Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Habari zenu wakuu,
Leo katika pita pita zangu katika mtandao wa YouTube nikakutana na vipande vinavyoonesha mechi mbalimbali za Simba na Yanga. Nikiwa kama mdau ma mfuatiliaji wa soka la nyumbani mara nyingi huwa naona mechi zinazoikutanisha Miamba hii ya soka nchini huwa zinakosa mvuto kutokana na kukamiana sana.
Kwa kusema haya, haimaanishi mechi zote wanazokatana Timu hizi huwa zinakosa mvuto. Binafsi licha ya kupenda sana soka huwa napenda sana kitu tunaita 'COMEBACK' au kwa kiswahili cha kisoka tunaita 'kuchomoa'. Kwahiyo, miongoni mwa mechi pekee zilizonivutia ni ile ya "Kichuya Kona" na ile ya Yanga 3 na Simba tatu kwa sababu zilionesha maana halisi ya Mpira dakika tisini.
Vipi kwa upande wenu wanasoka wenzangu gemu ipi ya Watani wa Jadi unaikumbuka na ilikuvutia zaidi? inakukumbusha nini gemu hiyo?
Nini unakiona katika mechi ijayo kati ya miamba hii?
Karibuni tujadili wazee wenzangu.
Leo katika pita pita zangu katika mtandao wa YouTube nikakutana na vipande vinavyoonesha mechi mbalimbali za Simba na Yanga. Nikiwa kama mdau ma mfuatiliaji wa soka la nyumbani mara nyingi huwa naona mechi zinazoikutanisha Miamba hii ya soka nchini huwa zinakosa mvuto kutokana na kukamiana sana.
Kwa kusema haya, haimaanishi mechi zote wanazokatana Timu hizi huwa zinakosa mvuto. Binafsi licha ya kupenda sana soka huwa napenda sana kitu tunaita 'COMEBACK' au kwa kiswahili cha kisoka tunaita 'kuchomoa'. Kwahiyo, miongoni mwa mechi pekee zilizonivutia ni ile ya "Kichuya Kona" na ile ya Yanga 3 na Simba tatu kwa sababu zilionesha maana halisi ya Mpira dakika tisini.
Vipi kwa upande wenu wanasoka wenzangu gemu ipi ya Watani wa Jadi unaikumbuka na ilikuvutia zaidi? inakukumbusha nini gemu hiyo?
Nini unakiona katika mechi ijayo kati ya miamba hii?
Karibuni tujadili wazee wenzangu.