Pre GE2025 MDAHALO: Wagombea Uenyekiti wa CHADEMA kuhojiwa na Chief Odemba. Ni tarehe 18.01.2025 Jumamosi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mbowe atakuwa ni mpuuzi kushiriki mdahalo ambao atakuwa anashambuliwa Mwanzo mwisho
kwani kama anashambuliwa kwa tuhuma au mambo ya kweli hauoni ni afya kwa ustawi wa siasa zetu na taifa?

Tunataka mijadala ya namna hii zaidi na zaidi,sio mambo za mitano tena!
Njoo ueleze umefanya nini na utafanya nini, period!
 
Mbowe na ccm yake hawapendi midahalo kwa sababu hawana hoja
Hapana, mkuu. Sisi hoja zetu ni bora kuliko vijembe na vijimaneno maneno vya majukwaani visivyokuwa na tija. Tunafokasi kwenye maendeleo zaidi.

Nasemaje? Tukutane kwa boksi hiyo tarehe 21 Jan. 2025!
 
Mdahalo unaweza kuwa mchungu kwa Mbowe. Unawaambia ni watu kwanini unataka kuendelea kuwa Mwenyekiti baada ya kukalia kiti kwa miaka 21?

Una jipya gani? Lipi ambalo hujafanya kwa miaka yote na sasa unataka mitano mingine?

Huu Mdahalo zaidi utakwenda kukivua nguo Chama. CCM watarecord mwanzo mwisho na hizo missiles watazi unleash huko mbele mwezi wa tisa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu
 
Nashauri Mbowe usiende utakuja kunishukuru
 
Tupe nukuu ya majibu ya mwenzake
 
Hata kama ni energy nitakunywa tu ili nisilale hiyo siku.

Mdahalo sio wa kukosa, na hapo ndipo Lissu atakapochukua point zote za ushindi.
Litakuwa somo kwa greens maana midahalo huwa sumu kwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…