Mdogo wa Gwajima amtetea Makonda, asema Josephat apuuzwe vita ya madawa ya kulevya

Mdogo wa Gwajima amtetea Makonda, asema Josephat apuuzwe vita ya madawa ya kulevya

Sasa mimi hapa huwa siwaelewi. Kama wanauza si wakamatwe? Au kutangaza ndio vita vyenyewe? Na kama huyo Daudi si kolomije kweli, si angeshaonesha vyeti?
Vyeti ni vya kwake, kasoma yeye, akuonyeshe wewe vyeti vyake? kama unapenda mabago ya kutangaza vyeti vyako tangaza wewe yeye vyakwake mamalaka iliyompa ajira inavijua na wakataka kuvihakiki tena watamjulisha na atawapelekea.
 
Huyu naye ana matatizo; yaani Gwajima atuhumiwe hadharani kuwa drug-dealer halafu anyamaze tu? How? Very very wrong approach ya kujisafisha na tuhuma za wizi wa vyeti ...
Ukituhumiwa unajibu kwa tuhuma, malezi gani ya kimila, utamaduni na dini umepata?
 
Kama Huyo John si Muuza madawa kweli
asinge shupalia ujinga huo.
Huyu kajificha nyuma ya uchungaji kuuza madawa,
Wengine wamejificha nyuma ya Uenyekiti wa chama kuendesha Biashara mbaya!!
Hawata penya
waendelee kuwatumia hao mamluki
lakini hawata penya kamwe
Mtaongea lugha zote na kumtetea huyo kihiyo lkn ili Gwajima aoekane muongo wekeni vyeti,lkn hata mseme nini Daudi anahitajika ashitakiwe mahakani kwa kutumia cheti cha MTU mwingine ni kosa kisheria.
 
Huyo sio mdogo wake kwakweli...yani ndugu yako wa dam kabisa anatuhumiwa kuuza unga anadakwa na kulala central ...badala ya kumsaidia unasema ujinga kama huo..ety serikali inamlea sana Gwajima....ety anatuhumiwa vingi sana...hajamfufua baba wa watoto yatima ....huyu ni mjinga....kwaiyo anaisapport serikali imkandamize kaka yake...imfunge...imtuhumu kwa kuuza unga...huyu dogo anabidi akapimwe akili...Na sidhani kama ni mdogo wake wa kweli
 
Sasa mimi hapa huwa siwaelewi. Kama wanauza si wakamatwe? Au kutangaza ndio vita vyenyewe? Na kama huyo Daudi si kolomije kweli, si angeshaonesha vyeti?
Kama unaamini ana vyeti vya kugushi, kuwa jasiri wende ofisini kwake akuoneshe siyo kuviomba nyuma ya keyboard. Akikuonesha ni vyeti feki urudi humu jamvini kutupasha
 
Kwa ufupi mdogo wake mchungaji wa kanisa la ufufuo na uzima, Josephat Gwajima amesema mchungaji Gwajima anatakiwa aache kutumika na kuhoji kuna nani nyuma yake. Amedai mchungaji hawezi kujiingiza kwenye malumbano na mipasho ya kidunia.

Ameendelea kusema vyeti vya Makonda viachiwe mamlaka husika kuchunguza kwani kumuandama sana inaweza kusababisha watu wengine siku zijazo kuogopa kujihusisha kupambana na madawa ya kulevya.

Amesema serikali imemlea sana Gwajima na waziri wa mambo ya ndani anatakiwa amuangalie na ana tuhuma nyingi ikiwemo kadai angemfufua baba wa watoto yatima ilhali yeye anajua hajawahi kufufua hata panya.

Amedai tabia ya kubeza shughuli za maendeleo zinazofanywa na serikali sio tabia njema na haiisadii nchi. Amesema anajua vita ya madawa ya kulevya ni ngumu na hugharimu maisha, atoa wito kwa watanzania wote kuunga mkoni juhudi za kutokomeza madawa ya kulevya hasa Dar es Salaam.

Amesema anafahamu yeyote atakayejitokeza kuunga mkono juhudi za kupambana na madawa ya kulevya ataandamwa tu na hivyo kwa namna ya pekee anamshukuru mkuu wa mkoa wa Dar Paulo Makonda na atakumbukwa na vizazi vyote kwa kujitoa Muhanga kusimamia vita ya madawa ya kulevya Dar es Salaam na kila mmoja amefahamu athari za madawa ya kulevya hadi kwa watoto wadogo ndio maana anaandamwa kila kona na kuhoji walikuwa wapi kuyasema yote kabla ya vita ya madawa ya kulevya.


jina la huyu mdogo wa gwajima ni nani?
 
Back
Top Bottom