Mchezo mchafu unaofanywa na benki kuwapora wateja pesa zao

Mshahara mkubwa na kuweka akiba ni vitu viwili tofauti

Kuweka akiba kunahitaji nidhamu ya hali ya juu na kujikanya nafsi yako zaidi ya mahakama inavyojikanya kabla haijapokea ushahidi wa mtoto mdogo ambao haujaungwa mkono na ushahidi mwingine

Kuna watu mapedesheee watu maarufu, wafanya kazi waliokuwa wanatunza wasanii wa bendi kwenye mabaa kabla ya utawala wa magufuli, wakifa wanafamilia kutokana na umaharufu wao hukimbilia kadi za benki mweee hakuna kitu

So tusisingizie benki tuu , tukumbuke kuweka akiba, ukishakuwa mlevi wa mikopo ya benki na vikoba sahau kitu kinachoitwa akiba
 
NMB wanatisha na cha ajabu maafisa wa benki mkiwa mnajuana ndo anakumaliza.Wana tabia kama Askari wetu wasio na maadili, akikujua ndo anakulengesha
 
Na mikopo ya watu binafsi, nuksi tupu
 
Hawa NMB nikipata muda nitaenda na slip zangu tupige hesabu polepole bila kupigizana kelele. pesa niliyoweka na kutoa haziendani kuna gap la hamsini na kitu

Sasa nimeshapata mwangaza nilijua nimejichanganya kumbe mmenichanganya sasa mtajua hamjui
 
Kufwatilia Kuna siku nilibank 600,000 jamaa akaweka 60,000 akala 540,000
Na sikuwahi kuweka pesa chini ya laki ,manger akaniomba radhi Ila yula mtumishi alihamishwa pale drishani
Why alihamishwa na si kufutwa kazi??


Branch manager anahusika na huo wizi si bure kuna paceee wanampa
 
Wewe utakua mmoja wapo sio bure
 
Sister wangu alifiwa na mumewe mwaka alikua mhasibu kwenye wizara flan,same alipopata usimamizi wa mirathi alikutana na hali kama hiyo,stanbic hakukua na pesa,crdb kuna deni ambalo mkewe alitambui,nmb kuna laki 4!nchi ngumu sana hii!
 
Mimi mzee wangu alifariki 2018 na alikuwa analipwa pension PSSF baada ya kustaafu na alikuwa mkulima na walilipwa fedha kwa ajili ya Kilimo, aliuza mazao yake na kuweka pesa benki kwa kumshirikisha Mama ila Aliyekuwa anasimamia Mirathi kaenda benki na kukuta ana laki nane tu. Dunia inasikitisha sana.
 
Naona unataka kuubariki uovu,hivi unazani watu wanafanana,kuna watu wanapata hela zao kihalali hawaibi hata senti ya mtu.Kwa hiyo style yako tutakuwa tunajenga kizazi cha ajabu sana cha wizi kilicho kosa uaminifu.
 
Mpesa ndo iko salama kuliko hata benk. Mm sina bank a/c kwa sasa naona ni ujinga.hela ipo benk haiongezeki imelala tu? Hapana
 
Mpesa ndo iko salama kuliko hata benk. Mm sina bank a/c kwa sasa naona ni ujinga.hela ipo benk haiongezeki imelala tu? Hapana
Shida Mpesa huwezi hold ela nyingi labda mils kadhaa.
 
Nami kuna siku nilienda weka hela. Nilizitenga mafungu mafungu. Yaan nilitumia lisaa kwa utulivu sana pale bank. Na nilikua nimedress kama beki 3. Halafu nimenyoa. Ghafla teller ananambia imepelea 2m... yaan tena anaanza kunibunia eti utakua umekosea kuhesabu. Yaan natetemeka. Bora angesema imepelea elf 20. Yaan mil 2 nzima? Na vile nilikua rafu ile siku ndo akazidi kuniharass.
Na mimi nikambadilikia nioamwambia nazijua tabia zenu. Naomba twende camera room na baada ya hapo namtaka branch manager wenu maana naona huduma mnagawa kwa kuangalia outlook za watu. Akawa kama anakaza na mimi sasa nikaongeza loudspeaker. Nikagonga na meza. Nikauliza kwanguvu qhere is rhe branch meneja office... i want to see the camera room alsoo.. weee akaanza tetemeka. Yule dada anaanza nibembeleza anieleweshe. Nikamwambia camera ndo zitanielewesha.. nikaonyeshwa meneja chaap nikamfata. Nikamwelezea scenario. Akaniomba sana nitulie. Tukaenda kwa lile dirisha la yule mama wa makamo nikakuta ameshaandika amount yote... nikamwuliza mbele ya meneja hii 2mil ulosema imepelea umeidownload eh? Nikamwomba ahudumie watu kwa kutokuangalia mavazi. Hii bank ovyo sana. Yaan imeoza sana siku hizi. Sasa sijui kama huwa wanapewaga adhabu ama lah.
 
Mfanyakazi wa UN na analipwa mil 2?

Ina maana mishahara ya UN sivyo ambavyo watu tunafikiria ni minono kupindukia

Sent using Jamii Forums mobile app
Inategemea anafanya kazi gani, kuna madaraja pia. Lakini alama UN huwa inatumika ndivyo sivyo wao wanashirikiana na mashirika mengine mengi madogomadogo ambayo wanayafadhili kuendesha miradi, kwa taratibu zao magari wanayowapa hayo mashirika na hata official documents zote zinaandikwa UN

Sasa ndio watu wa nje wasiojua huita wafanyakazi wa mashirika hayo kama wafanyakazi wa UN
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…