Mchungaji Anthony Lusekelo, aionya Serikali ya Rais Samia juu ya amani ya Tanzania

Mchungaji Anthony Lusekelo, aionya Serikali ya Rais Samia juu ya amani ya Tanzania

Mungu yupi? Huyu aliyeletwa na wazungu kwenye meli na kumtumia kama njia yao mojawapo ya kuwatawala na kuwatumikisha waafrika? Siwezi kuamini hiyo kitu!! Wanaojiita watumishi wa mungu ni wahuni tu wanaotumia ujinga wa "kondoo" kujinufaisha. Wako wapi waliomuua Galileo kisa alisema dunia ni duara siyo flat kinyume na maandiko ya bible kipindi Hicho? Leo hii wamebadilika wanakubaliana naye, dini, bible na huyo Mungu wako ni elements zilipandikizwa na wajanja wachache ili wawaswage vizuri nyie "makondoo".
Asante sana.
 
Kwanza tutaje uonevu wa serikali kwa Watanzania wanyonge.

- FAO LA KUJITOA NSSF liliondolewa, watu wanalia na hawasikilizwi.

- TOZO ZA MPESA, AIRTEL MONEY AND TIGO PESA

- MAFUTA YA MAGARI KUPANDA SANA, UKILINGANISHA NA NCHI JIRANI.

- MAFUTA YA KUPIKA KUPANDA

kwa hiyo ndio uonevu wa serikali, WOTE wanaumia, CCM, CUF, NCCR, UDP, CDM, etc. Tozo Haina itikadi wala dini

Mapolisi, wanajeshi, nao wanaumia na Tozo, Bei kubwa za mafuta ya kula..
 
Kwa Hiyo Mchungaji Luseleko, ameongea uonevu wa serikali kwa Wananchi kwa mapana, kwa mambo mengi. Watu wengi, wamekimbilia kuongea kisiasa tu, wameacha kucomment kijamii.

Panueni wigo wa mjadala, ili serikali isikie na kujisahihisha. Tujadili uonevu wa serikali kama Skilled labor kuporwa FAO LA KUJITOA NSSF

Tozo za simu na mafuta ya kula kupanda Bei
 
hawa ndio viongozi wa dini tunaowataka kwenye jamii,viongozi wanaoweza kuinuka na kuikosoa serikali pale inapofanya vibaya
Yaani miaka sita hajaona shida kwa Mungu wa palamakandalasi bali miezi sita ya Suluhisho, mwe mwe mwe
 
Hii nchi haiitaji elimu kubwa ili uiongoze ni kitu kidogo tu kinahitaji kwa kiongozi ili kuongoza nchi hii.

Wapo wasomi ila Taifa linameguka kwa sababu za kijinga sana, nashangaa huko mashuleni walienda kufanya nini! Bora darasa la saba mwenye akili anaweza kuongoza watu 1000 kuliko mhitimu wa chuo kikuu ambaye hawezi kuongoza watu hata 10.

Viongozi wetu watumie utashi kuipa nchi maendeleo na raia wake wanufaike na taifa lao. Nchi ni ya wananchi, tufanye vitu kwa ajili yao si kuwakandamiza.
 
Atakuwa kaanza kunywa KIWINGU huyu, kinywaji kipya mjini.


Everyday is Saturday............................... 😎
 
Ukiona mawe yameanza kuzungumza ujue kumekucha
Viongozi wa dini wetu wengi ni wanafiki tu, maslahi yao yakiguswa tu ndio utawasikia wanapiga kelele!!!lakini kila siku waumini wao wanaumizwa hawana habari ya kuwatetea, sana sana wanakuwa upande wa mnyonyaji tena kwa ku nukuu mistari toka kwenye vitabu vitakatifu, il kuhalalisha!!
 
Kwanza naomba nieleze wazi kwamba utawala huu ni laini Sana ndio maana unachezewa ,hakuna anaeuonea.

Na hizi chokochoko mara nyingi hutokea kipindi cha viongozi wakiwa Waislamu wakristo na Waislamu huanza mivutano.

Nilichojifunza hii hutokana na upole wa viongozi wa kiislamu,Magu aliwanyoosha Sana kuanzia wakubwa wa makanisa hadi akina gwajiboy walipekuliwa hatukusikia kelele za watu wa imani kuungana au sijui eti kuonewa,hakuna utawala ulikuwa kandamizi kama wa Magu.

Mama stuka kuwa mkali Sana Hawa watakuchezea sharubu na usiwape airtime ya kuongea waufyate kama awamu iliyopita la sivyo watatoa kila matamko na kukupaka uchafu wote.

