Aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini na Butiama na pia Wakili maarufu Nchini Nimrod Mkono amefariki asubuhi ya leo kwa saa za Marekani.
Akiongea na @ayotv_ kwa njia ya simu Mdogo wa Marehemu, Zadock Mkono amethibitisha kutokea kifo cha Kaka yake.
“Nimepewa taarifa na Shemeji (Mke wa Wakili Mkono) kwamba Mzee amefariki nimempigia Shemeji alikuwa analia tu ameshindwa kuongea vizuri, Mzee aliondoka Tanzania tangu mwaka 2018 akaelekea Marekani kwa matibabu kwasababu alikuwa anasumbuliwa na tatizo la kusahausahau, kumbukumbu zilikuwa zinapotea”
“Mimi nipo Tanzania kwa sasa ninachoweza kuthibitisha ni kwamba kweli amefariki taarifa zaidi za kama alikuwa anaugua ugonjwa mwingine na kama alikuwa Hospitali au amefariki ghafla hizo bado sijajua, nitawapa taarifa zaidi baadaye”
View attachment 2592241
Nailaumu sana Serikali ya Awamu ya Tano ( ya Hayati Magufuli ) na Watendaji wake hasa Ofisi ya Bunge chini ya aliyekuwa Spika Ndugai.
Kwanini?
Kuondoka kwa Marehemu Mzee Mkono kwenda huko alikofia ( nchini Marekani ) hakukutokana na Matakwa yake bali ni Utashi wa Mkewe ( Mama Leah ) na Binti mkubwa wa Marehemu Leah.
Mgogoro
Ndani ya miaka Mitano au Sita hii kumekuwa na Mgogoro mkubwa kwa Familia ya Marehemu Mzee Mkono ulioratibiwa vyema na Mkewe ( ambaye nimeshangaa leo kusikia eti nae alikuwa analia ) wakati Yeye na .Bintiye huyo Leah wamechangia Kumtesa na Kumdhalilisha Mzee wa Watu Marehemu Nimrod Mkono.
Tamaa ya Mali
Sababu Kuu ya Marehemu Mzee Mkono kupelekwa kuishi Kimasikini ( katika Nyumba za Kulea Wazee wasiojiweza ) huko Marekani ni Mkakati wa Bintiye Leah na Mama yake ( Mjane ) kujimilikisha Mali za Baba yake ambazo wamefanikiwa kwa 85% japo kuna mahala walikwama ili kumalizia hiyo 15% iliyobakia.
Cha Kusikitisha
Mkewe ( Mjane ) tokea amsafirishe Mumewe huko nchini Marekani amekuwa akimzuia Marehemu Mzee Mkono asiwe anawasiliana na Nduguze ( Wadogo zake ) Mzee Zadock Mkono ( Baba Mzazi wa Msanii Nahreel ) na Dokta Japhet Mkono mwenye Vituo vyake vya Afya viitwayo Salama Kimara Baruti na Sinza.
Kila mara Ndugu Hawa Watajwa wa Marehemu Mzee Mkono walipokuwa wakijaribu Kumpigia Simu Kaka yao huko Marekani alikokuwa Mkewe ( Mjane Mama Leah ) alikuwa akimpokonya Simu Mumewe huku akiwajibu hovyo Mashemeji zake hawa.
Miaka Minne ( 4 ) iliyopita Mzee Mkono ( sasa Marehemu ) alipokuwa bado hajapelekwa Nyumba za Kutunzia Wazee Wasiojiweza alidiriki kuamka Usiku na kwenda Chooni kisha kuwapigia Simu Wadogo zake walioko Tanzania ( Zadock na Dokta Japhet ) kuwa wamfuate kwani anateseka na anataka kurudi Tanzania ila Mkewe Mama Leah ( sasa Mjane ) akawa anawajibu kuwa Mzee Mkono haumwi na hana shida.
Kwanini lawama kwa Hayati Magufuli na Spika Ndugai?
Baada ya kutokea kwa hali hii na huu Mgogoro baadhi ya Marafiki Wakubwa na Wazanaki Wenzake Mzee Butiku na Mzee mwingine ( namhifadhi ) aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Nje na Msaidizi wa Karibu wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa Kushirikiana na Wadogo hawa wa Marehemu Mzee Mkono waliomba Msaada kutoka Serikalini na Bungeni ili Mzee Mkono arejeshwe Tanzania ila Bintiye Leah kwa Kushirikiana na Watu wa Serikali na Bungeni waliweza Kudanganya Watu wa Ikulu na Ofisi ya Bunge huku baadhi ya Nyaraka za Hali ya Mzee Mkono zikifojiwa ( kwa Msaada wa Mbunge Mmoja ) ambaye amezaa na Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu ) Kuonyesha kuwa Mzee Mkono hana matatizo huko aliko.
