukua pamoja hadi kufanya Kazi ) Serikalini Mzee Butiku na huyo Mzee mwingine wa Usalama wa Taifa ( aliyekuwa Mkurugenzi upande wa Nje ) kwani najua Wataumia mno na huu Msiba kwakuwa walijitahidi mno kuhakikisha Mzee Mkono anarudishwa Tanzania, Mali zake hazipotei na hadhulumiwi ila wakaishia kupokea Majibu ya Dharau na Kashfa kutoka kwa Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu Mzee Mkono ) na Wao kuamua kukaa Kando na Kumuachia kila Kitu ambapo hakuna alichokiweza na kama kipo basi labda ni kuacha Nyumba ya Kifahari ya Baba yake ya Masaki Kuota Nyasi hadi Ghorofa ya Pili, Panya, Paka na Popo Kuzaliana na Rangi za Kuta kubanduka hovyo.

Ombi

Niwaombe sana Watani Wakuu wa Wazanaki Makabila ya Wahaya, Wanyaturu, Waha, Wanyiramba, Warangi, Wakerewe na Wanyamwezi tafadhali mkienda / mkiuhudhuria Msiba huu pale Masaki Nyumbani kwa Marehemu Mzee Mkono mpigeni mno Madongo ya Kuuma huyu Bintiye Mzee Mkono Leah kwani kwa 85% akishirikiana na Mama yake Mzazi wamechangia Mzee Mkono Kuteseka na Kunyanyasika tokea alipopelekwa Kimabavu na Kimkakati huko Shidani nchini Marekani.

Hitimisho

Mzee Mkono nenda Baba, umefanya makubwa nchini, umetufanyia makubwa na Wengine akina MINOCYCLINE "Gifted Intellectually, Knowledgeable, Challenger and Well Informed Person" tunasikitika umeondoka hata hujala angalau 5% tu Fadhila zetu Kwako kwa Mambo mema, mengi na makubwa uliyotufanyia.

Mzee Mkono naandika hii Aya huku Nikilia kwa Uchungu mno kwani umewafanyia makubwa sana Wazanaki ( hasa Butiama na Musoma Vijijini ), Musoma Mjini na kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu ( hasa upande wa Bodi ya Mikopo ) ambapo ulikuwa ni Mmoja wa Viongozi wa Juu wa hiyo Bodi na Wanafunzi wengi walipata Mkopo na Kuelimika kutokana na Juhudi zako Binafsi kwani kuna nyakati Bodi ya Mikopo iliishiwa Fedha na Wewe ukawa unatoa zako ili tu kuhakikisha Wanafunzi wa Tanzania wanasoma na waje kuwa Msaada na Chachu ya Maendeleo kwa Taifa letu Teule la Tanzania. Asante Baba Mzee Mkono.

Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akusamehe Dhambi zako zote na akupumzishe kwa Amani.

Nisalimie sana Mpwa wako uliyempenda mno Tumaini Mkono aliyefariki Mwezi Mei mwaka Jana na pia nisalimie zaidi mwana Busegwe Mwenzako na aliyewahi pia kuwa Daktari wako ( Former Lugalo Hospital Neurologist ) Brigedia Profesa Yardon Kohi aliyefariki dunia Mwezi huu wa April na hata wana Busegwe hawana Wiki Mbili tokea Wamzike na tena wanaenda Kukuzika nawe eneo Jirani na Makazi yenu yanayotazamana

Nitajitahidi nije Kukuaga Mzee wetu.

Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa Jina lake Lihimidiwe. Poleni nyingi pia Wasabato wote.

Cc: Bujibuji Simba Nyamaume, Lambardi na GENTAMYCINE nae akitoka BAN nataka aisome hii ili aniambie nimeipatia au nimeikosea.
Umeandika vema na kwa weledi sana
 
Nailaumu sana Serikali ya Awamu ya Tano ( ya Hayati Magufuli ) na Watendaji wake hasa Ofisi ya Bunge chini ya aliyekuwa Spika Ndugai.