Bora uwe dikteta kuliko kuwapa watu uhuru wakautumia vibaya kwa propaganda za kijinga,na hii nchi imejaa wajinga huamini Sana propaganda.Magu alikuwa dikteta akawaaminisha watu propaganda wakawa upande wake huku anawaminya wanaonyanyua mdomo.

Ukiniuliza huyo uonevu gani hasa hana majibu,akikwambia Mbowe sijui gwajima ila atajifanya haelewi kwamba gwajiboy alipekuliwa uchi kwake,Akina Mbowe na wengine walikula mapanga,risasi na watu kupotea nk na hakuna alikuwa ananyanyua mdomo juu.Sasa Maza wachekee tuu na uwe unakaa kimya unaogopa kutoka hadharani kuongea kwa ukali na kwa vitendo.

Sasa hivi mzigo wa chanjo kaachiwa Waziri nyie kimyaa,subiri wakuoneshe shoo.
Jambo ambalo unapaswa kulielewa ni kwamba-Hakuna Makanisa yalilokuwa na mgogoro wa waziwazi na serikali ya magufuli kama Makanisa katoliki na KKKT,na ilifika mahali Mwendazake akawasingizia baadhi ya Maaskofu wa RC siyo raia wa Tanzania na hata mwendazake alijaribu ku-retaliate kwa kuwabambikia makodi na bado hawakukaa kimya na mambo mengine chungu nzima.Licha ya Magufuli kuwa muumin wa RC,Lakin kanisa halikuacha kumpinga pale alipokuwa anafanya mambo ya kihuni.At least try to be fair in your reporting
 
shida ni dini ya uraisi tu hapo, hakuna kingine.....hivyo visababu vinavyowekwa ni vya kulazimisha tu. Raisi wa kiislamu nchi hii hukutaka na vikwazo na matatizo sana. Watu waliminywa haki zao, walibanwa wasiongee, malisasi yalilindima, utekaji ulishamiri n.k lakini alikuwa kimya km hakuwepo au alikuwa haoni.

Mama kumtikisa mbowe kidogo (jambo ambalo ni la kawaida kisiasa...isitoshe lina sababu zake), na kujibiwa gwajima kidogo (mtu ambaye chokochoko amezianza na kuziendeleza mwenyewe kinyume na utaratibu wa kinidhamu ulizoeleka) tayari huyu anajitokeza na kuongea haya. UDINI, UDINI, UDINI. NI CHOKOCHOKO ZA KIDINI!
Kipindi cha JPM kulikuwa na Dr Shoo. Vilevele kulikuwa na WARAKA WA WAKATORIKI. Umesahau? Vip kauli za Kakobe mwanzoni mwa utawala wa JPM. Yote haya umesahau?
Mimi naona serikali iwe tayari kukosolewa masuala ya UDINI UDINI ni hisia zako tu.
Ni kuulize mwanaharakati machachari Shehe Ponda hatumsikii kipindi hiki vp?
 
Jambo ambalo unapaswa kulielewa ni kwamba-Hakuna Makanisa yalilokuwa na mgogoro wa waziwazi na serikali ya magufuli kama Makanisa katoliki na KKKT,na ilifika mahali Mwendazake akawasingizia baadhi ya Maaskofu wa RC siyo raia wa Tanzania na hata mwendazake alijaribu ku-retaliate kwa kuwabambikia makodi na bado hawakukaa kimya na mambo mengine chungu nzima.Licha ya Magufuli kuwa muumin wa RC,Lakin kanisa halikuacha kumpinga pale alipokuwa anafanya mambo ya kihuni.At least try to be fair in your reporting
Wapi lilimpinga wakati muliufyata ? Sasa unajiuliza huyu mpuuzi Kusekelo katoa wapi upuuzi wake? Acheni kuleta taharuki na chokochoko za kijinga
 
Mzee Lusekelo naona busara zake zinapungua kwa kasi sana!!
namshauri awe anafikiria kwanza kabla ya kuzungumza, maana yeye ni kiongozi wa waumini, hivyo asije akadharauliwa.

Kinacho fanywa na Serikali hii sio jambo jipya .
Serikali hawezi kuchokonoa taasisi za dini bali serikali inao wajibu wa kulinda Amani na utulivu wa kila raia bila kujali dini.
ni kweli kila raia anao uhuru wa kuabudu lkn uruhu huo lazima uwe na utaratibu na mipaka, Serikali ndio yenye jukumu la kusimamia utaratibu huo.
Serikali haiwezi kuachia makanisa na misikiti ianzishwe kiholela tu bila kufuata utaratibu wa kusajiliwa n.k. inawezekana kuanzishwa vikundi vya kigaidi, waumini kupotoshwa na kuangamizwa n.k, ndio maana serikali imeweka utaratibu wa kusajili Misikiti na Makanisa ili kuzuia makundi maovu na wabaya kutumia mwanya wa kujificha ktk vyombo vya kidini.

