Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Shukuru Mungu baba yako hakuoa mshirikina akamleta kwenye familia yenu! Hilo ndio jambo pekee naweza kukwambia kwa sasa.
Mkuu Extrovert sikatai hayo mambo kuwepo na huenda na mimi yameniathiri, ninachosema ni kwamba unatakiwa kumtegemea Mungu kwa hali yoyote ile. Kinyume cha hapo unakuwa unachanganya au kutegemea nguvu nyingine tofauti. Hakuna binadamu aliyetumika kwa viwango vya juu katika utumishi wa Mungu kama Mtume Paulo, lakini alikuwa na ugonjwa sugu mwilini mwake hadi kumwomba Mungu amponye lakini hakupona, alipozidi kuomba, Yesu akamwambia neema yangu yakutosha. Ndo maana katika maneno yake ameandika hivi "Nitajivunia udhaifu wangu ili uweza wa kristo ukae juu yangu, maana ninapokuwa dhaifu ndipo nilivyo na nguvu" ingekuwa sasa ungesema aende kutafuta mitishamba au waganga wa kienyeji......nilipotafakari kuhusu haya maneno ya Mtume Paulo alimaanisha kwamba pamoja na kwamba anaishi katika hali ya udhaifu wa mwili, lakini imani yake katika Mungu au nguvu zake za kiroho zinaongezeka siku baada ya siku. Ndo maana mahala pengine kaandika hivi "Japokuwa utu wangu wa nje unachakaa, bali utu wangu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku" haya ni maneno kutoka kwa mtu mwenye imani iliyovuka viwango vya kawaida vya kiimani.......​
 
Mkuu pole sana..

Sijui nisemeje, ila kama umeamua kukaa kwenye hayo maombi mwenyewe , basi shikilia hapo hapo, lakin inabidi utafakari sana hio vita, na approach unayochukua, mwanamke huyo na wanaomsaidia wanaachwaje huku wameua baba wakubwa na wazee wa ukoo wanakufa tu, naona kama mission yake ni kuwamaliza wote upande wako na mama yenu

Kuna mdau humu alikuja kuelezea stori yake jinsi walivyommaliza mzee wake, nadhan ni kama wewe tu, ila yeye aliamua kuchukua kisasi kwa wote waliohusika, aliwajua, na alifanikiwa lengo lake la kuwamaliza

Shangaz yangu yeye alikuaga anatumua approach ya maombi, lakin kuna dada wa mume wake ndio alikua na chuki na kaka yake na familia yake, aliona sijui anafaidi sana, mana mjomba alikua ofisi ya rais, na walikua wanaishi maisha mazuri, ( oneni watu walivyo na roho mbaya na roho za kwanini), chuki hio ilipelekea akaanza kuiangamiza familia, alianza na watoto, mtoto wa kwanza ( dada yangu) , aliugua na anachoumwa hakijulikani, na siku anakata roho alimtaja huyo mama..haitoshi, akaja mama ( shangaz yangu) , kifo chake kilikua kibaya nashindwa kusema, akafata mtoto mwingine, naye akaondoka, akaja baba , naye akaondoka, akaja mtoto mwingine yeye akapata uchizi, akaja mtoto mwingine maisha yake yakarudi nyuma sana na kua magumu sana, aliyesalimika ni mmoja tu ambaye ndio kidogo anajiweza,..ngoja niishie hapa.
Anatumia ID gani huyo jamaa nikasome hiyo post yake?

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Extrovert sikatai hayo mambo kuwepo na huenda na mimi yameniathiri, ninachosema ni kwamba unatakiwa kumtegemea Mungu kwa hali yoyote ile. Kinyume cha hapo unakuwa unachanganya au kutegemea nguvu nyingine tofauti. Hakuna binadamu aliyetumika kwa viwango vya juu katika utumishi wa Mungu kama Mtume Paulo, lakini alikuwa na ugonjwa sugu mwilini mwake hadi kumwomba Mungu amponye lakini hakupona, alipozidi kuomba, Yesu akamwambia neema yangu yakutosha. Ndo maana katika maneno yake ameandika hivi "Nitajivunia udhaifu wangu ili uweza wa kristo ukae juu yangu, maana ninapokuwa dhaifu ndipo nilivyo na nguvu" ingekuwa sasa ungesema aende kutafuta mitishamba au waganga wa kienyeji....
Nimefunguka kitu hapa

