Mbwa aina ya Bulldog wajeruhi familia

Mbwa aina ya Bulldog wajeruhi familia

Hilo limbwa ni pitbull, haya mambwa hajawahi kua na akili timamu. Inaonekana jamaa alishikishwa kwa ni juavyo mimi bulldog ana miguu mifup na mkia mfupi. Sasa inaonekana jamaa aliangalia uso tu akajua ni bulldog kumbe ni pitbull jibwa wehu lilo pigwa marufuku kufugwa na nchi zaidi ya 50 ulimwenguni.
Mzee pitbull ashawahi ku
Kukugeuka nini?
 
bahati ni kwamba meno ya bull dog hayana ncha kali kama german sherfad au rottweiler,meno yao yapo kama punje za mahindi,,lakini kiuhalisia bull dog hawana akili wala kumbukumbu nzuri,na ni wazito sana wakati kuwafundisha,ni mbwa niliobahatika kuwafundisha lakini kichwani hamna ki2 tofauti na german shrfad
Boerbol vipi?
 
Masai walikuwa zamani. Siku hizi ni wataalamu wa kuchora michoro na kuwapa ramani wezi. Utakuta nyumba inavamiwa na masai wako kafungwa kamba mikononi kama geresha tu.
Au mlinzi akiondoka au kuacha kazi Ni rahisi kuchorea ramani wezi kwasababu mazingira ya nyumba yako anayajua
 
kwa uzoefu wangu wa picha hiyo hao mbwa sio bulldog....huyo ni boerbol ...kifupi kwa wafugaji wa mbwa hasa ukiwa na familia mbwa yeyote kama hawa jamii wa bulldog sio wakufuga.
Mbwa mzuri mwenye kukumbuka fadhila ni German Shepherd pekee. Kwa anayehitaji pure shepherd puppy anidm natuma mikoani pia
Boerbol wana mikia mifupi huyo mbona ana mkia mrefu
 
Tatizo hapo ni moja tu hawa walioshambuliwa wamekuwa wakiishi na hao mbwa kama mbwa na si kama rafiki. Yawezekana mtu aliyetoka nje mara ya kwanza hana mazoea na hao mbwa. Na wakati anatoka ndani ya nyumba mbwa walikuwa upande mwingine hivo wamestuka kumwona na baada ya mbwa kumfuata hakuonyesha ishara kuwafaham mbwa ikiwa ni pamoja na kuwaita kwa majina.

Jambo la pili yawezekana hawa mbwa amewanunua wakiwa wakiwa tayari wakubwa na kuna baadhi ya tabia walikuwa nazo awali au kuna vitu walikuwa wanafanyiwa na sasa havifanyiki.

Jambo la tatu je hao mbwa wana mafunzo kwa maana ya kutii amri za master wao wao? mbwa wanaishi kwa tabia ya makundi maanake ni kuwa lazima kuwa na Pack na awepo master. Mfugaji usipochukuwa jukumu la kuwa master mbwa atatake over na yeye kuwa master.

Jambo la nne je kama familia wametenga muda wa kuwafanyisha mbwa wao mazoezi ili wasiwe bored na kujiona kama wana adhibiwa? Kama umeaamua kufuga mbwa wa kundi hili:- 1. Rottweiller 2. Bull Dog 3. American Pitt Bull 4. Great Dane 5. Bull mastiff 6. Pitt Bull Terrier 7. Cane corso na BoreBorel kama hauna muda wa kutosha kuwafanyisha mazoezi tafadhari achana nao. Fuga mbwa kama German Shepherd nk. Na endapo familia yako hawapendi mbwa weka mipaka mbwa wakishafunguliwa mtu asitoke nje.

Niliwahi kuandika kwa urefu sana kuhusu mbwa hawa wakizungu kwa wao wenyewe wazungu wanakwambia hiyo jamii hapo juu ni loaded guns on the table, muda wowote inaweza kufyatuka.

