Mechi gani ya Watani wa jadi (Simba na Yanga) unaikumbuka zaidi?

Mechi gani ya Watani wa jadi (Simba na Yanga) unaikumbuka zaidi?

Duuh mzee heshima yako! Wenzetu mlifaidi kuona vipaji halisi kipindi hichoi! Siku hizi msisimko wa pambano la watani wa jadi umepungua sana! Mzee tukumbushe na ile simba aliyotia mpira kwapani!

hahahahahaha ile game nilikuwepo uwanjani uwanja wa taifa sasa uwanja wa Uhuru...Yanga ilikuwa na kikosi kikali sana...Akina Sanifu Lazaro na wengineo..Simba nayo ilikuwa na vijana wazuri lakini kiukweli Simba walikuwa underdog kwa Yanga...Simba katika game ile kipindi cha kwanza walicheza rafu za ajabu na za kushangaza lakini hakuna kadi nyekundu iliyotolewa kwa mshangao wa wengi...Refa alikuwa ni Hafidh kutoka Zanzibar sasa ni marehemu ...wakati anafariki alikuwa ni Mbunge....Kipindi hicho cha kwanza mpira ulikuwa unachezwa kwenye lango la Simba lakini matokeo bado yalibaki 0-0 na hakuna kadi iliyotolewa kwa Simba pamoja na rafu za ajabu...Kepteni wa Simba alikuwa nadhani ni Method Mogella akicheza namba nane...msimu uliofuatia Method alihamia Yanga ambako alikuwa anacheza namba 4 au 5...sasa katika game ile Simba wakagoma kuingia uwanjani kipindi cha pili...Ilifahamika baadaye kuwa Simba walikuwa wanafanya rafu makusudi ili wapewe kadi nyekundu na iwe ndiyo sababu ya wao kususia mechi kwa kisingizio cha kuonewa...Ilifahamika baadaye kuwa refa aligundua janja hiyo ya Simba na ndiyo maana akawa hawapi kadi....Na habari ambazo hazijathibitishwa zinasemma kuwa ndani ya uwanja Hafidhi aliwaambia wachezaji wa Simba kuwa hatawapa kadi nyekundu ila watafungwa tu kihalali...Kiukweli Simba walizidiwa mno game ile na wangerudi tu uwanjani wangepigwa nyingi...hawakuingia uwanjani kipindi ha pili kukwepa aibu ya kufungwa.....
 
hahahahahaha ile game nilikuwepo uwanjani uwanja wa taifa sasa uwanja wa Uhuru...Yanga ilikuwa na kikosi kikali sana...Akina Sanifu Lazaro na wengineo..Simba nayo ilikuwa na vijana wazuri lakini kiukweli Simba walikuwa underdog kwa Yanga...Simba katika game ile kipindi cha kwanza walicheza rafu za ajabu na za kushangaza lakini hakuna kadi nyekundu iliyotolewa kwa mshangao wa wengi...Refa alikuwa ni Hafidh kutoka Zanzibar sasa ni marehemu ...wakati anafariki alikuwa ni Mbunge....Kipindi hicho cha kwanza mpira ulikuwa unachezwa kwenye lango la Simba lakini matokeo bado yalibaki 0-0 na hakuna kadi iliyotolewa kwa Simba pamoja na rafu za ajabu...Kepteni wa Simba alikuwa nadhani ni Method Mogella akicheza namba nane...msimu uliofuatia Method alihamia Yanga ambako alikuwa anacheza namba 4 au 5...sasa katika game ile Simba wakagoma kuingia uwanjani kipindi cha pili...Ilifahamika baadaye kuwa Simba walikuwa wanafanya rafu makusudi ili wapewe kadi nyekundu na iwe ndiyo sababu ya wao kususia mechi kwa kisingizio cha kuonewa...Ilifahamika baadaye kuwa refa aligundua janja hiyo ya Simba na ndiyo maana akawa hawapi kadi....Na habari ambazo hazijathibitishwa zinasemma kuwa ndani ya uwanja Hafidhi aliwaambia wachezaji wa Simba kuwa hatawapa kadi nyekundu ila watafungwa tu kihalali...Kiukweli Simba walizidiwa mno game ile na wangerudi tu uwanjani wangepigwa nyingi...hawakuingia uwanjani kipindi ha pili kukwepa aibu ya kufungwa.....
Hii match nilikuwepo Uwanjani nikiwa bado Kijana mdogo kabisa.
 