Kwanini?

Kuondoka kwa Marehemu Mzee Mkono kwenda huko alikofia ( nchini Marekani ) hakukutokana na Matakwa yake bali ni Utashi wa Mkewe ( Mama Leah ) na Binti mkubwa wa Marehemu Leah.

Mgogoro

Ndani ya miaka Mitano au Sita hii kumekuwa na Mgogoro mkubwa kwa Familia ya Marehemu Mzee Mkono ulioratibiwa vyema na Mkewe ( ambaye nimeshangaa leo kusikia eti nae alikuwa analia ) wakati Yeye na .Bintiye huyo Leah wamechangia Kumtesa na Kumdhalilisha Mzee wa Watu Marehemu Nimrod Mkono.

Tamaa ya Mali

Sababu Kuu ya Marehemu Mzee Mkono kupelekwa kuishi Kimasikini ( katika Nyumba za Kulea Wazee wasiojiweza ) huko Marekani ni Mkakati wa Bintiye Leah na Mama yake ( Mjane ) kujimilikisha Mali za Baba yake ambazo wamefanikiwa kwa 85% japo kuna mahala walikwama ili kumalizia hiyo 15% iliyobakia.

Cha Kusikitisha

Mkewe ( Mjane ) tokea amsafirishe Mumewe huko nchini Marekani amekuwa akimzuia Marehemu Mzee Mkono asiwe anawasiliana na Nduguze ( Wadogo zake ) Mzee Zadock Mkono ( Baba Mzazi wa Msanii Nahreel ) na Dokta Japhet Mkono mwenye Vituo vyake vya Afya viitwayo Salama Kimara Baruti na Sinza.

Kila mara Ndugu Hawa Watajwa wa Marehemu Mzee Mkono walipokuwa wakijaribu Kumpigia Simu Kaka yao huko Marekani alikokuwa Mkewe ( Mjane Mama Leah ) alikuwa akimpokonya Simu Mumewe huku akiwajibu hovyo Mashemeji zake hawa.

Miaka Minne ( 4 ) iliyopita Mzee Mkono ( sasa Marehemu ) alipokuwa bado hajapelekwa Nyumba za Kutunzia Wazee Wasiojiweza alidiriki kuamka Usiku na kwenda Chooni kisha kuwapigia Simu Wadogo zake walioko Tanzania ( Zadock na Dokta Japhet ) kuwa wamfuate kwani anateseka na anataka kurudi Tanzania ila Mkewe Mama Leah ( sasa Mjane ) akawa anawajibu kuwa Mzee Mkono haumwi na hana shida.

Kwanini lawama kwa Hayati Magufuli na Spika Ndugai?

Baada ya kutokea kwa hali hii na huu Mgogoro baadhi ya Marafiki Wakubwa na Wazanaki Wenzake Mzee Butiku na Mzee mwingine ( namhifadhi ) aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Nje na Msaidizi wa Karibu wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa Kushirikiana na Wadogo hawa wa Marehemu Mzee Mkono waliomba Msaada kutoka Serikalini na Bungeni ili Mzee Mkono arejeshwe Tanzania ila Bintiye Leah kwa Kushirikiana na Watu wa Serikali na Bungeni waliweza Kudanganya Watu wa Ikulu na Ofisi ya Bunge huku baadhi ya Nyaraka za Hali ya Mzee Mkono zikifojiwa ( kwa Msaada wa Mbunge Mmoja ) ambaye amezaa na Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu ) Kuonyesha kuwa Mzee Mkono hana matatizo huko aliko.

