The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,541
Hata hatujafika mbali sana, tayari wanaanza kusema waziwazi wenyewe mbinu haramu na za wizi wa kura walizotumia kushinda uchaguzi huu.
Katika video hii inayomwonesha mbunge mpya wa CCM - Jimbo la Kawe - DSM, Mch. Josephat Gwajima kuanzia dakika ya 8:50 ukitazama na kumsikiliza bila kujua ana kwa kujua asemacho, anaeleza jinsi jina la Rais John P. Magufuli lilivyotumika kuwapatia kura bila kutegemea watu (voters) kupiga kura.
Na hiki ndicho kinacholakamikiwa na vyama shindani vilivyopambana na CCM ya Magufuli katika uchaguzi ulioisha wiki juzi...
Wanasema kuwa huu haukuwa uchaguzi bali maigizo tu ya uchaguzi kwa sababu washindi walikuwa tayari wameshaandaliwa akiwemo Gwajima mwenyewe ambaye kwa kinywa chake anathibitisha hili.
Hakika kumbe ni kweli kabisa kuwa, MDOMO ULIPONZA KICHWA!
Hii maana yake ni kusema kuwa, kwa kuwatumia watu wao, walienda kwa wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wakurugenzi wa halmashauri za wilaya/miji/manispaa/majiji ambao ni wateule wa Rais Magufuli na kutoa amri ya utekelezaji tu kilichokwisha kuamuliwa;
Rejea kauli hizi za CCM;
"....nimekuteua mimi uwe DED, nimekupa mshahara mzuri mnono, nyumba nzuri na gari nzuri halafu sasa uende umtangaze mpinzani ameshinda uchaguzi ....", Rais John Pombe Magufuli (CCM)
".... hata kama mtapiga kura nyie, lakini CCM ndiyo itakayounda serikali...", Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan (CCM)
".... siyo kwamba 'Mungu akipenda tutashinda uchaguzi', HAPANA. Sisi tunasema Mungu apende ama asipende, CCM ni LAZIMA ishinde uchaguzi huu...", Hayati Marehemu Mary Edward..
Hivi ndivyo jina la Rais John Pombe Magufuli lilivyotumika kuleta ushindi. Je, unahitaji wapiga kura hapa kukupigia kura?
Kinachonipa shida na taabu mimi zaidi ni ushiriki wa Mchungaji huyu, mtumishi wa Mungu kwenye uharamia na unyang'anyi huu wa haki za wananchi mchana kweupe bila yeye kuukemea na kuukataa.
Je, mchungaji huyu anaweza kusimama madhabahuni na kuukuemea uovu na unyang'anyaji wowote iwapo yeye mwenyewe akiwa mshiriki mshiriki na sehemu ya unyang'anyi huo?
I am afraid to say this, that he might have a bad ending like his counterpart the late Rev. Getrude Lwakatare!
Katika video hii inayomwonesha mbunge mpya wa CCM - Jimbo la Kawe - DSM, Mch. Josephat Gwajima kuanzia dakika ya 8:50 ukitazama na kumsikiliza bila kujua ana kwa kujua asemacho, anaeleza jinsi jina la Rais John P. Magufuli lilivyotumika kuwapatia kura bila kutegemea watu (voters) kupiga kura.
Na hiki ndicho kinacholakamikiwa na vyama shindani vilivyopambana na CCM ya Magufuli katika uchaguzi ulioisha wiki juzi...
Wanasema kuwa huu haukuwa uchaguzi bali maigizo tu ya uchaguzi kwa sababu washindi walikuwa tayari wameshaandaliwa akiwemo Gwajima mwenyewe ambaye kwa kinywa chake anathibitisha hili.
Hakika kumbe ni kweli kabisa kuwa, MDOMO ULIPONZA KICHWA!
Hii maana yake ni kusema kuwa, kwa kuwatumia watu wao, walienda kwa wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wakurugenzi wa halmashauri za wilaya/miji/manispaa/majiji ambao ni wateule wa Rais Magufuli na kutoa amri ya utekelezaji tu kilichokwisha kuamuliwa;
Rejea kauli hizi za CCM;
"....nimekuteua mimi uwe DED, nimekupa mshahara mzuri mnono, nyumba nzuri na gari nzuri halafu sasa uende umtangaze mpinzani ameshinda uchaguzi ....", Rais John Pombe Magufuli (CCM)
".... hata kama mtapiga kura nyie, lakini CCM ndiyo itakayounda serikali...", Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan (CCM)
".... siyo kwamba 'Mungu akipenda tutashinda uchaguzi', HAPANA. Sisi tunasema Mungu apende ama asipende, CCM ni LAZIMA ishinde uchaguzi huu...", Hayati Marehemu Mary Edward..
Hivi ndivyo jina la Rais John Pombe Magufuli lilivyotumika kuleta ushindi. Je, unahitaji wapiga kura hapa kukupigia kura?
Kinachonipa shida na taabu mimi zaidi ni ushiriki wa Mchungaji huyu, mtumishi wa Mungu kwenye uharamia na unyang'anyi huu wa haki za wananchi mchana kweupe bila yeye kuukemea na kuukataa.
Je, mchungaji huyu anaweza kusimama madhabahuni na kuukuemea uovu na unyang'anyaji wowote iwapo yeye mwenyewe akiwa mshiriki mshiriki na sehemu ya unyang'anyi huo?
I am afraid to say this, that he might have a bad ending like his counterpart the late Rev. Getrude Lwakatare!