4-3 2010 hilary echesa anapiga mashine moja toka katikati ya uwanja dk za majeruhi
 
Hivi kwanini yanga wakifungwa na Simba wanadai hujuma lakini wao wakishinda wameshinda kihalali hata Kama goli limefungwa kwa mkono
 
Usipotoshe,Yanga ilizidiwa kiuwezo.
Kama Yanga walikula mlungula je mechi ya Jana walikula nini
Ile mechi ya 4-1 iliuzwa...Wale wafanyabiashara wa kiasia waliokuwa wamejazana Yanga kwa madai ya kuifadhili walikula njama kwa lengo la Yanga ifungwe ili George mpondela ''Castro' aliyekuwa madarakani kama Katibu Mkuu ang'oke madarakani...'Castro' alikuwa hataki Yanga ijiegemeze kwa wafayabiashara hao wa kiasia...Hii ni sawa na mechi ya 5-0 ambapo mfanyabiashara mmoja wakiwemo baadhi ya vizee vya Yanga walikula njama Yanga ifungwe nyingi ili mwenyekiti Nchunga ang'oke madarakani na alifanya hivyo baada ya kichapo hicho ...Mechi ya kihistoria ya Yanga na Simba ni ile ya mwaka 1974 pale Nyamagana Mwanza ambapo Simba alilala 2-1. Wafungaji Yanga ni Gibson Sembuli na Sunday Manara na Simba ni Adam Sabu. Mechi hii ilichezwa dakika 120 ...Sunday alifunga goli la 2 kwenye dakika za nyongeza ...Yaani kwenye dakika 15 za mwanzo za nyongeza. Sembuli alisawazisha dakika ya 87...Adam Sabu alifunga goli la Simba kipindi ha kwanza kati ya dakika 16 na 20....Hiyo ndiyo ilikuwa game ya ukweli...Simba walilalamika kwa goli la Sembuli wakidai kuwa alifunga wakati dakika 90 zimemalizika ...waliwasilisha malalamiko hadi CAF lakini haikusaidia kitu...ukweli goli lile lilifungwa ndani ya dakika 90....Mechi hii ilikuwa na hisia kali sana miongoni mwa mashabiki wa timu zote mbili..Yanga ilikuwa ikiigaraza Simmba kwa miaka mitano mfululizo kuanzia mwaka 1968 hadi mwaka 1972. Na mwaka 1973 Simba ilijikomboa kwa kuifunga yanga goli 1-0 goli lililofungwa na Willy Mwaijibe kama sijakosea..kumbukumbu zinanitupa kidogo inawezekana ni Haidari Abeid...........Mwaka 1974 timu zote mbili zikajiandaa vilivyo..Kabla ya michuano ya ubingwa kuanza Simba ikaenda Poland kwa mazoezi Yanga nayo ikaenda Romania ...Ikawa ni vita...Yanga anataka kuifunga Simba akidai kuwa simmba ilibahatisha tu mwaka 1973...Simba nayo ikaona kuwa ni lazima iendeleze kichapo kwa Yanga...Siku ya mechi pale Nyamagana nchi ikasimama...masikio ya mamilioni ya mashabiki wa pande zote mbili yakaelekezwa Mwanza...Kulikuwa hakuna TV watu wanasikiliza kupitia RTD na viredio vvya dudu proof...betri za redio kabla ya mechi zikawa zinaanikwa ili kuongeza nguvu ..Baada ya game wapenzi kadhaa wa Simba waliripotiwa kujinyonga na kufa kukwepa muendelezo wa masimango mitaani..kwa mfano kule Tabora mnazi mmoja wa Simba aliamua kujitumbukiza kwenye pipa la pombe aina ya kangara iliyokuwa jikoni....Baadhi yetu tulikuwa wanafunzi sekondari na wakati wa mechi hiyo tulikuwa likizo...sasa shule zilipofunguliwa baadhi ya wanafunzi manazi wa Simba walichelewa kuja shuleni kukwepa kejeli za manazi wa Yanga...Mchezo ule ulitungiwa kitabu na goli la kusawazisha la Sembuli likawa kwenye mchoro kitabuni kuelezea namna lilivyofungwa...Kama sijakosea mwandishi wa kitabu kile aliitwa Hadji Konde.....Nakummbuka Sembuli alifunga goli lile kwa pasi ya Kichwa ya Kitwana Manara ....Aisee ilikuwa raha sana...Kwangu mimi haitatokea mechi kama ile iliyojaa hisia kali..Katika mechi ile ya Nyamagana mchezaji nyota wa Simba, Saad Alli...alizirai uwanjani dakika za mwanzo kabisa na kukimbizwa hospitali ya mkoa wakati ule nadhani ni Sekou Toure pale Mwanza....ilikuwa ni katika dakika za mwanzo kabisa za mchezo...Mengi yalisemwa kuhusu kuzirai kwa Saad Alli wengi wakihusisha na imani za ushirikina... .
Screenshot_20191111-182947_Instagram.jpeg
 