Lengo Kuu la Bintiye Mzee Mkono ( sasa Marehemu ) la kufanya hivyo ni kuendelea Yeye kama Yeye kupokea Pesa zote za Mshahara wa Bunge wa Baba yake na Malipo mengine yote ya Bungeni Kitu ambacho kwa 99% alifanikiwa na Pesa zingine akawa Anamtumia Mama yake ( Mratibu Mkuu wa Mateso ya Mzee Mkono huko alikofia nchini Marekani ) na Pesa zingine zikitumika Kuhongea Watu wa Serikalini na Bungeni ili Waamini Uwongo wa Leah kuhusu hali ya Baba yake ( sasa Marehemu )

Balaa alilolisababisha Binti wa Marehemu Leah Mkono

Leah Mkono ndiye kasababisha Kampuni ya Uwakili ya Baba yake Kufilisika na Kufungwa huku baadhi ya Floor pale Exim Bank kupokonywa.

Leah Mkono amesababisha Kampuni ya Baba yake kuwa na Madeni makubwa ambayo kwa sasa yanamfanya aishi kama DigiDigi kwa Kukimbia, Kujificha na Kuhamahama Mitaa na Mikoa.

Leah Mkono kasababisha mpasuko mkubwa baina ya Watoto wa Marehemu Wambura, Walter ( Mkono Junior ) na Mirembe.

Miaka Minne ( 4 ) nyuma Leah kwa Tamaa zake alitaka Kuiuza Nyumba ya Baba yake ( sasa Marehemu ) Mzee Mkono ila Kaka yake Mkono Junior ( Walter Mkono ) Mtoto pekee wa Kiume wa Marehemu akakataa ndipo Dada yake akapiga Simu Kituo cha Polisi cha Oysterbay na Kuwadanganya kuwa Kaka yake anamfanyia Fujo ambapo kweli alikamatwa ila aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani kipindi hicho Kangi Lugola na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ( sasa IGP ) Camilius Wambura ( Wote hawa kutokea Mkoa wa Mara atokako Marehemu Mzee Mkono ) Mmoja akiwa ni Mkurya ( Lugola ) na mwingine akiwa ni Mzanaki ( IGP Wambura ) waliingilia kati na Kijana huyo wa Mkono Walter kutoka Polisi Oysterbay.

Leah ametengeneza Uadui mkubwa baina ya Wafanyakazi ( hasa Chacha aliyekuwa Dereva Mkuu wa Marehemu Baba yake ), Waliokuwa Wafanyakazi wa Kampuni ya Uwakili ya Baba yake, Ndugu za Baba yake na Marafiki Wakubwa akiwemo Mzee Butiku ( Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ) na huyo Mzee mwingine ( niliyemhifadhi Jina ) aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Nje na Msaidizi wa Karibu wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

Tetesi zilizokuwepo tokea mwaka Juzi

Ni kwamba inadaiwa / inasemekana kuwa pamoja na kwamba Utawala wa Hayati Magufuli ulikuwa unamdai Pesa nyingi Mzee Mkono ila baada ya Ukaguzi wa Kina kufanyika ikagundulika kuwa Yeye Marehemu Mzee Mkono ndiyo anaidai hasa Serikali ( Mabilioni ) kutokana na Kusimamia Kesi zao ( mojawapo iliyoihusu TANESCO ) ila akawa anazungushwa Kulipwa.

Hata hivyo baada ya Ujio wa Rais Samia na Serikali yake kuingia Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu Mzee Mkono ) akisaidiwa na Mpenzi wake ( Mbunge wa Jimbo ninalolihifadhi kwa sasa ) waliyezaa nae Mtoto Mmoja wakapeleka tena Ombi na kusemekana kuwa waliahidiwa Kulipwa hivyo sijajua kama walishalipwa tayari ndiyo maana zinazomstahili ameshatangulia mbele ili Binti, Mpenziwe na Mama Mzazi wazigawane na Kuzisosomola huku Watoto wengine wa Marehemu Daktari Wambura, Mkono Junior ( Walter ) na Mirembe wagawiwe kidogo.

