Mdogo wangu wa kike ndiyo kamaliza Form 6, safari ya chuo imekaribia. Nawaza ataukwepa vipi "Ukware" wa vyuoni?

Kwa nini uwe na hofu kwa jambo usiloweza kulizuia?.
Wanadamu wote wameumbiwa Hofu. Lakini sasa inakuja kuwa na utofauti katika viwango vya kuidhibiti (control) hofu yako.
Ni kweli katika jambo usiloweza kulizuia basi walau unaweza kujizatiti namna ya kukabiliana (mitigate) endapo litatokea kama matarajio yako yalivyo.
Kwa mfano; Je, likitokea uta deal na binti, uta deal na aliyehusika(kisababishi) au utakaa kimya?
 
Kama mkoa UNAO ishi kunachuo, asome hapo hapo tu, akiwa anatokea nyumbani
 
Wallah watambandua
 
Kwanini haukumtengenezea mazingira ya kujichunga mwenyewe mpaka umchunge mtu mzima mwenye akili timamamu?
Yeah. Ndo mana nimesema ni rahisi kuchunga kundi la ng'ombe kuliko mtu mmoja mwenye akili timamu.
Hapo utakuja kujawa na hasira bure na mwisho msemo huu utadumu kukushtaki nafsini mwako: "Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu" Lakini napo hapo bado kale kahuruma kana kuwepo. Huwezi na sio rahisi kumtelekeza ndg.yako na kumwachia ulimwengu umfundishe.
 
Hadi umri huo ulimkagua ukajua Yuko sealed? Huyo ni mwenyeji so acha kuhangaika na mambo yasiyo na msingi
 
Mshauri tu azingatie Elimu ya Kujilinda(Kinga)..
Kukwepa Mishale inahitaji Kujitoa kweli kweli.
 
Unaweza kuwa sahihi kwa baadhi ya situation. Kwa kesi ya mleta mada ni ngumu sana kulithibiti hilo linalomtia hofu. Labda amfungie ndani asiende chuo wala asichangamane na jamii kabisa au ampe ushauri wa namna ya kwenda kuishi huko chuoni. Hilo la pili ni gumu kwani litafanikiwa kutokana na misingi ya malezi na makuzi ya mtoto, na si kwa nasaha na mikwara kibao. Ni kumuasa tu akafocus na kilichompeleka, awe na mpenzi mmoja mwaminifu na maisha yaendelee, hayo mengine hayazuiliki kamwe.
 
Mwelekeze kila kitu bila kumwonea aibu wala kumficha.
Mweleze kila janja na mbinu za vijana na walimu wakware.

Sent from my SM-G970U using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…