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
 
Mungu alimuumba mwanadamu akiwa kakamilika kwa kumpatia akili Ili avitawale vyote vilivyomo.
Shetani kupitia majini ndio waliomfunza mwanadamu uchawi kwa lengo kuu moja ni kuupunguza uwezo wa kufikiri wa mwanadamu aache kutumia akili zake alizopewa na Mwenyezi Mungu bali ategemee ushirikina ktk kutatua changamoto zake.Washirikina na wachawi wameharibu mindset za waafrika wengi kwa kuwaamisha huwezi fanya jambo iwe biashara,kilimo, elimu, mahusiano, kuchimba madini nk bila ndumba huu ni uwongo mkubwa kabisa lengo lake ni kufifisha uwezo wa kufikiri, wenzetu wazungu baada ya kuijua Siri hii ya kwamba ushirikina unapunguza uwezo wa kufikiri kwa kuleta utegemezi wa fikra wakaamua kuachana na fikra za kuamini ushirikina ikiwemo hata kuwaua na kuharibu kabisa Kazi za wachawi lengo kuu lilikuwa ni kupata Jamii inayotumia akili ilizopewa na Mwenyezi Mungu Ili kutatua changamoto mbalimbali.
Unapokuja mtazamo wa maendeleo waliotumia akili zao wenyewe Wana maendeleo makubwa Sana sababu wanatumia akili zao wenyewe tofauti na sisi waafrika tunaotumia akili na mawazo ya kishirikina.
Mtu yeyeto au Jamii yeyeto inayohusudu ushirikina uwezo wake wa kufikiri upo chini sana.
Hebu zaliwa na ufanye Mambo yako bila kufunuliwa nakiumbe fulani Cha kiroho. Utakufa ivoivo, hata soksi itakushinda kuumba.
 
Mkuu pole sana hiki kisa kinatisha sema matatizo aliyaleta baba yenu baada ya kuoa mke mshirikina. Kuna haja ya kuwa makini sana na wanawake tunaooa hawa.

Sikufichi mie mzee katuletea balaa kama hilo mpaka leo maendeleo hamna kwenye familia watoto hamna aliyechomoka kabisa ni majanga tu. Nishafatilia na nikagundua ukweli ndio napambana now huu mwaka kuwe na mabadiliko. Shule tulipiga vizuri tu ila sasa kazi kukutana nayo nahisi mpaka nikavunje nazi njiapanda. Unapanga mambo hayakamiliki mzee yani kila jambo ukiliweka sawa lilete hela hutaipata kuna kitu kitajitokeza tu...Kazi pia ni hivyo hivyo hata mtu mwenye connection anafeli yani acha tu kmmmk!
Uko sawa na maisha yangu kaka..ila kuna suluisho Mungu yupo
 
Mwanamke Ni mtu hatari sana, Mimi ni mfano Hai wa Matendo ya ukatili wa Mwanamke:

Hii naongea kutoka Moyoni mwangu wanao Bisha tabia za wanawake hawazijui.

Sikia hii story ya kweli katika Familia yangu,

Mama mkubwa mke wa Baba yangu walio oana na Baba yangu bonge la Harusi ujanani wali Dumu katika ndoa yao kwa miaka 5tu na wakazaa watoto wa3. Ila ugomvi ulikuwa daily tatizo mwanamke Alikuwa hafanyi majukumu yake ya nyumbani bali alipenda sana starehe na waganga kumchezea mume, Mume akapewa taarifa na majirani akafuatilia aka kuta kweli mkewe na vitu vya ajabu kwenye kabati la nguo na kitandani kwenye mto wa Baba na uvunguni kaweka dawa za mitishamba..

Mume kufuatilia vizuri aka gundua Mwanamke pia alikuwa anaiba hela ndani na kujenge kwao.. Wakaachana ndai ya miaka mi5 ya ndoa.