Nimeupokeaje huu Msiba

Nimeupokea huu Msiba kwa Machungu mno na Umeniumiza kwakuwa Marehemu Mzee Mkono kachangia 35% ya Ustawi wangu Kimaisha tokea nikiwa Mdogo na Kanisaidia vingi sana.

Pole zangu hasa nazipeleka kwa Wanawe Watatu tu Wambura, Walter na Mirembe ila kamwe abadan ( Mwenyezi Mungu anisamehe ) Mkewe ( sasa Mjane ) na Bintiye Mkubwa Leah siwapi Pole zangu sana sana nitamwachia Mwenyezi Mungu Jukumu Kuu la Kuwahukumu kwa waliyomfanyia huyu Mzee wa Watu Mkono ambaye hakuwa na baya.

Pole zangu nyingi kabisa nazipeleka kwa Wadogo zake Marehemu Mzee Zadock Mkono na Mzee Dokta Japhet Mkono pamoja na Ndugu wote wa Marehemu pale Kijijini Uzanakini Busegwe.

Pole zangu za mwisho ( kwa Umaalum wake ) nazipeleka kwa Marafiki zake Wakubwa ( waliosoma Wote na Kukua pamoja hadi kufanya Kazi ) Serikalini Mzee Butiku na huyo Mzee mwingine wa Usalama wa Taifa ( aliyekuwa Mkurugenzi upande wa Nje ) kwani najua Wataumia mno na huu Msiba kwakuwa walijitahidi mno kuhakikisha Mzee Mkono anarudishwa Tanzania, Mali zake hazipotei na hadhulumiwi ila wakaishia kupokea Majibu ya Dharau na Kashfa kutoka kwa Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu Mzee Mkono ) na Wao kuamua kukaa Kando na Kumuachia kila Kitu ambapo hakuna alichokiweza na kama kipo basi labda ni kuacha Nyumba ya Kifahari ya Baba yake ya Masaki Kuota Nyasi hadi Ghorofa ya Pili, Panya, Paka na Popo Kuzaliana na Rangi za Kuta kubanduka hovyo.

Ombi

Niwaombe sana Watani Wakuu wa Wazanaki Makabila ya Wahaya, Wanyaturu, Waha, Wanyiramba, Warangi, Wakerewe na Wanyamwezi tafadhali mkienda / mkiuhudhuria Msiba huu pale Masaki Nyumbani kwa Marehemu Mzee Mkono mpigeni mno Madongo ya Kuuma huyu Bintiye Mzee Mkono Leah kwani kwa 85% akishirikiana na Mama yake Mzazi wamechangia Mzee Mkono Kuteseka na Kunyanyasika tokea alipopelekwa Kimabavu na Kimkakati huko Shidani nchini Marekani.

Hitimisho

Mzee Mkono nenda Baba, umefanya makubwa nchini, umetufanyia makubwa na Wengine akina MINOCYCLINE "Gifted Intellectually, Knowledgeable, Challenger and Well Informed Person" tunasikitika umeondoka hata hujala angalau 5% tu Fadhila zetu Kwako kwa Mambo mema, mengi na makubwa uliyotufanyia.

Mzee Mkono naandika hii Aya huku Nikilia kwa Uchungu mno kwani umewafanyia makubwa sana Wazanaki ( hasa Butiama na Musoma Vijijini ), Musoma Mjini na kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu ( hasa upande wa Bodi ya Mikopo ) ambapo ulikuwa ni Mmoja wa Viongozi wa Juu wa hiyo Bodi na Wanafunzi wengi walipata Mkopo na Kuelimika kutokana na Juhudi zako Binafsi kwani kuna nyakati Bodi ya Mikopo iliishiwa Fedha na Wewe ukawa unatoa zako ili tu kuhakikisha Wanafunzi wa Tanzania wanasoma na waje kuwa Msaada na Chachu ya Maendeleo kwa Taifa letu Teule la Tanzania. Asante Baba Mzee Mkono.

Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akusamehe Dhambi zako zote na akupumzishe kwa Amani.