Again dogs are very friendly animals only if you know and understand their ABC. Pole sana kwa waanga na next time achukuwe somo ni namna gani ya kuishi na hawa viumbe. Mimi nimefuga hawa wadudu kwa muda mrefu na ninao jamii tofauti nyumbani kwangu mpaka mtaani wanaita kwa Mambwa lakini sijawhi pata kesi nyumbani zaidi ya kesi za mtaani ambapo nilikuwa na mbwa jamii ya Belgium Malinious ambaye alikuwa anaruka ukuta wa kozi kumi za block na kwenda kuattack wapita njia. Nilitafuta namna ya kumdhibiti ikiwa ni pamoja na kumhasi then hamna tena shida.
Vyakula vipi....inasemekana wana vyakula vyao special ...hawali pumba na dagaa hao....ukiwaletea pumba wanakasirika[emoji3][emoji3] hawapendi shida
 
Yanii nikae na kitu chenye garama kuliko hata nikiongeza mke wa pili hizo mambo siwez asee
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] mbwa anahitaji nyama kilo tano....mzee endelea kufuga tu wa kawaida Hawa wakina bobi mgeni akipiga hodi wanabweka huku wamefyata mkia
 
Hapana huyo anajua kila kitu, jambo la kwanza kwa mtu yoyote anapokwenda nunua kitu lazima ataulizia model ili ajue anafuga nini.

Huyu aliambiwa na alijua anachukua toleo gani la mbwa. Ni wale watu wajuaji wanapoambiwa kitu fulani hakifai yeye anataka kujifunza kwa gharama anata kuprove kuwa yeye ana maamuzi ya kitofuti.

Kuna m'moja hapo Arusha na yeye aliyachukua haya maumbwa akafuga, yalimuulia mtoto wake mdogo wa miaka 2. Hadi leo nadhani akiona hawa mbwa kwenye tivi anaweza vunja.

Imagine kupoteza mtoto wako kizembe sababu ya ujuaji mwingi na kujifanya wewe unajua sana mbwa. Maumbwa mawili yalikamata shingo ya mtoto yalimrarua huku mwingine amekata paja.

Nadhani jamaa akikumbuka ile tukio anakaa chini analia sana right kama angesikiliza maneno ya watu wenye hekima walipomwambia haya maumbwa sio ya kufuga yeye akasikiliza maneno ya dog trainer aliyekuwa anamwambia hawa mbwa ni wazuri ukiishi nae hivi na vile.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] tufuge tu Hawa wakina bobi wa kawaida
 
Umeambiwa huwa wanawapaga chakula it means wameshachangamana nao. Mbona watu wengine mnakuwa na vichwa vizito kuelewa, unatetea vitu ambavyo ni hatari.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] hahahaaa.....mzee hawapendi sana Hawa mbwa
 
Nilipokua.kijana mdogo kwetu nimefuga sana mbwa hawa wa kawaida.Sasa hivi nimekua baba wa familia nimefuga Germany Shephard...jike..ana miaka 2 sasa.Nimekuja kugundua kuna utofauti mkubwa sana nikilinganisha na hawa wengine....yuko composed, hapanick, habweki ovyo ovyo, royal.muda wote anakuangalia straight machoni kama vile anasubiri umwambie kitu.Akibweka mishindo miwili tu mtu wa kawaida lazima a-feel.
Nawaza nitafute Rotweiler dume, nimix
Sena GS wana maumbo madogo
 
Hiyo mimbwa siyo ya kufuga. Nina jirani yangu yalitaka kumpeleka kuzimu!!! Yalimshambulia majibwa manne!!! Imagine yeye ndiye alikuwa anayalisha, anacheza nayo na kufanya kila kitu!!!


But siku isiyo na jina yalimshambulia kidogo yamuue!!! Alilazwa hospital miezi miwili yuko kwenye coma!!!
Alivotoka akayaua yote
 
Mbwa hao ni hatari sana tena sana. Hao ni Pitbull.

Mwenyewe anajuwa kawawekea ulinzi familia yake kumbe ndiyo kawawekea hatari.

Inasikitisha sana.

Kuna jamaa yangu mmoja anao, lakini yeye ana uwezo kifedha, kawawekea watu wa kuwatazama mwanzo mwisho, kuanzia usafi wao, kula yao, mazoezi yao na mafunzo yao.

Anao hao pitbull kama wanane kwake, akitoka au kurudi mtu wa nyumbani kwake wana banda lao la chuma wahudumu wao wanapigiwa simu wawafungie ndiyo atoke au aingie ndani kukatiza yadi yao.

Bila kuwa na pesa za maana iusijaribu kuwafuga hao, kuna siku watakugeukia.

Hao mbwa ni wehu kabisa. Kula kwa wakati wake, kukojowa kwao kwa wakati wake, kunya kwao kwa wakati wake, kukogeshwa kwao kwa wakati wake.

Ukibadili ratiba yao, ushakuwa adui kwao, hawana sijuwi nilisahau. Utakoma kusahau.

Watanzania awashauri msiwafuge hao kabisa, hawana ujanja wala mazowea ya kudumu hao.
Uislamu unasemaje kuhusu kufuga mbwa...Hivi si marufuku?
 
Back
Top Bottom