Mechi ya 3-3 haiwezi kusahaulika kwa muda mrefu. Haikuwa mechi yenye msisimko sana nje ya uwanja lakini uwanjani ilikuwa ni burudani mwanzo mwisho. Hakuna dkk ya mchezo ambayo haikuwa na maana.

Yanga iliperform kwa kiwango cha juu sana katika kipindi cha kwanza huku Simba ikionekana kuzidiwa kila eneo. Kipindi cha pili ilionekana kinyume chake. Vijana wadogo wa Simba wakiongozwa na Said Ndemla na William Lucian, walitandaza kabumbu la karne na kadri muda ulivyokuwa ukienda ndivyo vijana walizidi kuwa watamu. Ni mechi ambayo kila timu ilicheza kwa kiwango cha fainali ya Ligi ya mabingwa Africa lakini katika dkk 45 tu kila moja.
 
Mechi ya 3-3 haiwezi kusahaulika kwa muda mrefu. Haikuwa mechi yenye msisimko sana nje ya uwanja lakini uwanjani ilikuwa ni burudani mwanzo mwisho. Hakuna dkk ya mchezo ambayo haikuwa na maana.

Yanga iliperform kwa kiwango cha juu sana katika kipindi cha kwanza huku Simba ikionekana kuzidiwa kila eneo. Kipindi cha pili ilionekana kinyume chake. Vijana wadogo wa Simba wakiongozwa na Said Ndemla na William Lucian, walitandaza kabumbu la karne na kadri muda ulivyokuwa ukienda ndivyo vijana walizidi kuwa watamu. Ni mechi ambayo kila timu ilicheza kwa kiwango cha fainali ya Ligi ya mabingwa Africa lakini katika dkk 45 tu kila moja.
Nakumbuka hii mechi kwenye kibandaumiza mashabiki wa simba tulikuwq wqtatu tu lakin was Jangwan walikuwa kama wote
 
Ile game I think it was 1994, naikumbuka sana kwa sababu 1993 yote Yanga walitutesa kupitia Kizota na Lunyamila.

Sasa siku ile George Masatu ndo alianza kufunga, Kimanda akarudisha. Tukaja kumaliza na goli 4, nakumbuka tulizunguka mji mzima tunashangilia.

Nilirudi home saa 6 usiku, mama akagoma kunifungulia, dingi anauliza nilikuwa wapi nikamwambia. Akasema ingia ndani, bila zengwe.
Mechi hii akina Azim Dewji na wenzie walinunua.
 
Kwa umri wangu, ile mechi ya goli 3 - 3
Picha linaanza Ngasa anaahidi kama hataifunga Simba, atachoma moto nyumba yake Mwanza. Daah!! Kweli kijana akatufunga Simba, huku nikikerwa na Shangilia ya Hamis Diego Kiiza ile kama anatetema aiseeee....Kipindi cha kwanza tumeloa 3 nunge, napigiwa simu na watu wa Yanga, wakiongozwa na Kaka yangu mnazi mkubwa wa kwasukwasu akijinasibu leo tunawalipa zile 5. Kipindi cha Pili anaingia Ndemla na William Lucian, huku kocha Kibaden akionekana hana wasiwasi kabisa.... Yule beki mrundi anachomoa bao la 3 aisee nilishangalia sana. NAIPENDA SIMBA.....(kama isingekua ubora wa Kakolanya 2018 Yanga ilikua afe 5 tena, bahati ilikua upande wao)
 
Mwaka 1947 hii mechi ni kama naiona hivi.game ilikuwa tight kinyama. Wanaume walikuwa wanatunduana uwanjani kunawaka moto.ile mechi ilikuwa inashuhudiwa na maelfu ya watanzania uwanjani. Simba walikuja kushinda kwa mbinde bao 3-0 kama sikosei.
 
Simba ilishinda 5-0; nilikuwa Taifa kushuhudia hii kipande ya historia.
 