Nisalimie sana Mpwa wako uliyempenda mno Tumaini Mkono aliyefariki Mwezi Mei mwaka Jana na pia nisalimie zaidi mwana Busegwe Mwenzako na aliyewahi pia kuwa Daktari wako ( Former Lugalo Hospital Neurologist ) Brigedia Profesa Yardon Kohi aliyefariki dunia Mwezi huu wa April na hata wana Busegwe hawana Wiki Mbili tokea Wamzike na tena wanaenda Kukuzika nawe eneo Jirani na Makazi yenu yanayotazamana

Nitajitahidi nije Kukuaga Mzee wetu.

Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa Jina lake Lihimidiwe. Poleni nyingi pia Wasabato wote.

Cc: Bujibuji Simba Nyamaume, Lambardi na GENTAMYCINE nae akitoka BAN nataka aisome hii ili aniambie nimeipatia au nimeikosea.
Safi sana umenena vyema sana
 
Kuna kipindi nilisikiaga tetesi kwamba huyu Marehemu alikuwa anashindana na Marehemu Liyumba kutembea na warembo macelebrit na kuwapatia zawadi Magari yenye rangi nyekundu.
Yaani Liyumba akipita naye , naye anapita naye, Yeye akipita naye Liyumba akisikia na yeye Liyumba anapita naye. Yaani full kushindana.
Ila huyu Mzee alikuwa unique kidogo kama mrembo alikuwa na boyfriend au mume na yeye boy friend au mume alikuwa anapewa gari pia.
Kwamba yeye na Liumba Lao kulikuwa moja kusambaza Umeme Kwa warembo na macelebrit.
Mwenyezi Mungu amhifadhi anapostahili
 
Umesoma kwa makini comments za pacha wa Gentamycine?

Sasa rudi kwenye thread ya Le Mutuz na Neema Ngwilulupi hivi ndivyo alivyotaka kumalizwa Baharia akastukia mchezo mapema.

Hivi tajiri kama Mkono ni wa kwenda kutunzwa nyumba za wazee?

Aisee wanawake mnaupiga mwingi mpaka unamwagika aisee, nimeogopa sana.

Cc: MINOCYCLINE
Mjane ( Mama Leah ) na Bintiye mkubwa na Marehemu Mzee Mkono aitwae Leah wametuumiza Wengi kwa walichomfanyia Mzee wa Watu Mkono wakishirikiana na Mbunge ( EK ) aliyezaa Kimkakati na Leah Mkono ili apige Fedha za Mzee Mkono na ajipatie Mali.
 
Kuna kipindi nilisikiaga tetesi kwamba huyu Marehemu alikuwa anashindana na Marehemu Liyumba kutembea na warembo macelebrit na kuwapatia zawadi Magari yenye rangi nyekundu.
Yaani Liyumba akipita naye , naye anapita naye, Yeye akipita naye Liyumba akisikia na yeye Liyumba anapita naye. Yaani full kushindana.
Ila huyu Mzee alikuwa unique kidogo kama mrembo alikuwa na boyfriend au mume na yeye boy friend au mume alikuwa anapewa gari pia.
Kwamba yeye na Liumba Lao kulikuwa moja kusambaza Umeme Kwa warembo na macelebrit.
Mwenyezi Mungu amhifadhi anapostahili
"Kuna kipndi nilisikia"
 
Kuna kipindi nilisikiaga tetesi kwamba huyu Marehemu alikuwa anashindana na Marehemu Liyumba kutembea na warembo macelebrit na kuwapatia zawadi Magari yenye rangi nyekundu.
Yaani Liyumba akipita naye , naye anapita naye, Yeye akipita naye Liyumba akisikia na yeye Liyumba anapita naye. Yaani full kushindana.
Ila huyu Mzee alikuwa unique kidogo kama mrembo alikuwa na boyfriend au mume na yeye boy friend au mume alikuwa anapewa gari pia.
Kwamba yeye na Liumba Lao kulikuwa moja kusambaza Umeme Kwa warembo na macelebrit.
Mwenyezi Mungu amhifadhi anapostahili
Tuache kujitafutia Dhambi na Laana. Marehemu Mzee Mkono hakuwa Muhuni hivyo / hivi na hakuwahi Kushindana na Mtu kwa Kulala hovyo na Warembo kama usemavyo.