Mzee akachiwa watoto wa3 wadogo sana, akaishi bila mke kwa miaka4 , wazazi wake wakamshauri Aowe mke mwingine baada ya taarifa za yule mke wake kusambaa kuwa anaishi na mawanaume Mwingine Arusha na nimja mzito, wakati kamuachia watoto tena kwenye Nyumba ya kupanga uja nani akiwa na hali ya kawaida sana kimaisha kwa maana ya kipato cha kawaida.

Mzee kweli akajiongeza aka chukua mke mwingin ambaye ndio mama Yangu, tukazaliwa sisi, baada ya miaka kama 25 kupita tukiwa tusha zaliwa watoto6, Baba alisha pandishwa cheo na kusoma zaidi maisha yakawa makubwa na akawa msaidizi wa mkurugenzi wa Bank kuu ya tanzania na baadaye mkuu wa Azina, akawa kesha wekeza sana kila kona ya jiji la Dar na kwao Mkoani..

Ghafl mauza uza ya ugomvi ndani yakaibuka mzee kawa kama anachanganyikiwa haishi kumpiga mama kila mara yaani akawa kama siyo yeye tena.. Mara afukuze watoto mara hili mara lile, Baadaye Mama yangu akaugua ugonjwa wa ajabu sana akabaki mifupa tupu mm nikiwa ndio nimezaliwa nina mwaka 1 , mzee akawa hajali huduma wala hataki kuangali watoto,

Mama akaja kuchukuliwa apelekwe matibabuni, walizunguka mahospitali yote tanzania na ukumbuke hadi kenya na South africa alipelekwa lakini haponi wala ugonjwa hauonekani, Mwishoe akawa anakaribia kukata roho kabaki mifupa tu waka mrudisha Kijijini kwao asubirie kufa tu. Lakini kule kijijini wazee wa upande wa Mama wakajiongeza wakampeleka kwa mtaalamu wa Jadi aka aguliwa na ukweli ukajulikana alitupiwa jini na mke mkubwa na mambo mengine mengi tu.. bahati nzuri akatibiwa akapona akarudi kwenye hali yake baadaye Wakati anarudishwa nyumbani kwa wazazi wake maana alitokea kwa Matibabu ya jadi.. aka kuta watoto wote wame teletwa na kutelekezwa kwa wazazi wote. . wamekonda nusu ya kufa yule mkubwa kuliko wote aliye kuwa ana mika15 ndio kachangnyikiwa wengine wote wameacha shule na hawataki kabisa kusikia shule wala hawajielewi. Wazee wakoo waka jiongeza kuwapokea na kuwalea.

Mama alipo fuatilia aka ambiwa alivyo ondoka tu kwenda matibabuni, Week ile ile Mke mkubwa aliyekuwa ame achana na baba kwa miaka 25 alirudi na kugina ndani kwenye nyumba aliyejenga Mama yetu na Baba, na wakati huo Mzee hajitambui tena kawa kama mjinga wala hakumbuki watoto ana itwa ustawi wa jamii anaulizwa matumizi ya watoto ana sema mbona yeye hana watoto zaidi ya watatu aliyo nao nyumbani,?? watu wakadhani ni utani, kuja kumbana sana wakaagundua kweli hana kumbukumbu .. ila kesi ikaenda mahakamani ika amuliwa ahudumie watoto na aangaliwe kama akili ziko sawa. baadaye Ikaisha kienyeji Majaji wakapewa hongo na yule mke kubwa maana sasa yeye ndio alishikilia account zote za baba na mzee alifukuzwa kazi maana alikuwa haeleweki tena..

