Mdomo wa mtu wangu unanuka, namwambiaje?

Mdomo wa mtu wangu unanuka, namwambiaje?

C & P

Kumjulisha mtu kuhusu harufu mbaya ya mdomo ni jambo la hisia na linahitaji busara ili asijisikie vibaya. Hapa kuna mbinu kadhaa unazoweza kutumia:

1. Ulizia kuhusu Afya ya Kinywa kwa Ujumla
Unaweza kuanzisha mazungumzo kuhusu afya ya kinywa kwa ujumla, ukijumuisha usafi wa kinywa kama vile kupiga mswaki na kutumia dawa ya kusukutua. Unaweza kusema, "Nimeona dawa fulani ya kusukutua inasaidia sana kwa afya ya kinywa, unaweza kuijaribu kama unataka."


2. Toa Kinywaji cha Kusukutua au Pipermint kwa Ukarimu
Wakati mwingine, kumshirikisha mtu pipermint au kinywaji cha kusukutua inaweza kuwa njia ya moja kwa moja bila kuumiza hisia zake. Unaweza kusema, "Nina pipermint, unataka moja?" Hii inaweza kumfanya afikirie kuhusu harufu ya mdomo wake kwa upole.


3. Zungumzia Jinsi Harufu Mbaya ya Mdomo Inaweza Kuathiri Wengi
Unaweza kuanzisha mazungumzo kuhusu jinsi harufu ya mdomo ni suala linalowakumba watu wengi na si kitu cha kawaida. Unaweza kusema kitu kama, "Watu wengi wanapata harufu mbaya ya mdomo bila kujua; nimegundua vidokezo fulani vya kusaidia."


4. Shirikisha Uzoefu Wako
Kama una uzoefu na harufu ya mdomo au umewahi kupitia jambo kama hilo, unaweza kushiriki hadithi yako kwa njia ambayo itampa mshawisho wa kuchukua hatua. Unaweza kusema, "Kuna wakati niligundua kuwa mdomo wangu unanuka, nikaamua kutumia pipermint mara kwa mara."



Njia hizi zinaweza kusaidia kufikisha ujumbe bila kumuumiza mtu hisia zake.
Fact mpwa
 
Wewe ndo unanuka mdomo sema unazunguuuka wadau chukueni hii mbinu ni mujarabu kabisa.Mwambie kuna jamaa nimekutana nae ameniambia nanuka mdomo ila ameniambia kuna dawa inabidi nitumie alafu unamwambia mbona wewe huniambii kwamba nanuka mdomo kisha mwambie kila mtu ampumulie mwenzake pumzi ili kupima alafu mwambie aanze yeye kukupumulia pumzi akishafanya hivyo na wewe fuata alafu muulize je nanuka kweli? lazima yeye atasema haunuki kuhusu yeye mwambie leo ndo kwa mara ya kwanza nakusikia unanuka mdomo kishenzi itakuwa nilikuambukiza alafu mtajie dawa ukijifanya hizo ndo zimekuponyesha.
Hii ni njia nzuri. Ukishamweka kwenye hii angle basi hata kesho yake kama ataendelea kunuka inakuwa rahisi kumwambia ''na leo bado una ka-harufu japo kadogoo, ulitumia ile dawa kweli''. Kuanzia hapa itakuwa rahisi sana ku-control kwani anakuwa ameshajua tatizo.
 
Kwa uelewa wangu mdogo suala la kutoa harufu mbaya kinywani sio kwa ajili ya aina ya dawa Bali ni jinsi kupiga mswaki vizuri,nakumbuka Bi mkubwa miaka alinifundisha sana coz alikua ni mtaalamu wa kinywa na meno
 
Wewe ndo unanuka mdomo sema unazunguuuka wadau chukueni hii mbinu ni mujarabu kabisa.Mwambie kuna jamaa nimekutana nae ameniambia nanuka mdomo ila ameniambia kuna dawa inabidi nitumie alafu unamwambia mbona wewe huniambii kwamba nanuka mdomo kisha mwambie kila mtu ampumulie mwenzake pumzi ili kupima alafu mwambie aanze yeye kukupumulia pumzi akishafanya hivyo na wewe fuata alafu muulize je nanuka kweli? lazima yeye atasema haunuki kuhusu yeye mwambie leo ndo kwa mara ya kwanza nakusikia unanuka mdomo kishenzi itakuwa nilikuambukiza alafu mtajie dawa ukijifanya hizo ndo zimekuponyesha.
Ahahaha KAZI IPO
 
Back
Top Bottom