Alikuwa ni Mnywaji mzuri wa Wine na Bia mara moja moja sana na wa pembeni alikuwa nao Wamama Wawili tu ( nje na Mkewe ) ambao kwa Kimaadili nawahifadhi.

Na kwa Wazanaki kuwa na Nyumba Ndogo / Hawara wenyewe wanaita Ekitungo ni Kitu cha Kawaida mno na ndiyo maana hata huwa sishangai Kumuona Rafiki yake Bujibuji Simba Nyamaume na Dr Matola PhD hapa JamiiForums aitwae GENTAMYCINE akiwa ni Mpenda Wanawake ( Mwenyewe huita Mbunye ) kwani ni Asili yao Wazanaki.
 
Yule shetani alikuwa na uwezo wa kufanya ushetani wake wote lakini siyo kumgusa Mkono ambaye ana mahusiano ya moja kwa moja na familia ya Mwalimu.

Huwezi kuiongelea Musoma vijijini/ Butiama bila Mkono, hiyo ni vita angekuwa anaitafuta, na unajuwa vizuri ule siyo ukanda wa wazaramo au walugulu, wale watu hawajaribiwi.
Umenena vyema na kama kuna Mtu ambaye nina uhakika ameumizwa zaidi pia na huu Msiba ni Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere alimpenda mno Mwanae Kiukabila Marehemu Mzee Mkono kwa tabia yake ya Kupenda Kusaidia Watu na kufanya Maendeleo makubwa Butiama na Musoma Vijijini.

Kwa Wazanaki huu ni Msiba mkubwa na mzito mno na natabiri atapata Maziko makubwa pamoja na kwamba aliondoka nchini tokea mwaka 2018 kwa Roho Mbaya za Mkewe ( Mama Leah ) na Mwanae ( Bintiye ) Leah.
 
Hivi lipo bado

Ova
Lipo na ndiyo Leah anaishi hapo / humo na hata Mimba ya Mtoto aliyezaa Kimkakati na Mbunge ( EK ) nayo pia iliingilia moja kwa moja hapo hapo japo Mtoto akaenda Kuzaliwa nchini Marekani ambako Leah kwa muda mrefu ni Raia wa huko.

Kuishi Kwake hapa Tanzania ni kwa Makosa na Uzembe tu wa Watu wa UHAMIAJI ambao ( baadhi yao ) walikuwa Wakihongwa nae Leah ili wasimsumbue kuhusu Kuishi Kwake hapa Tanzania Kinyemela wakati Yeye ni Mmarekani na ana Uraia wa huko.

Cc: Bujibuji Simba Nyamaume na Dr Matola PhD
 
Lipo na ndiyo Leah anaishi hapo / humo na hata Mimba ya Mtoto aliyezaa Kimkakati na Mbunge ( EK ) nayo pia iliingilia moja kwa moja hapo hapo japo Mtoto akaenda Kuzaliwa nchini Marekani ambako Leah kwa muda mrefu ni Raia wa huko na kuishi Kwake hapa Tanzania ni kwa Makosa na Uzembe tu wa Watu wa UHAMIAJI ambao ( baadhi yao ) walikuwa Wakihongwa nae Leah ili wasimsumbue kuhusu Kuishi Kwake hapa Tanzania Kinyemela wakati Yeye ni Mmarekani na ana Uraia wa huko.

Cc: Bujibuji Simba Nyamaume na Dr Matola PhD
Duh

Ova
 
Back
Top Bottom