Endapo hakutokuwa na utaratibu kama anavyo taka Lusekelo kutasababisha vurugu.
Lusekelo asiifundishe Serikali namna ya kusimamia Amani ya nchi, kwenye jambo hili namshauri akae afikirie au azungumze na Waziri wa mambo ya ndani Simbachaweni.


Waziri Simbachaweni amekuwa kimya sana kwenye mambo ya msingi, tuna muomba awe anajitokeza kwa wakati kujibu upotoshaji unapo jitokeza.
wizara ya mambo ya ndani ndio wizara iliyo pewa dhamana ya kusimamia Amani ya nchi hiii, hivyo tusiwaachie watu wanapotosha ukweli either kwa maksudi au kwa kutoelewa au kwa malengo binafsi.
tusinywee kwenye masuala ya Amani ya nchi, tujitokeze kwenye vyombo vya habari tutoe ufafanuzi, tusiachilie upotoshaji uchukue nafasi.
Mawaziri wetu mmepewa dhamana ya kutuongoza na kusimamia, acheni kukaa kimya kama mmeshindwa kazi ni bora mkaomba kustaafu kuliko kuamua kula ganzi.
 
Katika hali ya kushangaza, siku zote mzee wa Upako huwa upande wa serikali.
Lakini leo ameamua kuvunja ukimya na kuinyoshea serikali kidole tena kwa ukali kuwa ijihadhari isije kuharibu amani ya Tanzania.

Wakati akitoa angalizo hilo, amewataja kwa majina akianza na Kassim Majaliwa waziri mkuu, Rais Samia na Mpango.

Amewakumbusha kuwa sio vyama vya upinzani pekee huleta machafuko bali hata Serikali huwa ni chanzo cha machafuko.

Ameonya kuwa uonevu ukizidi hata askari taratibu huungana na raia kinyume cha watawala kwani hata wanao onewa ni jamaa zao na maaskari.

Zaidi ameionya serikali kujiepusha na kuingilia mambo ya kidini kwani hata wakizifuta imani za dini ziko mioyoni mwa watu na sio kwenye usajili wa kiserikali.

Amekumbusha kuwa miaka ya 80 serikali ilijaribu kufuta usajili wa makanisa hata kuwafunga wengine lakini ilishindwa na tena wakristo waliungana.

Amesema watu wa imani moja huungana wakati wa kuonewa hivyo wajihadhari na jambo hilo.

Amesema kwasasa serikali ina matatizo makubwa kisiasa, corona nk kwa hiyo isiongezee mzigo wa kidini haitabaki salama.
Zaidi msikilize hapo chini kwenye link.

View attachment 1897536
Copy kwa mama Chokochoko!
KATIBA KATIBA KATIBA!
 
Hawa wahuni wanaojiita viongozi wa dini JPM aliwadekeza sana, huyu alimjengea hadi barabara ya lami waumini wake wapite, kila mara alikuwa anawaalika ikulu na kuwapa upendeleo wa juu, na hiyo yote ni kutokana na uoga wake na kutojiamini, akipenda kusifiwa na kila mtu!! Wale wa upande mwingine ilikuwa ni kuwalisha ubwabwa na kuwahonga misikiti, miezi hii mitano wamepotezewa tayari wameanza mayowe! Ni wengi wataibuka, vikiwemo vyombo vya habari kama Clouds ambavyo vimekuwa yatima kwa sasa ambavyo mbeleko walilolitegemea lipo Chato milele. Kila utawala na namna yake ya kutawala. Itatuchukua siyo chini ya miaka 3 sumu na propaganda alizosambaza JPM nchi kuisha
Wajameni,
Kama kuna kitu Mwendazake alifanikiwa ni kujenga HOFU miongoni mwa waTZ kutokana na vitisho muda wote. WaTZ wakawa ni waoga na wanafiki. Wasomi na Viongozi wa dini wakishangilia udhalimu na kusifu udikteta, wakati nchi ikiendeshwa kwa matamko.
Yaonekana kama vile hofu hiyo yaanza kuondoka na legacy uchuro kufutika.
Lakini TAIFA letu litaponywa kikwelikweli na uwepo wa vi-miunguwatu kwa ujio wa KATIBA MPYA iliyo bora.
-
 
