Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Mkuu kila mtu ashinde mechi zake, pengine na battle na baba paroko bila kujua. Nimekupa fact kama huamini we endelea tu mkuu.

Kuna tofauti kubwa sana ya watu mliozaliwa na kukulia masaki na sisi wa uswahilini huku Tembomgwaza!
 
Output wanayopata kwa kukuumiza wewe ni nini hasa? nilitarajia wakuone wewe ni asset kwao na hivyo wawe na shauku ya kuona umefanikiwa ili nao wafaidike.
Ukikulia Masaki ama Oysterbay shule IST, kanisani Cardinal Rugambwa hospitali Aga Khan huwezi kaa ukaamini kama kuna mambo ya shiriki!

Hizo akili wanazo wa ushuani tu ila sie wa Kisukuru ulizia uambiwe habari yake. Mshana Jr naomba uje umueleweshe huyu kijana
 
Uchawi uchawi uchawi aaagh ptuu inachosha sasa..kila sehemu watu wanalia na madhara yatokayo na uchawi.
Mm nashindwa hata kuandika,nimeamua kumuachia Mungu tu kama ataamua kuniacha niendelee kuteswa,kunyanyaswa na kuonja joto ya jiwe na wachawi sawa tu si ameamua iwe hivyo bhana Ila mm nimechoka na sina msaada wowote kutoka popote zaidi yake.

Nimechoka kuona wenzangu wakisonga mbele mm nikiwa nyuma na wamwisho kila siku, nimechoka kudharaulika sababu sina maendeleo kama wenzangu,nimechoka pesa zangu kuishia kwenye matibabu,nimechoka na kuugua maradhi yasiyoisha mwilini mwangu.

Nimechoka kutibia wazazi,nimechoka kutibia wadogo zangu,nimechoka kutibia familia,nimechoka kuishi kwa huzuni na mateso.

Nimechoka kujaza namba za simu za madaktari na manesi,nimechoka kitembelea maduka yamadawa,nimechoka kunywa dawa,nimechoka kugeuza dawa mbadala wa Chakula.

Nimechoka dharau,kebehi,masengenyo na vijembe juu ya uduni wangu unaosababishwa na wao wenyewe,nimechoka nimechoka nimechoka.

Eeh Mungu Mwenyezi,Mfalme wa falme,Mmiliki wa mbingu na dunia na ukazisimamisha pasipo nguzo,Mfalme wa siku ya Malipo,Mwingi wa Rehma mwnye kurehemu.

Ulieniumba mm ukamuumba baba na mama yangu,ukawaumba bibi na babu zangu, ukaumba wanangu,ukaumba ulimwengu na vyote vilivyomo ndani yake,Nakuomba eeh Rabbi uninusuru mm pamoja na kizazi changu chote dhidi ya udhalimu wa shetani na hila Zake zote.

Ewe Mola wangu mtukufu,usieshindwa na chochote mana vyote ni Mali yako,hakuna kilichopo nje matakwa yako,hakuna linalowezekana ila kwa idhini yako..nakuomba uniponywe mm,waponye wazazi wangu, iponyewe familia yangu,iponye jamii yangu liponye taifa langu dhidi ya uchawi, ulozi,ushirikina,na hila zote ovu za shetani.

Ninakuomba utufungulie milango ya rizki zetu ziwe za halali,za wepesi na uzikinge dhidi ya mabaya yoyote.sisi bila ww hatuwezi kitu Mungu wangu.

Tupe afya tuondolee maradhi,tupe Neema tuondolee ufakiri na umaskini,tupe mioyo safi tuondolee chuki na husda,tupe upendo tuondolee huzuni fitna na majungu.

Eeh mola wetu mlezi,mwenye huruma,mwenye upendo na msikivu, tunaomba usikie Dua yetu,tunakuomba usikie kilio chetu.sisi ni wakosefu tu si wakamilifu,ukamilifu unao ww Mungu wetu mtukufu.

Ninaomba yote haya kwa imani yangu kwangu,na kwa imani za wenzangu ila naamini sisi sote tunakutukuza ww kwa njia tofauti.
Amiiin
Amiiin
Amiiin
 
Mkuu kila mtu ashinde mechi zake, pengine na battle na baba paroko bila kujua. Nimekupa fact kama huamini we endelea tu mkuu.

Kuna tofauti kubwa sana ya watu mliozaliwa na kukulia masaki na sisi wa uswahilini huku Tembomgwaza!
Kwamba unamwomba Mungu huku umefunga booster, hahahaha........wewe jamaa bhana, Mungu hachanganywi na uganga wala ulozi. Ukisoma biblia waisreali walitakiwa kujitakasa kwanza kwa kutubu dhambi na kutupa hirizi na masanamu ya miungu yao kabla Mungu hajashuka. Huwezi kuita nguvu au uwepo wa Mungu huku umefunga hirizi na mitishamba, that will be suicidal.......ukikutana na waisraeli waliokuwepo kipindi Mungu anashuka mlima Sinai waulize mtiti wake ulikuwaje.......
 
Mkuu pole sana hiki kisa kinatisha sema matatizo aliyaleta baba yenu baada ya kuoa mke mshirikina. Kuna haja ya kuwa makini sana na wanawake tunaooa hawa.

Sikufichi mie mzee katuletea balaa kama hilo mpaka leo maendeleo hamna kwenye familia watoto hamna aliyechomoka kabisa ni majanga tu. Nishafatilia na nikagundua ukweli ndio napambana now huu mwaka kuwe na mabadiliko. Shule tulipiga vizuri tu ila sasa kazi kukutana nayo nahisi mpaka nikavunje nazi njiapanda. Unapanga mambo hayakamiliki mzee yani kila jambo ukiliweka sawa lilete hela hutaipata kuna kitu kitajitokeza tu...Kazi pia ni hivyo hivyo hata mtu mwenye connection anafeli yani acha tu kmmmk!
 
Hakuna kitu kama hicho, mimi mwenyewe nimekulia na kusoma kijijini na hata huku naishi jirani na watu wanaoaminiwa kwa uchawi lakini sina hofu hiyo....inagawaje sijui mganga wala mitishamba.
 
We jamaa acha uchizi! Booster ndio kitu gani wewe???
Chumvi ya mawe ni uchawi? Magadi ni uchawi?
 
Hakuna kitu kama hicho, mimi mwenyewe nimekulia na kusoma kijijini na hata huku naishi jirani na watu wanaoaminiwa kwa uchawi lakini sina hofu hiyo....inagawaje sijui mganga wala mitishamba.
Shukuru Mungu baba yako hakuoa mshirikina akamleta kwenye familia yenu! Hilo ndio jambo pekee naweza kukwambia kwa sasa.
 

Pole mkuu inaumiza mno tena mno …. Uchawi upo ila kaza na maombi have faith mambo yatakaa Sawa tuu mkuu
 
Sijui kwa kweli nambie lengo ni nini?
Kumpunguzia mwanadamu uwezo wa kufikiri yaani awe tegemezi asitumie akili yake kutatua shida.
Hakuna shida yeyeto duniani ambayo huwezi itatua kwa akili yako.Sema akili za wengi zimeisha chaji thus utegemea waganga na manabii kufikiri badala yao.
Mungu alimuumba mwanadamu akiwa kakamilika na wala haitaji msaada toka kwenye nguvu nyingine.
 
Pole sana kwa mengi magumu unayopitia

M. Mungu akufanyie wepesi
 
Mkuu huu mti ni upi na mimi niwe naweka kwemye ka mkweche Kangu kila siku kulipa 2000 imenichosha.
 
Akili gani na hela hupati wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…