4-3 2010 hilary echesa anapiga mashine moja toka katikati ya uwanja dk za majeruhi
Hiyo mech ilikuwa mzuri sana. Tegete alitia 2 kama sikosei. Kwa simba uhuru suleiman alikuwa kwenye kiwango bora sana.japo timu yangu ya yanga ilifungwa lakin ilicheza vena sana
 
Habari ya jioni wakuu,

Leo katika pita pita zangu katika mtandao wa YouTube nikakutana na vipande vinavyoonesha mechi mbalimbali za Simba na Yanga. Nikiwa kama mdau ma mfuatiliaji wa soka la nyumbani mara nyingi huwa naona mechi zinazoikutanisha Miamba hii ya soka nchini huwa zinakosa mvuto kutokana na kukamiana sana.

Kwa kusema haya, haimaanishi mechi zote wanazokatana Timu hizi huwa zinakosa mvuto. Binafsi licha ya kupenda sana soka huwa napenda sana kitu tunaita 'COMEBACK' au kwa kiswahili cha kisoka tunaita 'kuchomoa'. Kwahiyo, miongoni mwa mechi pekee zilizonivutia ni ile ya "Kichuya Kona" na ile ya Yanga 3 na Simba tatu kwa sababu zilionesha maana halisi ya Mpira dakika tisini.

Vipi kwa upande wenu wanasoka wenzangu gemu ipi ya Watani wa Jadi unaikumbuka na ilikuvutia zaidi?
inakukumbusha nini gemu hiyo?

Karibuni tujadili wazee wenzangu.
FB_IMG_15739881222502234.jpg
 
Yanga unijitetea tu
Mechi nyingi simba anakuwa na nafasi ya kupata matokeo chanya kuliko Yanga.
hahahahahaha ile game nilikuwepo uwanjani uwanja wa taifa sasa uwanja wa Uhuru...Yanga ilikuwa na kikosi kikali sana...Akina Sanifu Lazaro na wengineo..Simba nayo ilikuwa na vijana wazuri lakini kiukweli Simba walikuwa underdog kwa Yanga...Simba katika game ile kipindi cha kwanza walicheza rafu za ajabu na za kushangaza lakini hakuna kadi nyekundu iliyotolewa kwa mshangao wa wengi...Refa alikuwa ni Hafidh kutoka Zanzibar sasa ni marehemu ...wakati anafariki alikuwa ni Mbunge....Kipindi hicho cha kwanza mpira ulikuwa unachezwa kwenye lango la Simba lakini matokeo bado yalibaki 0-0 na hakuna kadi iliyotolewa kwa Simba pamoja na rafu za ajabu...Kepteni wa Simba alikuwa nadhani ni Method Mogella akicheza namba nane...msimu uliofuatia Method alihamia Yanga ambako alikuwa anacheza namba 4 au 5...sasa katika game ile Simba wakagoma kuingia uwanjani kipindi cha pili...Ilifahamika baadaye kuwa Simba walikuwa wanafanya rafu makusudi ili wapewe kadi nyekundu na iwe ndiyo sababu ya wao kususia mechi kwa kisingizio cha kuonewa...Ilifahamika baadaye kuwa refa aligundua janja hiyo ya Simba na ndiyo maana akawa hawapi kadi....Na habari ambazo hazijathibitishwa zinasemma kuwa ndani ya uwanja Hafidhi aliwaambia wachezaji wa Simba kuwa hatawapa kadi nyekundu ila watafungwa tu kihalali...Kiukweli Simba walizidiwa mno game ile na wangerudi tu uwanjani wangepigwa nyingi...hawakuingia uwanjani kipindi ha pili kukwepa aibu ya kufungwa.....
 
Ile Volley ilikuwa hatari sana.
Japo kwangu mimi game nzuri ni ile tuliyosawazisha goli tatu tukiwa na kikosi dhaifu kuwa wao.
4-3 2010 hilary echesa anapiga mashine moja toka katikati ya uwanja dk za majeruhi
 
Yanga unijitetea tu
Mechi nyingi simba anakuwa na nafasi ya kupata matokeo chanya kuliko Yanga.

Wewe inaelekea ni shabiki wa Simba wa kizazi cha kuanzia miaka ya 2000....inawezekana ulizaliwa miaka ya 2000...waulize wanaojua historia ya timu hizi mbili ni ipi kati ya Simba na Yanga imemfunga mwenzie mara nyingi...
 
Back
Top Bottom