Baada ya Muda Baba kaja kufa kiajabu ajabu tu.. tuka mzika, mama mkubwa kaendelea kuishi ndani na wanawe, Ukoo ukasema kuwa kila kitu kwenye nyumba aliyokimbilia kuishi Mke mkubwa nicha watoto wa mke mdogo kwa kuwa Marehemu alisha Andika na kuwambia Wazazi wake kuwa Nyumba ya ujanani aliyo jenga kabla ya mama yangu kuishi naye na kuzaa naye ni ya watoto wake watatu aliye zaa n mke wake wandoa, ila hii mpya aliyojenga akiwa na mke mdogo yaan maa yang ni ya watoto 6 aliyo zaa na mama yangu.. Una ambiwa kile kikao cha ukoo kilivurugika kwa ugomvi mke mkubwa akawa moto na yule aliye kuwa kiongozi wa ukoo alikufa ndani ya week iliyofuata, Kukawa na viongozi wengine wanao chaguliwa Kushika nafasi ya Ukoo ila wakigusia haki za watoto wa mama yangu tu wanakufa, mpaka sasa Ninavyo ongea Baba wakubwa wa5 wote wamekufa kimaajabu. . na haki yetu hatuja ipata .. ndugu zangu karibia wote ni vichaa . nime baki mm tu ndio angalao nina jitambua..ingawa vita ya maisha yangu ni kubwa kama siyo kujificha katika maombi wangesha ni maliza..

Lakin kikubwa kinacho ni shangaza ni kuwa Baba anaonekana kule kijijin watu kazaa wana muona akiwa mchafu na manywele ila waki msogelea anapotea, mwanzoni tulidhani ni utani tukasema labda watu wanongea tu kwa kuwa yaliyotokea kweye familia yangu yameumiza watu wengi hadi majirani wa kule kijiji hivyo wanazusha tu kwa hasira walizo nazo juu ya mateso wanayo yaona kwa ndugu zangu.. Lakin sasa Hivi ni navyo ongea juzi tu mwezi wa kumi na moja mwaka huu uliyoisha. Kaka yangu mkubwa akiwa ndani kwake Katokewa na baba, kaamka zake aka kojoe ghafla akamuona mzee kakaa kwenye kochi ila haongei kitu alipo piga kelele mzee kapotea.


Jamani Uchawi Upo.. Ila naku hakikishia siku nikiingia kwenye Uchawi.. Nita angamizaa kizazi cha huyu Mwanamke mpaka kitukuu cha mwisho.. Naupima tu Uvumilivu wangu katika maombi.. Mungu aniongoze maana naijua nafsi yangu ilivyochoka na siku nikihamia kwa Shetani nitakuwa Shetani Halisi wala sita Igiza kabisa.
Pole Sana.
 
Mkuu pole sana..

Sijui nisemeje, ila kama umeamua kukaa kwenye hayo maombi mwenyewe , basi shikilia hapo hapo, lakin inabidi utafakari sana hio vita, na approach unayochukua, mwanamke huyo na wanaomsaidia wanaachwaje huku wameua baba wakubwa na wazee wa ukoo wanakufa tu, naona kama mission yake ni kuwamaliza wote upande wako na mama yenu

Kuna mdau humu alikuja kuelezea stori yake jinsi walivyommaliza mzee wake, nadhan ni kama wewe tu, ila yeye aliamua kuchukua kisasi kwa wote waliohusika, aliwajua, na alifanikiwa lengo lake la kuwamaliza

Shangaz yangu yeye alikuaga anatumua approach ya maombi, lakin kuna dada wa mume wake ndio alikua na chuki na kaka yake na familia yake, aliona sijui anafaidi sana, mana mjomba alikua ofisi ya rais, na walikua wanaishi maisha mazuri, ( oneni watu walivyo na roho mbaya na roho za kwanini), chuki hio ilipelekea akaanza kuiangamiza familia, alianza na watoto, mtoto wa kwanza ( dada yangu) , aliugua na anachoumwa hakijulikani, na siku anakata roho alimtaja huyo mama..haitoshi, akaja mama ( shangaz yangu) , kifo chake kilikua kibaya nashindwa kusema, akafata mtoto mwingine, naye akaondoka, akaja baba , naye akaondoka, akaja mtoto mwingine yeye akapata uchizi, akaja mtoto mwingine maisha yake yakarudi nyuma sana na kua magumu sana, aliyesalimika ni mmoja tu ambaye ndio kidogo anajiweza,..ngoja niishie hapa.
Kaka ina uma sana.. Napitia magumu sana
 
Back
Top Bottom