TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

R.I.P Mch mtikila.

Barabara za mkoa wa pwani ni chanzo cha ajali nyingi. Barabara inateleza kama imepakwa mlenda.

Waziri husika awajibishwe haraka

Ni kweli kabisa ukiwa unaendesha gari bara bara Hiyo ni vema kuwa makini inateleza na INA mawimbi sana. Sote njia yetu ni moja R.I.P mchungaji Mtikila.
 
Chinembe ni Mungu yupi huyo????? Mungu ni wa rehema na hataki hata mmoja apotee.

Kama huyo Mungu wa Lowasa anaua kila atakayemsema basi atauwa watu wengi sana. Lile kusudi la kazi ya msalaba litakuwa limefitinika.

Bwana wetu Yesu Kristo alifanyiwa kila namna ya uovu akasema Baba wasamehe hawajui wafanyalo. Huyo Mungu wa kulipiza papo kwa papo !!!!!!! Mh!!!!! Wapi kazi ya MSALABA???

Damu zilizomwagika hata sasa kama ni mapenzi ya Mungu zitaenda kwa AMANI. Kama ni umafya na ushirikina basi tegemeeni KISASI cha Bwana.

Queen Esther

R.I.P Rev.Mtikila
Huyu alikuwa mtumishi wa Mungu ni ajali ya kawaida tu. Wachawi na wamafya hawana nafasi kwa mtumishi wa Mungu.
 
Tunatakiwa kumuheshimu MUNGU na kuacha dhihaka dhidi yake!
 
hizo nyanya wananchi walivyo wakatili itakuwa walizibeba kwenda kuungia mboga
Hahaha, sasa wafanyaje na maisha ni magumu!! Hata kama alikuwa na vichenji chenji vimebaki mfukoni wanachukua kwenda kununulia mboga!!
 
Inasikitisha kwa namna ilivotokea, ingawa sote tu katika safari hiyo.

Kwa muonekano wa picha na aina ya gari, binafsi naendelea kuwa na wasiwasi na mfumo wa kuisalama kwenye baadhi ya magari ambao umepitwa na wakati. Ingawa ni asilimia ndogo yenye uwezo, lakini nadhani tufike mahali tuwe na uchaguzi, kwa maana ya magari ya kutumia maeneo yasiyoruhusu mwendo mkubwa, mfano maeneo ya makazi/miji ya safari fupifupi; na magari ya kusafiri safari za mwendo wa kasi ambayo yana usalama unaokidhi na unaoweza kupunguza kiasi cha madhara kwa watumiaji.

(Note; nimewahi kupata ajali; gari ile hakuna airbag hata moja iliyotoka, na mikanda hai kujilock kudhibiti mgongano?).
 
Lete ushahidi Kwamba Lowassa Amemuua Mch: Mtikila? Endeleeni Kumsema Lowassa Hata wewe Mungu Atakushugulikia, Mungu Yupo upande wa Lowassa. Ndiyo Mjue Afanyaye Mtu Kuwa Mzima Au Mgonjwa Au Kuua Ni Mungu Chungeni Midomo yenu. Wambie na wenzako. Mtafinywa sana.

Dah, unaongea utadhani ndiye msemaji wa Mungu. UKAWA mmechanganyikiwa vibaya
 
Kwanza,natoa pole kwa wote walioguswa na kifo rev Mtikila.

Pili,kwa tabia zetu watanzania tunampamba marehemu kwa sifa njema hata kama hakuwa nazo.

Tatu,Kama Mungu hafurahi kufa kwake mtu mwovu ni zaidi sana BAOBAO

Nne, ni vema kuwa kuelezea mazuri na mabaya ya Rev.Mtikila kwa nia ya jamii kujifunza.
 
Tatizo mkuu, uko mbali kwenye siasa za Tanzania ndio maana unashangaa kuwa hapa Mungu anaingiaje. Ni miongoni mwa wanasiasa waliomdhihaki sana Mungu juu ya afya EL hivi karibuni. Kama ni kweli Mungu awatie nguvu wafiwa. Na sisi twaendelea kujifunza kwamba kuumwa sio kufa. Anaweza kuondoka mzima mgonjwa anabaki, haya yote yanatokea ktk jamii zetu.

Kwani mtu akiwa mgonjwa ukisema hivyo umemdhihaki Mungu? Naona watu wengi humu wanachuma laana kwa kumhusisha Mungu na siasa nyepesi
 
Ni kweli kabisa ukiwa unaendesha gari bara bara Hiyo ni vema kuwa makini inateleza na INA mawimbi sana. Sote njia yetu ni moja R.I.P mchungaji Mtikila.

Hasa kipande cha kutoka mlandizi kuelekea chalinze, unaona kabisa mnachora z barabarani.

Waziri husika awajibishwe kwa hili.
 
Nape learn from this, You may be the next....Mungu hadhihakiwi, wala watanzania mamilioni kwa mamilioni wanaomsapoti Lowassa hawafurahishwi na matusi yenu dhidi ya mtu wanayemuona wao kuwa ni sahihi, huwa wanasali ili Mungu awabadilishe mioyo yenu iache kuwa migumu, lakini kama hamtaki kubadilika, endeleeni kututukania baba yetu, lakini Mungu atajibu...!
 
Shukrani kubwa kwa rais mtarajiwa una moyo wa kipekee sana.
 
Kila mtu ana uhuru wa kuongea anachotaka kuongea. Semeni Lowasa mgonjwa semeni chochote mtakacho. Lakini mimi na nyumba yangu na jirani zangu wote tunampa kura zetu Lowasa pamoja na ugonjwa wake akafie ikulu.

Kwa hiyo unakiri ni mgonjwa?
 
Back
Top Bottom