Lengo Kuu la Bintiye Mzee Mkono ( sasa Marehemu ) la kufanya hivyo ni kuendelea Yeye kama Yeye kupokea Pesa zote za Mshahara wa Bunge wa Baba yake na Malipo mengine yote ya Bungeni Kitu ambacho kwa 99% alifanikiwa na Pesa zingine akawa Anamtumia Mama yake ( Mratibu Mkuu wa Mateso ya Mzee Mkono huko alikofia nchini Marekani ) na Pesa zingine zikitumika Kuhongea Watu wa Serikalini na Bungeni ili Waamini Uwongo wa Leah kuhusu hali ya Baba yake ( sasa Marehemu )
Balaa alilolisababisha Binti wa Marehemu Leah Mkono
Leah Mkono ndiye kasababisha Kampuni ya Uwakili ya Baba yake Kufilisika na Kufungwa huku baadhi ya Floor pale Exim Bank kupokonywa.
Leah Mkono amesababisha Kampuni ya Baba yake kuwa na Madeni makubwa ambayo kwa sasa yanamfanya aishi kama DigiDigi kwa Kukimbia, Kujificha na Kuhamahama Mitaa na Mikoa.
Leah Mkono kasababisha mpasuko mkubwa baina ya Watoto wa Marehemu Wambura, Walter ( Mkono Junior ) na Mirembe.
Miaka Minne ( 4 ) nyuma Leah kwa Tamaa zake alitaka Kuiuza Nyumba ya Baba yake ( sasa Marehemu ) Mzee Mkono ila Kaka yake Mkono Junior ( Walter Mkono ) Mtoto pekee wa Kiume wa Marehemu akakataa ndipo Dada yake akapiga Simu Kituo cha Polisi cha Oysterbay na Kuwadanganya kuwa Kaka yake anamfanyia Fujo ambapo kweli alikamatwa ila aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani kipindi hicho Kangi Lugola na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ( sasa IGP ) Camilius Wambura ( Wote hawa kutokea Mkoa wa Mara atokako Marehemu Mzee Mkono ) Mmoja akiwa ni Mkurya ( Lugola ) na mwingine akiwa ni Mzanaki ( IGP Wambura ) waliingilia kati na Kijana huyo wa Mkono Walter kutoka Polisi Oysterbay.
Leah ametengeneza Uadui mkubwa baina ya Wafanyakazi ( hasa Chacha aliyekuwa Dereva Mkuu wa Marehemu Baba yake ), Waliokuwa Wafanyakazi wa Kampuni ya Uwakili ya Baba yake, Ndugu za Baba yake na Marafiki Wakubwa akiwemo Mzee Butiku ( Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ) na huyo Mzee mwingine ( niliyemhifadhi Jina ) aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Nje na Msaidizi wa Karibu wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere.
Tetesi zilizokuwepo tokea mwaka Juzi
Ni kwamba inadaiwa / inasemekana kuwa pamoja na kwamba Utawala wa Hayati Magufuli ulikuwa unamdai Pesa nyingi Mzee Mkono ila baada ya Ukaguzi wa Kina kufanyika ikagundulika kuwa Yeye Marehemu Mzee Mkono ndiyo anaidai hasa Serikali ( Mabilioni ) kutokana na Kusimamia Kesi zao ( mojawapo iliyoihusu TANESCO ) ila akawa anazungushwa Kulipwa.
Hata hivyo baada ya Ujio wa Rais Samia na Serikali yake kuingia Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu Mzee Mkono ) akisaidiwa na Mpenzi wake ( Mbunge wa Jimbo ninalolihifadhi kwa sasa ) waliyezaa nae Mtoto Mmoja wakapeleka tena Ombi na kusemekana kuwa waliahidiwa Kulipwa hivyo sijajua kama walishalipwa tayari ndiyo maana zinazomstahili ameshatangulia mbele ili Binti, Mpenziwe na Mama Mzazi wazigawane na Kuzisosomola huku Watoto wengine wa Marehemu Daktari Wambura, Mkono Junior ( Walter ) na Mirembe wagawiwe kidogo.
Nimeupokeaje huu Msiba
Nimeupokea huu Msiba kwa Machungu mno na Umeniumiza kwakuwa Marehemu Mzee Mkono kachangia 35% ya Ustawi wangu Kimaisha tokea nikiwa Mdogo na Kanisaidia vingi sana.
