TANZIA Mbunge wa zamani, Nimrod Mkono amefariki dunia nchini Marekani

TANZIA Mbunge wa zamani, Nimrod Mkono amefariki dunia nchini Marekani

Akakutane sasa na mfumo wa haki. I hope amebeba pesa za kutosha kuhonga huko aendako maana huko utasomewa kila shitaka hadi la kulamba sukari utotoni kisha ukasema "sio mimi".

Wanadamu huwa tunaviburi sana ila tunasahau kuwa maisha and the days tunaishi hapa huwa hatuna uwezo wa kurenew uzee ukishatufika.
Mbona Chuki / Usununu hivi? Alikudhulumu chochote kile labda ili Wanawe ( hasa Uncle's ) wake tukurejeshee?
 
Huyu mtu achana naye, amejenga masecondary Butiama kwa pesa zake binafsi akazipa majina ya machifu wa kizanaki na kuzikabidhi shule zote serikalini ni Mali ya serikali, Hakuna hata shule moja amejipa jina lake, siyo Utapeli kama wa kina Gertrude Lwakatare na Saint Marys zake kumbe zilitakiwa kusomesha yatima bure.

Leo kuna majitu yanapenda tu vitu vya umma kupachika majina yao kiholela tu.
Masahihisho kidogo siyo zote zina Majina ya Machifu kwa mfano ile ya Oswald Mang'ombe ( Baba yake Mkubwa mwana JamiiForums mkubwa, machachari na maarufu mno hapa ) hakuwa Mtemi ila alikuwa ni Mtoto wa Mtemi wa Watuguri Mang'ombe ( Omary ) Isyesya.

Huyu Oswald Mang'ombe ndiyo alikuwa Rafiki mkubwa wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere mpaka kufikia Kuamua kuwa na Undugu wa Kuchanja Damu na ndiyo maana hata huyo Member maarufu, mkubwa na mtata hapa JamiiForums ameishi mno Ikulu na Msasani enzi za Mwalimu Nyerere kutokana na hii Historia ya huu Undugu.

Na huyu Oswald Mang'ombe ( Archtecturer by Profession ) ndiyo alikuwa Mkuu wa Mkoa ( zamani Area Commissioner ) wa Mbeya.

Marehemu Mzee Mkono aliamua kuiita Jina lake hiyo Shule kwakuwa tokea Yeye ( Mkono ) akiwa Mdogo alikuwa akiona Utendaji mkubwa wa Oswald Mang'ombe na alivyokuwa akipambana Kuwaendeleza hasa Kielimu Wazanaki wa Butuguri, Busegwe ( Kwao Mzee Mkono ) na hata Butiama kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.

Cc: Bujibuji Simba Nyamaume
 
Mkono alizaliwa Agosti 18, 1943 katika Kijiji cha Busegwe, Kata ya Busegwe, Wilaya ya Butiama mkoani Mara.

Mkono ni miongoni mwa matajiri wachache nchini waliojitoa kwa hali na mali kusaidia maendeleo ya kijamii.

Katika Jimbo la Musoma Vijijini na baadaye Butiama, Mkono amejenga shule za msingi na sekondari nyingi. Baadhi ya shule hizo ni Chifu Ihunyo, Chifu Wazangi, Oswald Mang’ombe, Shule ya Sekondari Butuguri na Shule ya Sekondari Kasoma.

Shule zote hizi zimegharimu mabilioni ya shilingi. Shule mbili – Oswald Mang’ombe na Busegwe aliikabidhi serikali. Chifu Wanzagi inaendeshwa na madhehebu ya dini.

Jimbo la Musoma Vijijini lililokuwa na kata 36 na vijiji 119, hakuna sehemu ambayo haikupata kufikiwa na Mkono kimaendeleo.

Pamoja na shule, Mkono amechimba visima vingi katika vijiji vingi. Amejenga vyumba vya madarasa na maabara, amefungua barabara zote za enzi ya utawala wa wakoloni na mpya, amejenga mabweni katika shule nyingi kuanzia Busekela (magharibi) hadi Kyagata na Sirori Simba (mashariki). Amejenga zahanati, vituo vya afya, wodi, vituo vya polisi na majengo ya utawala sehemu nyingi.

Pia amejenga na kukarabati mabwawa na ameshirikiana na serikali kufanikisha kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere. Majengo ya Sekondari ya Oswald Mang’ombe yamekubaliwa yatumike kuanzisha chuo hicho.

