Mdahalo wa Katiba (UDASA) kupitia Star TV - Agosti 3, 2014

Mdahalo wa Katiba (UDASA) kupitia Star TV - Agosti 3, 2014

Ukitaka kumua nyani usimuangalie usoni. CCM wanafikiri sura ya Wassira itamponya! Tundu Lissu usimuangalie Wassira usoni maana unaweza kuingiwa na huruma.

BTW hivi msimamo wa ACT kuhusu katiba mpya ni upi Dr Mkumbo?

Matusi jadi yenu, watanzania wanajua mchango wa Wasira katika kunusuru nchi isigawanywe vipande vipande na UKAWA.
 
Msije anza kuzomea zomea sasa maana amkawii jamaa wa Bunda akianza vijembe mnaanza maana atakuwa anasaidiwa na Nape pia mtulie msikilize mambo na pia msikilize na Tundu Lissu

kumbe vijembe nilidhani hoja
 
umesahau kuwa ni juzi tu WASIRA aliwachachafia UKAWA watatu akiwemo LISSU, leo atakuwa na jipya gani mbele ya Wasira?

hawa UKAWA wanachekesha sana mkuu, eti na wao wanataka ku-preempty kwa kusema eti leo ni UKAWA mmoja na Tanzania kwanza watatu, wakati wana mtoto wao wa kubagua Kitila Mkumbo.
 
TUNDU LISSU is an educated but uncivilized person I have never seen in this country.
 
Maccm yataendelea kuaibishwa kama jana walivyogaragazwa ITV
 
Lisu kashawaharibia mdahalo hao magamba dah!!! Itabidi Muongoza mada ajaribu kuwapa muda mwingi magamba angalau masaa 3 yapite ...
 
Wassira ni kiboko ya Lissu na leo atagalagazwa kama mdhalo uliopita! Lissu ana tapa tapa tuu hana pakushika.
 
Namuomba sana Tundu Lisu amtake Mzee wa Gombe aeleze maboresho ya serikali mbili ni yapi , mbona hawataji?
 
Wassira ni kiboko ya Lissu na leo atagalagazwa kama mdhalo uliopita! Lissu ana tapa tapa tuu hana pakushika.
Mkuu naona hivi sasa umegeuka kuwa mtetezi wa CCM mzuri sana.

Nakumbuka siku si nyingi sana nawe ulikuwa unakosoa utawala huu huu.

Nanukuu posts zako ambazo si za zamani sana.

Na inavyo onekana ilitumwa kabisa.
Sijui ule msemo wa sisiemu chama sikivu ndio maana yake!

Hawa jamaa ni hatari na inaonesha wako tayari kumwaga damu ili mradi wasitoke madarakani.

Ninacho jiuliza ni kwamba kwa nini siasa zina tupeleka huku, leo kutishiana silaha imekuwa kawaida hasa wafuasi wa ccm na viongozi wao wame kuwa mstari wa mbele kutishia watu kwa silaha na wamekuwa wanaangaliwa yamkini wako juu ya sheria.

Ni vyema CCM waka jua hii nchi siyo ya kwao ni yetu sote na safari yao wame iandaa wenyewe.

Na kamwe CCM hamtozuia mabadiliko kwani ni wakati wake!

Hakuna wanachokifanya zaidi ya kutete uongo na kutumiwa kama daraja la wengine! Umoja usio ona maovu ya wakubwa wao na kuya kemea ni umoja gani,.

Yan anazani yeye anavyo danganywa kwa tishert na khanga za kijani basi anajua kila wanawake wana danganyika kama yeye.

Amesahau kuwa wanawake sikuhizi wamebadilika hawafati mkubo kama yeye anavyo endeleza style hiyo.

Umenena vema! Kwanza wanaonekana kabisa wako nyuma kabisa kwani hakuna asiye jua kuwa ccm yao ndio inachochea vurugu na hasa kwa kipindi hiki bora wange kaa kimya kuliko kuonekana vituko.

Nilitegemea watachangisha pesa za kumsaidia mke wa marehemu na familia yake kumbe wao wanajali uhai wa ccm kuliko binadamu!

Nina maswali kidogo kwako.

1. Hivi CCM imebadilika nini hasa ambacho kimekufanya uanze kuona nia njema kwao, nia ambayo mwanzoni hukuiona?

2. Nini kimetokea kwako hata ukabadili msimamo mara moja na kuanza kuwaunga mkono hao uliowaona mwanzo ni wakandamizaji?

3. Ni mabadiliko yako mwenyewe binafsi, au kuna ushawishi wa watu wengine?

Majibu ya maswali haya yatatusaidia hata sisi wengine tunaoona ukandamizaji wa CCM mpaka sasa.
 
Wale waongo na wazushi wa Chadema akina Yeriko walidai wanaalikwa kwa laki mbili kwahiyo Tundu Lissu kakubali kupokea mlungula?


Niwaombe wahusika wakague audience mlangoni ili waliyolewa gongo na viroba wasiyo na usikivu wa hoja na wasiyojua maana ya mdahalo wasije kupata nafasi ya Kuzomea na kupiga kelele maana wao hawana hoja, wanachojua ni ushabiki na kelele tu.
 
Nahisi wasira atakimbia kwa kuwa hana hoja ya msingi zaidi ya vaporization

Hoja ya wassira ni moja tu :- Ukawa warudi bungeni wakapigane ndani ya ukumbi wa bunge, kukimbia nikukwamisha upatikanaji wa katiba mpya.

Wakati huohuo wassira anafanya hivyo akijuwa ccm wataitumia nafasiyo kulazimisha maamuzi kwa 100% na huu ndio

unafiki wa ccm na wassira kutumia wingi wao kulazimisha kisichowezekana ndani ya mjengo.
 
Wale waongo na wazushi wa Chadema akina Yeriko walidai wanaalikwa kwa laki mbili kwahiyo Tundu Lissu kakubali kupokea mlungula?


Niwaombe wahusika wakague audience mlangoni ili waliyolewa gongo na viroba wasiyo na usikivu wa hoja na wasiyojua maana ya mdahalo wasije kupata nafasi ya Kuzomea na kupiga kelele maana wao hawana hoja, wanachojua ni ushabiki na kelele tu.

Mbona kama unaandaa mazingira ya kuruhusu watu walioandaliwa kwa malengo maalum
 
Wote mnaoshsbikia serikali 3 hamna nia njema na Tanzania maana mnataka kuvunja muungano kwa bao ls kisigino, tumeishawashtukia.
 
Mbona kama unaandaa mazingira ya kuruhusu watu walioandaliwa kwa malengo maalum

Mkuu kuna watu wanakera sana..badala ya kutulia tupate mawazo ya wazungumzaji wao wanabaki kupiga mikelele ya kuzomea...unajua kwenye mdahalo inabidi watu washindane kwa hoja mwishowe wananchi nao watapima kulingana na hoja zinazotolewa..ila watu wanaleta ushabiki wa vyama mwishowe wanaanzisha kelele zisizo na faida.
 
Back
Top Bottom