Pole zangu hasa nazipeleka kwa Wanawe Watatu tu Wambura, Walter na Mirembe ila kamwe abadan ( Mwenyezi Mungu anisamehe ) Mkewe ( sasa Mjane ) na Bintiye Mkubwa Leah siwapi Pole zangu sana sana nitamwachia Mwenyezi Mungu Jukumu Kuu la Kuwahukumu kwa waliyomfanyia huyu Mzee wa Watu Mkono ambaye hakuwa na baya.
Pole zangu nyingi kabisa nazipeleka kwa Wadogo zake Marehemu Mzee Zadock Mkono na Mzee Dokta Japhet Mkono pamoja na Ndugu wote wa Marehemu pale Kijijini Uzanakini Busegwe.
Pole zangu za mwisho ( kwa Umaalum wake ) nazipeleka kwa Marafiki zake Wakubwa ( waliosoma Wote na Kukua pamoja hadi kufanya Kazi ) Serikalini Mzee Butiku na huyo Mzee mwingine wa Usalama wa Taifa ( aliyekuwa Mkurugenzi upande wa Nje ) kwani najua Wataumia mno na huu Msiba kwakuwa walijitahidi mno kuhakikisha Mzee Mkono anarudishwa Tanzania, Mali zake hazipotei na hadhulumiwi ila wakaishia kupokea Majibu ya Dharau na Kashfa kutoka kwa Leah ( Binti mkubwa wa Marehemu Mzee Mkono ) na Wao kuamua kukaa Kando na Kumuachia kila Kitu ambapo hakuna alichokiweza na kama kipo basi labda ni kuacha Nyumba ya Kifahari ya Baba yake ya Masaki Kuota Nyasi hadi Ghorofa ya Pili, Panya, Paka na Popo Kuzaliana na Rangi za Kuta kubanduka hovyo.
Ombi
Niwaombe sana Watani Wakuu wa Wazanaki Makabila ya Wahaya, Wanyaturu, Waha, Wanyiramba, Warangi, Wakerewe na Wanyamwezi tafadhali mkienda / mkiuhudhuria Msiba huu pale Masaki Nyumbani kwa Marehemu Mzee Mkono mpigeni mno Madongo ya Kuuma huyu Bintiye Mzee Mkono Leah kwani kwa 85% akishirikiana na Mama yake Mzazi wamechangia Mzee Mkono Kuteseka na Kunyanyasika tokea alipopelekwa Kimabavu na Kimkakati huko Shidani nchini Marekani.
Hitimisho
Mzee Mkono nenda Baba, umefanya makubwa nchini, umetufanyia makubwa na Wengine akina MINOCYCLINE "
Gifted Intellectually, Knowledgeable, Challenger and Well Informed Person" tunasikitika umeondoka hata hujala angalau 5% tu Fadhila zetu Kwako kwa Mambo mema, mengi na makubwa uliyotufanyia.
Mzee Mkono naandika hii Aya huku Nikilia kwa Uchungu mno kwani umewafanyia makubwa sana Wazanaki ( hasa Butiama na Musoma Vijijini ), Musoma Mjini na kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu ( hasa upande wa Bodi ya Mikopo ) ambapo ulikuwa ni Mmoja wa Viongozi wa Juu wa hiyo Bodi na Wanafunzi wengi walipata Mkopo na Kuelimika kutokana na Juhudi zako Binafsi kwani kuna nyakati Bodi ya Mikopo iliishiwa Fedha na Wewe ukawa unatoa zako ili tu kuhakikisha Wanafunzi wa Tanzania wanasoma na waje kuwa Msaada na Chachu ya Maendeleo kwa Taifa letu Teule la Tanzania. Asante Baba Mzee Mkono.
Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akusamehe Dhambi zako zote na akupumzishe kwa Amani.
Nisalimie sana Mpwa wako uliyempenda mno Tumaini Mkono aliyefariki Mwezi Mei mwaka Jana na pia nisalimie zaidi mwana Busegwe Mwenzako na aliyewahi pia kuwa Daktari wako ( Former Lugalo Hospital Neurologist ) Brigedia Profesa Yardon Kohi aliyefariki dunia Mwezi huu wa April na hata wana Busegwe hawana Wiki Mbili tokea Wamzike na tena wanaenda Kukuzika nawe eneo Jirani na Makazi yenu yanayotazamana
Nitajitahidi nije Kukuaga Mzee wetu.
Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa Jina lake Lihimidiwe. Poleni nyingi pia Wasabato wote.
Cc:
Bujibuji Simba Nyamaume,
Lambardi na
GENTAMYCINE nae akitoka BAN nataka aisome hii ili aniambie nimeipatia au nimeikosea.