Wapi lilimpinga wakati muliufyata ? Sasa unajiuliza huyu mpuuzi Kusekelo katoa wapi upuuzi wake? Acheni kuleta taharuki na chokochoko za kijinga
Ni either huna uelewa wa mambo au umeamua kushupaza shingo kwa kivuli cha udini.Nikupe mifano michache-Askofu Niwemugizi wa Ngara alinyang'anywa pasipoti baada ya kuongelea masuala ya katiba mpya;Askofu Juda Thadeus Ruwaichi alipambana sana na magufuli kuhusiana na msimamo wa serikali kuhusiana na CORONA,Askofu Shoo KKKT aliongelea sana madhila viongozi wa upinzani wanayofanyiwa nchini kwamba siyo sawa,TEC waliwahi kutoa Ujumbe wa pasaka kuhusiana na baadhi ya matukio mabaya yaliyokuwa yanafanyika nchini kiasi cha kuichukiza serikali ambayo ilipanga mkakati wa kuyafuta makanisa na baadaye kupiga U-turn.Swali la msingi-Mashehe wa Kiislamu zaid ya 150 nchi nzima waliwekwa Jela na Viongozi wa kikristo?? Kwa hiyo hata kama kitu kilichozungumzwa na Lusekelo (ambaye wewe unasema ni mchafu) ni sahihi,Je,tukipinge tu kwa sababu ni Lusekelo kasema au tupime usahihi wa jambo lenyewe?
 
Hawa wahuni wanaojiita viongozi wa dini JPM aliwadekeza sana, huyu alimjengea hadi barabara ya lami waumini wake wapite, kila mara alikuwa anawaalika ikulu na kuwapa upendeleo wa juu, na hiyo yote ni kutokana na uoga wake na kutojiamini, akipenda kusifiwa na kila mtu!! Wale wa upande mwingine ilikuwa ni kuwalisha ubwabwa na kuwahonga misikiti, miezi hii mitano wamepotezewa tayari wameanza mayowe! Ni wengi wataibuka, vikiwemo vyombo vya habari kama Clouds ambavyo vimekuwa yatima kwa sasa ambavyo mbeleko walilolitegemea lipo Chato milele. Kila utawala na namna yake ya kutawala. Itatuchukua siyo chini ya miaka 3 sumu na propaganda alizosambaza JPM nchi kuisha
Hili lilevi lusekelo likiitwa ikulu na kuhakikishiwa wizi wake wa sadaka utalisikia linaanza kuponda wapinzani..
Hivi watanzania ni wapuuzi kiasi gani hadi kuwaamini majizi kama haya(kakobe,gwajiporn etal
 
Katika hali ya kushangaza, siku zote mzee wa Upako huwa upande wa serikali.
Lakini leo ameamua kuvunja ukimya na kuinyoshea serikali kidole tena kwa ukali kuwa ijihadhari isije kuharibu amani ya Tanzania.

Wakati akitoa angalizo hilo, amewataja kwa majina akianza na Kassim Majaliwa waziri mkuu, Rais Samia na Mpango.

Amewakumbusha kuwa sio vyama vya upinzani pekee huleta machafuko bali hata Serikali huwa ni chanzo cha machafuko.

Ameonya kuwa uonevu ukizidi hata askari taratibu huungana na raia kinyume cha watawala kwani hata wanao onewa ni jamaa zao na maaskari.

Zaidi ameionya serikali kujiepusha na kuingilia mambo ya kidini kwani hata wakizifuta imani za dini ziko mioyoni mwa watu na sio kwenye usajili wa kiserikali.

Amekumbusha kuwa miaka ya 80 serikali ilijaribu kufuta usajili wa makanisa hata kuwafunga wengine lakini ilishindwa na tena wakristo waliungana.

Amesema watu wa imani moja huungana wakati wa kuonewa hivyo wajihadhari na jambo hilo.

Amesema kwasasa serikali ina matatizo makubwa kisiasa, corona nk kwa hiyo isiongezee mzigo wa kidini haitabaki salama.
Zaidi msikilize hapo chini kwenye link.

View attachment 1897536

Ni mnafiki kama wanafiki wengine tu huyu mzee. Mara ngp serikali imefanya mambo ndivyo sivyo kwa wananchi wake amekaa kimya? Yaani leo taasisi za kidini zimeguswa ndiyo anafungua hilo domo lake? Alikuwa wapi miaka na miaka wengine walipoonewa?
 
Back
Top Bottom