Nimrod Elirehema Mkono tutamkumbuka kwa mema yake mengi, apumzike kwa amani mahala pema peponi
 
Nimrood Elirehema Mkono
Mkono Kwa Mkono
Mbunge Wangu 2000-2015 Mpka alipokuja Prof Muhongo 2015-2020
2005 nikiwa namaliza la 7 aliitembea shule yetu ... Alikua anaongea Sauti yake ndogo sana afu kama Ina kimkwaruzo anavalia tarbush na kaunda au Kisela tu jinsi na magari ya kutosha afu ana macho mekundu sana ....
Ila anatoa misaada sana hasa kwenye upande wa Elimu miundo mbinu na Afya ...

Alikua na Hela Nyingi Sana
Anatoa pale pale bila Mbamba Mbamba
Next time akaja na Mh Jakaya...
Amefanya Mengi sana Mkoa wa Mara ( Nchini)
Aliupenda sana mkoa wa Mara hasa wakati akiwa Mbunge alipenda kulitembea Jimbo lake la Musoma vijijini ( Butiama)
Rest Easy Home Boy .
 
Rest well Mzee Mkono
Pole kwa familia na wote walioguswa na msiba huu
Umesoma kwa makini comments za pacha wa Gentamycine?

Sasa rudi kwenye thread ya Le Mutuz na Neema Ngwilulupi hivi ndivyo alivyotaka kumalizwa Baharia akastukia mchezo mapema.

Hivi tajiri kama Mkono ni wa kwenda kutunzwa nyumba za wazee?

Aisee wanawake mnaupiga mwingi mpaka unamwagika aisee, nimeogopa sana.

Cc: MINOCYCLINE
 
Umesoma kwa makini comments za pacha wa Gentamycine?

Sasa rudi kwenye thread ya Le Mutuz na Neema Ngwilulupi hivi ndivyo alivyotaka kumalizwa Baharia akastukia mchezo mapema.

Hivi tajiri kama Mkono ni wa kwenda kutunzwa nyumba za wazee?

Aisee wanawake mnaupiga mwingi mpaka unamwagika aisee, nimeogopa sana.

Umeandika nini hapo!?
Halafu tusipangiane vya kuandika
 
Aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini na Butiama na pia Wakili maarufu Nchini Nimrod Mkono amefariki asubuhi ya leo kwa saa za Marekani.

Akiongea na @ayotv_ kwa njia ya simu Mdogo wa Marehemu, Zadock Mkono amethibitisha kutokea kifo cha Kaka yake.

“Nimepewa taarifa na Shemeji (Mke wa Wakili Mkono) kwamba Mzee amefariki nimempigia Shemeji alikuwa analia tu ameshindwa kuongea vizuri, Mzee aliondoka Tanzania tangu mwaka 2018 akaelekea Marekani kwa matibabu kwasababu alikuwa anasumbuliwa na tatizo la kusahausahau, kumbukumbu zilikuwa zinapotea”

“Mimi nipo Tanzania kwa sasa ninachoweza kuthibitisha ni kwamba kweli amefariki taarifa zaidi za kama alikuwa anaugua ugonjwa mwingine na kama alikuwa Hospitali au amefariki ghafla hizo bado sijajua, nitawapa taarifa zaidi baadaye”

View attachment 2592241
R.i.p taikon wewe ni jabali la siasa za bongo....
Japo wew ni CCM ila uliona potentiality za wanasiasa wa upinzani na uliwapa TAG...
NIMROD MKONO JUHUDI ZAKO ZA KUWAPAMBANIA WATANZANIA NA WANA MUSOMA HAZIWEZI SAHAULIKA DAIMA.....
Pumzika Baba sote safar yetu ni Moja.....
UFUNUO 14:13 tunapata faraja kupitia hili andiko.....

🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿
 
Licha ya maradhi, kwa mwaka huo, isijekuwa pia alimkibia bwana yule.
Yule shetani alikuwa na uwezo wa kufanya ushetani wake wote lakini siyo kumgusa Mkono ambaye ana mahusiano ya moja kwa moja na familia ya Mwalimu.

Huwezi kuiongelea Musoma vijijini/ Butiama bila Mkono, hiyo ni vita angekuwa anaitafuta, na unajuwa vizuri ule siyo ukanda wa wazaramo au walugulu, wale watu hawajaribiwi.
 
kweli hapa Nimrod Amenishangaza shule hata moja haina jina lake kama mafisadi na wanasiasa makanjanja wapendavyo kuandika majina yao katika taasisi. kwa Advocate Mkono ni tofauti.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaha, eti Hadi mrisho Gambo fisadi wa juzi tuu, kawaibia wahindi kina Tanga general na bulk mavifaa ya ujenzi, nae ana shule inaitwa mrisho Gambo tena ya government
 
Back
Top Bottom