Mchungaji aliedai Corona ni kagonjwa kadogo mbele ya Mungu, amefariki kwa Corona

Wala haifuti kuwa mungu ni mueza wa kila kitu na ni Mkuu kuliko corona
 
Okay brother, let me ask you. Is COVID19 too big for God? Is God incapable of rescuing us from it?

Kumbuka maandiko yanasema kupitia kwa Yeremia, "....chombo kilichofinyangwa kitamwambia nini mfinyanzi?"
Tena maandiko yanasema kwa Zaburi
"Nchi na vyote vijazavyo ni mali ya Bwana...."
 
Mungu hai Mungu haiondoi korona yeye Bali nguvu alioiweka kwa binadamu(akili).Akili no nguvu ya kimungu.Mungu hashughuloki na vitu Bali wanadamu aliowaumba.Binadamu ana akili aliopewa na mungu na ndio atakayotumia kuponta korona.Utengano na ubinafsi wa binadamu umechangia korona kushinda.
 
Hata Kama amekufa na corona bado Mungu atabaki kuwa Mungu
Hakuna aliye mkuu zaidi yake corona ni kitu kidogo sana kwa Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
Uko sahihi! Ila usipochukua tahadhari itakula kwako.

Ni sawa na kunywa kinywaji chenye sumu huku ukijua kina sumu ila ukajiaminisha Mungu atakuponya.

Kutochukua tahadhari dhidi ya Corona huku ukikiri ukuu wa Mungu, huko ni sawa na kumjaribu Mungu jambo ambalo ni kosa.
 
Hata Kama amekufa na corona bado Mungu atabaki kuwa Mungu
Hakuna aliye mkuu zaidi yake corona ni kitu kidogo sana kwa Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
Na nyie mnaingia kwenye mtego wa imani au imani yenu haiko sawa. Unapolinganisha janga la korona na ukubwa wa Muungu maana yake janga hili halitokani na yeye Muumba bali ni kazi ya mamlaka nyingine inayoshindana naye (shetani). Huu ni udhaifu wa imani.

Ukiamini korona na majanga mengine au kifo ni hujuma za shetani na kwamba Mungu anapambana nayo kuwakinga/kuwaokoa wanadamu, basi ni lazima ukubali kuwa shetani huwa anamshinda Mungu katika mapambano na kwa maana hiyo shetani ni mkubwa/ana nguvu kuliko Mungu. Hii ni kwasababu majanga yanatokea na watu wanakufa.

Ukweli ni kwamba Mungu ndo muumba wa ulimwengu na vyote vinavyoonekana na visivyoonekana pamoja na virusi vya korona na shetani mwenyewe. Shetani hapambani na Muumba wake, bali Mungu anamtumia shetani kama nyenzo ( mtihani) wa kupima akili (imani) ya binadamu.

Mungu ana mamlaka juu ya kila kitu; anachotaka kiwe na kinakuwa na kinyume chake. Janga la korona limetokea kwasababu Mungu ametaka litokee na si kwa sababu shetani ametaka litokee. Kwa msingi huu hakuna haja bali ni makosa kupima ukubwa wa Mungu na janga la korona ambayo ni kazi yake hata kama itahitimishwa kuwa Mungu ni Mkubwa kuliko korona.

Tuwekeni sawa imani zetu vinginevyo tutapotea.
 
Duh... naogopa haya yasije tokea kwa aliyesema “kacorona kaugonjwa kadogo”
P
 
Ubinafsi wa baadhi ya viongozi wa dini kuona sadaka na matoleo mengine ni muhimu kuliko uhai wa watu vitatuangamiza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakika wewe wasema.
 
Ubinafsi wa baadhi ya viongozi wa dini kuona sadaka na matoleo mengine ni muhimu kuliko uhai wa watu vitatuangamiza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Haishauriwi Wala hairuhusiwi kuishi Kwa kumtegemea Mwanadamu, Mjue zaidi Mungu wako kuliko mkuu wako wa dini, Vinginevyo utaishi Kwa utumwa na kufanyia kazi za watu wanaoikalia akili na ufahamu wako!

Funguka na uwe huru mkuu, ishughurishe Akili yako, shauri yako
 
Hata kama amekufa kwa Corona, alichokisema ni ukweli mtupu, Mungu ni mkuu kuliko Corona.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiwa "objective" utabaini kuwa maandiko haya yanadhihirisha shetani ana uwezo juu ya Yesu. Yaani kile kitendo cha shetani kumchukua Yesu na kumsimamisha kwenye paa za majumba ya Mji Takatifu na kumtaka ajirushe ni wazi kuwa Yesu aligeuzwa na kuwa "subject" na kujaribiwa. Yaani shetani anampima imani "mtoto wa mungu" ...!!

Tushukuru tu kwamba Yesu alikuwa mjanja na hakujirusha (bila shaka) kwa vile aling'amua mtego na vinginevyo angedhurika. Shetani alitaka mungu afe au apate ulemavu...!!😂😂😂
 
Nilimsikia Gwajima akiwalisha ujinga waumini wake. Ole wao wazingatia mafundisho ya kijinga namna ile.
 
Umemjibu vizuri sana! Haipaswi kulinganisha ukubwa wa Mungu na kile alichokiumba. Watu wanapotoka kwa kuamini covid si kazi ya Mungu bali ya shetani na Mungu anapambana nayo kutuokoa.
 
Binafsi ninaona yuko sahihi kwa 100%, kwa sababu ameendelea kumuona Mungu ni mkuu katikati ya vitisho vya kufa kwa Corona.

Katikati ya mambo yote, Mungu atabakia kuwa Mungu. Na katika mambo yote Mungu ni mkuu.
Hakuna anayeukataa ukuu wa Mungu. Lakini unatakiwa kujua kuwa hata anayekupa tahadhari, ni mjumbe wa Mungu pia kwa sababu maarifa yote hutoka kwake.

Mungu nyakati zote, ili kuwaokoa watu wake aliwatumia wajumbe wake kuwaelekeza watu wake wafanye nini ili wasiangamie.

Kuna watu ni wajinga wa neno la Mungu. Ukuu wa Mungu haupo katika wewe kuamua kulala katikati ya barabara usiku kucha wakati Mungu kakupa akili ya kujua kuwa barabara hiyo yanapita magari, yanaweza kukukanyaga na ukafa. Mbaya zaidi unakuja unaambiwa, ondoka barabarani kuna lorry halina hata taa linakuja, wewe unasema, Mungu ni mkubwa, atanilinda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…